Kikwete aamuru mitambo ya IPTL iwashwe mara moja!

Ninajiquote nilichosema tarehe 15/10/2009

Ninapendekeza;

  • Serikali ihakikishe mitambo ya IPTL inawashwa mara moja wakati mazungumzo yake na IPTL yakiendelea kwa kuharakishwa (fast tracking). Hali ya nchi ni mbaya, ni sawa na vita, haiwezekani serikali yenye mamlaka ishindwe kuhakikisha IPTL inazalisha umeme wakati mazungumzo yakiendelea. Haiwezekani.Labda kama haina uchungu na maisha ya watu wake.
  • Sikutaka kusema chochote nikiamini kwamba Shirika la TANESCO, Serikali, na kwa upande wa bunge, Kamati ya masuala ya Nishati na Madini, wangeweza kutoa majibu ya tatizo linatukabili. Badala yake, juhudi nyingi zimetumika kutafuta chanzo cha tatizo na kuchelea kutoa suluhuInaumiza sana kuona kuwa tunaendekeza siasa rahisi tunaposhugulikia masuala mazito ya kitaifa kama Nishati. Inasikitisha zaidi pale tunapoona kuwa serikali inashindwa kuchukua hatua mahususi za kuhami uchumi wa Taifa letu. Serikali na Bunge hazitoi suluhisho la hali hii na ni wazi kuna kutupiana mpira wakati nchi inaumia. Serikali imewekwa madarakani ili ifanye maamuzi na tuihukumu kwa maamuzi hayo. Serikali ni lazima sasa iamue.
  • Mazingira magumu kama haya yanahitaji maamuzi magumu (extra ordinary circumstances require extra ordinary decisions). Ninaamini serikali itazingatia ushauri wangu.
Mnisamehe kwa kujiquote!

Ikulu inasema wafanyabiashara ndio wamemwomba Rais. Ni sawa tu........


 
Mkuu Kevo heshima mbele kiongozi.

JK alikuwa anajua waziri Ngeleja angeweza kutatua hili tatizo, kumbe hakujua jamaa ni bomu vibaya sana.

Si kila kitu anatakiwa kufanya yeye ndiyo maana ana mawaziri na mawaziri ni watu wakubwa sana serikalini, sisi wetu sijui hawajui hilo.

Kwani JK alitumia kigezo gani kumteua Ngeleja?
 
Wameona wakikubali kwamba wamefuata ushauri wa Zitto wataonekana wajinga, sasa wanabadilisha story, lakini werevu tushagundua.

Kuna watanzania kwa maelfu walikuwa hawajui kama mitambo ya IPTL imezimwa, ni mpaka Zitto alipoanika kila kitu.
 
hili si moja ya pendekezo la Zitto la juzi? Walikuwa wapi mda wote huo? Eti mpaka raisi afanye where is ze minister?
 
Ikulu inasema wafanyabiashara ndio wamemwomba Rais. Ni sawa tu........

Mh.

Nasubiri waje wengine wamwombe ataifishe ile mingine.

Kama ameamuru iwashwe ya IPTL wakati kesi iko mahakamani anashindwa nini kutaifisha DOWANS na kesi iko mahakamani vile vile.?

Au one thing at a time.

NAOMBENI MUONGOZO.
 
Huu ushauri wa kutumia IPTL ndio unasifiwa kiasi hiki?

Ama kweli miafrika ndivyo tulivyo. Yaani tatizo la umeme limekuwa linatabiriwa kwa mwaka mzima sasa na Kikwete hakufanya chochote ila leo ndio anaamka na kuanza kutoa amri kuwa IPTL iwashwe?

Alikuwa wapi siku zote? Zitto alikuwa wapi muda wote?
 
kuna kitu mwanakijiji kadokeza in one if the threads sijui ndo hivi vinaanza kitokea.... Lets wait. Huenda mapendekezo yote ya Zitto yakatekelezwa lakini wakatwambia kiujanja ujanja ni initiative zao. Ama kwelu serekali yetu.
 
kuna kitu mwanakijiji kadokeza in one if the threads sijui ndo hivi vinaanza kitokea.... Lets wait. Huenda mapendekezo yote ya Zitto yakatekelezwa lakini wakatwambia kiujanja ujanja ni initiative zao. Ama kwelu serekali yetu.

Ina maana mapendekezo ya Zitto - kuwasha IPTL na kutaifisha Dowans - ndio silver bullet ya matatizo ya umeme Tanzania?
 
Amri atoe mwingine sifa apewe mwingine...Duh! Mwenye kupenda chongo huona kengeza!


Kibungano ufike mahali uone aibu.Zitto kichwa wewe hata ana kasoro zake kama mtu lakini the man anaipenda Tanzania na watanzania . Alisha yasema hapa mapema akaungwa mkono na wana sheria .Kama kawaida CCM wakawa wagumu kwa kuwa kasema Zitto . Now wageni wanatumika kama njia tu lakini ukweli ni kwamba Zitto na Chadema wako very focused .
 
Huu ushauri wa kutumia IPTL ndio unasifiwa kiasi hiki?

Ama kweli miafrika ndivyo tulivyo. Yaani tatizo la umeme limekuwa linatabiriwa kwa mwaka mzima sasa na Kikwete hakufanya chochote ila leo ndio anaamka na kuanza kutoa amri kuwa IPTL iwashwe?

Alikuwa wapi siku zote? Zitto alikuwa wapi muda wote?

Mkuu,

katika pita pita zangu katika thread hii sijaona mahali huu ushauri wa kutumia IPTL ukisifiwa kama unavyodai labda kama nimeona kengeza!

Wengi wa wachangiaji wanashangaa JK alikuwa wapi siku zote hizi haya maamuzi hayachukuliwa mpaka wawekezaji na wafanya biashara wakubwa walamike wakati kuna wazalendo kama akina Zitto walikwisha suggest similar things!
 
Ina maana mapendekezo ya Zitto - kuwasha IPTL na kutaifisha Dowans - ndio silver bullet ya matatizo ya umeme Tanzania?

Solomon Vipi bana, kwani hujui hawa jamaa hawaoni mbali...zima moto...zima zima...wanapigania 140MW wakati watanzania 88% wako gizani, hili hawaongelei na wala hawalioni, hili ndilo kubwa zaidi.
 
Ina maana mapendekezo ya Zitto - kuwasha IPTL na kutaifisha Dowans - ndio silver bullet ya matatizo ya umeme Tanzania?

Zitto aliongelea kwa solution ya haraka ya kuokoa Taifa na giza na hakusema ndiyo ufumbuzi wa kudumu .Zitto aliuliza kwa nini Nchi iko kwenye giza na mitambo ipo ?
 
Back
Top Bottom