Kikwete aahirisha ziara ya Mbeya

Lazima kuna kitu uko mbeya si bure!
Ni mara ya 3 sasa,labda anaogopa kuzomewa kama rafiki wa mafisadi.

Kwa medani ya Siasa, Mkoa wa Mbeya na hasa Wilaya mbili za Rungwe na Kyela mambo si mazuri sana kwa JK na kundi lake. Kibaya zaidi Wanamtandao kwa njia moja ama nyingine ndio wamekuwa wakichangia hali hii. JK alichopaswa kufanya mara tu baada ya Uchaguzi ni kushirikiana kwa KARIBU na wananchi wa Mbeya na kukubali kuwa kisiasa Mbeya siyo ENEO lake. Kosa kubwa la kwanza la JK alilolifanya mara tu baada ya Uchaguzi ni kumteua Samson Mwakipesile kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya. Kwenye kura za maoni Mwakipesile alibwagwa mbali na Mbunge wa sasa hivi Dk. Samson Mwakyembe kule Kyela. Kwa wana Mbeya kumuweka Mwakipesile ilionekana kama JK alikuwa hakuridhishwa na namna walivyomkataa na kama alikuwa akiwakomoa.

Mkuu huyo wa Mkoa baada ya kuteuliwa alipaswa kumaliza CHUKI zote za kisiasa na mahasimu wake lakini alichoamua kufanya ni kupandikiza na kuendeleza chuki zisizo na msingi. Nadhani alifanya hivi kwa maelekezo ya wanamtandao ambapo tunaambiwa yeye ni mwanakikundi.

Jambo jingine baya kwa JK na wapambe wake ni namna ambavyo wamekuwa wanajaribu kummaliza Prof Mwandosya kisiasa. Kumbuka namna Thomson Apson Mwang'onda alivyoteuliwa kuwa Mbunge wa nafasi maalum za JK na baadaye kuletwa kugombea ujumbe wa NEC Mkoa wa Mbeya akipambanishwa na Mwandosya. Wapambe wa Thom ni wazi mitaani walikuwa wakiongea kwamba dogo alikuwa na baraka la JK. Sina uhakika na hilo lakini kwa kuwa ilikuwa inatangazwa hadharani ilipaswa JK kwa kutumia wasemaji wake ndani ya CHAMA angelikanusha.

Inasemekana wanamtandao tena walimpandikiza Nawab Mulla ambaye ana nasaba ya karibu na Rostam Aziz kuwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mbeya. Hili nalo limeleta kizaazaa kweli ukizingatia historia 'mbaya' ya Nawab katika biashara kwani ni majuzi tu alihusishwa na kukamatwa kwa pembe za ndovu kule Iringa. Nawab pia anahusishwa katika kumsaidia Rostam hadi kufanikiwa kuuziwa yale mashamba ya Mbarali.

Kwa wana Mbeya, Mwandosya ni CHAGUO lao kwa kila hali. Sipendi kusema kwa nini amekuwa KIPENZI chao labda wengine watakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kulisemea.

Likaja hili la Richmond na Dk Mwakyembe. Kwa kila hali wanamtandao wa JK hawakufurahishwa kabisa na Kamati ya Mwakyembe na kimsingi kuna vita baridi inayoendelea dhidi ya Dk Mwakyembe na Wanamtandao. Wananchi wa Mbeya na hasa wapiga kura wake wanafuatilia kwa karibu sana suala hili na hasa kipindi kile alichoanguka na kuugua ghafla bungeni, wengi wanaamini pale kulikuwa na 'mkono wa mtu' kimsingi Dk Mwakyembe amekuwa akipewa ulinzi usio wa kawaida kwa wadhifa wake wa Ubunge na wapiga kura wake.

Kama nilivyosema JK alipaswa kushirikiana na watu wa Mkoa wa Mbeya ikiwemo kufanya ziara za mara kwa mara. Kama anaweza kwenda Mwanza kila mwezi anashindwa nini kwenda Mbeya kila baada ya miezi sita? Yawezekana ziara ya Lowassa iliwashitua sana wanamtandao kwani tunaambiwa hakupokelewa vizuri pamoja na CCM 'kuandaa mapokezi mazito'

BADO NAAMINI JK ANAPASWA KWENDA MBEYA NA LABDA KUUNGAMA HADAHARANI KWAMBA AMEKUWA HAUTENDEI HAKI MKOA HUO VINGINEVYO LABDA KIMAHESABU MKOA HUO SI TISHIO KWA UCHAGUZI WA 2010.
 
RC anaitwa Livingstone siyo Samson. Yeye ndiye amekuwa msitari wa mbele kuahirisha ziara za Rais na uongo wake.Mara Mwandosya kaandaa watu kumzomea, mara watoto wanafanya mitihani, mara hiki, mara kile. Rais anaenda Mbeya week ijayo, Mwakipesile kaisha msingizia kijana Rungwe eti anajiandaa kumpiga mawe Rais!!!
Hakuna maendeleo Mbeya ni malumbano ya kisiasa tu.Eti Rais kaandaliwa kutembelea kiwanda cha chai, Rungwe ambacho kinakarabatiwa, hakijafanya kazi tangu 1999!!!!Hive kweli hakuna hata mashule yakuweka jiwe la msingi!!!
 
RC anaitwa Livingstone siyo Samson. Yeye ndiye amekuwa msitari wa mbele kuahirisha ziara za Rais na uongo wake.Mara Mwandosya kaandaa watu kumzomea, mara watoto wanafanya mitihani, mara hiki, mara kile. Rais anaenda Mbeya week ijayo, Mwakipesile kaisha msingizia kijana Rungwe eti anajiandaa kumpiga mawe Rais!!!
Hakuna maendeleo Mbeya ni malumbano ya kisiasa tu.Eti Rais kaandaliwa kutembelea kiwanda cha chai, Rungwe ambacho kinakarabatiwa, hakijafanya kazi tangu 1999!!!!Hive kweli hakuna hata mashule yakuweka jiwe la msingi!!!

RC wa Mbeya ni John Livingstone Mwakipesile na Mbunge wa Kyela ni DK. Harrison Mwakyembe.
 
Kwa medani ya Siasa, Mkoa wa Mbeya na hasa Wilaya mbili za Rungwe na Kyela mambo si mazuri sana kwa JK na kundi lake. Kibaya zaidi Wanamtandao kwa njia moja ama nyingine ndio wamekuwa wakichangia hali hii. JK alichopaswa kufanya mara tu baada ya Uchaguzi ni kushirikiana kwa KARIBU na wananchi wa Mbeya na kukubali kuwa kisiasa Mbeya siyo ENEO lake. Kosa kubwa la kwanza la JK alilolifanya mara tu baada ya Uchaguzi ni kumteua Samson Mwakipesile kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya. Kwenye kura za maoni Mwakipesile alibwagwa mbali na Mbunge wa sasa hivi Dk. Samson Mwakyembe kule Kyela. Kwa wana Mbeya kumuweka Mwakipesile ilionekana kama JK alikuwa hakuridhishwa na namna walivyomkataa na kama alikuwa akiwakomoa.

Mkuu huyo wa Mkoa baada ya kuteuliwa alipaswa kumaliza CHUKI zote za kisiasa na mahasimu wake lakini alichoamua kufanya ni kupandikiza na kuendeleza chuki zisizo na msingi. Nadhani alifanya hivi kwa maelekezo ya wanamtandao ambapo tunaambiwa yeye ni mwanakikundi.

Jambo jingine baya kwa JK na wapambe wake ni namna ambavyo wamekuwa wanajaribu kummaliza Prof Mwandosya kisiasa. Kumbuka namna Thomson Apson Mwang'onda alivyoteuliwa kuwa Mbunge wa nafasi maalum za JK na baadaye kuletwa kugombea ujumbe wa NEC Mkoa wa Mbeya akipambanishwa na Mwandosya. Wapambe wa Thom ni wazi mitaani walikuwa wakiongea kwamba dogo alikuwa na baraka la JK. Sina uhakika na hilo lakini kwa kuwa ilikuwa inatangazwa hadharani ilipaswa JK kwa kutumia wasemaji wake ndani ya CHAMA angelikanusha.

Inasemekana wanamtandao tena walimpandikiza Nawab Mulla ambaye ana nasaba ya karibu na Rostam Aziz kuwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mbeya. Hili nalo limeleta kizaazaa kweli ukizingatia historia 'mbaya' ya Nawab katika biashara kwani ni majuzi tu alihusishwa na kukamatwa kwa pembe za ndovu kule Iringa. Nawab pia anahusishwa katika kumsaidia Rostam hadi kufanikiwa kuuziwa yale mashamba ya Mbarali.

Kwa wana Mbeya, Mwandosya ni CHAGUO lao kwa kila hali. Sipendi kusema kwa nini amekuwa KIPENZI chao labda wengine watakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kulisemea.

Likaja hili la Richmond na Dk Mwakyembe. Kwa kila hali wanamtandao wa JK hawakufurahishwa kabisa na Kamati ya Mwakyembe na kimsingi kuna vita baridi inayoendelea dhidi ya Dk Mwakyembe na Wanamtandao. Wananchi wa Mbeya na hasa wapiga kura wake wanafuatilia kwa karibu sana suala hili na hasa kipindi kile alichoanguka na kuugua ghafla bungeni, wengi wanaamini pale kulikuwa na 'mkono wa mtu' kimsingi Dk Mwakyembe amekuwa akipewa ulinzi usio wa kawaida kwa wadhifa wake wa Ubunge na wapiga kura wake.

Kama nilivyosema JK alipaswa kushirikiana na watu wa Mkoa wa Mbeya ikiwemo kufanya ziara za mara kwa mara. Kama anaweza kwenda Mwanza kila mwezi anashindwa nini kwenda Mbeya kila baada ya miezi sita? Yawezekana ziara ya Lowassa iliwashitua sana wanamtandao kwani tunaambiwa hakupokelewa vizuri pamoja na CCM 'kuandaa mapokezi mazito'

BADO NAAMINI JK ANAPASWA KWENDA MBEYA NA LABDA KUUNGAMA HADAHARANI KWAMBA AMEKUWA HAUTENDEI HAKI MKOA HUO VINGINEVYO LABDA KIMAHESABU MKOA HUO SI TISHIO KWA UCHAGUZI WA 2010.

Mkuu,

Wewe huijui Mbeya na afadhali ukae kimya tu. Haya mambo ya kusikia vijiweni na kujifanya ndio msimamo wa mkoa ni ujinga mtupu.

Kama unashindwa hata kujua jina la huyo mkuu wa mkoa, unataka tuamini hayo maneno yako mengine?

JK hajaenda mikoa mitano mpaka sasa, je mbona hiyo mingine hamuisemi?

Hakuna ugomvi kati ya JK na prof. Mwandosya. Mwang'onda aligombea sawa tu na mwananchi mwingine anavyoweza kugombea. Aliungwa mkono na baadhi ya watu wa mtandao lakini hiyo haina maana alitumwa na JK.

Prof. Alishinda kwa kura nyingi kwasababu Mbeya tunajua nani anatufaa.

Hivi hamna mkoa mwingine wa kuongelea na kila siku ni kurudia Mbeya tu?

Ugomvi wa Mwakyembe na Mwakipesile hauna tofauti na ugomvi wa wanasiasa wa wilaya na mikoa mingine. Shauri ya ujinga na umaskini wote wanawatumia baadhi ya vijana kuendeleza chuki zao kwa cost ya wilaya. JK anaingizwa tu ili kusaidia hayo mapigano yao ambayo hayana faida yoyote kwa Kyela.
 
Kinachoshangaza ni kwamba JK anaingizwa au anasingiziwa katika mambo mengi ya kisiasa Mbeya na kungine mbona hakatai au kukemea??
 
Kinachoshangaza ni kwamba JK anaingizwa au anasingiziwa katika mambo mengi ya kisiasa Mbeya na kungine mbona hakatai au kukemea??

Mwanasiasa ukianza kujiingiza kwenye kukanusha kila umbeya jua utakuwa bogged down humo mpaka ushindwe pa kutokea.

Prof. Mwandosya na viongozi wengine wameshakanusha. JK mwenyewe alikanusha mwaka 2005 wakati wa uchaguzi na akawaomba Mbeya wampatie hao maprofesa wawili, na kweli kawapa kazi tena za maana.

Suala la Mwang'onda kupewa ubunge wa kuteuliwa lina uhusiano zaidi na mchango wa babake katika ushindi wa JK kuliko siasa za Mbeya.

Mimi nafikiri tuchape kazi na kuleta maendeleo kwenye mkoa badala ya kila siku kuongelea ugomvi ambao haupo. Waheshimiwa wote hawa wana wajibu wa ku deliver na hicho ndicho watakachoulizwa mwaka 2010. Kyela na Rungwe hakuna vurugu yoyote, kama kuna mbunge anashindwa ku deliver ni kwasababu hana uwezo na wala sio vinginevyo.

Dr. Mwakyembe na Mwakipesile ni wana Kyela kama tulivyo wengine. Tunaweza kuwa na maugomvi yetu lakini naamini kila mtu anaitakia Kyela mema, hivyo tofauti zetu za kisiasa inabidi zisaidie kuleta challenges ambazo zinasukuma maendeleo na wala sio kukwamisha.
 
Mkuu,

Wewe huijui Mbeya na afadhali ukae kimya tu. Haya mambo ya kusikia vijiweni na kujifanya ndio msimamo wa mkoa ni ujinga mtupu.

Kama unashindwa hata kujua jina la huyo mkuu wa mkoa, unataka tuamini hayo maneno yako mengine?

JK hajaenda mikoa mitano mpaka sasa, je mbona hiyo mingine hamuisemi?

Hakuna ugomvi kati ya JK na prof. Mwandosya. Mwang'onda aligombea sawa tu na mwananchi mwingine anavyoweza kugombea. Aliungwa mkono na baadhi ya watu wa mtandao lakini hiyo haina maana alitumwa na JK.

Prof. Alishinda kwa kura nyingi kwasababu Mbeya tunajua nani anatufaa.

Hivi hamna mkoa mwingine wa kuongelea na kila siku ni kurudia Mbeya tu?

Ugomvi wa Mwakyembe na Mwakipesile hauna tofauti na ugomvi wa wanasiasa wa wilaya na mikoa mingine. Shauri ya ujinga na umaskini wote wanawatumia baadhi ya vijana kuendeleza chuki zao kwa cost ya wilaya. JK anaingizwa tu ili kusaidia hayo mapigano yao ambayo hayana faida yoyote kwa Kyela.

Mtanzani,

Kinachonishangaza kabisa ni namna wewe usivyopenda watu wajadili hali ya kisiasa ya Mbeya. Wewe unalazimisha watu wajadili Mikoa mingine ambayo JK hajafika. Sijajua lengo lako ni nini kwa kutafuta hiyo 'balance' lakini ninachoamini mtu hawezi kujadili kitu ambacho hakijui.

Wewe ndiye hujui chochote kuhusu Mbeya ila kwa sababu ni kwenu unaona aibu watu wakieleza UOZO na UJINGA wenu. Nataka kukwambia matatizo yapo UKUBALI USIKUBALI, UPENDE USIPENDE. Ishu ya kukosea majina ya mwanzo haiondoi hoja ya msingi niliyokuwa naiongelea. Kumbuka wakati tunaandika humu JF tunakuwa tunaiba muda wa shughuli zingine za kutafuta MAISHA. Kwa hiyo habari niliyoiandika sikuwa nakopi mahali ilikuwa inatoka kichwani. Silazimiki kuyakariri majina yote ya Mwakipesile au Mwakyembe au Mwandosya.

Turudi kwenye hoja ya msingi.

Kwa taarifa yako wakati wa uchaguzi wa NEC Mkoa wa Mbeya, Profesa Mwandosya alimwandikia rasmi barua Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais JK akilalamika kuwa kuna mgombea anatumia jina lake kutafuta kura za MNEC Mkoa wa Mbeya. Sasa sijui wewe ambaye hufuatilii habari za kijiweni UNALIJUA HILO.

Kwa taarifa yako, Dk Harrison Mwakyembe wakati anarudi toka Dodoma baada ya Kamati ile ya Richmond, Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya kilimwandikia barua rasmi kumzuia asipokelewe kishujaa na wapiga kura wake. Pamoja na kuzuiliwa alipokelewa unajua kilichotokea baada ya hapo ni nini? Tuambie kama unajua kama hujui NYAMAZA milele.

Wiki mbili zilizopita Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Nawab Mulla aliongea na waandishi wa habari na kutangaza kuwa Vikao vya CCM Mkoa vimekaa na kumaliza tofauti zilizokuwepo baina ya wanasiasa WOTE ofkoz wa CCM wa Mbeya. Sasa sijui utasema na hizi ni za KIJIWENI! Kwa taarifa yako hicho KIKAO cha viongozi wa CCM, Mwandosya na Mwakyembe hawakuhudhuria. Sasa sijui kama unaona hapo kuna suluhu.

Mtanzania 'mwenzangu' siye wengine tunaandika haya si kwa sababu tunaichukia Mbeya ila tunaona UPEPO wa KISIASA Mbeya si mzuri na ushahidi ni hili la JK kuwa anaahirisha 'trip' za kwenda huko. Hiyo Mikoa mingine unayosema JK hajafika ni SAWA kabisa ila tofauti na Mbeya ni kwamba hajawahi kuahidi kwenda huko na kuahirisha mara kibao. UPO HAPO. Mbeya si SHWARI UKUBALI USIKUBALI. Tunayasema ya Mbeya kwa sababu tunayajua hatuyasemi ya Mikoa mingine kwa sababu HATUYAJUI na wewe kama unayajua ya Mikoa mingine ni ruksa kusema na kama hujui kama usivyojua ya Mbeya, USHAURI wa bure ni KUNAYAMAZA tu na sio kuja juu bila sababu ya msingi. MUUNGWANA ni VITENDO kaka yangu.
 
Mwanasiasa ukianza kujiingiza kwenye kukanusha kila umbeya jua utakuwa bogged down humo mpaka ushindwe pa kutokea.

Prof. Mwandosya na viongozi wengine wameshakanusha. JK mwenyewe alikanusha mwaka 2005 wakati wa uchaguzi na akawaomba Mbeya wampatie hao maprofesa wawili, na kweli kawapa kazi tena za maana.

Suala la Mwang'onda kupewa ubunge wa kuteuliwa lina uhusiano zaidi na mchango wa babake katika ushindi wa JK kuliko siasa za Mbeya.

Mimi nafikiri tuchape kazi na kuleta maendeleo kwenye mkoa badala ya kila siku kuongelea ugomvi ambao haupo. Waheshimiwa wote hawa wana wajibu wa ku deliver na hicho ndicho watakachoulizwa mwaka 2010. Kyela na Rungwe hakuna vurugu yoyote, kama kuna mbunge anashindwa ku deliver ni kwasababu hana uwezo na wala sio vinginevyo.

Dr. Mwakyembe na Mwakipesile ni wana Kyela kama tulivyo wengine. Tunaweza kuwa na maugomvi yetu lakini naamini kila mtu anaitakia Kyela mema, hivyo tofauti zetu za kisiasa inabidi zisaidie kuleta challenges ambazo zinasukuma maendeleo na wala sio kukwamisha.

Hamkani si SHWARI ndugu yangu. Watu wanataka hayo maendeleo ILA wanasiasa wetu ndio KIKWAZO. Hivi ni kwa nini Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Songwe ulisimama mara tu Serikali ya JK ilipoingia madarakani? Fuatilia vizuri huo Uwanja ulikuja vipi Mbeya. Fedha za kujenga huo Uwanja zilipaswa kupanua Uwanja wa Mwanza, Sumaye akang'ang'ania fedha ziende kupanua Uwanja wa Arusha. Kilichowashangaza wengi unapanua Uwanja wa Arusha wakati tayari Arusha ina Uwanja ule wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Mwandosya akiwa Waziri mwenye dhamana alitumia kete hiyo kuhamisha fedha zile kujenga Uwanja wa Songwe, Mbeya. Serikali ya JK ilipoingia madarakani iliacha kujenga ule Uwanja kwa kuogopa kumpa 'ujiko' MJM. Sasa huoni maugomvi hayo ya wanasiasa yanavyotuumiza sisi wananchi.

Narudia tena kusema HAMKANI SI SHWARI MBEYA!
 
Mtanzani,

Kinachonishangaza kabisa ni namna wewe usivyopenda watu wajadili hali ya kisiasa ya Mbeya. Wewe unalazimisha watu wajadili Mikoa mingine ambayo JK hajafika. Sijajua lengo lako ni nini kwa kutafuta hiyo 'balance' lakini ninachoamini mtu hawezi kujadili kitu ambacho hakijui.

Wewe ndiye hujui chochote kuhusu Mbeya ila kwa sababu ni kwenu unaona aibu watu wakieleza UOZO na UJINGA wenu. Nataka kukwambia matatizo yapo UKUBALI USIKUBALI, UPENDE USIPENDE. Ishu ya kukosea majina ya mwanzo haiondoi hoja ya msingi niliyokuwa naiongelea. Kumbuka wakati tunaandika humu JF tunakuwa tunaiba muda wa shughuli zingine za kutafuta MAISHA. Kwa hiyo habari niliyoiandika sikuwa nakopi mahali ilikuwa inatoka kichwani. Silazimiki kuyakariri majina yote ya Mwakipesile au Mwakyembe au Mwandosya.

Turudi kwenye hoja ya msingi.

Kwa taarifa yako wakati wa uchaguzi wa NEC Mkoa wa Mbeya, Profesa Mwandosya alimwandikia rasmi barua Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais JK akilalamika kuwa kuna mgombea anatumia jina lake kutafuta kura za MNEC Mkoa wa Mbeya. Sasa sijui wewe ambaye hufuatilii habari za kijiweni UNALIJUA HILO.

Kwa taarifa yako, Dk Harrison Mwakyembe wakati anarudi toka Dodoma baada ya Kamati ile ya Richmond, Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya kilimwandikia barua rasmi kumzuia asipokelewe kishujaa na wapiga kura wake. Pamoja na kuzuiliwa alipokelewa unajua kilichotokea baada ya hapo ni nini? Tuambie kama unajua kama hujui NYAMAZA milele.

Wiki mbili zilizopita Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Nawab Mulla aliongea na waandishi wa habari na kutangaza kuwa Vikao vya CCM Mkoa vimekaa na kumaliza tofauti zilizokuwepo baina ya wanasiasa WOTE ofkoz wa CCM wa Mbeya. Sasa sijui utasema na hizi ni za KIJIWENI! Kwa taarifa yako hicho KIKAO cha viongozi wa CCM, Mwandosya na Mwakyembe hawakuhudhuria. Sasa sijui kama unaona hapo kuna suluhu.

Mtanzania 'mwenzangu' siye wengine tunaandika haya si kwa sababu tunaichukia Mbeya ila tunaona UPEPO wa KISIASA Mbeya si mzuri na ushahidi ni hili la JK kuwa anaahirisha 'trip' za kwenda huko. Hiyo Mikoa mingine unayosema JK hajafika ni SAWA kabisa ila tofauti na Mbeya ni kwamba hajawahi kuahidi kwenda huko na kuahirisha mara kibao. UPO HAPO. Mbeya si SHWARI UKUBALI USIKUBALI. Tunayasema ya Mbeya kwa sababu tunayajua hatuyasemi ya Mikoa mingine kwa sababu HATUYAJUI na wewe kama unayajua ya Mikoa mingine ni ruksa kusema na kama hujui kama usivyojua ya Mbeya, USHAURI wa bure ni KUNAYAMAZA tu na sio kuja juu bila sababu ya msingi. MUUNGWANA ni VITENDO kaka yangu.

Gottee,

Najua yote uliyoandika na ni mambo yale yale mnayoyarudia kila siku.

Pili sijasema mujadili hiyo mikoa mingine, ninachosema kama JK hajaenda mikoa mitano, kwanini mutumie hiyo sababu kama ishara ya kwamba anaichukia Mbeya au Mbeya inamchukia JK?

Mnakuza mno migogoro ya Mwakyembe na Mwakipesile ili ionekane JK anahusika. Migogoro ya kisiasa ya Mwang'onda na Prof. eti JK anahusika.

Hizo barua kuandikwa kuna jipya gani? Kila mwaka kuna wanasiasa wanaandika barua kulalamikia wanasiasa wenzao. Mbona akina Gama waliandika barua kama hizo wakati wanagombea na Nchimbi. Rwegasira alishaandika barua kama hizo kwa Mkapa wakati anagombea na Kamala (Kamala akidai katumwa na Mkapa), hizo ni siasa.


Acheni Mbeya washughulikie maendeleo, kama ni siasa basi 2010 ipo mtapiga siasa mtakavyo.

Mimi nawajua kwa karibu sana wahusika wanaotajwa. Ukiacha vijembe vya kisiasa, hakuna mgogoro wowote. Kwa mfano baadhi walitaka Dr. Mwakyembe asipokelewe lakini wengine wakataka apokelewe, na waliotaka apokelewe walikuwa wengi na wakashinda, na wote ni CCM hiyo hiyo, sasa hapo kweli ni mgogoro? Hata huyo mkuu wa wilaya ambaye mnasema aliongoza hiyo njama, alikuwepo kwenye sherehe ya kumpokea Dr.

Hata uchaguzi wa mwenyekiti wa CCM, prof. alimuunga mkono huyo Mullah, japo sio watu wa upande mmoja kisiasa.

Hayo ya uwanja ni matokeo ya mipango mibovu ya serikali ambayo inategemea nani ni waziri. Mawaziri wanatumia hizo nafasi zao kupeleka baadhi ya miradi ya maendeleo kwao. Wakipoteza uwaziri, akija mwingine naye anahamishia kwingine. Ndiyo TZ yetu hiyo na imetokea mara nyingi tu na wala sio Mbeya peke yake. Si ajabu hata ilipotakiwa kuwa Mwanza, huenda waziri alikuwa anatoka huko. Kuna mifano mingi sana juu ya miradi ya maendeleo kufutwa baada ya waziri mhsuika kupoteza kazi au kuhamishwa.

Sisemi kwamba kuna maelewano 100% kati ya wanasiasa wa Mbeya, HAPANA, kuna mikwaruzano mingi tu ya kisiasa lakini haijafikia hiyo level ambayo watu mnataka tuamini.

Madhara ya haya maneno mnayoyasema ni makubwa sana kwa watu wa chini, wanashinda kwenye vigenge wakiamini hayo, wanashindwa kujituma kwenye maendeleo kwasababu eti itamsaidia mbunge huyu au yule. Wakati wanadumaa, vigogo hao wao wanaalikana kwenye sherehe na mambo mengine.
 
Mkuu,

Wewe huijui Mbeya na afadhali ukae kimya tu. Haya mambo ya kusikia vijiweni na kujifanya ndio msimamo wa mkoa ni ujinga mtupu.

Kama unashindwa hata kujua jina la huyo mkuu wa mkoa, unataka tuamini hayo maneno yako mengine?

JK hajaenda mikoa mitano mpaka sasa, je mbona hiyo mingine hamuisemi?

Hakuna ugomvi kati ya JK na prof. Mwandosya. Mwang'onda aligombea sawa tu na mwananchi mwingine anavyoweza kugombea. Aliungwa mkono na baadhi ya watu wa mtandao lakini hiyo haina maana alitumwa na JK.

Prof. Alishinda kwa kura nyingi kwasababu Mbeya tunajua nani anatufaa.Hivi hamna mkoa mwingine wa kuongelea na kila siku ni kurudia Mbeya tu?

Ugomvi wa Mwakyembe na Mwakipesile hauna tofauti na ugomvi wa wanasiasa wa wilaya na mikoa mingine. Shauri ya ujinga na umaskini wote wanawatumia baadhi ya vijana kuendeleza chuki zao kwa cost ya wilaya. JK anaingizwa tu ili kusaidia hayo mapigano yao ambayo hayana faida yoyote kwa Kyela.


Mkuu,

Mbona unajibu kwa jazba sana? Sasa wewe unataka tukuamini kwa lipi? Wewe umemkataza mwenzako ku-generalize mambo na kuchukulia ni msimamo wa mkoa mzima,mbona wewe umefanya hayo hayo? angalia hapo nilikobold,pia mkuu jaribu kumjibu mwenzako bila kutumia neno 'Ujinga'.
 
Hamkani si SHWARI ndugu yangu. Watu wanataka hayo maendeleo ILA wanasiasa wetu ndio KIKWAZO. Hivi ni kwa nini Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Songwe ulisimama mara tu Serikali ya JK ilipoingia madarakani? Fuatilia vizuri huo Uwanja ulikuja vipi Mbeya. Fedha za kujenga huo Uwanja zilipaswa kupanua Uwanja wa Mwanza, Sumaye akang'ang'ania fedha ziende kupanua Uwanja wa Arusha. Kilichowashangaza wengi unapanua Uwanja wa Arusha wakati tayari Arusha ina Uwanja ule wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Mwandosya akiwa Waziri mwenye dhamana alitumia kete hiyo kuhamisha fedha zile kujenga Uwanja wa Songwe, Mbeya. Serikali ya JK ilipoingia madarakani iliacha kujenga ule Uwanja kwa kuogopa kumpa 'ujiko' MJM. Sasa huoni maugomvi hayo ya wanasiasa yanavyotuumiza sisi wananchi.

Narudia tena kusema HAMKANI SI SHWARI MBEYA!

.....kwi kwi kwi kwi kwi....gottee acha kuwaonea wala ndizi wenzetu kwi kwi kwi kwi..............hapo juu kwenye rangi nyekundu HAKUNA HATA CHEMBE YA UKWELI.......kwi kwi kwi kwi......duuhh nilianza kufuatilia hoja zako nikifikiri ni makini........sasa nimekatishwa tamaa.......kweli kama asemavyo Mtanzania hizo ni data za vijiweni..............
 
Mkuu,

Mbona unajibu kwa jazba sana? Sasa wewe unataka tukuamini kwa lipi? Wewe umemkataza mwenzako ku-generalize mambo na kuchukulia ni msimamo wa mkoa mzima,mbona wewe umefanya hayo hayo? angalia hapo nilikobold,pia mkuu jaribu kumjibu mwenzako bila kutumia neno 'Ujinga'.

Hapo nime generalize vipi wakati nimekwambia prof. alishinda kwa kura nyingi? Nini kipimo cha mwanasiasa kuonekana anafaa kama sio kwa kupata kura nyingi?

Afterall hakuna hata sehemu nilipomlaumu mtu kwa kugeneralize mambo? Mimi nimeongelea
watu kutoa maneno ya kijiweni na kutaka kuyafanya ndio ukweli. Kama maana ya hiyo ni ku generalize, basi labda mimi sielewi maana ya hilo neno.

Kama ni jazba ni kweli maana nimechoshwa na hizi blah blah za kila siku na kuleta siasa kwenye kila kitu huku maendeleo yanarudi nyuma.
 
.....kwi kwi kwi kwi kwi....gottee acha kuwaonea wala ndizi wenzetu kwi kwi kwi kwi..............hapo juu kwenye rangi nyekundu HAKUNA HATA CHEMBE YA UKWELI.......kwi kwi kwi kwi......duuhh nilianza kufuatilia hoja zako nikifikiri ni makini........sasa nimekatishwa tamaa.......kweli kama asemavyo Mtanzania hizo ni data za vijiweni..............

Ogah,

Zinaweza kuwa ni DATA za kijiweni. Lakini na wewe huoni kama hujaitendea HAKI akili yako kwa kuhitimisha haraka haraka! Au ndio yale aliyoyasema BWM kwamba watanzania tu wavivu wa kufikiri (naongeza kufanya utafiti). Changamoto yangu kwako kabla hujahitimisha HITIMISHO lako fanya utafiti kwanza. Wako wengi tu wanajua hili ninalolisemea.

Tatizo kubwa la Serikali ya Awamu ya Tatu na hasa miaka ya mwisho lilikuwa ni Mawaziri kutunishiana MISULI hadharani na KIRANJA wao MKUU alikuwa akiuchuna muda wote. Chukulia na heka heka za kutafuta Urais. Ukienda pale Wizara ya Miundombinu nina uhakika wanajua na wanazo dokyumenti za Upanuzi wa Uwanja wa Mwanza. Watakuambia kwa nini ULISITISHWA! Kuhusu upanuzi wa Uwanja wa Arusha nina hakika hata Hansadi za bunge la JMT zinasema. Nikipata muda nitajaribu kufuatilia.

Profesa Mwandosya akiwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi na kwa kuona ule ujinga wa Sumaye kung'ang'ania fedha za upanuzi wa Uwanja wa Mwanza ziende zikapanue Uwanja wa Arusha alikuja na hoja nzuri tu, kwamba zile fedha ziiende zikajenge Uwanja wa Songwe ukizingatia Kanda ya Nyanda za Juu Kusini haikuwa na Uwanja wowote wa maana. Ujenzi wa Uwanja huu Mbeya ni muhimu sana kwa maendeleo ya Kanda yote na unaweza kuwanufaisha wakazi wa Mbeya kiuchumi ukizingatia kuwa Mbeya imepakana na nchi za Zambia na Malawi. Sina hakika ila nasikia Mwaka huu umetengewa fedha lakini pamoja na kutengewa DANADANA zinaweza zikaendelea vile vile. Tanzania kuna Siasa na Sihasa Mkuu.
 
Ogah,

Zinaweza kuwa ni DATA za kijiweni. Lakini na wewe huoni kama hujaitendea HAKI akili yako kwa kuhitimisha haraka haraka! Au ndio yale aliyoyasema BWM kwamba watanzania tu wavivu wa kufikiri (naongeza kufanya utafiti). Changamoto yangu kwako kabla hujahitimisha HITIMISHO lako fanya utafiti kwanza. Wako wengi tu wanajua hili ninalolisemea.

Tatizo kubwa la Serikali ya Awamu ya Tatu na hasa miaka ya mwisho lilikuwa ni Mawaziri kutunishiana MISULI hadharani na KIRANJA wao MKUU alikuwa akiuchuna muda wote. Chukulia na heka heka za kutafuta Urais. Ukienda pale Wizara ya Miundombinu nina uhakika wanajua na wanazo dokyumenti za Upanuzi wa Uwanja wa Mwanza. Watakuambia kwa nini ULISITISHWA! Kuhusu upanuzi wa Uwanja wa Arusha nina hakika hata Hansadi za bunge la JMT zinasema. Nikipata muda nitajaribu kufuatilia.

Profesa Mwandosya akiwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi na kwa kuona ule ujinga wa Sumaye kung'ang'ania fedha za upanuzi wa Uwanja wa Mwanza ziende zikapanue Uwanja wa Arusha alikuja na hoja nzuri tu, kwamba zile fedha ziiende zikajenge Uwanja wa Songwe ukizingatia Kanda ya Nyanda za Juu Kusini haikuwa na Uwanja wowote wa maana. Ujenzi wa Uwanja huu Mbeya ni muhimu sana kwa maendeleo ya Kanda yote na unaweza kuwanufaisha wakazi wa Mbeya kiuchumi ukizingatia kuwa Mbeya imepakana na nchi za Zambia na Malawi. Sina hakika ila nasikia Mwaka huu umetengewa fedha lakini pamoja na kutengewa DANADANA zinaweza zikaendelea vile vile. Tanzania kuna Siasa na Sihasa Mkuu.

Gottee,

Wanasema uwanja wa Songwe utakuwa wa SADC ingawaje nina wasiwasi je hizo ndege za SADC zitakuwa zinaenda kufanya nini Mbeya?

Inatakiwa upanuzi wa uwanja uendane na mambo mengine kama kukuza utalii na kukuza uzalishaji ili kuwe na mtililiko wa bidhaa na watu na hivyo kuhalalisha ujenzi wa uwanja.

Nyanda za juu Kusini kuna opportunities kibao ambazo lazima tuzitumie vizuri, bahati mbaya watu hawafaidiki, sawa tu na Magharibi au kusini. Kaskazini wana nafuu kuliko hizo nyanda zingine.
 
Hapo nime generalize vipi wakati nimekwambia prof. alishinda kwa kura nyingi? Nini kipimo cha mwanasiasa kuonekana anafaa kama sio kwa kupata kura nyingi?

Afterall hakuna hata sehemu nilipomlaumu mtu kwa kugeneralize mambo? Mimi nimeongelea
watu kutoa maneno ya kijiweni na kutaka kuyafanya ndio ukweli. Kama maana ya hiyo ni ku generalize, basi labda mimi sielewi maana ya hilo neno.

Kama ni jazba ni kweli maana nimechoshwa na hizi blah blah za kila siku na kuleta siasa kwenye kila kitu huku maendeleo yanarudi nyuma.

Wewe huwa nakupenda unamzungumzia Prof Mwandosya. Lakini unapokuja masuala mengine unaandika kwa roho ya korosho. Bado unadhani Mtikila ni shujaa na mwanasiasa bora zaidi?

Asha
 
Hapo nime generalize vipi wakati nimekwambia prof. alishinda kwa kura nyingi? Nini kipimo cha mwanasiasa kuonekana anafaa kama sio kwa kupata kura nyingi?

Afterall hakuna hata sehemu nilipomlaumu mtu kwa kugeneralize mambo? Mimi nimeongelea
watu kutoa maneno ya kijiweni na kutaka kuyafanya ndio ukweli. Kama maana ya hiyo ni ku generalize, basi labda mimi sielewi maana ya hilo neno.

Kama ni jazba ni kweli maana nimechoshwa na hizi blah blah za kila siku na kuleta siasa kwenye kila kitu huku maendeleo yanarudi nyuma.

Tatizo la 'Mtanzania' anatumia nguvu nyingi sana kuhakikisha kwamba anauvunja mjadala huu. Sasa ameibuka na hoja nyingine kwamba kuna akina Gama na wenzake mbona walishawahi kulalamika. Ninachoweza kumwambia ni kwamba kama anaona kuna umuhimu wa kuwajadili nao kwa nini asianzishe Thread zao.

Mtanzania kuacha kujadili matatizo ya kisiasa ya Mbeya sio kuisaidia Mbeya. Matatizo yapo na si madogo. Hata kama uko karibu na wanasiasa hao kiujomba, kiubabu, kiushemeji, kiuanasiasa haitusaidii sisi. Na sisi pia tunawafahamu na ndio maana tunawaongelea. Hatuwezi kuwajadili akina Gama hapa kwa sababu mjadala unahusu Mkoa wa Mbeya. Mwezi uliopita nilikuwa Mbeya. Nimekaa Mbeya Mjini wiki mbili, nimekaa Tukuyu siku tatu, nimekaa Suma siku mbili, nimekaa Mwakaleli siku tatu, nimekaa Kyela siku tano, nimekaa Ipinda siku tatu. Kwa sehemu zote nilizopita mtu ambaye wanamuona kuwa ni Rais wao ni Profesa Mwandosya na sio Jakaya Kikwete. Hapo ndipo tatizo linapoanzia. Kama wanambeya wanamuona Mwandosya yuko juu ya JK lazima ukubali kuwa Mbeya kuna tatizo. Tatizo hili linaweza kuwa linasababishwa na Wanambeya au Utawala wa JK. Sisi wafuatiliaji wa siasa za Tanzania tunasema lazima kuwepo na 'compromise' baina ya pande zote.

JK kuendelea kuahirisha safari zake za kwenda huko ni kuendelea kuzua mengi tu ambayo nina imani hayatamsaidia kisiasa.

Mtanzania mimi nakubaliana na wewe kuwa kuna Mikoa mingine JK hajatembelea ila nataka UNITHIBITISHIE ni mara ngapi wakuu wa mikoa hiyo wamekuwa wakitokea hadharani kueleza kuwa JK ameahirisha ziara zake kwa 'vijisababu' anavyotuambia Meshimiwa Mwakipesile?

Binafsi sijui JK ana ukaribu gani na MJM kisiasa kwa sasa ila nina uhakika Wanamtandao wa JK hawamtaki Mwandosya. Soma gazeti la Mwanahalisi la Wiki iliyopita ile Makala ya Saed Kubenea kuwa 'Makundi ya 2000 hayajafutwa'. Kubenea anamkariri Kingunge akitamka hadharani kwamba 'Mwandosya hafai' wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Rungwe. Kuwemo kwa Mwandosya kwenye serikali ya Kikwete haimaanishi kuwa hawana tofauti. Yawezekana yumo mle kwa sababu wanataka kuwa karibu naye kufuatilia nyendo zake za kila siku. Unakumbuka miezi michache nyuma Gazeti la Rai ambalo linamilikiwa na Rostam Aziz ambaye ni swahiba wa karibu sana na JK (Kwa maneno yake JK alishatamka hadharani) liliandika kuwa Mwandosya anatumia ziara za kiserikali kufanya kampeni za urais mwaka 2010. Sina hakika na maneno hayo ya Rai lakini siwezi kuyapuuzia pia kwa sababu huo ndio mchezo wa siasa. Lakini ninachotaka kukwambia HAMKANI si SI SHWARI kule Mbeya. Nawakilisha.
 
Gottee,

Wanasema uwanja wa Songwe utakuwa wa SADC ingawaje nina wasiwasi je hizo ndege za SADC zitakuwa zinaenda kufanya nini Mbeya?

Inatakiwa upanuzi wa uwanja uendane na mambo mengine kama kukuza utalii na kukuza uzalishaji ili kuwe na mtililiko wa bidhaa na watu na hivyo kuhalalisha ujenzi wa uwanja.

Nyanda za juu Kusini kuna opportunities kibao ambazo lazima tuzitumie vizuri, bahati mbaya watu hawafaidiki, sawa tu na Magharibi au kusini. Kaskazini wana nafuu kuliko hizo nyanda zingine.

Mtanzania,

Uwanja wa SADC!! Labda wamegundua Uranium! Enewei kuna Kitulo ambayo sasa ni Hifadhi rasmi ya Taifa. Kama ujuavyo huko kuna ndege wazuri, kuna maua mazuri na kuna wale Nyani ambao wanapatikana Tanzania tu. Hivyo yawezekana Uwanja huo ukaleta Watalii wengi pia.
 
Tatizo la 'Mtanzania' anatumia nguvu nyingi sana kuhakikisha kwamba anauvunja mjadala huu. Sasa ameibuka na hoja nyingine kwamba kuna akina Gama na wenzake mbona walishawahi kulalamika. Ninachoweza kumwambia ni kwamba kama anaona kuna umuhimu wa kuwajadili nao kwa nini asianzishe Thread zao.

Mtanzania kuacha kujadili matatizo ya kisiasa ya Mbeya sio kuisaidia Mbeya. Matatizo yapo na si madogo. Hata kama uko karibu na wanasiasa hao kiujomba, kiubabu, kiushemeji, kiuanasiasa haitusaidii sisi. Na sisi pia tunawafahamu na ndio maana tunawaongelea. Hatuwezi kuwajadili akina Gama hapa kwa sababu mjadala unahusu Mkoa wa Mbeya. Mwezi uliopita nilikuwa Mbeya. Nimekaa Mbeya Mjini wiki mbili, nimekaa Tukuyu siku tatu, nimekaa Suma siku mbili, nimekaa Mwakaleli siku tatu, nimekaa Kyela siku tano, nimekaa Ipinda siku tatu. Kwa sehemu zote nilizopita mtu ambaye wanamuona kuwa ni Rais wao ni Profesa Mwandosya na sio Jakaya Kikwete. Hapo ndipo tatizo linapoanzia. Kama wanambeya wanamuona Mwandosya yuko juu ya JK lazima ukubali kuwa Mbeya kuna tatizo. Tatizo hili linaweza kuwa linasababishwa na Wanambeya au Utawala wa JK. Sisi wafuatiliaji wa siasa za Tanzania tunasema lazima kuwepo na 'compromise' baina ya pande zote.

JK kuendelea kuahirisha safari zake za kwenda huko ni kuendelea kuzua mengi tu ambayo nina imani hayatamsaidia kisiasa.

Mtanzania mimi nakubaliana na wewe kuwa kuna Mikoa mingine JK hajatembelea ila nataka UNITHIBITISHIE ni mara ngapi wakuu wa mikoa hiyo wamekuwa wakitokea hadharani kueleza kuwa JK ameahirisha ziara zake kwa 'vijisababu' anavyotuambia Meshimiwa Mwakipesile?

Binafsi sijui JK ana ukaribu gani na MJM kisiasa kwa sasa ila nina uhakika Wanamtandao wa JK hawamtaki Mwandosya. Soma gazeti la Mwanahalisi la Wiki iliyopita ile Makala ya Saed Kubenea kuwa 'Makundi ya 2000 hayajafutwa'. Kubenea anamkariri Kingunge akitamka hadharani kwamba 'Mwandosya hafai' wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Rungwe. Kuwemo kwa Mwandosya kwenye serikali ya Kikwete haimaanishi kuwa hawana tofauti. Yawezekana yumo mle kwa sababu wanataka kuwa karibu naye kufuatilia nyendo zake za kila siku. Unakumbuka miezi michache nyuma Gazeti la Rai ambalo linamilikiwa na Rostam Aziz ambaye ni swahiba wa karibu sana na JK (Kwa maneno yake JK alishatamka hadharani) liliandika kuwa Mwandosya anatumia ziara za kiserikali kufanya kampeni za urais mwaka 2010. Sina hakika na maneno hayo ya Rai lakini siwezi kuyapuuzia pia kwa sababu huo ndio mchezo wa siasa. Lakini ninachotaka kukwambia HAMKANI si SI SHWARI kule Mbeya. Nawakilisha.

Samahani nilikuwa na maana "Makundi 2005 Hayajafutwa" kuweka rekodi vizuri.
 
.....kwi kwi kwi kwi kwi....gottee acha kuwaonea wala ndizi wenzetu kwi kwi kwi kwi..............hapo juu kwenye rangi nyekundu HAKUNA HATA CHEMBE YA UKWELI.......kwi kwi kwi kwi......duuhh nilianza kufuatilia hoja zako nikifikiri ni makini........sasa nimekatishwa tamaa.......kweli kama asemavyo Mtanzania hizo ni data za vijiweni..............

Sasa kama ni data za vijiweni kwanini mpaka leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Mbeya haujaisha kujengwa? Na tuliambiwa ungekamalika tangu 2006 kama sikosei...!!! Hivi ujenzi wake unaendelea? Au umesiamama? Maana yasije kugeuka magofu pale Songwe!

Nchi hii inakatisha tamaa sana!
 
Tatizo la 'Mtanzania' anatumia nguvu nyingi sana kuhakikisha kwamba anauvunja mjadala huu. Sasa ameibuka na hoja nyingine kwamba kuna akina Gama na wenzake mbona walishawahi kulalamika. Ninachoweza kumwambia ni kwamba kama anaona kuna umuhimu wa kuwajadili nao kwa nini asianzishe Thread zao.

Mtanzania kuacha kujadili matatizo ya kisiasa ya Mbeya sio kuisaidia Mbeya. Matatizo yapo na si madogo. Hata kama uko karibu na wanasiasa hao kiujomba, kiubabu, kiushemeji, kiuanasiasa haitusaidii sisi. Na sisi pia tunawafahamu na ndio maana tunawaongelea. Hatuwezi kuwajadili akina Gama hapa kwa sababu mjadala unahusu Mkoa wa Mbeya. Mwezi uliopita nilikuwa Mbeya. Nimekaa Mbeya Mjini wiki mbili, nimekaa Tukuyu siku tatu, nimekaa Suma siku mbili, nimekaa Mwakaleli siku tatu, nimekaa Kyela siku tano, nimekaa Ipinda siku tatu. Kwa sehemu zote nilizopita mtu ambaye wanamuona kuwa ni Rais wao ni Profesa Mwandosya na sio Jakaya Kikwete. Hapo ndipo tatizo linapoanzia. Kama wanambeya wanamuona Mwandosya yuko juu ya JK lazima ukubali kuwa Mbeya kuna tatizo. Tatizo hili linaweza kuwa linasababishwa na Wanambeya au Utawala wa JK. Sisi wafuatiliaji wa siasa za Tanzania tunasema lazima kuwepo na 'compromise' baina ya pande zote.

JK kuendelea kuahirisha safari zake za kwenda huko ni kuendelea kuzua mengi tu ambayo nina imani hayatamsaidia kisiasa.

Mtanzania mimi nakubaliana na wewe kuwa kuna Mikoa mingine JK hajatembelea ila nataka UNITHIBITISHIE ni mara ngapi wakuu wa mikoa hiyo wamekuwa wakitokea hadharani kueleza kuwa JK ameahirisha ziara zake kwa 'vijisababu' anavyotuambia Meshimiwa Mwakipesile?

Binafsi sijui JK ana ukaribu gani na MJM kisiasa kwa sasa ila nina uhakika Wanamtandao wa JK hawamtaki Mwandosya. Soma gazeti la Mwanahalisi la Wiki iliyopita ile Makala ya Saed Kubenea kuwa 'Makundi ya 2000 hayajafutwa'. Kubenea anamkariri Kingunge akitamka hadharani kwamba 'Mwandosya hafai' wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Rungwe. Kuwemo kwa Mwandosya kwenye serikali ya Kikwete haimaanishi kuwa hawana tofauti. Yawezekana yumo mle kwa sababu wanataka kuwa karibu naye kufuatilia nyendo zake za kila siku. Unakumbuka miezi michache nyuma Gazeti la Rai ambalo linamilikiwa na Rostam Aziz ambaye ni swahiba wa karibu sana na JK (Kwa maneno yake JK alishatamka hadharani) liliandika kuwa Mwandosya anatumia ziara za kiserikali kufanya kampeni za urais mwaka 2010. Sina hakika na maneno hayo ya Rai lakini siwezi kuyapuuzia pia kwa sababu huo ndio mchezo wa siasa. Lakini ninachotaka kukwambia HAMKANI si SI SHWARI kule Mbeya. Nawakilisha.

Gottee,
Nakuhakikishia kitu kimoja, sina nia ya kuzuia mijadala kuhusu matatizo mkoani Mbeya. Binafsi ni mwumini wa uhuru wa kujadili jambo lolote.

Ninachopinga mimi ni watu kuja na madai makubwa sana ambayo hayana ukweli. Inabidi tuwe responsible kidogo kwasababu haya mambo yote yanaikwamisha Mbeya. Kuna vijana kule kwasababu ya ujinga wao, wanaona kila kitu kilichoandikwa magazetini ni ukweli na wanaanza kuamini.

Hata nikiwa Kyela au Mbeya nawaambia hivyo hivyo kama nilivyoandika hapa, kwamba sio kweli. Ukiwauliza umesikia wapi, wanasema yaliandikwa gazetini.

Prof. Mwandosya na JK walikuwa makundi tofauti na sio marafiki wa karibu kwa miaka mingi, huo ni ukweli lakini je kunachuki kubwa kati yao kwasasa? Siamini hivyo na wala sijaona ushahidi huo.

Kuna watu kwenye kundi la JK wangependa kuendeleza huo mgogoro kama ambavyo wangependa kuendeleza mgogoro wa JK na Salim. What matters here ni msimamo wa JK na profesa mwenyewe. Pia kuna watu wa prof. ambao wangependa kuendeleza mgogoro na JK.

Kuna watu wanafikiri hata kuanguka kwa Lowassa ni njama za prof. eti Dr. Mwakyembe alitumiwa na prof. kumlima JK na kundi lake. Jamani, ina maana wajumbe wale wote wa ile kamati, wataburuzwa na Mwakyembe kwa faida ya prof.?

Kuhusu vijana kumwita Prof. rais wao, kuna tofauti gani na vijana wa CHADEMA kumwita Mbowe rais? Kuna tofauti gani na TLP au NCCR huko nyuma kumwita Mrema rais? Ni kundi dogo la vijana ndio wanaendeleza hayo mambo kwenye vijiwe vyao badala ya kwenda kwenye uzalishaji mali.

Kule Mbeya kuna watu wamefanya ni career kupeleka majungu kwa Mwakipesile au Mwakyembe. Na kukiwa na wanasiasa njiwa, ni rahisi mno kukubaliana na watu kama hao ambao kwa kweli ni waganga njaa.

Nikupe mchapo wangu mmoja wa kweli. Nikiwa likizo Kyela, wakati napita ile barabara ya Kyela, nilimwona diwani mmoja ambaye mimi nilisoma naye msingi, alikuwa pamoja na diwani mwenzake ambaye nilikuwa simfahamu kabla ya hapo. Nikaenda kuwasalimia, tukaanza michapo mbalimbali, baadaye wakaniomba kama kuna mtu namjua Dar awasaidie, wametumwa na wilaya kwenda kutafuta wanunua Kokoa wameuza kiasi gani nje ili wajue kama Halmashauri ya Kyela imelipwa ipasavyo. Mimi nikatafuta contacts zangu na kuwaunganisha na mhusika.

Baada ya siku kama tatu, jamaa yangu mwingine ambaye ni rafiki yake Dr. Mwakyembe akaanza kuniuliza juu ya mimi kuongea na hao madiwani. Akasema kuna wapambe wa Dr wameniona na habari imeenda kwake. Nikacheka tu, hata Dr. naamini aliwadharau tu. Wengine tumekuwa tukiambiwa tunataka kugombea toke 95, 2000, 2005 na sitashangaa tukitajwa 2010. Kumbe hao madiwani wawili ni watu wa mkuu wa mkoa, mimi hata sikujua ingawaje huyu niliyesoma naye niliwahi kusikia alimwunga mkono Mwakipesile mwaka 2005.

Mimi wanaoniuliza nawaambia wazi, siku ikifika nitasema mwenyewe, wala sitasingizia nimefuatwa na wazee au nini. Nikiamua kuingia kwenye siasa kila mtu atajua wala hakuna haja ya kuficha. Kwasasa muhimu ni kwamba tuna viongozi wacha watimize majukumu yao bila bugudha za majungu.

Huko mikoani kuna madudu mengi sana, ndio maana wakati mwingine mimi huwa nachukia juu ya jambo hili. Majungu ya kisiasa na ushirikina yanaua zile wilaya zetu.
 
Back
Top Bottom