Kikulacho ki nguoni mwako

Lekanjobe Kubinika

JF-Expert Member
Dec 6, 2006
3,020
576
TRUE STORY in the late eighties, DSM:
Kuna huyu bwana mwingine daktari ambaye alikwenda kusoma Urusi digree ya pili. Alikuwa anakaa Flat moja na daktari mwingine milango ikitizamana. Wake zao wote walikuwa wauguzi hospitali moja lakini vitengo tofauti. Hawa mabwana walikuwa ni marafiki wakubwa sana.

Wa kusoma alimwomba mwenzake kwamba kwa kuwa mkewe hajui kuendesha gari, anamwomba awe anamsaidia pale uhitaji ukijitokeza. Akaitikiwa vizuri sana. Safari ilipotimia, huku nyuma jirani alijituma sana kumsaidia shemeji yake kwa kumpeleka Karakoo na sehemu nyingine kila ilipohitajika. Pia alilazimika kutembelea ndani ya jirani yake ili kujua usalama na kujionea kama kuna mambo mengine shemejiye angeogopa kuyasema ili ajionee mwenyewe na atafute namna ya kusaidia.

Safari na gari zikaongezeka sana na wakajikuta wako karibu zaidi. Haikuchukuwa muda mrefu wakajikuta wanaanza kutengeneza mikasi. Kwa kuwa wote ni watu wazima walijitahidi kuyafanya in low profile in public. Lakini si unajua kikohozi kinavyosumbua mapaka ukohoe? Bila kutegemea wakanogewa na ikawa mara mbili, mara tatu , mara nne kila siku. Mama mwenye hati miliki ya bwana yule alilazimika kukaa na njaa mfululizo kama vile mwenza kasafiri, wakati mwenye mume aliyesafiri ndio aliona bukheri wa afya kuliko mume akiwapo.

Mke wa huyu daktari mtoa msaada alisikia pia kwamba fimbo yake inatumiwa na jirani yake, tena basi wamama hawa walisoma pamoja chuoni na wakajikuta wanafahamiana vizuri. Ujirani wa makazi yao ukawafanya wawe marafiki zaidi. mama akamuuliza mumewe kama kweli anayoyasikia mitaani ni kweli. Mumewe alipobanwa alilazimika kukubali. Mkewe akamwambia aachane na mambo hayo haraka sana japo amemsamehe. Yule bwana akasema akijitetea, kwamba ataacha lakini asingeweza kuacha mara moja kwa sababu kufanya hivyo kungemuumiza sana mwanamke jirani, Akaahidi kuachia polepole mpaka jamaa akirudi ndipo asitishe kabisa. Ilikuwa pata shika usemi huo kukubalika.

Wapambe walianza kumtonya jamaa akiwa bado masomoni, hasa Matron wao wa harusi. Aliporudi jamaa kutoka Urusi, aliwajia juu wapambe akiwasakama kwamba hawaamini maneno yao na wanaihatarisha ndoa yake. Akafanya mpango kumbamisha kituo cha kazi mkewe akafanye kazi mbali na wabaya wake.

Je, kama ingekufika wewe ungefanyaje? Nimeepusha undani watu waliopita maeneo yale lazima watakumbuka songombingo hilo, ni pamoja na kutunza heshima ya JF lakini kutumia matukio hayo kujifunza kitu katika maisha.

USIMWAMINI MTU!!!!!
 
Duh hii hatari sana ...kwa hiyo jamaa hakuamini kama wife wake alikuwa anamegwa ?
 
Wa kusoma alimwomba mwenzake kwamba kwa kuwa mkewe hajui kuendesha gari, anamwomba awe anamsaidia pale uhitaji ukijitokeza. Akaitikiwa vizuri sana.


Mumewe alipobanwa alilazimika kukubali. Mkewe akamwambia aachane na mambo hayo haraka sana japo amemsamehe. Yule bwana akasema akijitetea, kwamba ataacha lakini asingeweza kuacha mara moja kwa sababu kufanya hivyo kungemuumiza sana mwanamke jirani, Akaahidi kuachia polepole mpaka jamaa akirudi ndipo asitishe kabisa. Ilikuwa pata shika usemi huo kukubalika
.

Kwenye bold: Huyu daktari aliyeenda masomoni atakuwa ana upungufu wa akili. Mbuzi umuachie fisi mwenye njaa kali?
Kwenye red: Daktari aliyechiwa mke naye taahira: Unawezaje kumuambia mkeo eti utaacha taratibu kumega mke wa mtu, tena mke wa rafiki yako?

Nashindwa kujibu swali lako kuwa kama ingekuwa mimi ningefanyaje kwakuwa hujawa specific kuwa kama ningekuwa nani kati ya hao wanne.
 
hehhehhe umeniachia kali na 'mama mwenye hati miliki' lol

anyway mimi kwa upande wangu nakubaliana na wewe............usimuamini mtu. kaka yako mzazi usimuamini na mkeo kiasi hicho achilia jirani!

akiwemo mwanamme na mwanamke kwa ukaribu lazima shetani atapita tu
 
hawa madoctor wote na wake zao naona wana akili za kiaina hivi maana mi si imagn itakuwaje mr anaamua kukiri anatoka nje na ataacha taratibu? how come?
 
hehhehhe umeniachia kali na 'mama mwenye hati miliki' lol

anyway mimi kwa upande wangu nakubaliana na wewe............usimuamini mtu. kaka yako mzazi usimuamini na mkeo kiasi hicho achilia jirani!

akiwemo mwanamme na mwanamke kwa ukaribu lazima shetani atapita tu

Samahani naomba kufahamishwa, kaka mzazi ndio nani?
 
Duh hii hatari sana ...kwa hiyo jamaa hakuamini kama wife wake alikuwa anamegwa ?
Si unajua kipenda roho hula nyama mbichi, na mapenzi hupofusha macho. Mapenzi ni dumuzi wa akili. Kuna kumuamini mwenzio kupita kiasi hata usisikie unachoambiwa tofauti. Huyu daktari alikuwa mbogo kwa mtu yeyote anayeonekana kutaka kuongelea hayo, watu wakaamua kunyamaza tu. Namuona mama huyo hata leo hajastaafu bado, tena sasa ana cheo kikubwa sana kwenye system za uuguzi hospitalini hapo. Alirudishwa baadaye kutoka alikohamishiwa. Yote ni maisha. Tatizo ni je, wameacha kamchezo kale?
 
Mkuu... dakitari aliyekua urusi alichagua lililo bora sana!!! hakutaka mtu kuingilia ndoa yao, na ameonyesha imani kwa mkewe, time will tell kama alikua right or wrong

Ila naskia kusisimka maana siamini kwa namna yoyote ile [no disrespect to any woman in this world] mtu kukabidhi familia yake kwa mwanaume mwingine, its like you are hadning over your responsibilities to your deputy. before leaving a family kwa long term lazima mama awezeshwe kuishi mwenyewe with minimum dependency kwa wengine hata kama ni ndugu
 
mtu kukabidhi familia yake kwa mwanaume mwingine, its like you are hadning over your responsibilities to your deputy. before leaving a family kwa long term lazima mama awezeshwe kuishi mwenyewe with minimum dependency kwa wengine hata kama ni ndugu

Ni kweli De Novo; vinginevyo utawataka ubaya watu bure ni heri ukamwacha yeyey mwenyewe ili kama kuanzisha aanzishe kwa matakwa yake moja kwa moja lakini ukishawaweka akribu yakitokea haya utajilaumu kwa kuweka misingi ya hilo kutokea!
 
Ni kweli De Novo; vinginevyo utawataka ubaya watu bure ni heri ukamwacha yeyey mwenyewe ili kama kuanzisha aanzishe kwa matakwa yake moja kwa moja lakini ukishawaweka akribu yakitokea haya utajilaumu kwa kuweka misingi ya hilo kutokea!
kamanda tuko pamoja.. we hebu fikiria unakabidhi kabisa maa kwa mshkaji wakati unajua physiology ya binadamu na mahitaji mengine ya jamii. bora ungeacha tu
 
:closed_2:
TRUE STORY in the late eighties, DSM:
Kuna huyu bwana mwingine daktari ambaye alikwenda kusoma Urusi digree ya pili. Alikuwa anakaa Flat moja na daktari mwingine milango ikitizamana. Wake zao wote walikuwa wauguzi hospitali moja lakini vitengo tofauti. Hawa mabwana walikuwa ni marafiki wakubwa sana.

Wa kusoma alimwomba mwenzake kwamba kwa kuwa mkewe hajui kuendesha gari, anamwomba awe anamsaidia pale uhitaji ukijitokeza. Akaitikiwa vizuri sana. Safari ilipotimia, huku nyuma jirani alijituma sana kumsaidia shemeji yake kwa kumpeleka Karakoo na sehemu nyingine kila ilipohitajika. Pia alilazimika kutembelea ndani ya jirani yake ili kujua usalama na kujionea kama kuna mambo mengine shemejiye angeogopa kuyasema ili ajionee mwenyewe na atafute namna ya kusaidia.

Safari na gari zikaongezeka sana na wakajikuta wako karibu zaidi. Haikuchukuwa muda mrefu wakajikuta wanaanza kutengeneza mikasi. Kwa kuwa wote ni watu wazima walijitahidi kuyafanya in low profile in public. Lakini si unajua kikohozi kinavyosumbua mapaka ukohoe? Bila kutegemea wakanogewa na ikawa mara mbili, mara tatu , mara nne kila siku. Mama mwenye hati miliki ya bwana yule alilazimika kukaa na njaa mfululizo kama vile mwenza kasafiri, wakati mwenye mume aliyesafiri ndio aliona bukheri wa afya kuliko mume akiwapo.

Mke wa huyu daktari mtoa msaada alisikia pia kwamba fimbo yake inatumiwa na jirani yake, tena basi wamama hawa walisoma pamoja chuoni na wakajikuta wanafahamiana vizuri. Ujirani wa makazi yao ukawafanya wawe marafiki zaidi. mama akamuuliza mumewe kama kweli anayoyasikia mitaani ni kweli. Mumewe alipobanwa alilazimika kukubali. Mkewe akamwambia aachane na mambo hayo haraka sana japo amemsamehe. Yule bwana akasema akijitetea, kwamba ataacha lakini asingeweza kuacha mara moja kwa sababu kufanya hivyo kungemuumiza sana mwanamke jirani, Akaahidi kuachia polepole mpaka jamaa akirudi ndipo asitishe kabisa. Ilikuwa pata shika usemi huo kukubalika.

Wapambe walianza kumtonya jamaa akiwa bado masomoni, hasa Matron wao wa harusi. Aliporudi jamaa kutoka Urusi, aliwajia juu wapambe akiwasakama kwamba hawaamini maneno yao na wanaihatarisha ndoa yake. Akafanya mpango kumbamisha kituo cha kazi mkewe akafanye kazi mbali na wabaya wake.

Je, kama ingekufika wewe ungefanyaje? Nimeepusha undani watu waliopita maeneo yale lazima watakumbuka songombingo hilo, ni pamoja na kutunza heshima ya JF lakini kutumia matukio hayo kujifunza kitu katika maisha.

USIMWAMINI MTU!!!!!

Hayo yanatokea sana kwenye jamii yetu, mke wa mtu sumu sana, ningekuwa mimi ningemkojolesha dagaa jamaa au ningemchukulia ile dawa ya kunatana ya mbeya waadhilike. Toooo bad.
 
:closed_2:

Hayo yanatokea sana kwenye jamii yetu, mke wa mtu sumu sana, ningekuwa mimi ningemkojolesha dagaa jamaa au ningemchukulia ile dawa ya kunatana ya mbeya waadhilike. Toooo bad.

Wewe unajiweka wapi kwenye hili anguko?
 
:closed_2:

Hayo yanatokea sana kwenye jamii yetu, mke wa mtu sumu sana, ningekuwa mimi ningemkojolesha dagaa jamaa au ningemchukulia ile dawa ya kunatana ya mbeya waadhilike. Toooo bad.
Hivi wakinatana si ndio wanazidi kufaidiana?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom