Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 576
TRUE STORY in the late eighties, DSM:
Kuna huyu bwana mwingine daktari ambaye alikwenda kusoma Urusi digree ya pili. Alikuwa anakaa Flat moja na daktari mwingine milango ikitizamana. Wake zao wote walikuwa wauguzi hospitali moja lakini vitengo tofauti. Hawa mabwana walikuwa ni marafiki wakubwa sana.
Wa kusoma alimwomba mwenzake kwamba kwa kuwa mkewe hajui kuendesha gari, anamwomba awe anamsaidia pale uhitaji ukijitokeza. Akaitikiwa vizuri sana. Safari ilipotimia, huku nyuma jirani alijituma sana kumsaidia shemeji yake kwa kumpeleka Karakoo na sehemu nyingine kila ilipohitajika. Pia alilazimika kutembelea ndani ya jirani yake ili kujua usalama na kujionea kama kuna mambo mengine shemejiye angeogopa kuyasema ili ajionee mwenyewe na atafute namna ya kusaidia.
Safari na gari zikaongezeka sana na wakajikuta wako karibu zaidi. Haikuchukuwa muda mrefu wakajikuta wanaanza kutengeneza mikasi. Kwa kuwa wote ni watu wazima walijitahidi kuyafanya in low profile in public. Lakini si unajua kikohozi kinavyosumbua mapaka ukohoe? Bila kutegemea wakanogewa na ikawa mara mbili, mara tatu , mara nne kila siku. Mama mwenye hati miliki ya bwana yule alilazimika kukaa na njaa mfululizo kama vile mwenza kasafiri, wakati mwenye mume aliyesafiri ndio aliona bukheri wa afya kuliko mume akiwapo.
Mke wa huyu daktari mtoa msaada alisikia pia kwamba fimbo yake inatumiwa na jirani yake, tena basi wamama hawa walisoma pamoja chuoni na wakajikuta wanafahamiana vizuri. Ujirani wa makazi yao ukawafanya wawe marafiki zaidi. mama akamuuliza mumewe kama kweli anayoyasikia mitaani ni kweli. Mumewe alipobanwa alilazimika kukubali. Mkewe akamwambia aachane na mambo hayo haraka sana japo amemsamehe. Yule bwana akasema akijitetea, kwamba ataacha lakini asingeweza kuacha mara moja kwa sababu kufanya hivyo kungemuumiza sana mwanamke jirani, Akaahidi kuachia polepole mpaka jamaa akirudi ndipo asitishe kabisa. Ilikuwa pata shika usemi huo kukubalika.
Wapambe walianza kumtonya jamaa akiwa bado masomoni, hasa Matron wao wa harusi. Aliporudi jamaa kutoka Urusi, aliwajia juu wapambe akiwasakama kwamba hawaamini maneno yao na wanaihatarisha ndoa yake. Akafanya mpango kumbamisha kituo cha kazi mkewe akafanye kazi mbali na wabaya wake.
Je, kama ingekufika wewe ungefanyaje? Nimeepusha undani watu waliopita maeneo yale lazima watakumbuka songombingo hilo, ni pamoja na kutunza heshima ya JF lakini kutumia matukio hayo kujifunza kitu katika maisha.
USIMWAMINI MTU!!!!!
Kuna huyu bwana mwingine daktari ambaye alikwenda kusoma Urusi digree ya pili. Alikuwa anakaa Flat moja na daktari mwingine milango ikitizamana. Wake zao wote walikuwa wauguzi hospitali moja lakini vitengo tofauti. Hawa mabwana walikuwa ni marafiki wakubwa sana.
Wa kusoma alimwomba mwenzake kwamba kwa kuwa mkewe hajui kuendesha gari, anamwomba awe anamsaidia pale uhitaji ukijitokeza. Akaitikiwa vizuri sana. Safari ilipotimia, huku nyuma jirani alijituma sana kumsaidia shemeji yake kwa kumpeleka Karakoo na sehemu nyingine kila ilipohitajika. Pia alilazimika kutembelea ndani ya jirani yake ili kujua usalama na kujionea kama kuna mambo mengine shemejiye angeogopa kuyasema ili ajionee mwenyewe na atafute namna ya kusaidia.
Safari na gari zikaongezeka sana na wakajikuta wako karibu zaidi. Haikuchukuwa muda mrefu wakajikuta wanaanza kutengeneza mikasi. Kwa kuwa wote ni watu wazima walijitahidi kuyafanya in low profile in public. Lakini si unajua kikohozi kinavyosumbua mapaka ukohoe? Bila kutegemea wakanogewa na ikawa mara mbili, mara tatu , mara nne kila siku. Mama mwenye hati miliki ya bwana yule alilazimika kukaa na njaa mfululizo kama vile mwenza kasafiri, wakati mwenye mume aliyesafiri ndio aliona bukheri wa afya kuliko mume akiwapo.
Mke wa huyu daktari mtoa msaada alisikia pia kwamba fimbo yake inatumiwa na jirani yake, tena basi wamama hawa walisoma pamoja chuoni na wakajikuta wanafahamiana vizuri. Ujirani wa makazi yao ukawafanya wawe marafiki zaidi. mama akamuuliza mumewe kama kweli anayoyasikia mitaani ni kweli. Mumewe alipobanwa alilazimika kukubali. Mkewe akamwambia aachane na mambo hayo haraka sana japo amemsamehe. Yule bwana akasema akijitetea, kwamba ataacha lakini asingeweza kuacha mara moja kwa sababu kufanya hivyo kungemuumiza sana mwanamke jirani, Akaahidi kuachia polepole mpaka jamaa akirudi ndipo asitishe kabisa. Ilikuwa pata shika usemi huo kukubalika.
Wapambe walianza kumtonya jamaa akiwa bado masomoni, hasa Matron wao wa harusi. Aliporudi jamaa kutoka Urusi, aliwajia juu wapambe akiwasakama kwamba hawaamini maneno yao na wanaihatarisha ndoa yake. Akafanya mpango kumbamisha kituo cha kazi mkewe akafanye kazi mbali na wabaya wake.
Je, kama ingekufika wewe ungefanyaje? Nimeepusha undani watu waliopita maeneo yale lazima watakumbuka songombingo hilo, ni pamoja na kutunza heshima ya JF lakini kutumia matukio hayo kujifunza kitu katika maisha.
USIMWAMINI MTU!!!!!