Mlachake
JF-Expert Member
- Oct 13, 2009
- 4,412
- 4,558
My Dear Great Thinkers,
Mwanzoni mwa mwaka huu Karibu vyombo vyote vya habari Tanzania vilijawa na Habari za Babu wa Loliondo na Kikombe Cha Tshs.500/= habari hizi zilienea sio Tanzania Tu bali hata Nchi za Jirani.
Kulizuka hali ya kutofautiana sana katika Jukwaa hili la Magreat Thinkers, Kwakua ni sehemu watu wanaangalia mambo kwa upana na kwa Jicho la tatu, Mmoja wa member aliyekuwa akimpinga huyu babu wa Loliondo kwa nguvu zake zote Bila woga ni Miss Judith, wakiwemo wengine wengi.
Wakati huo Taifa Lilikua kwenye Mjadal mkubwa kuhusu kulipa Deni la Dowans. Kutokana na Umaarufu wa habari za kikombe cha Babu, watanzania waliipotezea habari ya malipo ya deni la Dowans ambalo mpaka sasa wengi hatujui kulichoendelea, kama deni limeshalipwa au bado.
Viongozi wengi wa siasa ambao ni kioo cha Jamii ndio walikua mstari wa mbele katika safari ya Loliondo kukifuata kikombe cha babu. Hatuna haja ya kuwataja majini ila wapo wengi.
Wengine waliichukulia hii kama nafasi muhimu ya kurudisha fadhila kwa wapiga kura wao kwa kuwagharamia safari ya Loliondo wapate kikombe cha Babu.
Wananchi kutoka kila pembe ya Tanzania walifurika katika kijiji cha Samunge, Wengi wa hawa watanzania ni maskini, waliishia kukopa angalau wapate nauli ya kwenda Samunge.
Jambo la kushangaza ni jinsi hizi habari za Samunge zimepoteza Mvuto hivi sasa.
Kwa maoni yangu ningetegemea Kipindi hiki Ndio hizi habari zishike kasi kwa Ushuhuda wa waliopona haya magonjwa sugu yanayotibika kwa Kunywa kikombe yaani UKIMWI, KANSA NA KISUKARI.
Mimi Binafsi sijamshuhudia aliyepona magonjwa haya kwa Kunywa kikombe, ila nimesikia watu wanasema wana ndugu au Rafiki aliyepona.
Je? Kuna mwana Jamvi yeyote mwenye shuhuda ya Mgonjwa aliyepona haya magonjwa sugu? Ningependa uwe ushahidi wa kujionea mwenyewe sio wa kusikia kwa watu kama mimi nilivyosikia.
Hii pia itatusaidia kuujua ukweli kuhusu hii dawa ya Babu.
Mwanzoni mwa mwaka huu Karibu vyombo vyote vya habari Tanzania vilijawa na Habari za Babu wa Loliondo na Kikombe Cha Tshs.500/= habari hizi zilienea sio Tanzania Tu bali hata Nchi za Jirani.
Kulizuka hali ya kutofautiana sana katika Jukwaa hili la Magreat Thinkers, Kwakua ni sehemu watu wanaangalia mambo kwa upana na kwa Jicho la tatu, Mmoja wa member aliyekuwa akimpinga huyu babu wa Loliondo kwa nguvu zake zote Bila woga ni Miss Judith, wakiwemo wengine wengi.
Wakati huo Taifa Lilikua kwenye Mjadal mkubwa kuhusu kulipa Deni la Dowans. Kutokana na Umaarufu wa habari za kikombe cha Babu, watanzania waliipotezea habari ya malipo ya deni la Dowans ambalo mpaka sasa wengi hatujui kulichoendelea, kama deni limeshalipwa au bado.
Viongozi wengi wa siasa ambao ni kioo cha Jamii ndio walikua mstari wa mbele katika safari ya Loliondo kukifuata kikombe cha babu. Hatuna haja ya kuwataja majini ila wapo wengi.
Wengine waliichukulia hii kama nafasi muhimu ya kurudisha fadhila kwa wapiga kura wao kwa kuwagharamia safari ya Loliondo wapate kikombe cha Babu.
Wananchi kutoka kila pembe ya Tanzania walifurika katika kijiji cha Samunge, Wengi wa hawa watanzania ni maskini, waliishia kukopa angalau wapate nauli ya kwenda Samunge.
Jambo la kushangaza ni jinsi hizi habari za Samunge zimepoteza Mvuto hivi sasa.
Kwa maoni yangu ningetegemea Kipindi hiki Ndio hizi habari zishike kasi kwa Ushuhuda wa waliopona haya magonjwa sugu yanayotibika kwa Kunywa kikombe yaani UKIMWI, KANSA NA KISUKARI.
Mimi Binafsi sijamshuhudia aliyepona magonjwa haya kwa Kunywa kikombe, ila nimesikia watu wanasema wana ndugu au Rafiki aliyepona.
Je? Kuna mwana Jamvi yeyote mwenye shuhuda ya Mgonjwa aliyepona haya magonjwa sugu? Ningependa uwe ushahidi wa kujionea mwenyewe sio wa kusikia kwa watu kama mimi nilivyosikia.
Hii pia itatusaidia kuujua ukweli kuhusu hii dawa ya Babu.