Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,756
Nimepata tetesi kuwa mgonjwa moja kutoka Marekani ambaye hakupewa nafasi yoyote ya kuendelea kuishi na madaktari zaidi ya watatu Marekani, hivi sasa kapona baada ya kupata kikombe cha Babu Loliondo. Huyu mgonjwa ambaye alisafiri kutoka Marekani akiwa kwenye kinachoitwa "wheel-chair" kwa kuzidiwa sana, karudi mzimaa na anatembea bila msaada wowote ule na kumwacha mdomo wazi daktari wake aliyekuwa anamtibu. Baada ya kuchukua vipimo vyote kama kawaida daktari hakuwa na kusema isipokuwa maneno yanayofanana na haya, "whatever it is that you are doing to your body, keep on doing it"
Kama tetesi hizi zitakuwa ni kweli basi Mungu aliyemwongoza Babu wa Loliondo lazima avuliwe kofia kwani huyu atakuwa mgonjwa wa kwanza kutoka nje ya nchi kupimwa kabla na baada ya kunywa kikombe na kuthibitika amepona. Pia nasikia mpaka sasa ameweza kutoa ushuhuda kanisani na mbele ya ndugu na marafiki zake waliokuwa wakimhudumia na kumpa msaada kwa wakati wote aliokuwa akiumwa. Namwomba kama kuna mwenye taarifa zaidi kuhusu tukio hili aendelee kutufahamisha zaidi, nawakilisha. Mods iacheni hii thread mpaka ithibitike kwanza ndiyo ihamishwe kama itakuwa lazima.
Kofia avuliwe Mungu !
Kama tetesi hizi zitakuwa ni kweli basi Mungu aliyemwongoza Babu wa Loliondo lazima avuliwe kofia kwani huyu atakuwa mgonjwa wa kwanza kutoka nje ya nchi kupimwa kabla na baada ya kunywa kikombe na kuthibitika amepona. Pia nasikia mpaka sasa ameweza kutoa ushuhuda kanisani na mbele ya ndugu na marafiki zake waliokuwa wakimhudumia na kumpa msaada kwa wakati wote aliokuwa akiumwa. Namwomba kama kuna mwenye taarifa zaidi kuhusu tukio hili aendelee kutufahamisha zaidi, nawakilisha. Mods iacheni hii thread mpaka ithibitike kwanza ndiyo ihamishwe kama itakuwa lazima.
Kofia avuliwe Mungu !