Kikao cha Siri Ridhwani na Membe Uwanja wa Ndege

Wana Jf
Leo majira ya saa Tisa mpaka saa kumi jioni Mh Bernad Membe alikutana na Prince walifanya kikao cha Siri kwa zaidi ya saa moja na baada ya kikao chao hicho Membe alisikika akimpigia sim Bwana Mukama na kumuambia Tayari ameongea na Mpiganaji na atamueleza mzee kwahiyo asiwe na Shaka aongee na wanahabari asipate Shaka

Jukumu la kumuelewesha mzee ni la dogo kwahiyo aongee baada ya hapo dogo alitoka na baadae bosi wa Mambo ya njee alibaki

yaani wawe na ishu ya siri halafu ikaongelewe uwanja wa ndege? khaaa jamani mbona umbeya unaanza kuvuka mipaka
 


Jamani, sometimes tukubali Riz1 anastahili uPrince,

tusiwe wasahaulifu, ni juzi tu tumefanya uchaguzi, pamoja na kuwa jk hakushinda!...lakini tumesahau kampeni ilikuwa ya familia baada ya wazee ccm kumsusia?...jk, riz1, na malkia salma walikuwa wanahaha mikoani kupiga kampeni..mmesahau? sasa kwanini asiwe Prince?

Tena kwa pesa yao wenyewe. Msisahau kuwa mtandao haukuwepo tena. Lowassa mchango wake ulikuwa ni kura 89% za monduli. na Muirani wa Igunga alishasusa.
 
Naongea na Ridhiwani

MAMBO vipi kaka, pole kwa majukumu ya kikazi pale ofisini na yale ya kichama, naamini unazimudu changamoto zinazokukabili na OK na familia yako. Upo kimya sana kaka, nakumbuka mara ya mwisho tulionana ‘Club' pake Dodoma na wadau, kwanza nakupongeza unavyojichanganya, ‘keep it up bro', maisha ndiyo haya, Ikulu isitutenganishe.

Pole kaka, nasoma tu ‘madongo' unayopigwa kwenye magazeti, ndiyo ukubwa huo, hizo ndo gharama za siasa, muulize hata ‘mshua', haikuwa rahisi kwake kufika alipo, amekwepa ‘mishale' mingi. Tulizungumza mengi nilipokuja nyumbani kwako wakati unaishi maghorofa ya Masaki, tutapanga tupate muda mwingine kama ule tubadilishane mawazo, ila leo nimeona nikuambie mawili matatu, ufikishe ujumbe wangu kwa ‘mshua' ili aweke mambo sawa.

Kwanza mpe hongera kwa kukubali kuzungumza na Kamati ya Chadema kuhusu mchakato wa Katiba mpya, huenda uamuzi wake umewachukiza wenzake ndani ya CCM lakini naamini kwamba amezingatia zaidi maslahi ya Taifa na si ya chama. Nampongeza kwa uungwana na ustaarabu wake, kaonesha kwamba hana kinyongo na Chadema kwa sababu kama unakumbuka baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita walisema hawamtambui, wakalithibitisha hilo kwa kukataa kumsikiliza bungeni mjini Dodoma, lakini sasa wameomba wazungumze naye Ikulu.

Kaka pamoja na hayo mwambie ‘mshua' anapaswa kutumia mbinu kadri anavyoweza kurudisha uzalendo wa Watanzania kwa nchi yao. Ninasema hivyo kwa sababu siamini kama mtazamo wa wananchi kwa viongozi na nchi yao upo kama ilivyokuwa zamani. Ipo mifano kuthibitisha kutetereka na dhana ya uzalendo, miaka ya nyuma, Mtanzania alikuwa anajisikia fahari kuufahamu na kuuimba wimbo wa Taifa, na kwa kiasi kikubwa shule zilisaidia, hali sasa ni tofauti, nenda maofisini, pita mtaani mwambie mtu akuimbie huo wimbo, utashangaa.

Unaweza ukaona ni jambo dogo na halina maana, lakini ninaamini kwamba, Mtanzania anayefahamu thamani ya wimbo wa Taifa ana mchango mkubwa katika kuulinda uhuru na utaifa wetu, kuondoa chuki kwa kundi fulani kwenye jamii hasa viongozi, na kuilinda amani ya nchi yetu na Afrika kwa ujumla. Kaka ukiongea na wananchi mitaani utabaini ukubwa wa hatari inayotokana na chuki waliyonayo wananchi dhidi ya viongozi, sanjari na bomu linalosababishwa na kujengeka kwa matabaka baina ya wenye nacho na mafukara.

Kwa mtazamo wangu, heshima ya wananchi leo kwa viongozi wao si kama zamani, kiongozi miaka ya nyuma alikuwa na mvuto kwa mwananchi, hivyo haikuhitajika hamasa kwamba Watanzania wawaamini viongozi, na waliwaona ni sehemu ya jamii yetu. Nadhani unafahamu namna matendo ya viongozi wa leo yalivyobadili mtazamo wa Watanzania kwao, kiasi kwamba wanaonekana wezi wa mali ya umma, walafi, wabinafsi, wana tamaa ya utajiri, wanajitenga, wana tabaka lao, si sehemu ya jamii yetu , sisi ni sisi, wao ni wao, hivyo hawana mvuto kwa wananchi, hivyo dhana ya upendo na utaifa ipo njia panda.

Kaka mwambie ‘mshua' ayafanyie kazi hayo ili Watanzania tuendelee kuwa wamoja, kama hali itaendelea kuwa ilivyo leo huko tunapokwenda hatutakuwa na muda wa kuisifu nchi yetu au kuimba wimbo wa uzalendo wenye maneno Tanzania nakupenda Tanzania, jina lako ni tamu sana. Siku njema.

Chanzo: HabariLeo | Naongea na Ridhiwani
 
Alichoongea mtoa mada sikioni; walichoongea wachangiaji nacho sikioni; mbaya zaidi, hata mwenyewe ninachoongea sikioni kwenye suala zima hili sikioni. Nazani JF ingekuwa disabled angalau kwa miezi mitatu, labda baada ya huo muda memberz watakuwa wame-sharpen uwezo wao wa kufikiri na hivyo kuanza kuandika mambo ya maana!!! Mi mwenyewe zamani nilikuwa haipiti wiki kabla cjaanzisha thread, hivi sasa nimebaki kuchangia ujinga tu !!!
Ni Wewe!
 
Wiki ijayo atamuona Membe akienda kwa mganga wa Kienyeji, kisha atasikia akimpigia simu Prince kuwa nimmalize au apate kiharusi tu, Prince atajibu ngoja nimuulize mzee. Let us be fair to both Camps, (BM & EL) kama hatuna habari za kuandika tusiwazushie uhasama usio wa lazima, tutajibu nini mbele za Mungu?
Mbona hueleweki wewe?Hebu Toka hapa!
 
hahahahahahahhahahahahaah du uwiiiiiiiiiiiiiiiiii heehehheee haahhhhhahah aisee mhhhhh! mi napita tu ngoja nikoleze zangu mkaa nipike mwaya maana umeme wenyewe umekatika toka asubuhi huku kwetu.
 
ukiwa mbunifu mahiri unatunga uongo unaokaribiana na ukweli na ndipo uongo unageuka kuwa ukweli
 
Membe ni moja ya watu muhimu sana wa JK akiwa mmoja wa the best 4 friends of Jk sasa habari unayoleta hapa inaonyesha kwamba ama Membe hawezi kumfikia Jk hadi apitie kwa mtoto wa Jk au Membe sio mmoja wa watu wa karibu na JK tena. Ukipika uongo usipoiva vizuri utakula chakula kibichi
 
Mnajuaje kama kilikuwa kikao??

Hawa ni wanaume wawili waliokutana kwa about one hr...........Mnakumbuka Cameroon alituambia nini??:juggle:
 
Hakuna ukumbi wa mikutano kwa wasafiri pale uwanja wa ndege kama ingekuwa ni kweli basi hakikuwa kikao bali inaonyesha walikutana tu kwa kila mmoja na safari yake.....kukiita kikao ni kuongeza chumvi lakini zaidi jambo hilo lingekuwa siri ya watu wawili sidhani kama wangepayuka hovyo pale uwanja wa ndege kwa kila mtu kusikia
 
Back
Top Bottom