Kijitabu Cha Orodha ya mafisadi wa Elimu Tanzania chagombewa sokoni

tatizo ni kusoma non accredited schools/universities

non accredited wapi? Tz au hizo nchi walizosoma??

TCU ina orodha ya vyuo world wide ambavyo wao ni non accredited? maana kwa Tz ukienda kwenye mtandao wao mzumbe university ni non accredited!!
 
Diallo, ni jina Sir Name iliyo maarufu kwenye nchi zilizokuwa chini ya Mali Empire. Utalisikia kwenye nchi kama Mali, Senegal, Ivory Coast, Guinea Conacry etc. Wanigeria hawana Diallo (linasomeka kwa wengine Jalo).

Kwa watu wa umri wao mtakuwa mnakumbuka wimbo wa Alpha Blondy "Fanta Diallo". Ila pana wakati nilisikia habari moja kuwa miaka ya uhuru, kuna jamaa wengi wa West Africa waliletwa Zenji na hawa waliacha majina/watoto wenye hizo sir name.

Ila Wasukuma huwa hawachelewi kujipa majina kama Carrington, MacBundala, Mzungu, Ulaya, Marekano, Meja, nk. Sintoshangaa kusikia jamaa si jina lake hasa la ukoo ila kajipachika jina la mshichana wake wa Kiguinea aitwaye Tigui Diallo (Diabate Coulibaly Keita).

dah! nimecheka yaani unawapiga dongo nduguzo! lol
mi nilidhani ni wamakonde pekee ndio wanajipa majina yanayowavutia
mfano, ikarus, achkofu (sic), dirisha, mkasi (lukasi), rais n.k lol
 
Call me stupid... ila niko a bit confused here.. huyu jamaa anasema kwamba hawa wakuu wamedanganya umma kwa kutoa vyeti vya uongo (vyeti fake) au nikwamba university walizosoma ni non-accreditable kwa tz?
 
Sikonge na wewe kwa fiksi umezidi!!

Ehh bwana wee, huo ulikuwa ni mfano tu na si kweli.

Nitamfahamia wapi GF wa Diallo wakati akisoma US?

Ila hilo laweza kuwa kweli. Kwa mfani wewe Amani unaweza ukajiita Amani Timaya au Amani Peter, hahaaaa hahahaaaa :) Hawajambo Jerusalem 94?
 
dah! nimecheka yaani unawapiga dongo nduguzo! lol
mi nilidhani ni wamakonde pekee ndio wanajipa majina yanayowavutia
mfano, ikarus, achkofu (sic), dirisha, mkasi (lukasi), rais n.k lol

Makonde kiboko.

Mmoja alijiita JULIUS KAMBARAGE NYERERE.......
 
Huyu muhaya nina wasiwasi hata kama na yeye ana akili nzuri au ni kutaka kuuza kitabu chake tuu,hao wote aliowataja wengi wao wamesoma hizo shule ila tatizo ziko non accredited na hilo sio kosa,mzumbe yenyewe ina fall hapo,huwezi kuita hii ni forgery au ufisadi au kushtaki mtu kwa kusoma non accredited schools,huyu analeta story za mtikila za kuchafua watu na kujaza watu ujinga
 
Ehh bwana wee, huo ulikuwa ni mfano tu na si kweli.

Nitamfahamia wapi GF wa Diallo wakati akisoma US?

Ila hilo laweza kuwa kweli. Kwa mfani wewe Amani unaweza ukajiita Amani Timaya au Amani Peter, hahaaaa hahahaaaa :) Hawajambo Jerusalem 94?

Asante mkuu kwa hayo madongo maana hiyo Timaya na Peter nimeshaelewa.
Mimi bado nasimama na wajumbe wengine ambao wameeleza kwa weledi wa hali ya juu kwa nini huyu Msemakweli inawezekana anasema uongo lakini hatambui.Uko wapi mwongozi wa kuvitambua vyuo vinavyokubalika katika nchi yetu ya Tanzania.Ama ni utaratibu gani unaotumika kukataa ama kukubali shule walizopitia akina Diallo.Je nchi nyingine elimu kama ya Diallo haitambuliki?
 
Sijui kama Mzee Mwanakijiji ataandika chake kwa Kiswahili juu ya USANII wa Tanzania. Hapa nikiwa na maana ya WASANII wote na zaidi iwekwe juu ya MSANII namba moja moja hadi tano wa Tanzania (the big five).

Hamna jhaja ya kuandika mengi maana kitakosa maana. Ikiwezekana hata wawe watatu tu au wawili. Waandishi anzeni kazi na sisi tutanunua. Inaweza kuwa ahadi HEWA za viongozi mwaka 2005, kushindwa kutimiza majukumu na takatala nyingine kibao. Uzembe na kutokufuatilia kazi. Vielelezo vipo kibao kama picha ya Gavana, hopsital ya watoto Temeke, shule za msingi nk.......


kwa mtindo huu nikiandika tu si kitanunuliwa nakala moja tu halafu inakuwa scanned..
 
Huyu muhaya nina wasiwasi hata kama na yeye ana akili nzuri au ni kutaka kuuza kitabu chake tuu,hao wote aliowataja wengi wao wamesoma hizo shule ila tatizo ziko non accredited na hilo sio kosa,mzumbe yenyewe ina fall hapo,huwezi kuita hii ni forgery au ufisadi au kushtaki mtu kwa kusoma non accredited schools,huyu analeta story za mtikila za kuchafua watu na kujaza watu ujinga

TCU deals with accreditation of Tanzanian Universities tu. Kuhusu vyuo nje ya nchi, sana sana watakupatia latest list kutoka UNESCO. Jambo hapa ni kwamba vyeti walivyo'present Bungeni hawa waheshimiwa ni kutoka vyuo feki, yaani havitambuliki na UNESCO. Na kusoma katika non-accredited University ni kwamba unataka njia ya mkato kwa kulipia ELIMU bila kuifanyia kazi ipasavyo.

[ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Washington_International_University[/ame]

Mfano: Lukuvi ameenda kutafuta cheki cha Washington University na kudanganya umma kuwa ana Degree ya Diplomasia. Kumbe digrii yenyewe feki. Hata kama aliandika insha 2 katika coursework. Mbona kuna long-distance degree's zinazotambulika? Mfano, University of London.
 
Koba,una tatizo gani?Jamaa ameandika kitabu,soma kwanza.
Ujuavyo kila mtu mwenye akili timamu anajua Phd za watajwa ni fake!
Huyu Mhaya(kama ulivyosema) ni decent guy,anataka kurudisha umuhimu wa elimu tanzania.
kama una Phd unayo kweli kweli.ukiangalia hawa wote wana pesa tayari,sasa walikuwa wanataka title za kielimu.

I tell you watu wana uhondo wa Phd Tanzania kama fisi.tulianza zamani
akina Salmin,Salim Ahmed Salim etc.Naoa hata JKwameanza kumwita Dr!Come on
worse enough magazeti ndiyo yanawakuza hawa watu na kuwaita ma dr???Hata Dr Karume.
For God sake,i am spitting blood for this stupidity
 
TCU deals with accreditation of Tanzanian Universities tu. Kuhusu vyuo nje ya nchi, sana sana watakupatia latest list kutoka UNESCO. Jambo hapa ni kwamba vyeti walivyo'present Bungeni hawa waheshimiwa ni kutoka vyuo feki, yaani havitambuliki na UNESCO. Na kusoma katika non-accredited University ni kwamba unataka njia ya mkato kwa kulipia ELIMU bila kuifanyia kazi ipasavyo.

http://en.wikipedia.org/wiki/Washington_International_University

Mfano: Lukuvi ameenda kutafuta cheki cha Washington University na kudanganya umma kuwa ana Degree ya Diplomasia. Kumbe digrii yenyewe feki. Hata kama aliandika insha 2 katika coursework. Mbona kuna long-distance degree's zinazotambulika? Mfano, University of London.

...non accredited doesnt mean fake,ila kuna matatizo kusoma katika hizo shule ambayo naona ni topic nyingine tena!
 
Kwa Afrika chuo ambacho kinatoa top class distance learning ni UNISA ya sauz !Huwezi kupata Phd ukiwa tanzania,unatakiwe uwe sauz full time!Unless professa anakuja bongo mara kwa mara

Also Uk kuna Open university na London University external degrees.Hizi vilevile huwezi kufanya Phd ukiwa nje ya Uk,maana unahitaji msimamizi (Professa) etc.sasa hizi za akina Nchimbi,Nagu sidhani waliandika chochote.Utakuta hata fees zililipwa na taxpayers !

Naona shaka sasa Phd za Tanzania ni kwa elites,hata UDSM penyewe.Watu wamemsifu Magufuli kwamba amepata UDSM!Unajiuliza huyu full time ni waziri anamajukumu.saa ngapi alikuwa anapata muda wa kufanya research?je hao maprosessor kwenye Panel walikuwa independent?

Sasa tuna utitiri wa Versities,nilisikia ila Mzumbe kama wanatoa Phd it is a big joke!
Maana chuo hiki ndio kimekuwa mbele kuwa na lectures wenye fake Phd kuanzia boss wao wa zamani Warioba!

We are doomed na uswahili wetu.
 
Namfahamu Mh. Diallo, na nakumbuka nilivyokuwa namuona akipiga book. na nisikuwa nikimsifia kwamba hakika yeye unawezo mkubwa kuliko vijana wengi, kwa maana kuweza kusoma, siasa, biashara etc. But I saw that man... is extraordinary.

Jamaa amesomea degree yake... sasa kama munadhani kusoma lazima uwe darasani... kama hamtambui distance learning... that is your proble.

Diallo ni msanii mzoefu tu hana cha kupiga book wala nini; kazi aliosomea na anaifahamu ni ya kufunga vidonda na wote wanaomfahamu watakwambia hivyo!! Ni mtu mjanja mjanja tu; Kasheshe inaelekea umeajiliwa kuwapigia debe mafisadi wa elimu!!!
 
Hivi kuna PhD ya long.distance, let alone ya Business Administration (kama ya Diallo)
 
Kwa Afrika chuo ambacho kinatoa top class distance learning ni UNISA ya sauz !Huwezi kupata Phd ukiwa tanzania,unatakiwe uwe sauz full time!Unless professa anakuja bongo mara kwa mara

Also Uk kuna Open university na London University external degrees.Hizi vilevile huwezi kufanya Phd ukiwa nje ya Uk,maana unahitaji msimamizi (Professa) etc.sasa hizi za akina Nchimbi,Nagu sidhani waliandika chochote.Utakuta hata fees zililipwa na taxpayers !

Naona shaka sasa Phd za Tanzania ni kwa elites,hata UDSM penyewe.Watu wamemsifu Magufuli kwamba amepata UDSM!Unajiuliza huyu full time ni waziri anamajukumu.saa ngapi alikuwa anapata muda wa kufanya research?je hao maprosessor kwenye Panel walikuwa independent?

Sasa tuna utitiri wa Versities,nilisikia ila Mzumbe kama wanatoa Phd it is a big joke!
Maana chuo hiki ndio kimekuwa mbele kuwa na lectures wenye fake Phd kuanzia boss wao wa zamani Warioba!

We are doomed na uswahili wetu.

Are you sure you cant do long distance PHD? as far as i am aware there is no leactures for PHD... and you can do PHD while u are in any country or u have to do is to meet ur superviour in regular bases (and regular bases doesnt mean each month or week)..
 
Ni kweli jamani mafisadi wa elimu wapo na ni wataalamu wa kuongea sana ili kujitengenezea mazingira fulani ya kiulaini katika ulaji wao wa day to day, hii inamaanisha wasomi wengi wataendelea kukosa nafasi za ajira kutokana na nafasi wanazostahili kuzipata kutumiwa na wajanja wachache, hili nadhani halina mjadala na wahusika inabidi wachukue hatua za dhati za kupambana na waovu kama hao wanaojichukulia sifa kede kede za usomi, siku hizi kuna elimu kwa njia ya mitandao labda iwe kwamba wamejisomea kwa ile wanayoita distance learning
 
Wasukuma wengi ni decent people,Dialllo amewaaibisha wasomi wa Mwanza,pamoja na mwenzake Chegeni!
 
Kwanza kabisa, miaka ya elimu si standard clear.

Pili, kusema nchi yetu haina standard haina maana kwamba mtu anatetea hawa wanasiasa.

Napingana na wewe kwenye red miaka ya elimu ni standard huwezi ukawaacha watoto wako hadi miaka 15 ndipo waanze class one au muda wowote utakaopenda ndiyo maana serikali inatoa data kila mwaka ni wanafunzi wangapi wameanza na kumaliza level fulani na vile vile huwezi kusoma darasa moja say kwa miaka mitano hata form two ukirudi mara moja next year ukifeli unapasishwa

ndiyo maana ukichelewa kuanza shule say na umri wa miaka 30 hautachanganywa na watoto wa miaka 7 utapelekwa madarasa ya elimu ya watu wazima kuna mzee mmoja kule Kenya aliingia form one na miaka 80 ilikuwa issue ya dunia nzima kama miaka isingekuwa standard hiyo wala isingekuwa habari
 
mnajadili zaidi ili iwe nini? Yeye katoa kitabu kama kuna aliye onewa akashitaki si basi??
 
Back
Top Bottom