Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Kijiji chadai hakina maji tangu uhuru
Na Raphael Okello, Rorya
WAKAZI wa Kijiji cha Panyakoo, Kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwapatia huduma ya maji ya mifugo na matumizi ya majumbani tangu uhuru na kusababisha kufuata huduma hizo katika nchi jirani ya
Kenya.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ngâope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.
Wamedai kutokana na hali hiyo baadhi ya mifugo yao imekuwa ikipotea au kuibwa na watu wasiojulikana hivyo wameiomba serikali kuwachimbia lambo kwa ajili ya mifugo yao na visima kwa matumizi ya nyumbani.
Wananchi hao wamekuwa wakipata maji katika msimu wa mvua katika visima vifupi vya asili kwa matumizi ya nyumbani, na Mto Ondoche kwa mifugo, lakini vyanzo hivyo huchukua muda mfupi tu kukauka mara baada ya msimu wa mvua kumalizika.
Na Raphael Okello, Rorya
WAKAZI wa Kijiji cha Panyakoo, Kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwapatia huduma ya maji ya mifugo na matumizi ya majumbani tangu uhuru na kusababisha kufuata huduma hizo katika nchi jirani ya
Kenya.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ngâope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.
Wamedai kutokana na hali hiyo baadhi ya mifugo yao imekuwa ikipotea au kuibwa na watu wasiojulikana hivyo wameiomba serikali kuwachimbia lambo kwa ajili ya mifugo yao na visima kwa matumizi ya nyumbani.
Wananchi hao wamekuwa wakipata maji katika msimu wa mvua katika visima vifupi vya asili kwa matumizi ya nyumbani, na Mto Ondoche kwa mifugo, lakini vyanzo hivyo huchukua muda mfupi tu kukauka mara baada ya msimu wa mvua kumalizika.