Kijiji chadai hakina maji tangu uhuru

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Kijiji chadai hakina maji tangu uhuru


Na Raphael Okello, Rorya

WAKAZI wa Kijiji cha Panyakoo, Kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwapatia huduma ya maji ya mifugo na matumizi ya majumbani tangu uhuru na kusababisha kufuata huduma hizo katika nchi jirani ya
Kenya.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ng’ope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.

Wamedai kutokana na hali hiyo baadhi ya mifugo yao imekuwa ikipotea au kuibwa na watu wasiojulikana hivyo wameiomba serikali kuwachimbia lambo kwa ajili ya mifugo yao na visima kwa matumizi ya nyumbani.

Wananchi hao wamekuwa wakipata maji katika msimu wa mvua katika visima vifupi vya asili kwa matumizi ya nyumbani, na Mto Ondoche kwa mifugo, lakini vyanzo hivyo huchukua muda mfupi tu kukauka mara baada ya msimu wa mvua kumalizika.
 
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ng’ope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.
Ni vyema wafugaji wetu wakaacha ushamba wa kuiona mifugo ni wa kuwaletea masifa au heshima kijijini kwao au kwa minajili ya kulipia mahari tu......................kwa kufanya hivyo wanakuwa ni watumwa wa mifugo hiyo wakati ambapo mifugo hiyo inapaswa kuwa ni ya kuwarahisishia maisha kama kuchimba malambo kwa kuiuza baadhi ya mifugo yao na wao kunufaika na kazi ya ufugaji.................
 
Hii nimoja kati ya Failures za Nyerere.

Alipo leta vijiji vya ujamaa, agriculture sector ndio ikafa kabisa, pamoja na yote hakuweza kuleta huduma za maji, umeme, nk, vijijini kama alivyo dai. kpumzike mzee,,,,,,
 
Inasikitisha kuona mafisadi wanavyotesa wakati kuna watu wana hali duni hivyo!Huko hata rais wanamjua kweli?
 
hao hao ndio wana ccm dam, na wanampenda mkwere na kundi lake. Tusimlaum nyerere sana alijitahidi kadri ya uwezo wake. Wakuwalaum ni hawa manyangau. Mkwere, mkapa na wenzao ambao wamefeli kwa asilimia zote kutatua matatizo ya wananchi.
 
Hii nimoja kati ya Failures za Nyerere.

Alipo leta vijiji vya ujamaa, agriculture sector ndio ikafa kabisa, pamoja na yote hakuweza kuleta huduma za maji, umeme, nk, vijijini kama alivyo dai. kpumzike mzee,,,,,,

Acha kumlaumu Mwl. Nyerere aliacha misingi kumbuka vizuri wewe Bull.
 
Kijiji chadai hakina maji tangu uhuru


Na Raphael Okello, Rorya

WAKAZI wa Kijiji cha Panyakoo, Kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwapatia huduma ya maji ya mifugo na matumizi ya majumbani tangu uhuru na kusababisha kufuata huduma hizo katika nchi jirani ya
Kenya.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ng’ope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.

Wamedai kutokana na hali hiyo baadhi ya mifugo yao imekuwa ikipotea au kuibwa na watu wasiojulikana hivyo wameiomba serikali kuwachimbia lambo kwa ajili ya mifugo yao na visima kwa matumizi ya nyumbani.

Wananchi hao wamekuwa wakipata maji katika msimu wa mvua katika visima vifupi vya asili kwa matumizi ya nyumbani, na Mto Ondoche kwa mifugo, lakini vyanzo hivyo huchukua muda mfupi tu kukauka mara baada ya msimu wa mvua kumalizika.

Ruta wewe vipi?Hivi unaifahamu Tanzania kweli?Mbona híi ndiyo kawaida.Kijiji changu nilichozaliwa hakijawahi kuwa na bomba na kwa sasa vijito vyote vilivyokuwa vinatiririsha maji vimekauka kabisa.Hali ni mbaya kupindukia.
 
mwenyetu paul kagame,kaanzisha program wanayoiita bye by nyakasi. Yaani kwaheri nyumba za majani.wanavunja nyumba zote za mbavu za mbwa na kujenga za kisasa. Ni aibu na fedheha kwetu. Na utajiri wote tulionao tuna shindwa na ka rwanda kwa maendeleo na utawala bora. Tatizo hapa ni uongozi mbovu na viongozi mazuzu waliosoma ili kufaulu mitihani na sio kuelimika. Inatia kichefu chefu ndio maana nimeoa mnyarwanda angalau wanangu wana cha kujivunia na sio huo ufisadi uliojaa nyumbani.
 
Hii nimoja kati ya Failures za Nyerere.

Alipo leta vijiji vya ujamaa, agriculture sector ndio ikafa kabisa, pamoja na yote hakuweza kuleta huduma za maji, umeme, nk, vijijini kama alivyo dai. kpumzike mzee,,,,,,

Babu hapo Nyerere unamuonea.Nyerere alijitahidi ukizingatia nchi ilikuwa changa sana sasa leo hii gharama ya chai na vitafunio ni bilioni kadhaa wakati wananchi hata maji bado ni hadithi..
 
Maskini kama wangejua kwamba kilio chao si cha kwao peke yao wasingetoa kura kwa Ayila. Sasa wasubiri Ayila atawajengea visima maana ilikuwa ahadi zake! Sina huruma na watu wanaojitakia shida wenyewe. Walidanganywa na wakina Sarungi weeee sasa wameingia choo ya kike!
 
Si wachimba maji wanakijiji wote (i mean wanaume wote hapo) kijijini wangeanza kuchimba maji kwenda chini ya ardhi tangu 1961 wakapokezana hadi leo wangepata maji nina hakika au siyo?

Mwishowe watasema kijiji hakina vyoo tangu uhuru

Wajiulize wamefanya nini kujiletea maendeleo wakiwa huru..siyo kuletewa maendeleo

Hizi line of thinking ndio zinatakiwa kubadilika period..chimbeni maji chini yapo tele
 
Si wachimba maji wanakijiji wote (i mean wanaume wote hapo) kijijini wangeanza kuchimba maji kwenda chini ya ardhi tangu 1961 wakapokezana hadi leo wangepata maji nina hakika au siyo?

Mwishowe watasema kijiji hakina vyoo tangu uhuru

Wajiulize wamefanya nini kujiletea maendeleo wakiwa huru..siyo kuletewa maendeleo

Hizi line of thinking ndio zinatakiwa kubadilika period..chimbeni maji chini yapo tele
Haya ndio majibu yenu wana ccm baada ya uchaguzi!!!!! Sawa bwana wamewasikia!!!
 
Vijiji vyenye matatizo haya vipo vingi mno na tena vijiji kama hvyo unakuta vina wanavijiji wao ambao wana nyadhifa za juu serikalini mfano mzuri ni kijiji cha Tanganyika Masagati ambako gavana wa benki kuu aliyepita ni mwenyeji wa kule lakini hakuna barabara wala maji pamoja na huduma nyingine za muhimu.....
 
Kijiji chadai hakina maji tangu uhuru


Na Raphael Okello, Rorya

WAKAZI wa Kijiji cha Panyakoo, Kata ya Goribe wilayani Rorya mkoani Mara wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwapatia huduma ya maji ya mifugo na matumizi ya majumbani tangu uhuru na kusababisha kufuata huduma hizo katika nchi jirani ya
Kenya.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki baadhi ya wakazi hao wamesema kutokana na ukosefu wa maji kijijini hapo na vijiji jirani vya Ng’ope, Charya na Nyamusi, wananchi wanalazimika kunywesha mifugo yao katika malambo ya Olasi nchini Kenya ambapo licha ya kutozwa fedha katika huduma hizo, lakini pia wanateseka kutembea umbali mrefu wa wastani wa km 30 kwenda na kurudi pamoja na mifugo yao.

Wamedai kutokana na hali hiyo baadhi ya mifugo yao imekuwa ikipotea au kuibwa na watu wasiojulikana hivyo wameiomba serikali kuwachimbia lambo kwa ajili ya mifugo yao na visima kwa matumizi ya nyumbani.

Wananchi hao wamekuwa wakipata maji katika msimu wa mvua katika visima vifupi vya asili kwa matumizi ya nyumbani, na Mto Ondoche kwa mifugo, lakini vyanzo hivyo huchukua muda mfupi tu kukauka mara baada ya msimu wa mvua kumalizika.


Waongo hao. yaani wakati wa ukoloni maji yalikuepo baada ya uhuru yakaisha hadi leo!!!!!!!! wanakunywa nini? Halafu wana JF wilaya ya rorya inapakana na ziwa victoria wanavua samaki humo kwa kitoweo halafu maji hawana? si wahame Miaka hamsini wapo na maji hakuna is it possible? tuache uongo bana!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom