Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Leo nataka kufanya utafiti mdogo kwa akina dada ambao hawajaolewa. Swali langu ni hili:
Kwa mfano una elimu ya ngazi ya shahada na unafanya kazi nzuri yenye mshahara na marupurupu si haba, halafu inatokea mvulana wa mtaani ambaye hana kazi lakini ana elimu ya wastani ukilinganisha na ya kwako anakuomba uwe na uhusiano naye kimapenzi na anakuahidi kwamba lengo lake si kukuchezea bali kukuoa kama mkikubaliana…
Je utakuwa tayari kuingia katika uhusiano huo?