View attachment 63371
Mwenye picha hiyo hapo kwenye attachment ni kijana wa kwanza wa ndugu Cornel Mujungu anayefanyia kazi Kasulu.
Kijana huyo ametoroka kwao katika mazingira ya kutatanisha tangu jana tarehe 29/08/2012 alipomuaga mdogo wake wa miaka kumi na moja kuwa anaenda Moshi, ambako hakujui tena hakuwa na pesa yoyote kulingana na mazingira ya nyumbani kwao yalivyo kwani hakuna access yoyote ya kupata kiasi cha pesa kiasi cha kumsafirisha hadi Moshi bila ruhusa ya wazazi wake.
Lakini pia kijana huyo Tumaini Cornel Mujungu anao umri wa miaka kumi na mitano na anasoma Kidato cha kwanza katika shule ya secondary ya Rev. A. Bungwa iliyoko mjini Kasulu wanakoishi wazazi wake na kwa kipindi hiki alikuwa likizo hadi tarehe 11/09/2012 wanapotarajia kufungua shule hiyo.
Kwa hiyo ndugu zangu naomba wanajamii wenzangu popote mtakapomuona au kusikia habari zake naomba tuwasiliane kwa namba zifuatazo:
+255 754 401806
+255 782 367288
+255 755 094760
+255 789 179294
+255 754 622023.
Nashukuru wanajamii kwa kushirikiana katika hili.
Mbarikiwe sana
Poleni sana wanafamilia! Lakini pia msiache kufuatilia hata maeneo ya machimboni kama Mirerani na kwingineko kwakua vijana wa sasa wanatafuta utajiri wa haraka haraka sana!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.