Kiini macho cha Kamati ya January Makamba na Dowans


what makes it being crap?
Unataka mpaka CDM wakisema ndio manakubali?
tunapingana kwa hoja sio chuki binafisi zisizoweza kujenga nchi yetu
Unaweza kunyea kambi wewe? Usilaumu tu ndugu. Hata Salva akitoka ikulu usishangae akaigeuka

1.Ukifuata mambo ya wanasiasa wakati mwingine Nchi inaweza isifike Mbali.

2.Huyu dogo alikuwa karibu na Rais wakati madudu yote yanatokea ,Je alichukua hatua gani ya kukemea wakati yeye yupo pale State house...alimshauri nini Rais

3.Hili suala kama anaona lina umuhimu sana na yeye haogopi mtu alipeleke bungeni..

4.Haya mbiyo za 2015
 
ntajiua akigombea:bump::msela::hungry:

Kiduku؛‎ unataka kuniliza mapema, uwe mwangalifu. Kumbuka Sugu yu bungeni licha ya viapo vya watangazaji wa radio maarufu. Kumbuka ukoo huo hauna hiana maana kama wangekuwa wanajitazama basi ccm ingekuwa na katibu. Kwa faida yako tu angalia hili: katibu mkuu wa chama-Baba, katibu mwenezi-kaka, mfadhiri mkuu wa miradi ya maendeleo ya wananchi jimboni-dada................ Kwa nini lolote lisiwezekane?!
 
Mbwa mwitu kuvaa ngozi ya kondoo. Amekuwepo Ikulu na yote yaliyokuwa yanafanyika alikuwa anayaona na kuyajua, leo anaibuka na hayo, mbona alipogombea ubunge hakuongelea hayo, sasa upepo unawageukia ndio unaona wanaanza kuhaha.

Kumbukeni hotupa ya Kikwete kule dodoma juzi alivyosema wanageuka sasa kuanza kuambaa kama nyoka ili kujenga upya chama. Hii ni janja na mbinu yao kuteka hoja ya Chadema.
 
Mbunge wa CCM aibua siri nzito Dowans, IPTL Monday, 07 February 2011 21:51
AHOJI UADILIFU WA WANASHERIA WALIOITETEA TANESCO
Ramadhan Semtawa
MBUNGE wa Bumbuli, January Makamba, amemwandikia waraka Waziri wa Nishati na Madini kumtaka afafanue bungeni mambo kadhaa yanayohusu wizara hiyo, likiwamo sakata la Kampuni ya Dowans.Sehemu ya waraka huo imeibua jambo kwa mwanasheria wa Tanesco aliyesimamia kesi ya Dowans ambapo mbunge huyu anaeleza jinsi alivyocheza karata pande zote mbili kwa kushauri mkataba dhidi ya kampuni hiyo uvunjwe huku upande mwingine akiisifia na kuiombea mkopo wa Sh 20 bilioni katika Benki ya Stanbic.

Katika waraka huo wenye kichwa cha habari, "Yah: Taarifa ya Serikali Bungeni kuhusu Umeme Nchini," Mbunge Makamba ambaye ni mtoto wa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba anataja mambo hayo kumi ambayo Waziri William Ngeleja, anapaswa kuyafafanua kwa umma kupitia Bunge.

Waziri Ngeleja alipoulizwa kwa njia ya simu alikiri kuupata waraka huo na kuongeza, "Lakini, hadi sasa sijaufanyia kazi. Upo ofisini nimeambiwa umefika."

Wakati Ngeleja akikuna kichwa, Makamba katika waraka huo ambao nakala imeenda kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema:, "Kuhusu shauri la Dowans, Watanzania wameshuhudia kioja cha mawaziri wa serikali kujibizana na kupingana kwenye magazeti kuhusu malipo ya tuzo ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC) kwa kampuni ya Dowans."

...Taarifa ya Serikali bungeni kuhusu jambo hili ni muhimu ili kuweka bayana kwa Watanzania kwamba ni wakati gani, kwa njia gani na kwa jinsi gani Serikali inawasiliana na umma ili kuondoa mkanganyiko kwa wananchi na sisi wabunge kuhusu msimamo wa Serikali kwenye masuala mbalimbali."

Mwanasiasa huyo kijana aliongeza, "Mheshimiwa waziri, mnamo tarehe 6 Januari 2011, ulizungumza na waandishi wa habari na kueleza Serikali inajipanga kuilipa Dowans tuzo iliyoamuliwa na ICC."

"Lakini, kwa kuwa mzigo huu ni mzito kwa umma..., kumekuwa na fikra ikiwemo pendekezo la kamati ya wabunge wote wa CCM kwamba ni muhimu kutumia mianya ya kisheria iliyopo kupinga rasmi kutekelezwa kwa hukumu hiyo."

Akionyesha msisitizo katika hilo alisema, kwa kuwa hiyo imekwishasajiliwa Mahakama Kuu nchini na huku kila siku inayopita faini kwa Tanesco huongezeka kwa Sh 17milioni ni wakati wa Serikali kueleza ni lini itapeleka pingamizi la hukumu hiyo.

"Na hatua hii inamuweka wapi Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na tamko lako la Januari 6, 2011 kwamba kupinga utekelezaji wa hukumu ya ICC ni kupoteza muda," alihoji Makamba.

Akikazia katika Dowans, Makamba aliibua hoja akisema, katika viambatanisho vya hukumu ya ICC kama ilivyosajiliwa Mahakama Kuu zipo nyaraka zinazoonyesha mwanasheria aliyeishauri Tanesco kuvunja mkataba na kampuni hiyo akisema haukuwa halali na kusingekuwa na madhara kwa kuuvunja, ndiye huyo pia aliyeishauri Benki ya Stanbic kutoa mkopo wa dola za Kimarekani 20 milioni kwa Dowans.

"Na ndiye huyo huyo aliyeiwakilisha Tanesco kwenye kesi iliyofunguliwa na Dowans, kesi ambayo imetokana na ushauri wake... Na baada ya hukumu, ndiye huyo huyo kwa mujibu wa maelezo yako aliyekuja kutoa ushauri kwamba hakuna njia nyingine zaidi ya kuilipa Dowans baada ya hukumu," aliibua hoja hiyo nzito na kuongeza,

"Mheshimiwa Waziri, jambo hili likibaki hivi hivi bila maelezo inaweza kujengeka sura kwamba Serikali ilikosa umakini kwenye jambo hili zima na maadili hayakuzingatiwa... Itakuwa vyema kama taarifa ya serikali ikaeleza ni wanasheria gani waliotumiwa na Tanesco kwenye kila hatua shauri la Dowans."

Katika barua hiyo yenye kurasa tano, Makamba alitaka taarifa hiyo itaje wanasheria walioshiriki kuanzia kwenye ushauri kabla ya kuvunjwa kwa mkataba hadi ushauri baada ya kesi kuamuliwa na kiasi cha fedha walizolipwa kwa kila hatua, na utaratibu uliotumika.

Alienda mbali akisema, katika kuondoa Watanzania wasiwasi ambao wanaamini Tanesco ilishindwa kwenye kesi hiyo ya Dowans kutokana na upungufu wa weledi kwa wanasheria walioiwakilisha kwenye kesi hiyo, "Nashauri taarifa ya Serikali ieleze utaratibu uliotumika kuwapata wanasheria walioiwakilisha Serikali na Tanesco kwenye mashauri yaliyofunguliwa."

Amtaka atoe maelezo kesi mbili za IPTL
Mbunge huyo alisema anamsihi waziri atoe pia maelezo kuhusu kesi mbili zinazohusiana na mkataba wa uzalishaji wa umeme wa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).

Makamba anataka waziri aeleze mchakato wa kesi hizo zilizofunguliwa na Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong dhidi ya Serikali na Tanesco kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kesi za Uwekezaji (ICSID).

Makamba alifafanua, "Kesi hizo ni ICSID No ARB/10/20 dhidi ya Tanesco iliyofunguliwa Oktoba Mosi, 2010 na ICSID No ARB/10/12 dhidi ya Jamhuri ya Muungano iliyofunguliwa Juni 11, 2010, zinaweza kuwa na madhara makubwa kwa umma na zinaweza hata kuigharimu Serikali pesa nyingi kuliko zinazodaiwa katika kesi ya Dowans."

Alisema taarifa ya Serikali bungeni kuhusu kesi hizo mbili itasaidia Watanzania kufahamu:, "Nini kinadaiwa dhidi ya Tanesco na Serikali pamoja na maandalizi ya Serikali kushinda kesi hizi ili kuepukana na marudio ya zahama ya Dowans."

Katika kuonyesha msisitizo, mbunge huyo, alimtaka waziri kama ataona inafaa awajulishe Watanzania sababu za Serikali kutotoa taarifa za kesi hizo mbili muhimu kwa maslahi ya umma hadi sasa.

..Ahoji matamko sita ya Serikali kumaliza tatizo la umeme

Akizungumzia zaidi ahadi na matamko ya kumaliza tatizo la umeme, Makamba alisema tangu mwaka 2006 hadi sasa zimetoka ahadi na matamko sita ya Serikali ya kumaliza tatizo la mgawo wa umeme nchini, lakini hadi sasa bado mgawo unaendelea.

Makamba aliweka bayana kwamba, ingawa kila kunapotokea mgawo kumekuwa na maelezo na sababu mbalimbali, lakini ahadi hizo mara nyingi zimekuwa zikijirudia na kuongeza:, "Wewe (Ngeleja) mwenyewe umetoa ahadi kadhaa za kumaliza tatizo hili, lakini ahadi hizo hazikutumia."

Alisema matokeo ya hali hiyo ni wananchi kupoteza imani na uwezo wa Serikali yao kutatua tatizo la umeme nchini na hata matatizo yao mengine na kuonya:, "Kuna gharama kubwa kwa wananchi kupoteza imani na Serikali yao."

"Mimi naamini kwa dhati kabisa, kama Serikali ikitoa tamko la dhati kabisa bungeni linalobainisha kwa kina na uwazi sababu za ahadi hizi za mara kwa mara basi tutakuwa tumepiga hatua kwenye kuimarisha imani ya wananchi kwa Serikali yao," aliongeza.

IPTL inavyoigharimu Serikali
Akikazia katika IPTL, alisema mtambo unaozalisha umeme wa kutumia mafuta mazito aina ya HFO unaigharimu Serikali mabilioni ya shilingi kwa mwezi licha ya kuzalisha umeme chini ya nusu ya uwezo wake, kutokana na uhaba wa na bei kubwa ya mafuta.

Mbunge huyo alisema kutokana na gharama hizo kubwa, Serikali imeamua kulipia gharama zote za kubadilisha au kukarabati mitambo hiyo ambayo si mali yake bali IPTL ili itumie gesi asilia badala ya mafuta mazito ya HFO.

"Mwaka 2006, Serikali iliingia mkataba na Kampuni ya Alstom Power Rentals kuzalisha umeme mkoani Mwanza kwa kutumia mitambo ya mafuta, kutokana na shida na gharama ya upatikanaji mafuta na kuyasafirisha mpaka Mwanza, mtambo huo haukutumika kuzalisha umeme hata siku moja ndani ya miezi 12 ya mkataba, zaidi ya saa 20 tu kwa ajili ya majaribio kabla ya mtambo kukabidhiwa kwa Serikali," alisema na kuongeza,

"Kwa kifupi ni kwamba kampuni hiyo ililipwa kiasi cha dola za Marekani 1.7 milioni (takriban Sh 2.5bilioni), kwa mwezi za bure, bila kuzalisha umeme wowote. Ili wananchi waone kwamba Serikali yao ina uchungu na rasilimali za umma, nashauri taarifa ya Serikali ieleze hatua za uwajibikaji kwa hasara hii ya takriban dola 20 milioni."

Mzimu wa mikataba ya umeme Tanesco imekuwa ikiitikisa nchi ambayo mwaka 2008, ilisababisha Baraza la Mawaziri la kwanza la Serikali ya awamu ya nne kuvunjwa, baada ya Kamati Teule ya Bunge kubaini mkataba kati ya Kampuni ya Richmond na shirika hilo ulikuwa na walakini.

Mwananchi 8 Feb 2011

Huyu Mhesimiwa Makamba si alikuwa ikulu, yote si aliyaona, ua anatupiga changa la macho?????????????????? Ashinikize kura ya kutokuwa na imani na swahiba wake basi, apambane na mwenye mali asimuue mtumwa bure!!!
 
..tatizo lugha aliyotumia ni ya KUBEMBELEZA.

..hivi January anataka tuamini kwamba hajui kuwa JK ndiye mhusika mkuu wa Dowans?

..hiyo barua yake inalenga ktk kuwabebesha mzigo wa lawama watu wasiohusika, na kuwasafisha wanaohusika
 
Hivi Seacliff haya uliyatoa wapi??
SeacliffKuna rafiki yangu lawyer kwenye NGO moja hapa NY ambayo yule dada Lisa Rockefeller ni board member, amenidokeza kuhusu issue ya huyu dada na yule kijana wa Bumbuli – January Makamba. Hii issue imemkera sana huyu dada na anaichukulia serious sana. January na Lisa walikuwa na uhusiano mzuri sana ambao ulishamiri zaidi wakati alipokuwa Marekani kwenye safari na JK ya kuonana na investors na donors. Lisa pia ndiye aliye-organize na rafiki yake wa “The Economist” kuandika ile piece ya January Makamba ambayo ilikuwa na objective ya kumsaidia kukuza profile yake kwenye kampeni. Kwa Lisa, January alionekana ni mtu progressive anayependa maendeleo na quite possibly future leader wa Tanzania. Wakati Lisa alipokuja Tanzania mara ya mwisho akakuta mradi aliotolea hela nyingi kule Mbeya haujafanyika, wakati alipewa guarantee na rafiki yake January kuwa hela hiyo itatumiwa kwenye huo mradi, alikuja juu na kudai accountability. January apparently akamjia juu na kumtishia kuwa yuko Bongo asilete ukoloni wa Kimarekani. Apparently, alimpa threats nyingi zaidi na kwa sababu ya hizo threats dada Lisa alizipeleka nyumbani na familia ikapiga simu Homeland Security. Ilibidi wamarekani wa-launch formal investigation ambayo mpaka sasa inaendelea. Kuna matisho aliyoyatoa January bila kufikiria madhara yake na huyu dada akayachukulia serious na kwa hasira sana. Kumbuka yeye alikuwa anategemea appreciation huku na quite honestly sidhani kama alikuwa na mambo mengine mengi zaidi ya kusaidia. Sasa hiyo ndiyo inasemekana imemfanya Mkulu ashindwe kumpa ule uwaziri ambao kijana alikuwa ana uhakika wa kuupata. Kuna habari pia kwamba kijana January amewekwa kwenye list mbaya ya Homeland Security na itakuwa vigumu sana kusafiri huku mpaka hii issue iwe cleared.
Interesting....eeh
 
Hoja nzito kutoka kwa upinzani tu ndio zinazojadiliwa humu ndani. Ingawa huyu kijana wa Makamba kasema kwamba tumewalipia IPTL 20 Million USD kwa mwaka bila hata kuproduce umeme kwa sekunde moja, lakini great thinkers hawataki kujadili hoja, ila mtoa hoja. Amongst other things.

This is some place.
 
Hoja nzito kutoka kwa upinzani tu ndio zinazojadiliwa humu ndani. Ingawa huyu kijana wa Makamba kasema kwamba tumewalipia IPTL 20 Million USD kwa mwaka bila hata kuproduce umeme kwa sekunde moja, lakini great thinkers hawataki kujadili hoja, ila mtoa hoja. Amongst other things.

This is some place.

Ukiumwa na nyoka hata ukiona kamba unashtuka. Wengi hatuamini labda kuna mchezo nyuma yake kama ilivyo CCM! Ni nyoka kubadili magamba .....Kikwete Feb 5 2011 DODOMA
 
Selemani said:
Hoja nzito kutoka kwa upinzani tu ndio zinazojadiliwa humu ndani. Ingawa huyu kijana wa Makamba kasema kwamba tumewalipia IPTL 20 Million USD kwa mwaka bila hata kuproduce umeme kwa sekunde moja, lakini great thinkers hawataki kujadili hoja, ila mtoa hoja. Amongst other things.

This is some place.

Selemani,

..huyo kijana wa Makamba anapenda kuandika-andika.

..if he really means business aitishe press conference na kuwatoa nishai makada wenzake wa chama.

..halafu barua yenyewe kaandika kwa lugha ya KUBEMBELEZA utafikiri anamuandikia ...
 
Mimi akili yangu inanipeleka kuamini kwamba hii ni mbinu madhubuti ambayo inataka kutumika kushusha habari mbaya kwa wananchi na watu wengine kubebeshwa mzigo. Haikai kabisa akilini. Ila lazima nikubali kama ipo kama ambavyo nahisi basi wameamua geuza hili suala zima kuwa kama mchezo wa 'Chess'.

All in all it is a very smart move ambayo mwisho wa siku itatufanya Watanzania wa chini kama mimi na wewe tubaki tunalaumiana wenyewe... Jambo la msingi zaidi hapa ilikuwa ni watendaji waliovurunda kuwajibishwa kabla ya mambo mengine. Naungana na Ng'wanangwa kusema hii ni 'real smart crap.'
 
what makes it being crap?
Unataka mpaka CDM wakisema ndio manakubali?
tunapingana kwa hoja sio chuki binafisi zisizoweza kujenga nchi yetu

kwel uyasemayo,lakini kwa hali ilivo sasa inakuwa ngumu kuwaamin wabunge wa chama tawala na watendaj wake,c umeona uvccm walivyosh2kiwa?binafsi naona hakutakuwa na jipya,january makamba anapayuka tu,kwni ni nani alosaini IPTL?kwani sakata la dowanz halielewek?rais anajua kuwa richmond waz a ghost but leo anakubali dowanz,so ngeleja afanyeje?kumpelekea barua ndo kutafanyaje?mi nilipoisoma hbr ya january,nikaona ni porojo tu,tambua kuwa hakuna mbunge atakaeikosoa au kuihoj serikali toka chama tawala,weng wataunga mkono hoja kabla ya kuchangia kwa % zote,waikosoe wakose ulaji?
 
Hoja nzito kutoka kwa upinzani tu ndio zinazojadiliwa humu ndani. Ingawa huyu kijana wa Makamba kasema kwamba tumewalipia IPTL 20 Million USD kwa mwaka bila hata kuproduce umeme kwa sekunde moja, lakini great thinkers hawataki kujadili hoja, ila mtoa hoja. Amongst other things.

This is some place.

Selemeni, na wewe upo hapa; jadili au unataka kina nani wajadili? Maana wengine wakianza kujadili haichelewi kuonekana wanapinga tu! Kama unaona kuna hoja ijadili, ichambue, iongeze nguvu n.k Usisubiri wengine hapa kufanya hivyo...
 
Wanjaribu kuondoa attension yetu kwenye mambo mengine..........Hakuna lolote.........like father like son
 
Nimeisoma barua nzima na kuipitia kwa makini nina mambo mawili tu ya kusema "nice try" na la pili "try again". I'm impressed though na jaribio lenyewe lilivyo. Sidhani kama kuna lolote ambalo limesemwa ambalo lilikuwa halijulikani tayari. Ninachojaribu kutafutia majibu ni kuelewa tu:

a. Kwanini amemuandikiwa Waziri kutaka maelezo tu (fungu la mwisho la barua linatoa jibu) ila nimejiuliza tu tena.

b. Kwanini anafikiri jukumu lake kama mbunge ni kushauri na "kuomba" serikali?

c. Hajaeleza yeye mwenyewe hisia zake kuhusu masuala hayo ziko vipi; kwa mfano serikali ikitoa maelezo ya kina ya majibu yake na wananchi wakajua then what? kwa mfano serikali ikianza kuzungumza kwa kauli moja (wasipopingana) itakuwa imeondoa tatizo lake la serikali kugongana katika kutoa misimamo?

d. Maswali ambayo hakutaka kuyauliza: uhalali wa Dowans na malipo yake, uhalali wa mkataba wa Dowans, uongozi wa serikali katika suala zima; maana inaonekana kama analaumu serikali kutengeneza "perception" ya kutokuweza. Kwamba majibu ya serikali kwa barua hiyo yatasaidia kuwaelewesha Watanzania juu ya nini kinachoendelea. Kama mwandishi anavyosema:

Dhamira yangu ni kutaka kueleweka katika kile ninachokusudia katika kuandika barua hii, ambacho kwanza ni kutoa ushauri, kama wajibu wangu wa Ubunge unavyonitaka na pili ni kutoa ombi kwa Serikali kupitia kwako. Ninachoomba ni kwamba wananchi nao, kupitia Taarifa rasmi ya Serikali Bungeni, wapatiwe fursa ya kuzijua kwa kina changamoto hizi katika sekta ya nishati na jinsi Serikali inavyozishughulikia ili imani yao kuhusu uwezo wa Serikali yao kulishughulikia tatizo la umeme nchini isizidi kuporomoka. Naamini kwamba kwa taarifa hii, tutafungua ukurasa mpya kwa kuondoa siasa kwenye maamuzi na mijadala inayohusu sekta hii na kuweka uwazi kwenye mwenendo mzima wa uendeshaji wa sekta ya nishati, ikiwemo mikataba ya uzalishaji wa umeme.

Naamini angeweza kwenda mbali (labda anapanga kwenda mbali huko mbele) lakini barua haitudokezi hilo. Nice try, but try again buddy! One can not be blamed for attempting..
 
Mh. January Makamba, kwenye hili nakupa kudos bila kujali dhamira yako ni ipi au mchezo gani unachezwa. Kwa ufupi umemtaka Ngeleja aeleze bungeni huu upumbavu wa mgao utaisha lini TZ?? Kwa nini kugenerate extra 500MW inakuwa kama ni suala gumu wakati ni kitu kiko ndani ya uwezo wa serikali??

Ngeleja akieleza bungeni itawapa wabunge nafasi ya kumhoji na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike.

Issue kubwa TZ ni kuondoa MGAO PERIOD. Lazima tununue mitambo ya gas 250MW Wartsila na 250MW GE, mwaka huu 2011 ili itakapokuja online by say mid 2012, tuwe na miaka angalau 10 ijayo bila kudeal na mgao.

At the same time hoja za kutolipa dowans nk nazo ziendelee, lakini mgao lazima iwe history TZ in the next 12 months otherwise serikali na sisi wananchi wote tuitwe WAJINGA na tuwe proud na ujinga wetu.
 
Back
Top Bottom