Kiingereza kinampa shida mkuu wa mkoa Arusha, aogopa mikutano ya kimataifa

mpinga shetani

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
3,236
954
Imebainika kuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo, anakiogopa sana kiingereza kiasi cha kujitahidi kuiepuka mikutano mingi ya kimataifa inayofanyika mjini Arusha.

Mkuu huyo amekuwa akipata shida sana kusoma speech alizoandikiwa kwa lugha hiyo ngeni katika baadhi ya mikutano aliyoalikwa kuifungua na hivi sasa ameamua kuikacha jumla.

Hakuna dhambi kwa kiongozi kutojua lugha ya malkia lakini mtu akipewa eneo la kimataifa kama Arusha kigezo hicho kwa kweli ni muhimu maana kuna taasisi nyingi za kigeni hapa hii ikiwa ni pamoja na jiji kuwa mwenyeji wa mikutano mingi ya kimataifa.

Lakini watu wake wa karibu wanasema suala si kiingereza tu. Hata kusoma speech ya kiswahili kwa mtiririko ulio tulia huwa ni taabu kwake.

Hata hivyo Mulongo ambaye inadaiwa aliletwa mkoani hapa maalum kuja kumdhibiti mbunge wa Monduli anatekeleza jukumu hili kwa ufasaha ila kama atashinda ndicho hakijulikani.

Ki utendaji pia Mulongo ni mzuri kwani amefanikiwa kuwatimua maofisa wala rushwa na watendaji hovyo katika taasisi na ofisi za umma mkoani hapa. Hii ni pamoja na madai kuwa amekuwa akifanya hivyo kisiasa zaidi.
 
kikazi nimemkubali,juzi kati alileta jamba jamba pale mt.meru hospital pakabadilika.hilo la lugha ngoja tusubiri wanaomjua wa comment
 
Haaaa can somebody guess,eh which which eh,what globale womingi was? Ok ubah eh it it it iz it iz,ok kwa kiswahili!
 
Kama aliyemteua ni walewale wa to manufacture teachers what can u expect from him??soon worms will feast in their hollows!
 
Dah!! Mkuu wa mkoa unalo ndugu yangu,
anyway endelea kupiga kazi kwani wengi wanaojua hivi viingereza ndio wameendelea kutuletea mabalaa na matatizo mengi, ona migomo ya madaktar sasa wasio hatia wanakufa,
we inshu ya kizungu isikupe taabu sana hata kiswahili piga mbele zao ,watataka tu,
 
Kisheria Tanzania inatambua Kiswhahili na Kiingereza kuwa lugha rasmi.Kwa Mkuu wa Mkoa anatakiwa awe na mkalimani ,by the way pale Arusha International Conference Center si pana vifaa ambavyo vinatafisiri lugha nyingine?
 
Hana haja ya kujisumbua na kingereza bwana piga kiswahili au kijita tu watatafsiri wenyewe huko.
 
Imebainika kuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo, anakiogopa sana kiingereza kiasi cha kujitahidi kuiepuka mikutano mingi ya kimataifa inayofanyika mjini Arusha.

Mkuu huyo amekuwa akipata shida sana kusoma speech alizoandikiwa kwa lugha hiyo ngeni katika baadhi ya mikutano aliyoalikwa kuifungua na hivi sasa ameamua kuikacha jumla.

Hakuna dhambi kwa kiongozi kutojua lugha ya malkia lakini mtu akipewa eneo la kimataifa kama Arusha kigezo hicho kwa kweli ni muhimu maana kuna taasisi nyingi za kigeni hapa hii ikiwa ni pamoja na jiji kuwa mwenyeji wa mikutano mingi ya kimataifa.

Lakini watu wake wa karibu wanasema suala si kiingereza tu. Hata kusoma speech ya kiswahili kwa mtiririko ulio tulia huwa ni taabu kwake.

Hata hivyo Mulongo ambaye inadaiwa aliletwa mkoani hapa maalum kuja kumdhibiti mbunge wa Monduli anatekeleza jukumu hili kwa ufasaha ila kama atashinda ndicho hakijulikani.

Ki utendaji pia Mulongo ni mzuri kwani amefanikiwa kuwatimua maofisa wala rushwa na watendaji hovyo katika taasisi na ofisi za umma mkoani hapa. Hii ni pamoja na madai kuwa amekuwa akifanya hivyo kisiasa zaidi.
Simtetei lakini siamini, labda mtoa mada atusaidie kwa kutuambia kwamba ni mkutano gani, ulifanyika lini na ulihusu nini ili tufuatilie video pale IACC ili tuzione na tuthibitishe hilo.
Kwa kuwa bongo siasa kila sehemu tunaweza tukajikuta kwenye mtege wa maadui zake ikumbukwe kwamba kuwa mkuu wa mkoa sio single nyepesi hivyo majungu yanaweza kuwa ni mtaji rasmi.
 
Back
Top Bottom