Kiingereza cha kiTanzania

Ladslaus Modest

JF-Expert Member
Jun 27, 2008
635
20
Kiingereza cha kiTanzania

Wapendwa wana JF na wale wote wenye mapenzi mema na nchi yetu Tanzania; hapa ulimwenguni katika nchi zote zilizotawaliwa na mwingereza takriban kila moja ina kiingereza chake mfano kuna kiingereza cha Australia, Belize, Canada, Caribbean, Hong-Kong-S.A.R., India, Indonesia, Ireland, Jamaica, Malaysia, New-Zealand, Philippines, Nigeria, Singapore, South-Africa, Trinidad-&-Tobago, UK ,US, na Zimbabwe.

Ukifuatilia kwa makini kila nchi iliyotajwa hapo imeongeza au imepunguza au imebadili neno au herufi fulani kutoka kwenye kiingereza cha asili cha Uingereza.

Mfano Mwingereza anatumia neno POST CODE lakini mMarekani anatumia neno hilo hilo kama ZIP CODE

Kinachosikitisha ni kwamba sie waTanzania tunatumia either American English or British English.

Kuna maneno mengi ambayo wataalam wa lugha mnayafahamu (mie sio mtaalamu wa lugha bali ni Mchungaji) ambayo mnaweza kuyabainisha hapa ili tuweze kuwa na kiingereza chetu cha kiTanzania.

Mie nilikuwa ninapendekeza tuanzie hapa: - Badala ya kumuita baba mkubwa na/au baba mdogo UNCLE tuwe tunawaita ELDER FATHER na YOUNGER FATHER. Badala ya kumuita mama mkubwa na/au mama mdogo AUNT tuwe tunawaita ELDER MOTHER na YOUNGER MOTHER ... ... ... nakadhalika.

Naomba kuwasilisha.
 
Ur funny, young mother, sasa na mama aliyezaa akiwa na umri mdogo ataitwaje?

Hicho si Kiingereza cha Kitanzania, ni Kiswahili katika maneno ya Kiingereza.
 
Mie nilikuwa ninapendekeza tuanzie hapa: - Badala ya kumuita baba mkubwa na/au baba mdogo UNCLE tuwe tunawaita ELDER FATHER na YOUNG FATHER. Badala ya kumuita mama mkubwa na/au mama mdogo AUNT tuwe tunawaita ELDER MOTHER na YOUNG MOTHER ... ... ... nakadhalika.

Tukiwa kwenye kuelimishana, it is "Younger" not "Young"
 
Kiingereza cha kiTanzania

Wapendwa wana JF na wale wote wenye mapenzi mema na nchi yetu Tanzania; hapa ulimwenguni katika nchi zote zilizotawaliwa na mwingereza takriban kila moja ina kiingereza chake mfano kuna kiingereza cha Australia, Belize, Canada, Caribbean, Hong-Kong-S.A.R., India, Indonesia, Ireland, Jamaica, Malaysia, New-Zealand, Philippines, Nigeria, Singapore, South-Africa, Trinidad-&-Tobago, UK ,US, na Zimbabwe.

Ukifuatilia kwa makini kila nchi iliyotajwa hapo imeongeza au imepunguza au imebadili neno au herufi fulani kutoka kwenye kiingereza cha asili cha Uingereza.

Mfano Mwingereza anatumia neno POST CODE lakini mMarekani anatumia neno hilo hilo kama ZIP CODE

Kinachosikitisha ni kwamba sie waTanzania tunatumia either American English or British English.

Kuna maneno mengi ambayo wataalam wa lugha mnayafahamu (mie sio mtaalamu wa lugha bali ni Mchungaji) ambayo mnaweza kuyabainisha hapa ili tuweze kuwa na kiingereza chetu cha kiTanzania.

Mie nilikuwa ninapendekeza tuanzie hapa: - Badala ya kumuita baba mkubwa na/au baba mdogo UNCLE tuwe tunawaita ELDER FATHER na YOUNGER FATHER. Badala ya kumuita mama mkubwa na/au mama mdogo AUNT tuwe tunawaita ELDER MOTHER na YOUNGER MOTHER ... ... ... nakadhalika.

Naomba kuwasilisha.

Ladislaus,
Its very interesting topic, ila umeweka mada mbili, moja nikutaka kufahamu kama kuna maneno ya kiingereza cha kitanzania so kama yapo ni yapi????

Pili umepropose kutohoa maneno ya kiswahili kuwa kiingereza ama kutranslate swhili words to English as you have proposed two words.

Maoni yangu, kwanza kabisa pronounciation yetu inatutambulisha sisi kama watanzania mfano wa neno Determine (sisi tunasema ditamain badala ya ditamin, kuna maneno kama cafee, .....
 
kuna advert moja itv ya chuo kimoja called Gold.... something .. mtangazaji huyu sijui vipi .. mambo mengine yote anayasoma uzuri mathalan certificate for ..... mpaka mwisho kashese inakuja pale anaposema "wraiten" instead of written .. english .. naona aibu kama nimesema mm.
 
Sisi english sio first language kwetu Tanzania kwa hiyo ni vigumu kusema english ya Tz .Nchi wanaotumia english kama lugha yao ya kwanza kweli wantofautia vitu fulani kiwemo hata matamushi .Kama vile kiswahili cha Kenya ,Tanzania na pia ndani ya Tanzania Pwani kiasi fulani wanatofautiana na bara.
Sisi hatuna english yetu tunakopa na kutumia kama ilivyo ,wengi bongo wantumia english ya Uk ,na siku za karibuni american english kwa kuwa kunawatu wametokea kuishi US na kusikiliza american english kupitia movie na songs.

Unachoweza kusema ni kuwa uncle na aunt kwenye kiswahili tunatofautisha kama mjomba na shangazi tu ,na english wanaendelea kujumuisha baba mdogo na mkubwa kama uncle na mama mdogo na mkubwa.Na ukitaka hivyo sidhani kama kwenye kiswahili tuna nephew and neice.
Nikutumia tu english kulikana na sehemu unapokuwa kama US ,UK ,kukijichanga kwa Jamaica ukutnane na patois kazi unayo.
 
Tukiamua kuwa na Kiingereza chetu (Mmmh!) tutakuwa tunachangia kuharibu lugha ya wenyewe, kwani lugha si maneno tu bali hata utamaduni wa lugha husika unajumuishwa. Muhimu ni kuimarisha lugha yetu.

Hivi sasa tunaiharibu lugha yetu kwa kuichanganya na lugha nyingine za Kimagharibi, hasa Kiingereza. Kwa mfano, badala ya kutafuta neno sahihi la Kisw. la kutumia, mtu anasema: "Leo nimeboreka (akimaanisha I'm bored) sana!". Msemaji km huyu anaonesha manung'uniko, lkn anachosema, kikitafsiriwa kwa Kisw. si manung'uniko -- kwani kuboreka maana yake ni kuwa bora! Km tunavyoiharibu lugha yetu, ndivyo vivo hivyo tutachangia kuharibu za wengine.
 
Huku pwani ambako ni chimbuko la Kiswahili, dada hasa ni ndugu mkubwa wa kike, na kaka ni ndugu mkubwa wa kiume. K/sbb ya kuiga lugha na utamaduni wa Kiingereza, hata mdogo wangu (wa kike) ni dadangu, na mdogo wangu wa kiume naye ni kakangu!
 
Huwezi kusema,Younger Father,kwa sababu Younger Father inayo precise meaning. Kama watu wawili,wote ni fathers,na mmoja ni younger,basi yeye ni Younger Father. Kwa hiyo,hizi suggestion zako haziwezi kukubalika to the subconcious mind ambayo inachukua kila kitu very literally.
 
Niliwahi kuomba passport ya Tanzania. Katika sehemu ya Emergency contact niliandika jina la baba mdogo na sehemu ya uhusiano na mwombaji niliandika " baba mdogo" . Wakati nilipopata passport ilitafsiriwa kama: young father ...story ya mwaka 1992 approx.
 
Huku pwani ambako ni chimbuko la Kiswahili, dada hasa ni ndugu mkubwa wa kike, na kaka ni ndugu mkubwa wa kiume. K/sbb ya kuiga lugha na utamaduni wa Kiingereza, hata mdogo wangu (wa kike) ni dadangu, na mdogo wangu wa kiume naye ni kakangu!

Sidhani kama ni utamaduni wa kiingereza. Kwa waswahili, Dada ni 'ndugu wa kike' na Kaka ni 'ndugu wa kiume' bila kujali umri wao. Tizama kamusi zote za kiswahili, hasa zile zilizoandikwa zamani utaliona hili. Kwa asili neno 'ndugu' ni mtu ambaye mmechangia baba na/au mama. Kwa hivi ukimtambulisha mtu kwamba ni nduguyo, moja kwa moja mtu anajua huyo ni dada yako au kaka yako.
 
Sidhani kama ni utamaduni wa kiingereza. Kwa waswahili, Dada ni 'ndugu wa kike' na Kaka ni 'ndugu wa kiume' bila kujali umri wao. Tizama kamusi zote za kiswahili, hasa zile zilizoandikwa zamani utaliona hili. Kwa asili neno 'ndugu' ni mtu ambaye mmechangia baba na/au mama. Kwa hivi ukimtambulisha mtu kwamba ni nduguyo, moja kwa moja mtu anajua huyo ni dada yako au kaka yako.

Jaribu kuulizia kwa wazee wa pwani (hasa Kimtang'ata) khs tofauti kati ya "kaka/dada" na "mdogo" (eg wangu).
 
Sidhani kama ni utamaduni wa kiingereza. Kwa waswahili, Dada ni 'ndugu wa kike' na Kaka ni 'ndugu wa kiume' bila kujali umri wao. Tizama kamusi zote za kiswahili, hasa zile zilizoandikwa zamani utaliona hili. Kwa asili neno 'ndugu' ni mtu ambaye mmechangia baba na/au mama. Kwa hivi ukimtambulisha mtu kwamba ni nduguyo, moja kwa moja mtu anajua huyo ni dada yako au kaka yako.

Kizungu kimekuharibu!!!!!!!
 
Ha Ha ha kaka mi naiunga mkono hoja yako kimsingi hayo maneno yamekaa vibaya. Kwa kuwa shangazi anaitwa Aunt na Mjomba anaitwa Uncle nadhani nivema kumtofautisha baba mkubwa na mdogo vile vile mama mkubwa na mdogo.

Hii ni mada muhimu naomba wataalam wa lugha watusaidie si jambo la kupuuza.

cheers
 
Daaa!!!hapo umenipa mwanga maana nilijua ndugu ni jamaa yako,awe mtoto wa baba mdogo,mjomba au hata mliyetoka naye ukoo mmoja
 
Lugha yoyote mpaka ikaitwa ni lahaja ya sehemu fulani, lugha hiyo ama lahaja hiyo hujitengeneza yenyewe kutoka kwa wazungumzaji na si kwa kupanga kwamba waTanzania tuwe na kiingereza chetu tofauti na kungine. hata sasa kiingereza chetu(waTanzania tulio wengi) ni tofauti na wengine. hivyo tungoje ijitengeneze yenyewe.

Vilevile maneno ya BabaMdogo BabaMkubwa ama Shangazi, Mjomba. huu ni mfumo wa kiswahili si lazima mfumo huu utumike kwenye lugha nyingine. Kama kuna lazima kutofautisha basi ni bora utumie hivyohivyo BabaMdogo hata kwenye Kiingereza.
 
Back
Top Bottom