Le Grand Alexei
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 116
- 83
Wakati tukienda mitamboni nimepata habari kuwa Kigwangalla akiwahutubia wananchi wa Nzega leo jioni ametangaza kuwa na ndoto za kuwania Urais 2025! Alisema:
'Kwa hakika dunia inakuwa mahala. Pabaya pa kuishi si kwa sababu ya watau wabaya bali kwa sababu ya ukimya wa watu wazuri..watu safi na wazuri kama mimi, japokuwa tuko wachache, ni lazima tujipange na tusimame imara kuutafuta uongozi wa nchi yetu la sivyo kundi kubwa la watu wabaya litatutawala na tutabaki tukisaga meno - wanaodhani watanitoa ubunge kirahisi wanaota ndoto za fisi, wanasubiri nyuma ya mtembea kwa miguu wakidhani atadondosha mkono, sina mpango wa kuachia ubunge hata kidogo, wajiandae kupambana na mimi ndani ya chama na hata wale wa upinzani na nina hakika nitawashinda tu, maana safari hii haikomi mpaka 2025 nitakapogombea Urais'
Alitoa kauli hiyo huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wapiga kura wake. Sikuwahi kujua kama huyu dogo anapendwa na watu wake namna hii!! Wamemshangilia mpaka nikaogopa. Anaongea kwa kujiamini sana kiasi cha kumuaminisha kila anayemsikiliza
'Kwa hakika dunia inakuwa mahala. Pabaya pa kuishi si kwa sababu ya watau wabaya bali kwa sababu ya ukimya wa watu wazuri..watu safi na wazuri kama mimi, japokuwa tuko wachache, ni lazima tujipange na tusimame imara kuutafuta uongozi wa nchi yetu la sivyo kundi kubwa la watu wabaya litatutawala na tutabaki tukisaga meno - wanaodhani watanitoa ubunge kirahisi wanaota ndoto za fisi, wanasubiri nyuma ya mtembea kwa miguu wakidhani atadondosha mkono, sina mpango wa kuachia ubunge hata kidogo, wajiandae kupambana na mimi ndani ya chama na hata wale wa upinzani na nina hakika nitawashinda tu, maana safari hii haikomi mpaka 2025 nitakapogombea Urais'
Alitoa kauli hiyo huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wapiga kura wake. Sikuwahi kujua kama huyu dogo anapendwa na watu wake namna hii!! Wamemshangilia mpaka nikaogopa. Anaongea kwa kujiamini sana kiasi cha kumuaminisha kila anayemsikiliza