Kigwangalla ampiga vijembe Bashe baada ya kumshinda uchaguzi wilayani Nzega

mh dr H Kigwangalla, nakupongeza kwa kunitomeza na kujibu baadhi ya hoja hapa jamvini. KEEP IT UP, natamani na vijana wenzio huko katika ccm ( mwigulu nchemba, january, bashe, lusinde 'kibajaji')wataiga huu mfano wako mzuri.
MH, kuna siku ililetwa habari hapa kuwa umekamatwa nzega ukigawa rushwa ya vitumbua na tsh 2000 kwa wajumbe, tulikusubiri sana hapa jf uje uthibitishe au kukanusha KIMYA!
na mpaka leo hatuujui ukweli ni upI mkuu,,
kwa kuwa leo upo hapa naomba ufafanuzi wako
Niliandika status kwenye FB wall yangu, kwenye twitter, wanabidii na mabadiliko forums, na nilikanusha hilo, maana halikuwepo...sijawahi kukamatwa bali ilikuwa kinyume chake na kwamba waliofanya hivyo walikuwa wana-plot kunichafua ili wasababishe nisiteuliwe na Chama kugombea nafasi ya NEC kupitia Nzega (na wamefanikiwa, hongera zao). Namshukuru Mungu ka-bajeti nilikokuwa nikatumie kwa ajili ya kampeni yangu kwenye NEC nimekatumia kwa mambo mengine, na nimewashinda kwenye uenyekiti, uNEC, Uenezi n.k. Kama nilikamatwa waulize hao wenye magazeti kwa nini hawakupiga picha matukio hayo - kwanza la kugawa vitumbua na mbili la kukamatwa na PCCB? waambie waweke hapa kama ni hadithi za ukweli. Mimi niliishaga acha kuyaamini magazeti 100% siku nyingi sana, huwa nawapa 60% tu!
 

AND FINALLY... Kakimbia... Hawezi kugawa tena VITUMBUA !!!
nikimbie hoja gani sasa hizi blah blah zenu mnazofanya kuwa-please waliowanunulia gadgets? Hamna hoja za saizi yangu hapa nimepoteza muda kiasi cha kutosha tu
 
Hivi ndiyo alivyoandika kwenye ukurasa wake wa FaceBook:--

"Hamisi Kigwangalla


4 hours ago




"Uchaguzi Mkuu wa CCM Wilaya ya Nzega umemalizika salama na tumepata viongozi mahiri. Ni imani yangu tukiwapa ushirikiano wa kutosha CCM sasa itakuwa moja, imara na yenye kusonga mbele. Hongereni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Nzega kwa kung'oa kwa kiasi kikubwa vigogo na waasisi wa siasa za ufuasi na wenye kufanya siasa za kumridhisha mtu mmoja tu, pia kwa kuwakwamisha wengi wa wafuasi wa siasa hizo na kuingiza majembe ya ukweli! Mmedhihirisha pesa peke yake si kigezo cha kushinda uchaguzi, mmefanya kweli. Nawashukuruni nyote kwa kufuata na kutumia ushauri wangu kwamba tujenge CCM moja imara, kusiwe na watu wa Kigwangalla na wala wa Selelii, kuwe na wanaCCM wamoja...mlinipa faraja ya ushindi na pale mliponibeba juu juu niliogopa kwamba msije mkawa mmedhamiria kwenda kunitupa, ila nakushukuruni sana hamkufanya hivyo badala yake mlishukuru kwa ushauri wangu..."

"Mara baada ya fununu za matokeo ya uchaguzi kuwa wazi kuna watu wawili maarufu walizimia, na walipozinduka waliangua vilio na hawajaonekana Nzega tena...tunawapa pole na kuwatakia quick recovery huko waliko! Huo ndiyo ushindani...na sisi tunawaambia kuwa wasihofu kitu watatendewa haki siku zote katika chama hiki na katika uongozi huu. Malengo yetu ilikuwa ni kuondoa watu wa hovyo, wachumia tumbo na wanaofanya kazi kwa maelekezo ya mtu mmoja tu na sasa kuweka watu makini na mahiri watakaokisimamisha chama, hata kama itamaanisha kuniadhibu mimi pale itakapobidi...Chama Kwanza, Mtu baadaye! Hakuna mtu maarufu na wa maana ndani ya CCM kuliko CCM yenyewe. Nimesikia wanataka kuikimbia nchi, tunawasihi wasifanye hivyo, waendelee tu kuwa waadilifu na waaminifu kwa chama na kwa nchi na ipo siku mambo yao yatawanyookea tu!"



kichwa cha hii habari hakijakaa vizuri...
 
Inasikitisha sana kumuona mtu anayeitwa Mh Mbunge akijibizana kwa stahili hii. Mkuu, kuna stahili ya kujibu hoja, hoja hazijibiwi kimipasho mipasho hivi. Hapa sasa naanza kuamini kuwa tunaoimaliza CCM ni sisi wenyewe!
 
mmezoea udaku sasa dr kigwa yuko hapa mwenyewe ukiweka ugoko anaweka jiwe kudadadeki. JF ni ya ukweli sana .unaleta umbea unashtukia mwenyewe huyu hapa unaanza kula za uso
 
asante kwa majibu na ufafanuzi,wengine facebook tulihama siku nyingi ,tunaomba kama kuna taarifa za ufafanuzi uwe unatukumbuka hapa JF. labda hili moja la mis
2: una maoni gani kuhusu kuhusishwa kukatwa majina ya baadhi ya wagombea u nec ccm na kusaini kwao fomu ya kumng'oa mh waziri mkuu pinda?
1: una maoni gani na huu utaratibu (katabia) ka baadhi ya wenye nia kugombea/kutetea uongozi 2015 kupitia ccm kupanga safu yao ya viongozi wa kuwasafishia njia ktk ngazi ya wilaya? do you think this is HEALTHY to your party chama cha mapindizi?
 
Inasikitisha sana kumuona mtu anayeitwa Mh Mbunge akijibizana kwa stahili hii. Mkuu, kuna stahili ya kujibu hoja, hoja hazijibiwi kimipasho mipasho hivi. Hapa sasa naanza kuamini kuwa tunaoimaliza CCM ni sisi wenyewe!

Acha pumba na wewe .. angenyamaza hapa si mngeamini? Kwani dk na yeye si binadam kama wewe hapo . Dr mtu akiweka mguu wewe weka jiwe hivyo hivyo tuone kama wataendelea kukuzushia hapa.
 
Nakutakia siasa njema ,usikate tamaa kwani maadui katika siasa ni wengi na marafiki pia ni wengi, chukulia vyote kama changamoto.
 
ila dr kigwa we noma yani wananchi wako unawapa vitumbua elfu mbili hahaha...si bora ungegawa kofia sasa hivyo vitumbua wangeharisha si ungedakwa kwa kesi
 
Acha pumba na wewe .. angenyamaza hapa si mngeamini? Kwani dk na yeye si binadam kama wewe hapo . Dr mtu akiweka mguu wewe weka jiwe hivyo hivyo tuone kama wataendelea kukuzushia hapa.
Kuna namna ya kujibu hoja, siyo kwa stahili hii. Mbaya zaidi anajibizana na watu asiowafahamu!!!


Sent from my BlackBerry 9810 using JamiiForums
 
Dr. Hamisi Kigwangalla said:
  • Mara baada ya fununu za matokeo ya uchaguzi kuwa wazi kuna watu wawili maarufu walizimia, na walipozinduka waliangua vilio na hawajaonekana Nzega tena...!
  • Nimesikia wanataka kuikimbia nchi, tunawasihi wasifanye hivyo, waendelee tu kuwa waadilifu na waaminifu kwa chama...!
  • Malengo yetu ilikuwa ni kuondoa watu wa hovyo, wachumia tumbo na wanaofanya kazi kwa maelekezo ya mtu mmoja tu...!
Kigwangalla kaongea vizuri sijaona vijembe vyovyote.
Chama said:
...ameongea kama msomi na mwenye dira ya kukitakia chama mema, wengi mnasema vibaya kwa sababu mnachotaka ni migongano ndani ya CCM kwa faida yenu, BIG UP DR.Kigwangalla
Halafu kuna watu wanasema tunataka viongozi vijana... kadizooo!!!
Halafu kuna watu wanasema tunataka viongozi wasomi vijana...kaazi kweli kweli!
 
Naona mmjipanga vijana wa aliyewatuma hapa kwa kazi moja tu, kunichafua, kisa nini mmepewa Ipad za bure...bahati mbaya sana aliyewapeni hizo gadgets amekula hasara maana nyote mmejaa fallacy, hamna hoja na wala uwezo wa kujifunza chochote kwa kuwa na access na information kupitia vyombo hivyo... tatizo la JF ni hilo watu mnajificha nyuma ya alias

Dk inabidi utuombe msamaha sisi tuko hapa kuweka mambo sawa na hakuna aliyepewa i pad hapa wengine tupo JF toka mwaka 2006 i pad hata hazikuwepo kipindi hiko so usituchafukie majina hapa wewe tulia upewe ukweli wako kama ni kweli uligawa vitumbua
 
nikimbie hoja gani sasa hizi blah blah zenu mnazofanya kuwa-please waliowanunulia gadgets? Hamna hoja za saizi yangu hapa nimepoteza muda kiasi cha kutosha tu


Kaka tulia angalia NYUMA anza UPYA unakwenda MBIO sana KISIASA na hautakuwa hauna

maana mbeleni kama hautajirekebisha, ulianza kwa kasi NCHI yetu UFISADI una MIZIZI wewe

Mwenyewe hauwezi kuiondoa
Unatakiwa UWE Na UNYENYEKEVU na sio kujilimbikizia

MADARAKA UBUNGE ULITOSHA sio na U NEC PIA TULIZANA ANZA UPYA sasa hivi kweli

Una Maadui Wengi zaidi ya Marafiki lakini kazi njema itakurudishia MARAFIKI na NEEMA...

THERE IS ALWAYS SILVER LINING IN THE SKY !!!
 
Kuna namna ya kujibu hoja, siyo kwa stahili hii. Mbaya zaidi anajibizana na watu asiowafahamu!!!


Sent from my BlackBerry 9810 using JamiiForums

Rejao unachoongea ni sawa ila kuna muda inabidi tu afanane na hao anaowajibu kwa muda ili kuweza kuwajibu inavyotakiwa . mfano kaambiwa hapo kuwa "kakimbia jukwaa na hawezi kugawa tena vitumbua" so swali kama hilo ama kebehi kama hio angajibu nini? Ni kuipotezea ama kuivaa hivyo hivyo so jamaa hana kosa . Ila mwambie awe anagawa hata vitu vya ukweli kisela sio mavitumbua bhana.
 

Kaka tulia angalia NYUMA anza UPYA unakwenda MBIO sana KISIASA na hautakuwa hauna

maana mbeleni kama hautajirekebisha, ulianza kwa kasi NCHI yetu UFISADI una MIZIZI wewe

Mwenyewe hauwezi kuiondoa
Unatakiwa UWE Na UNYENYEKEVU na sio kujilimbikizia

MADARAKA UBUNGE ULITOSHA sio na U NEC PIA TULIZANA ANZA UPYA sasa hivi kweli

Una Maadui Wengi zaidi ya Marafiki lakini kazi njema itakurudishia MARAFIKI na NEEMA...

THERE IS ALWAYS SILVER LINING IN THE SKY !!!
Nimefuatilia posts zako na naona lazima kuna kitu baina yenu wawili. Haiwezekani umshambulie HKigwangalla kiasi hiki bila sababu yoyote. Labda mkuu ungetuweka wazi ili na sisi tuwe kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuchangia kwenye bifu lenu.
 
Last edited by a moderator:
Rejao unachoongea ni sawa ila kuna muda inabidi tu afanane na hao anaowajibu kwa muda ili kuweza kuwajibu inavyotakiwa . mfano kaambiwa hapo kuwa "kakimbia jukwaa na hawezi kugawa tena vitumbua" so swali kama hilo ama kebehi kama hio angajibu nini? Ni kuipotezea ama kuivaa hivyo hivyo so jamaa hana kosa . Ila mwambie awe anagawa hata vitu vya ukweli kisela sio mavitumbua bhana.
Ha ha ha hahahahaah Saint Ivuga, naona hapo kwenye vitumbua umepakomalia sana.
 
Last edited by a moderator:
Nimefuatilia posts zako na naona lazima kuna kitu baina yenu wawili. Haiwezekani umshambulie HKigwangalla kiasi hiki bila sababu yoyote. Labda mkuu ungetuweka wazi ili na sisi tuwe kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuchangia kwenye bifu lenu.

Sina Beef na yeye hata kidogo; Ninapenda SIASA nafuatilia SIASA za Tanzania... na kuna VIJANA

wengi
Wanaovutia kwenye SIASA za Tanzania; lakini kuna MAKOSA kuliko kunyamaza ni bora

kutoa constructive criticism;
Sio yeye tu... hadi NAPE PIA na Issue yake ya ile ya kuita 4MC C

stands for CHAGGA; kama UKabila; Kwanini
Vijana tuanza na Mambo ya UKABILA... Sasa kwa

Kigangwalla yuko kila Mahali; Simjui Mpinzani wake... Simuoni
Kila Mahali kama Kigangwalla...

ndio Maana nimeona nijaribu kumwuliza aangalie where he comes from and where he's


going... kwa MwanaSiasa hiyo ni BORA sio lazina niwe na BEEF naye... SIASA ni KAZI... it is a

lifetime...
 
Inasikitisha sana kumuona mtu anayeitwa Mh Mbunge akijibizana kwa stahili hii. Mkuu, kuna stahili ya kujibu hoja, hoja hazijibiwi kimipasho mipasho hivi. Hapa sasa naanza kuamini kuwa tunaoimaliza CCM ni sisi wenyewe!

mkuu,ulitaka ajibu vipi,?
mtu kuwa mbunge hakubadili utu wako na utashi,, mimi naamini wapo wabunge ccm wanaojibu kimipasho ( mfano;livingstone lusinde, mwigulu chemba) ila sio mh kigwangala !
mh kigwangala nakushauri utumie sana mitandao ya kijamii hasa jf, maana wewe humiliki magazeti na redio . huku ndiko utatendewa haki sawasawa na matendo.
 
Mipasho ni mipasho tu, hata hadija kopa husema ukweli

if our leaders wanaongea mipasho na sisi kuwashabikia, then we are lost dogs...........

Uongozi unaendana na utashi, heshima, na maarifa.... haijawahi kutokea popote mipasho ikawa na maarifa, utashi au heshima achilia mbali hekima

POLENI SANA

Pole jipe mwenyewe; mipasho ni tenzi na mashairi tu hakuna cha ajabu; ni mwandishi ndiye anayechagua lugha gani ya kutumia ya kiungwana au ya mitaani; alichongea Dr. Kigwangalla ni sahihi si lazima ukubaliane naye; lakini kwa sisi tunayoitakia CCM mema tupo naye 100%; huu ni wakati muafaka kwa kuangalia maslahi ya chama; hasa tukielekea kwenye uchaguzi wa 2015; haya ni maoni yangu mimi mwanaccm huru siwakilishi kundi lolote ndani ya CCM na wala sitegemei fadhila za CCM wala kiongozi wa CCM, silishwi; silipwi wala sitegemei ajira CCM wala serikali ya CCM, ninachotetea ni CCM imara ambayo itapigania maslahi ya watanzania wote. Nitamuunga mkono mwanaccm yeyote anayepigania kuunganisha nguvu ya Chama na kutetea maslahi ya watanzania

Chama
Gongo la mboto DSM.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom