Kigwangala Kadandia Treni kwa Mbele Hoja ya Kafulila

ludoking

Senior Member
Oct 5, 2008
124
71
Kama mdau nimefuatilia kwa makini mjadala wa bajeti ya Wizara ya Afya tangu iwasilishwe na Waziri. Nimeguswa na mchango wa mh Hamisi wakati anajibu hoja ya 'msingi' ya Mbunge wa Kigoma Kusini Mh Kafulila. Kimsingi naona Hamisi alichangia hoja hiyo kama "mwanamagamba' na siyo kama mteteaji wa watu wa Afya.

Kwa unyeti wa kazi za Wizara ya Afya kupewa 2% ya bajeti nzima si kitu ambacho Kigwangala ungesimama na kutetea. Nadhani Kigwangala anafahamu mambo mengi sana na kero nyingi sana za wadau wa Afya. Kama Mh Hamisi anakumbuka, Moja ya agenda katika mgomo wetu wa Interns wa mwaka 2005 pale Muhimbili (Tukiongozwa na kauli mbiu ya "kama noma na iwe noma") ilikuwa ni kukosekana kwa scheme of service ya Graduate nurses ambapo mpaka sasa bado wanaendelea kulipwa mshahara wa diploma nurse.

Kigwangala una mkumbuka yule bwana wa Physiotherapy pamoja na masters yake bado analipwa mshahara wa diploma sababu ikiwa ni kukosekana kwa scheme of service kwa kada hiyo. Hayo ni mambo ya msingi ambayo ungekomaa nayo bungeni. Kuendelea kudandia hoja za akina Kafulila, Tindu Lisu, Zitto zitaondoa mantiki ya wewe kuwepo hapo bungeni kama Daktari.

Namshukuru Mama Hilda Ngoyi kidogo jana aligusia vitu kama hivyo. Ni mbunge mmoja tu Dr Taarab ambaye katika Bunge la tisa alisismama kidete kutetea jambo hilo lakini wanamagamba wakawa wana mbeza.

Tuliambiwa na Wizara tutie Rasmi ambayo nidiyo imesaidia kubadilishwa kwa titles za Nurse pamoja na kuandaa scheme of services na salary scale ambayo iko katika Waraka mpya wa utumishi wa umma, lakini still watu bado wanalipwa kwa kukadiriwa.

Hayo ndiyo mambo ya Kuuliza Bungeni. Ukiendekeza Uanamagamba utatoka kwenye mstari kama kweli nia yako ni upiganaji. Kutetea hoja kama mwanamagamba utakuja kupoteza dignity yako
 
Kigwangala ni mnafiki tu na hata uso wake unaonyesha. Ndio maana wakati wa ule mgomo alimuwa mtu wa kwanza kwenda kupiga magoti kwa Sumaye kuomba msamaha, na kusema yuko chini ya miguu ya Sumaye. Huyo jamaa hana jipya hapo bungeni ni kama wana magamba wengine.
 
Huyo Kigwangala wenu ni mtu wa mara...Mwongozo wa Spika,...Taarifa Mwenyekiti...na kurukaruka plus kugonga meza kaa ngedere etc..pooleni wana Nzega kama walivyosema wabunge wa CDM Bungeni
 
Jamaa mkurupukaji!
Angalizo:awakurupukie vilaza wenzake na co vichwa km wakna Lisu.
 
Kigwangala ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) so analipa Fadhila kwa Serikali
 
Niliwasikia non Medics MPs walivyosimama kidete kutetea medical professionals kama Mh. Hilda Ngoye, Suzana Lyimo etc nikategemea Dr. Hamis Kingwangwala aka Said Nassoro Bagaile naye ange board the same boat lakini akandandia boat ya Kafulila ambayo mwishowe alikuja kuumbuka mwenyewe kwamba wakati tunakusanya bilion 280 exchange rate ya Dola to Sh ilikuwa 1:1,000.

Ambapo sasa tunakusanya bilion 380 exchange rate ya dola to Tsh ni 1:1,600 yaani kusema kweli Dr. Kingwangwala umetudhalilisha MDs wote kwa kushindwa kuone that simple fact na kuumbuliwa na Kafulila. Kusema kweli huko CCM kuna matatizo, nimekuwa nikisema hili, binadamu wanapoingia CCM uwezo wa kufikiri na kutafakuri huanguka vibaya, tumemuona jana Sitta alivyotetea ulegevu wa serikali kukusanya kodi kwa hoja dhaifu za POSHO na UNAFIKI.

Jamani hivi kuna nini huko CCM?
 
Hawezi akatetea hoja kwa sababu anajua so lake la kupora nafasi ya masomo ya sekondari
 
Kigwangala anataptapa tuu hana mbele wala nyuma, ni pupet wa kutupwa na mpenda madaraka kupindukia ... hafai kuwa hata kuongoza kikundi cha ng'ombe leave alone wananzega(sorry na poleni wana nzega) historia itamuhukumu siku zote kigwa niwape mfano akiwa mwanafunzi pale Muhimbili na raisi mstaafu wa serikali ya wanafunzi kigwangala bila ridhaa ya wanafunzi alishiriki katika kikao cha kanseli ya chuo ambacho kilipitisha maamuzi ya kufuta haki kibao za wanafunzi (kigwa akiwa si muwakilishi halali) aliyaridhia maamuzi hayo na kuuchuna (hakutoa taarifa kwa serikali ya wanafunzi kwani alihudhuria kinyemela).

Matokeo yake utekelezaji wa maamuzi yale ulipoanza ulisababisha mgomo na vurugu kubwa pale chuoni hadi chuo kikafungwa na baadhi ya wanafunzi kupewa suspension na wengine kufukuzwa kabisa . chanzo kikuuu alikuwa huyo kigwangala!
huyo ndiye kigwa ambaye kwake yeye maslahi yake yanakaa mbele ndipo ya wengine yanafuata bila kujali athari yeyote inayoweza kutokea!
aogopweee kuliko EL
 
kigwangala anataptapa tuu hana mbele wala nyuma, ni pupet wa kutupwa
na mpenda madaraka kupindukia ... hafai kuwa hata kuongoza kikundi cha ng'ombe leave alone wananzega(sorry na poleni wana nzega) historia itamuhukumu siku zote kigwa niwape mfano akiwa mwanafunzi pale muhimbili na raisi mstaafu wa serikali ya wanafunzi kigwangala bila ridhaa ya wanafunzi alishiriki katika kikao cha kanseli ya chuo ambacho kilipitisha maamuzi ya kufuta haki kibao za wanafunzi (kigwa akiwa si muwakilishi halali) aliyaridhia maamuzi hayo na kuuchuna (hakutoa taarifa kwa serikali ya wanafunzi kwani alihudhuria kinyemela)
matokeo yake utekelezaji wa maamuzi yale ulipoanza ulisababisha mgomo na vurugu kubwa pale chuoni hadi chuo kikafungwa na baadhi ya wanafunzi kupewa suspension na wengine kufukuzwa kabisa . chanzo kikuuu alikuwa huyo kigwangala!
huyo ndiye kigwa ambaye kwake yeye maslahi yake yanakaa mbele ndipo ya wengine yanafuata bila kujali athari yeyote inayoweza kutokea!
aogopweee kuliko EL
 
Kigwangala anataptapa tuu hana mbele wala nyuma, ni pupet wa kutupwa na mpenda madaraka kupindukia ... hafai kuwa hata kuongoza kikundi cha ng'ombe leave alone wananzega(sorry na poleni wana nzega) historia itamuhukumu siku zote kigwa niwape mfano akiwa mwanafunzi pale Muhimbili na raisi mstaafu wa serikali ya wanafunzi kigwangala bila ridhaa ya wanafunzi alishiriki katika kikao cha kanseli ya chuo ambacho kilipitisha maamuzi ya kufuta haki kibao za wanafunzi (kigwa akiwa si muwakilishi halali) aliyaridhia maamuzi hayo na kuuchuna (hakutoa taarifa kwa serikali ya wanafunzi kwani alihudhuria kinyemela).

Matokeo yake utekelezaji wa maamuzi yale ulipoanza ulisababisha mgomo na vurugu kubwa pale chuoni hadi chuo kikafungwa na baadhi ya wanafunzi kupewa suspension na wengine kufukuzwa kabisa . chanzo kikuuu alikuwa huyo kigwangala!
huyo ndiye kigwa ambaye kwake yeye maslahi yake yanakaa mbele ndipo ya wengine yanafuata bila kujali athari yeyote inayoweza kutokea!
aogopweee kuliko EL

Hapo kwenye bold ni kweli,Hata hivyo mtu yeyote mwenye nazo akienda na kuwa kiongozi CCM huwa kunatokea mabadiliko katika mfumo wa kufikiri sawa sawa
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom