sijui nini
JF-Expert Member
- Sep 29, 2010
- 2,553
- 1,285
Kigwangala akataliwa mbele ya JK Nzega
MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Nzega mkoani Tabora, Dk Khamis Kigwangala, amejikuta katika wakati mgumu baada ya wakazi wa jimbo hilo kudai kuwa hawatampa kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
Hatua ya wananchi ilikuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wampigie kura mgombea huyo, lakini walipaza sauti juu wakisema kwamba hawatamchagua.
Rais Kikwete, aliuliza wananchi waliofurika katika Uwanja wa Samora mjini Nzega, kwamba 'mtanipa kura Oktoba 31 mwaka huu, wakajibu ndiyo na kisha kumtambulisha Dk Kigwangalla na kuuliza 'mtampa kura' wakajibu kwa 'kuguna mmmmmhhhhh'.
Jibu hilo lilionekana kumchanganya Dk Kigwangala, ambaye wakati akitambulishwa alikuwa na sura iliyojaa tabasamu kubwa na kugeuka kuwa sura iliyokuwa na hofu na mshituko.
Hata hivyo, alipokuwa akiwasili uwanjani hapo sanjari na msafara wa Rais Kikwete, mshindi wa kura ya maoni ya CCM katika Jimbo la Nzega, Hussein Bashe, alishangiliwa kwa furaha kubwa na umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo, kitendo ambacho kilimfanya Rais Kikwete kushindwa kushindwa kumuita jukwaani kwa ajili ya kumpigia debe Dk Kigwangala.
Wakati akiondoka mara baada ya mkutano kuisha vijana wengi waliohudhuria kwenye mkutano huo, walilisukuma gari la Bashe, huku wakiimba " Bashe, Bashe, Bashe, Bashe" na "hatumpi kura Kigwangala" huku wakielekea Ikulu Ndogo Mjini Nzega, ambako mgombea wa CCM alifika kwa ajili ya mapumziko mafupi.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani hapo Ikulu Ndogo kulikuwa na mkutano mfupi wa dharura, ambao ulimtaka Bashe, avunje kundi lake ambalo linaoonekana kuinyima usingizi CCM na kuungana na chaguo la chama katika nafasi hiyo kwa ajili ya kuimarisha umoja na mshikamano.
Awali kabla ya tukio hilo, Rais Kikwete, aliwaahidi wakazi wa Wilaya ya Nzega kwamba akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kuwa ustawi wa Mji wa Nzega unaboreka kwa kusimamia miundombinu ya afya, elimu, maji na barabara.
Alisema anatambua matatizo kadhaa yanayoukabili Mji wa Nzega na kuahidi kufuatilia matatizo hayo kwa karibu ikiwa ni pamoja na kumaliza kabisa shida ya maji kwa kuwezesha uvutwaji wa maji kutoka katika Ziwa Victoria.
Alisema sambamba na kusimamia mambo hayo Rais Kikwete, aliahidi kutengeneza barabara ya Nzega hadi Tabora kwa kiwango cha lami na kuitengeneza pia barabara ya Tabora, Bukene, Itobo hadi Kahama kwa kiwango cha lami ili kuuwezesha Mkoa wa Tabora ufikike kwa urahisi.
Hata hivyo, mgombea huyo wa CCM alitoa kauli ya unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi ambao wanatumia dawa za kurefu maisha kwamba wamepata maambukizi hayo kutokana na kiherehere chao kwani wangeweza kujizuia na maambukizi hayo.
Wakati Kikwete akitoa kauli hiyo dhidi ya waathirika, takwimu zinaonyesha kwamba watu 9500 katika Mkoa wa Tabora wanatumia dawa hizo kati yao 2,700 wanaishi katika Manispaa ya Tabora.
MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Nzega mkoani Tabora, Dk Khamis Kigwangala, amejikuta katika wakati mgumu baada ya wakazi wa jimbo hilo kudai kuwa hawatampa kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
Hatua ya wananchi ilikuja baada ya Rais Kikwete kuwataka wampigie kura mgombea huyo, lakini walipaza sauti juu wakisema kwamba hawatamchagua.
Rais Kikwete, aliuliza wananchi waliofurika katika Uwanja wa Samora mjini Nzega, kwamba 'mtanipa kura Oktoba 31 mwaka huu, wakajibu ndiyo na kisha kumtambulisha Dk Kigwangalla na kuuliza 'mtampa kura' wakajibu kwa 'kuguna mmmmmhhhhh'.
Jibu hilo lilionekana kumchanganya Dk Kigwangala, ambaye wakati akitambulishwa alikuwa na sura iliyojaa tabasamu kubwa na kugeuka kuwa sura iliyokuwa na hofu na mshituko.
Hata hivyo, alipokuwa akiwasili uwanjani hapo sanjari na msafara wa Rais Kikwete, mshindi wa kura ya maoni ya CCM katika Jimbo la Nzega, Hussein Bashe, alishangiliwa kwa furaha kubwa na umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo, kitendo ambacho kilimfanya Rais Kikwete kushindwa kushindwa kumuita jukwaani kwa ajili ya kumpigia debe Dk Kigwangala.
Wakati akiondoka mara baada ya mkutano kuisha vijana wengi waliohudhuria kwenye mkutano huo, walilisukuma gari la Bashe, huku wakiimba " Bashe, Bashe, Bashe, Bashe" na "hatumpi kura Kigwangala" huku wakielekea Ikulu Ndogo Mjini Nzega, ambako mgombea wa CCM alifika kwa ajili ya mapumziko mafupi.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani hapo Ikulu Ndogo kulikuwa na mkutano mfupi wa dharura, ambao ulimtaka Bashe, avunje kundi lake ambalo linaoonekana kuinyima usingizi CCM na kuungana na chaguo la chama katika nafasi hiyo kwa ajili ya kuimarisha umoja na mshikamano.
Awali kabla ya tukio hilo, Rais Kikwete, aliwaahidi wakazi wa Wilaya ya Nzega kwamba akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kuwa ustawi wa Mji wa Nzega unaboreka kwa kusimamia miundombinu ya afya, elimu, maji na barabara.
Alisema anatambua matatizo kadhaa yanayoukabili Mji wa Nzega na kuahidi kufuatilia matatizo hayo kwa karibu ikiwa ni pamoja na kumaliza kabisa shida ya maji kwa kuwezesha uvutwaji wa maji kutoka katika Ziwa Victoria.
Alisema sambamba na kusimamia mambo hayo Rais Kikwete, aliahidi kutengeneza barabara ya Nzega hadi Tabora kwa kiwango cha lami na kuitengeneza pia barabara ya Tabora, Bukene, Itobo hadi Kahama kwa kiwango cha lami ili kuuwezesha Mkoa wa Tabora ufikike kwa urahisi.
Hata hivyo, mgombea huyo wa CCM alitoa kauli ya unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi ambao wanatumia dawa za kurefu maisha kwamba wamepata maambukizi hayo kutokana na kiherehere chao kwani wangeweza kujizuia na maambukizi hayo.
Wakati Kikwete akitoa kauli hiyo dhidi ya waathirika, takwimu zinaonyesha kwamba watu 9500 katika Mkoa wa Tabora wanatumia dawa hizo kati yao 2,700 wanaishi katika Manispaa ya Tabora.