Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Habari za kuaminika kutoka kigoma ni kwamba walimu wa sekondari na shule za msingi leo kuanzia saa 6 mchana waliwafungia wakuu wa idara katika manispaa ya kigoma ujiji akiwemo mkurugenzi wa manispaa hiyo kushinikiza walipwe mishahara yao ya mwezi Februari mwaka huu. Wakihojiwa na mwandishi wa habari wa RFA Richard Katunka kutoka kigoma, walimu hao walisema mpaka leo tarehe 5 Machi bado hajalipwa mishahara ya mwezi wa pili na wameapa kutorudi kazini mpaka watakapolipwa mishahara yao....mpaka saa 11 jioni walimu hao walikuwa bado wanawashikiria mateka wao na waliapa kufa na yeyote atakaenda hapo kujaribu kutumia nguvu kuwatimua walimu hao. My take: Ndio sirikali imefuli eh?! aibu ndio tunaota kuboresha elimu kwa mwendo huu!