Umechangia vyema sio kama wengi wanaotoa vitisho au chuki.
Inaonekana wachangiaji wengi wana siasa za kiCCM...."nikudhulumu au unahatarisha amani"
La msingi ni hilo ulilosema sheria za kiuhamiaji zichukue mkondo wake.Kutakuwa na kipindi cha mpito ambacho shughuli za muungano zitapiga reverse gear kurudi Tanganyika.
Lakini ukivunjika muungano hakuna Tanzania, kwa hiyo hao wataomba uraia wa Tanganyika.
Tunapochangia kuhusu kuvunjika kwa muungano wengine huona kama vile ndio mwisho wa dunia, hofu, chuki,hasira kwa wale wenye woga hutawala fikra zao na wale wanaoona kuvunjika kwa muungano ni mwisho wa usanii/mazingaombwe basi ndio hao watakaokula pizza na pilau na kujawa na furaha.
Tusisahau kuwa leo watanzania wapo kila kipembe cha dunia na wanamiliki majumba, biashara nk. na wala Tanzania haina muungano na nchi hizo walimo hawa watanzania. Wanaofuata sheria za uhamiaji hawakumbani na mkono mrefu wa sheria.
link Raia Mwema - Familia ya Lowassa yapelelezwa London
link diaspora
link Tanzania Event
link Tanzania's Diaspora - Investment-Citizenship and Relationship
Singapore na Malaysia walikuwa na muungano na ulivunjika.Singapore alifukuzwa kutoka muungano. Leo Malaysia na Singapore ni nchi mbili jirani zenye neema na ujirani mwema.
Ni vyema kuuvunja Muungano kwa amani kulikoni kwa vita.
Chakushangaza hakuna kiongozi mkuu kutoka Tanganyika tokea Nyerere mwenyewe mpaka kufikia Kikwete anaetaka kuvunjika kwa muungano huu kila anaekuja hujigamba ataulinda kwa nguvu zote hata ikibidi kutumia nguvu .
siku na wakati hazigandi zamani ukigusia muungano tu kama hujakolimbwa basi watakusokoine sasa kwa nini watu walinde kitu kisicho faida ? hapa ndo utagunduwa watanganyika vifuu tundu wanashindwa kujiuuliza . wazanzibari washaonyesha kila dalili kuchokwa na muungano huu kwanini viongozi wakuu hasa watanganyika wanaziba masikio ?
watanganyika vifuu tundu wao akili zao zipo katika kuiba na kudhulumu . hivi hakuna watanzania ama watanganyika wanoishi nchi za watu bila kuwa na muungano ? kuishi nchi nyengine na muungano ni vitu tofauti acheni kujidhalilisha kwa kudhihirisha wizi na njaa zenu wale wenye ndoto za mali za watu .
kama muungano hauna faida kwa znz waacheni waende ibaki tanganyika yenye faida hayo ya umeme ,vitunguu,nyanya ni biashara tu hivi bara hakuna watu wasioishi bila umeme ? ama nyumba zote zina umeme ?
WACHENI KUWATISHA WA ZANZIBARI ATI MTAWAIBIA MALI ZAO KUWAFUKUZA BARA HUU NI ZAIDI YA UDHAIFU.