nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
NA PETER KATULANDA, MWANZA
Thursday, 28 April 2011
MJUMBE wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa, Barnabas Mathayo, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumteka kwa silaha na kumbaka binti wa miaka 22.
Habari za kuaminika zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa Mwanza, Simon Sirro, zilisema Mathayo anadaiwa kutenda unyama huo Aprili 24, mwaka huu, kati ya saa mbili hadi nne usiku.
Ilidaiwa kuwa Mathayo ambaye pia ni mfanyabiashara mjini hapa, alimlazimisha binti huyo (jina linahifadhiwa), kufanya tendo la ndoa baada ya kumpa lifti kutoka baa ya Kembice, iliyopo mtaa wa Uhuru.
Awali, ilidaiwa kuwa alimuita binti huyo kwa shughuli za kikazi, lakini baada ya maongezi aliondoka naye kwa kutumia gari lenye namba za usajili T. 345 AWS, ambapo alimgeuzia kibao wakiwa njiani kwa kumtishia bastola.
"Alimweka chini ya ulinzi na kumtaka atii amri yake, vinginevyo atamtwanga risasi. Alipelekwa katika hoteli moja iliyopo mtaa wa Rwegasore na kufanya tendo hilo," kilisema chanzo kutoka ndani ya Jeshi la Polisi. Tayari Mathayo amefunguliwa jalada namba MW/RB/3988/2011, kwa kile kinachodaiwa matumizi mabaya ya silaha.
Kamanda Sirro alisema jana kuwa, mtuhumiwa huyo alitiwa mbaroni Aprili 27, mwaka huu na kuhojiwa katika Kituo cha Mjini Kati, ambapo aliachiwa huru kabla ya kukamatwa tena juzi.
"Hakuna aliye juu ya sheria, ukivunja sheria unawajibishwa, tunaendelea kumhoji Mathayo na kuchunguza tukio hilo kwa kina," alisema Kamanda Sirro.
Kwa upande wake Mathayo alipoulizwa juu ya tuhuma hizo, alidai binti huyo ni mpenzi wake na siku hiyo walipanga kupumzika faragha, lakini walitofautiana kidogo.
Thursday, 28 April 2011
MJUMBE wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa, Barnabas Mathayo, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumteka kwa silaha na kumbaka binti wa miaka 22.
Habari za kuaminika zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa Mwanza, Simon Sirro, zilisema Mathayo anadaiwa kutenda unyama huo Aprili 24, mwaka huu, kati ya saa mbili hadi nne usiku.
Ilidaiwa kuwa Mathayo ambaye pia ni mfanyabiashara mjini hapa, alimlazimisha binti huyo (jina linahifadhiwa), kufanya tendo la ndoa baada ya kumpa lifti kutoka baa ya Kembice, iliyopo mtaa wa Uhuru.
Awali, ilidaiwa kuwa alimuita binti huyo kwa shughuli za kikazi, lakini baada ya maongezi aliondoka naye kwa kutumia gari lenye namba za usajili T. 345 AWS, ambapo alimgeuzia kibao wakiwa njiani kwa kumtishia bastola.
"Alimweka chini ya ulinzi na kumtaka atii amri yake, vinginevyo atamtwanga risasi. Alipelekwa katika hoteli moja iliyopo mtaa wa Rwegasore na kufanya tendo hilo," kilisema chanzo kutoka ndani ya Jeshi la Polisi. Tayari Mathayo amefunguliwa jalada namba MW/RB/3988/2011, kwa kile kinachodaiwa matumizi mabaya ya silaha.
Kamanda Sirro alisema jana kuwa, mtuhumiwa huyo alitiwa mbaroni Aprili 27, mwaka huu na kuhojiwa katika Kituo cha Mjini Kati, ambapo aliachiwa huru kabla ya kukamatwa tena juzi.
"Hakuna aliye juu ya sheria, ukivunja sheria unawajibishwa, tunaendelea kumhoji Mathayo na kuchunguza tukio hilo kwa kina," alisema Kamanda Sirro.
Kwa upande wake Mathayo alipoulizwa juu ya tuhuma hizo, alidai binti huyo ni mpenzi wake na siku hiyo walipanga kupumzika faragha, lakini walitofautiana kidogo.