Kigogo Mwingine wa CCM Arusha amfuata Millya Chadema

Angalizo!
Usihamie CHADEMA kama huna nia nzuri na chama au una masilahi binafsi maana utaumbuliwa muda si mrefu!
Ni chama makini, hivo kuwa makini lengo ni kujenga Taifa sio watu binfsi!
 
CDM ni digitali, ikifikia tarehe 31 Decemba 2012 tunazima mitambo yote ya analogia, kama bado uko huko huwezi tena kutoka. Sumaye aliwahi kuimba bungeni kuwa mambo iko huku, akimaanisha kuwa ukitaka kukwepa kodi uhamie huko analogia, ukitaka kudhulumu mali ya umma uhamie huko analogia. Mimi namwambia watakaodumu huku digitali ni wale wasafi, wasiokwepa kodi, wala wasio wazulumati. DIGITALI BABA, USIKIVU MWANGAVU NA PICHA ISIYO NA CHENGA. PATA KING'AMUZI CHAKO LEO.
 
Jinamizi la viongozi na Chama cha Mapinduzi (CCM) la kukihama chama hicho limeendelea kushika kasi, baada ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa wa Arusha, Justine Genda, naye kutangaza kukihamia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Genda ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Kata ya Karatu Mjini, alitangaza uamuzi huo jana wilayani Karatu na tayari ameshapokelewa na viongozi wa Chadema katika hafla iliyohudhuriwa na Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Karatu Titus Lazaro na Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Karatu, Thomas Darabe.

Genda alisema ameamua kujiunga na wanaharakati wa kupigania haki na kuleta mabadiliko na kuongeza kuwa kwa sasa fursa hiyo inapatikana Chadema.

“Nimeamua kuhama CCM na kujiunga na Chadema na nina matumaini makubwa kwani nimeona kuwa Chadema kuna fursa ya kumuwezesha kila mmoja kutoa mchango wake katika mchakato mzima wa mabadiliko na ni chama kinachoweza kuleta ukombozi wa kweli katika taifa,” alisema Genda.

Akizungumza baada ya kumkabidhi kadi ya Chadema mwanachama huyo, Lazaro aliwataka wanachama na viongozi zaidi wa CCM na vyama vingine wanaotaka mabadiliko ya kweli kujiunga na Chadema kwani ni chama makini.

Wakati huo huo huko Ruvuma nako Katibu wa Chama Cha Tanzania Labour (TLP) Jimbo la Songea mkoani Ruvuma, Joseph Mkondora, amejiengua katika chama hicho na kujiunga na Chadema ambacho alisema ni chama pekee cha upinzani kinachoonyesha dira ya maendeleo kwa Watanzania.

SOURCE:NIPASHE JUMATATU

Ha ha ha haaaaaaaa waacheni wafu wawazike wafu wenzao, hata mjumbe wa mkutano nae ni kigogo? kweli magwanda mnapenda sifa za kipuuzi.
 
Sijui kachelewa wapi huyu jamaa, harakati hizi zilianza siku nyingi pale karatu.
 
Safi sana mungu ibariki CCM naona magamba yanajivua yenyewe kabla hayajavuliwa, ujue haya magamba yanajua huu ni mwaka wa uchaguzi wa nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya CCM sasa ndugu zanguni kuna kautaratibu ka kujaza form alafu unajadiliwa na kamati husika ndiyo jina lako linarudi kipigiwa kura sasa kwa sifa chafu walizonazo hawa jamaa magamba wanajua majina yao hayawezi kurudi ndiyo maana wanakimbia mapema hawana future ya kisiasa ndani ya CCM,mmeona Millya aliomba ubunge wa EAC kamati husika ndani ya CCM zikamuengua baada ya kuenguliwa ndiyo akahama chama,je hasingeenguliwa angehama CCM? Hapa utamjua Millya kama ni kiongozi maslahi au la,safi sana wachafu wote watahama mwaka huu ni bora tubaki wachache lakini tuwasafi kuliko tuwe wengi tukichangamana na wachafu,kidumu CCM!
 
CDM ni digitali, ikifikia tarehe 31 Decemba 2012 tunazima mitambo yote ya analogia, kama bado uko huko huwezi tena kutoka. Sumaye aliwahi kuimba bungeni kuwa mambo iko huku, akimaanisha kuwa ukitaka kukwepa kodi uhamie huko analogia, ukitaka kudhulumu mali ya umma uhamie huko analogia. Mimi namwambia watakaodumu huku digitali ni wale wasafi, wasiokwepa kodi, wala wasio wazulumati. DIGITALI BABA, USIKIVU MWANGAVU NA PICHA ISIYO NA CHENGA. PATA KING'AMUZI CHAKO LEO.

Naamini una uwezo wa kuwa great resource kwa idara ya mawasiliano CDM....
 
Mama porojo na wote wa taipu yako nataka kuwaambia kwamba vigogo mnaoringia hawatakiwi CDM kama unavyofikiri, ukitaka kujua ukuaji wa grafu ya CDM kwa kuongeza wanachama wapya wewe tafuta kujua idadi ya wahitimu wa kidato cha nne kila mwaka, huo mwendo usipime ndugu yangu ni kasi ya faiba optiki penda usipende lazima upitwe.
 
Mama porojo na wote wa taipu yako nataka kuwaambia kwamba vigogo mnaoringia hawatakiwi CDM kama unavyofikiri, ukitaka kujua ukuaji wa grafu ya CDM kwa kuongeza wanachama wapya wewe tafuta kujua idadi ya wahitimu wa kidato cha nne kila mwaka, huo mwendo usipime ndugu yangu ni kasi ya faiba optiki penda usipende lazima upitwe.
 
... itakua ni kosa kubwa ajabu IKULU kudhani kumnyanganya Kamanda Lema ubunge kupitia mahakama huenda ikawa ni suluhisho.

Kamanda Lema endelea kuonyesha TALANTA yako ya kupendwa na vijana wa Tanzania kwa kuhamisha Vijiji vyote nchini toka CCM na kujiunga na CDM.

Kamanda Lema, onyesha UWEZO wa 'Nguvu ya Umma' kote nchini kupitia hiki chombo mahiri cha M4C huku ukiambatana na Jenerali na Dokta wa ukweli, Dr Slaa, kwa kutetemesha mafisadi katika kila jimbo.

Jinamizi la viongozi na Chama cha Mapinduzi (CCM) la kukihama chama hicho limeendelea kushika kasi, baada ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa wa Arusha, Justine Genda, naye kutangaza kukihamia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Genda ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Kata ya Karatu Mjini, alitangaza uamuzi huo jana wilayani Karatu na tayari ameshapokelewa na viongozi wa Chadema katika hafla iliyohudhuriwa na Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Karatu Titus Lazaro na Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Karatu, Thomas Darabe.

Genda alisema ameamua kujiunga na wanaharakati wa kupigania haki na kuleta mabadiliko na kuongeza kuwa kwa sasa fursa hiyo inapatikana Chadema.

“Nimeamua kuhama CCM na kujiunga na Chadema na nina matumaini makubwa kwani nimeona kuwa Chadema kuna fursa ya kumuwezesha kila mmoja kutoa mchango wake katika mchakato mzima wa mabadiliko na ni chama kinachoweza kuleta ukombozi wa kweli katika taifa,” alisema Genda.

Akizungumza baada ya kumkabidhi kadi ya Chadema mwanachama huyo, Lazaro aliwataka wanachama na viongozi zaidi wa CCM na vyama vingine wanaotaka mabadiliko ya kweli kujiunga na Chadema kwani ni chama makini.

Wakati huo huo huko Ruvuma nako Katibu wa Chama Cha Tanzania Labour (TLP) Jimbo la Songea mkoani Ruvuma, Joseph Mkondora, amejiengua katika chama hicho na kujiunga na Chadema ambacho alisema ni chama pekee cha upinzani kinachoonyesha dira ya maendeleo kwa Watanzania.

SOURCE:NIPASHE JUMATATU
 
Watahama wale wanaojua kusoma alama za nyakati na wale bongo lala watakufa na chama chao
 
Huyu sio kigogo
Pole.

Ni kweli umemuelewa vyema Mr. Mkapa na kauli za kuwaogopa wazungu. Nina kutahadharisha kuwa kuendelea kunaamini katika uvigogo fisadi,hakika, wewe basi/gari la maendeleo halisi bila ufisadi lazima litakuacha.
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom