Kigoda aingia kwa mkwara: Charles Ekerege wa TBS out!

Ndo kibarua kimeota nyasi kesi zake hawezi kuachwa na aliyemsimamisha ni Waziri A. Kigoda
 
Kadai uchunguzi unafanyika hivi upo uchunguzi zaidi wa ule wa CAG?
 
Chami kaponzwa na ushamba,hata kama kateuliwa na Rais anauwezo wa kumtosa, bodi zote zipo chini ya waziri na bodi zina kazi ya kupendekeza majina ya wakurugenzi na kumshauri Rais, alitakiwa awe fast kufanya maamuzi
 
Nimeamini tatizo TBS lilikuwa ni Ekelege tu. Toka aondoke hatusikii upuuzi wa makampuni ya kitapeli tena

Naelekea kukubaliana nawe maana hali inavyojionyesha tatizi zaidi si mfumo maana ni mfumo huo huo uliokuwepo tangu enzi za awamu ya kwanza, tatizo ni watu na hili nimeliona sehemu nyingi tu hata kwenye taasisi za kibenki. Bank hizo hizo zamani zilikuwa zinafanya kazi vizuri na kwa ufanisi mkubwa kwa utaratibu huo huo lakini leo utaratibu huo haujabadilika lakini mizengwe leo hii ni kupindukia.
 
Naelekea kukubaliana nawe maana hali inavyojionyesha tatizi zaidi si mfumo maana ni mfumo huo huo uliokuwepo tangu enzi za awamu ya kwanza, tatizo ni watu na hili nimeliona sehemu nyingi tu hata kwenye taasisi za kibenki. Bank hizo hizo zamani zilikuwa zinafanya kazi vizuri na kwa ufanisi mkubwa kwa utaratibu huo huo lakini leo utaratibu huo haujabadilika lakini mizengwe leo hii ni kupindukia.
Tatizo mara nyingi ni wapuuzi wachache wakipewa madaraka huyatumia vibaya na matokeo yake kuchafua jina zima la bodi wanayoongoza. Ekelege aliigeuza TBS kijiwe cha kupiga dili za kipuuzi na alikuwa mjeuri sana, sijui ni kwa nini lakini Kigoda naona hakumuonea aibu kamtupilia mbali na vikampuni vyake vile vya Quality hongkong na Wtm uk hatuvisikii tena. Pia bidhaa feki zimekuwa adimu mitaani sasa at least watu tuna amani na vitu kutoka nje . Yule mzee angeachiwa aendelee pale tbs ingefikia siku tungeletewa dawa feki za malaria na ukimwi kwa sababu jamaa yeye alikuwa hajali uhai wa mtanzania. Hatukatai kila mtumikia zizini hula zizini lakini sio kula ng'ombe badala ya kunywa maziwa. Serikali sasa iangalie na wizara nyingine pia.
 
Back
Top Bottom