Kifupi sisi hatuna culture ya kuwa na vision na kuweka goals, tunaelea tu.....

Ndugu zangu,

Hili ni jibu langu ninalolirudia mara kwa mara katika topic za namna hii, sambamba na Julius na msimamo wake wa 'miafrika ndivyo tulivyo'. Basi, mimi nasema hivi:

Hata kama tungelikuwa hatuna scientific ingenuity au kuwa ma-proponent wa tafiti za kisayansi ya hali ya juu, kama wengi ya watu wetu (haswa viongozi tuwachaguao) kwenye jamii zetu tungelikuwa si wenye tamaa, si wanafiki, si wazembe, si watu wa kuridhishwa na kilichopo bali wa kutafuta kilichozaidi kwa ajili ya manufaa ya jamii nzima, si watu wa kudharau wasionacho ndani ya jamii zetu; hakika tungelikuwa tuna maendeleo makubwa kuliko tulivyo hivi sasa. Kwa mara nyingine tena nitamalizia kwa sentensi ifuatayo:

Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi.

Steve Dii

I see where you are coming from but your problem is you are too politically correct to call it as you see it.
 
Hakuna cha asili wala nini. Mambo yetu yalikuwa poa tu zamani. Hadi siku mvua ilipoanza kutunyea!

Kweli, kama TV basi inaonyesha chenga chenga, somethingi is wrong with Antenna, TV nina hakika genuine kabisa.
 
image001.jpgdd.jpg


- Tunaweza sana ku-create haya yasiyoweza kutuendeleza, that is all!

Respect.


FMEs!

FMES umedata wewe....yaani nipo hapa nakula cereal almanusura nipaliwe! Umemtoa wapi huyu mrembo lakini? LMAO.....but seriously, ulichosema ni kweli kabisa.
 
Umeshawahi kusikia nchi ya Malta?

Ndio nimeshawahi kuisikia hiyo nchi. Hakuna maskini huko? Umewahi kufika huko?

ndicho nilichokisema; ni uongozi.

Kwenye uongozi mbovu tunakubaliana ingawa wewe hutaki kuuita uongozi mbovu. Lakini nadhani tunazungumzia kitu kile kile tu.

sasa na leo sisi tunazo?

Ni kweli tunazo. Ila nilitaja tv kimatani tu.

swali zuri.

Vipi unalo jibu lake?

ni kwa sababu ya uongozi; mwanzoni tulikuwa tunapenda vya kwetu na kuvitumia kwa fahari.

Sijui hapa uongozi unaingia vipi maana watu wana macho yao na ladha zao. Sasa kama wanaona vya Ulaya na Marekani vina ubora kuliko vya kwao waache kuvitamani? Hivi kweli unataka kunambia vile viatu vya Bora vingeweza kushindana na viatu vya akina Bruno Magli au Donald J. Pliner? Au vile vitambaa vya Mwatex na yale mashati ya Urafiki yangeweza kushindana na ya akina Burberry na Boss? Come on son...

Yapo magonjwa mengine yanayowapata watu weupe zaidi vile vile lakini haina maana huwezi kupata mweupe mwenye sickle cell!

Okay...kwa hiyo unakubali kuwa kuna baadhi ya vitu viko zaidi kwa watu weupe kuliko weusi na vingine viko zaidi kwa watu weusi kuliko weupe?

sidhani kama hiyo ni hoja; wakati wa Warumi lugha iliyotawala ilikuwa ni Kilatini! Leo hii lugha kubwa ni kiingereza usije kushangaa huko tunakokwenda tukajifunza Kichina zaidi. Mambo mengine ni histojiografia inaoongoza.

Kwani hicho Kilatini si moja ya lugha za hao wazungu na weupe weupe tu....au Walatini sio weupe?

Hatuwezi kutengeneza vya kwetu kwa sababu ya uongozi. Hivi unajua hata huko kwa wazungu na wenyewe walikuwa wanafanya madudu tunayoyafana sisi wakati huu?

Wakati wao wanafanya haya madudu sisi tulikuwa tunafanya nini? Tunawinda? Maana hatukujifunza kitu kabisa toka kwao. Pathetic.

nope. It starts and ends with leadership; bear in mind I'm not speaking of political leadership only!

Ni kweli kuwa uongozi bora (mzuri) ni muhimu lakini sio the be all and end all. Kuna mambo mengine kama ingenuity ambayo ni ya muhimu vile vile.
 
if this was an examination question, i would just answer it this way--- "probably it is genetics"!!
 
Mkuu Weberoya, mimi naamini kabisa connection imekatika kati ya watawala ambao wameendekeza ubinafsi na kusahau wananchi na wananchi maskini ambao walitakiwa waonyeshwe njia na viongozi.
 
Mimi nafikiri
tuangalie university ya kwanza hawa jamaa wamekuwa toka lini akina Newton walikuwa university sisi je?

Japo mwingine ata argue kwamba na sisi wazee wa sengerema walikuwa wamegunduwa ulindi na ulimbombo.teh teh teh.
 
Wakati naamini viongozi wetu wakuu wanachangia kwa kiasi kiikuwa umasikini na ukosefu wetu wa maendeleo,the real culprit ni middle level leaders and management.

Hawa ndio wanatakiwa kuwa game changers,wakuu wa idara,wakurugenzi wa wilaya,wakuu wa taasisi za umma,n.k
Lakini hawa ndio wezi wakuu just behind they partners in crime-viongozi wakuu-wabunge,mawaziri,majaji,etc.
Viongozi wakuu wanatupeleka kubaya hawa wakina yakhe, wa hapa kati kwao ni hewala tu.wanashirikiana nao bega kwa bega kwa kigezo cha mkubwa ataniona,kula na kipofu etc..,

Kama ni elimu,vision,culture kila taifa duniani lina lowpoints zake,and if we measure on that alone we are just ok.better than most.

Binafsi hawa wazee mie nasubiri wafe tu(sorry for cruel comments).but out of all possibilities i do not see any in which hawa njemba wata-turn around the country.they are useless junk of leaders lucky enough to be in a country where people are too poor and weak to really care.

if they did half the things people suggested here in JF(mikataba mibovu,scandals,uongozi bora etc) we could have been whole lot better.just imagine what would happen if they did what their electorates expected them to do.

We are a poor nation yes,but we have infinite potential that takes the worst bunch of leaders to ever set their feet on the earths surface to fail to tap it!

it's like a coach taking a a coach team as talented as Barcelona to Tanzania Premium league (whatever name they call it) and fail to win a single game!
 
Interesting debate!

Let me shift a weight and focus on goals. I think I will be 95% right to state that most times we are more focused with quick gains rather than creating a strong everlasting legacy that has true and meaningful value.

Every start up of business or idea, the main focus is to realize the immediate gains, mavuno ya haraka, kujipatia fedha na sifa za haraka, but not a solid measurable work that has an everlasting effect and long term value.

As a result, we end up failing, miserable and always look for cheap ways to make up the differeces due to short falls of gain.

Kuna mtu kazungumzia kuhusu Mtanzania na Mchina kuwa na mtaji sawa lakini baada ya miaka kadhaa, utakuta Mtanzania yupo chali bin taaban.

It speak alot about us as People, as Culture.

Lakii tunapoongelea leadership, sidhani kuwa ni lazima liishie kwenye uongozi wa Nchi kisiasa na kiutendaji, ni hata kifamilia, kijamii na kiurafiki.

Kama hatutakaa chini na kubadili mindsets na kujihakiki kamwe hatutaweza kuendelea mbele, bali tutaendelea kuelea!
 
Mkuu Rev, good topic.

Tanzania in my opinion we lack what we call ""Cause and effect"" analysis.

As a leader before any decision is made u have to thoroughly look at what benefits it will bring today, tomorrow and in the future and what problems might be created and then U weigh the pros/cons and solutions or mitigation of the cons.

Sasa huwezi kuacha kuinvest kwenye kilimo, kudevelop vijiji kwa muda mrefu halafu baada ya muda vijana wote wakijaa Dar na kuanza kuchinja watu kwa kuwa vibaka, unaanza kushangaa watanzania unyama huu tunaotowa wapi?? Unaachia vitu vya nje kuingia TZ ovyo bila tax kubwa halafu unashangaa viwanda vya tanzania vinakufa!!

Mimi ningekuwa mshauri wa serikali, ningesema kabisa in the next say 5 yrs tuchague mikoa 5 yenye potential ya kuwa na success haraka kwenye kilimo, investment, viwanda nk na ndio serikali ipeleke asilimia kubwa ya funds na upendeleo huko ili maendeleo ya haraka yafanyike na iwe magnet ya watu kupunguza bomu la mauaji litakalofukuta Dar in the very near future.
Unaweza kupick Kilimanjaro/Arusha/Mbeya/Iringa/Ruvuma na kuanzia hapo.
 
Mwanakijiji, hayo yote au mengi ya uliyoyasema na kuyataja yanahusu Tanzania. Je, ina maana na kwingineko Afrika hususan kusini mwa sahara (black Africa) na kwenyewe tatizo lao ni uongozi mbovu? Kama ni hivyo ina maana uongozi mbovu ni common denominator Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara. Sasa kwa nini kote huko kuwe na uongozi mbovu? Ndivyo Tulivyo kuwa hatuwezi uongozi? What is it? Maana mimi siamini kabisa kuwa hizo nchi zingine za Kiafrika zimetuzidi kihivyo. Nimeshabahatika kutembela baadhi ya nchi za Kiafrika na sikuona lolote la ziada tulilozidiwa. Kama ufisadi hata Cameroun upo. Kama vya kupenda vya Ulaya basi hata Niger wanapenda vya Ulaya. Sasa nisichoelewa ni kwa nini Afrika nzima kusini mwa sahara ni sehemu iliyo ktk kundi la nchi za ulimwengu wa tatu. Sielewi kabisa hili. Inakuwa kuwaje eneo kubwa kama hili kiwango cha maendeleo kinakuwa kimefanana sana?

Bara la Ulaya sio nchi zote zilizoendelea saana kihivyo. Hakuna uniformity ya maendeleo. Huwezi kulinganisha kwa mfano maendeleo ya Ujerumani na Uholanzi na yale ya Romania. Lakini hata hao Romania wameendelea kuliko nchi karibu zote kama sio zote kabisa za Afrika, Sasa huu uongozi mbovu ina maana upo Afrika nzima? WTF.....

Nyani unanishangaza sana,na pia nashangazwa sana kuwa wengi wanakubaliana na wewe,yani nashangazwa haswa.

Kutokana na uzoefu wa mijadala mingi hapa JF,nilishawahi kusema kuwa kwenye mijadala yoyote ambayo inaelekea kuuliza maswali ya kwanini haya na kwanini yale,ni LAZIMA turejee kwenye historia,hilo ndilo hatupendi kujifunza inapokuja kwenye mijadala kama huu.

Na pia nilishawahi kukueleza kuhusu double standards....Kwenye maelezo yako hapo juu umetoa mfano kwa kulinganisha nchi za Ujerumani na uholanzi vs Romania bila ya kujali historia na hata issue za iron curtain countries nk.....Umezungumzia similarities za waafrika kwa kuwasingle out kama blacks na wakati unazugumzia mataifa hayo ya wazungu,unakuja kuyalinganisha tena kwa vigezo vingine bila kuzingatia historia.

Huwezi ukazungumzi mambo haya na haya yako hivi bila kusema ni kwanini yako hivyo,at least hapa JF tungeweza kuwa na standards hizo,za kujaribu kufikiria zaidi na zaidi.

Kwenye issue zako ulizozungumzia hapo juu kama unge include history,basi ungezungumzia mambo mengi tu kuanzia Neo Colonialism, colonialism and all the way back to slavery,certainly pia tungezungumzia kuhusu issues za Iron curtain countries kwasababu Romania ni mojawapo,tungezungumzia pia issue za east and west German,tungezungumzia pia kuhusu Benelux,yani Belgium,Nedherlands na Luxemborg,tusingesita pia kuzungumzia impact za Capitalism,Socialism na hata Communism.

Haya mambo ni more than just kuja tu na kusema eti hawa blacks hivi and ndivyo yalivyo,and then eti hata hawa wazungu wengine wa Romania ni better than blacks blah blah wahta crap!
Halafu watu weee!maajabu!

Kwa mfano hukujiuliza ni kivipi impacts za Iron curtain Countries ama za Cold wars zilivyo tofauti na zile za Slavery,Colonialism na Neo Colonialism.

Hatuna historia bado ya kujilinganisha na wazungu,jambo ambalo hatulitambui ni kwamba sisi kama waafrika bado tunahitajika tuwe kwenye struggles za uhuru wa kweli,uhuru tulionao ni wa bandia bado,lakini kwasababu viongozi wetu wamekuwa kama watoto waliopewa suckers toka tupate uhuru wa bandia,basi na wao wanatumia nyenzo kama za mataifa yaliyoendelea kwenye kutawala na wakati ukweli ni kinyume.

Hatuwezi kukaaa hapa JF na kusema eti sisi ndivyo tulivyo,ilitakiwa useme sisi bado tuko kwenye struggles za uhuru wa kweli ambao ndio utatupatia maendeleo ya kweli.

Umezungumzia uongozi mbovu kuwa ni common denominator ya Afrika bila kutaja ukweli kuwa common denominator ya Afrika ni unique history yake...Colonialism na mengineyo niliyoyasema hapo juu ni common denominator ya Afrika,kwanini ukutake that into consideration?Mjadala huu ni mpana sana na si wa kuparamia kwa maswali na majibu rahisi rahisi,at least nilitegemea hapa JF tungekuwa hivyo.

If you dont know where you coming from,how can you know where you goin?
Unashangazwa nini na Afrika nzima kuwa na uongozi mbovu na wakati historia yao ni moja?
 
Huwezi ukazungumzi mambo haya na haya yako hivi bila kusema ni kwanini yako hivyo,at least hapa JF tungeweza kuwa na standards hizo,za kujaribu kufikiria zaidi na zaidi.

Kwa mfano hukujiuliza ni kivipi impacts za Iron curtain Countries ama za Cold wars zilivyo tofauti na zile za Slavery,Colonialism na Neo Colonialism.


Hatuwezi kukaaa hapa JF na kusema eti sisi ndivyo tulivyo,ilitakiwa useme sisi bado tuko kwenye struggles za uhuru wa kweli ambao ndio utatupatia maendeleo ya kweli.
nimekugongea senksi for this useful argument.
 
Haya kama historia ni ishu

Go back and check maendeleo ya wazungu kabla ya ukoloni na maendeleo yetu wakati huo.

Vingine ni visingizio tu.Tena nafikiri wakati mwingine wasingekuja hawa wakoloni kutuchapa viboko hadi leo tungekuwa tunavaa ngozi.

Si angalieni ambako wakoloni hawakufika Umasaini, wasandawe.

ama tuache hao wamasai na wasandawe nini tofauti kati ya taifa ambalo halikukubwa na ukoloni Ethiopia na South Afrika ambalo limekuwa chini ya wakoloni mpaka juzijuzi? the fact is very strong.
 
Mkuu kama utakumbuka kuna document linaitwa vision 2025, hilo ndio wanaliita dira ya maendeleo ya Tanzania. Mkiweza tafuteni mlisome. Mimi nimelipitia, ukiangalia unaweza kusema ni mwelekeo mzuri kweli, lakini utekelezaji wake ni sufiri. Nililisoma miaka kumi iliyopita lakini leo miaka 10 baadaye nikijaribu kuoanisha yale yaliyosemwa, kuhusu siasa, uchumi, mambo ya jamii na miundo mbinu naona sifuri hakuna kitu, tumerudi nyuma kuliko kupiga hatua yoyote. At least Ben Mkapa alijaribu kupiga hatua kwenye miundo mbinu.

Wakati wa utawala wa awamu ya kwanza kulikuwa na clear vision, ambayo kiongozi wa wakati ule alikuwa akiipigania na kuitekeleza (leave alone uzuri au ubaya), na tulikuwa tunaona wazi kabisa.

Hili sio tatizo la JK, wala Pinda, ni la kwetu watanzania, may be ndivyo tulivyo, kazi zetu na mipango yetu ni ya mkono uende Kinywani. Tunaangalia mwaka huu tu, au mambo yanaweza kutufanya tushinde ubunge kipindi kinachofuata.

Mkuu BL nadhani unazungumzia MKUKUTA, nimepata bahati ya kusoma machache yaliyokuwemo kwenye mkukuta 1 kwa kweli ni mazuri sana kama yangeweza kutekelezwa lakini kwa maoni yangu sidhani utekelzaji wa yaliyomo ndani ya MKUKUTA 1 umefikia hata 5% halafu cha kushangaza sana hata kabla ya kuhakikisha kwamba angalau kunakuwa na implementation ya 70% ya yale yaliyokuwemo kwenye MKUKUTA 1 wakuu wameshaanza kukusanya maoni ya MKUKUTA II!. Mimi hili limenishangaza sana kwa sababu kwa maoni yangu kungekuwa na mkazo kwanza kuhakikisha yale yaliyomo kwenye MKUKUTA 1 yanatekelezwa angalau kwa 70% kabla ya kurukia MKUKUTA II kwa maoni yangu hii dalili ya viongozi ambao hawajali kabisa kuhusu utekezaji wa sera mbali mbali ambazo ni nzuri sana kwenye maandishi na hufukia mashimo tu huku wakitumia mabilioni ya fedha kwa masurufu ili kuandika sera nzuri sana lakini utekelezaji wake ni ZERO.
 
Haya kama historia ni ishu

Go back and check maendeleo ya wazungu kabla ya ukoloni na maendeleo yetu wakati huo.

Vingine ni visingizio tu.Tena nafikiri wakati mwingine wasingekuja hawa wakoloni kutuchapa viboko hadi leo tungekuwa tunavaa ngozi.

Si angalieni ambako wakoloni hawakufika Umasaini, wasandawe.

ama tuache hao wamasai na wasandawe nini tofauti kati ya taifa ambalo halikukubwa na ukoloni Ethiopia na South Afrika ambalo limekuwa chini ya wakoloni mpaka juzijuzi? the fact is very strong.

Haya we,yale yale....Kwanza kabla ya ukoloni it was slavery,go check the facts kwanza halafu urekebishe statement yako..

Pia kabla hatujaendelea mbele sana na mjadala kuna mambo ya msingi ya kujiuliza,je maendeleo ni nini? Je maendeleo hayo yanakuja vipi?Tuanzie hapo kwanza.

Pia wakati huo huo,tutambue kuwa kufanya biashara zaidi na kupata faida ni mojawapo ya nguzo za maendeleo,na ukweli ni kwamba njia kuu za maendeleo hapa duniani zimeshikiliwa na matabaka flani flani toka zamani sana historia iko wazi.

Kwa mfano si kweli kabisa kuwa nchi zilizotutawala zinataka tupate maendeleo,ama zinajali maslahi ya wananchi wa mataifa hayo,na kwahivyo utaratibu ulikuwa ni wa kuzalisha kwasababu yao na si kwasababu ya wananchi,halafu na sisi kwa kuparamia na kupenda mambo marahisi tunasema tu ni export and that is good,tunasahau kwamba kuzalisha tu kwasababu yao ni kuwasahau wananchi kwasababu ni wazi huwezi kupata maendeleo kwa kuwazalishia wengine kabla hujaweza kujizalishia na kujitosheleza wewe mwenyewe.

Baada ya kunaswa kwenye mtego wa kuwazalishia wao huku shughuli hizo zikiwanufaisha wachache,wachache hao hao ndio wamewarudisha tena moja kwa moja wakoloni,ukoloni,ubepari,ufisadi na mambo yote machafu na adui wa maendeleo ya jamii yoyote ile.

Tatizo ni kwamba chini ya mfumo huo huo wa kuwategemea na kuwauzia rasilimali,kumeibuka hatari kubwa sana ya uchumi wa Afrika kuwa wa aina moja na maendeleo vile vile,ni kama kamba iliyoko shingoni.......Wengi wanaamini kuwa mataifa hayo yaliyoendelea simply yanatupenda sana na yanataka tuendelee kama wao,Binafsi i dont buy that...Sasa kama mtu hataki upate maendeleo ya kweli,halafu njia ya kuyapata na namna ya kuyafikia "Maendeleo" hayo iwe ni kumtegemea huyo mwenye maendeleo ambaye hataki na wewe uendelee,je utaendelea?

Hizo solutions za kuchapwa viboko na eti ndivyo ilivyo miafrika ni za kipuuzi,sorry for that.
 
Tatizo la Watanzania ni ile Hali ya Kupenda Mteremko, tunapenda kufanyiwa kila kitu, Tujengewe Vyuo, tujengewe hospital kila Kila tufanyiwe, Hii hali ya Utegemezi imejaa katika Minds za Viongozi wetu na Mbaya Zaidi Hata Viongozi wajao na wao wanaandaliwa katika The same Mfumo wa Kuamini kwamba hatuwezi kufanya Kitu bila Kusema Vizuri na Wahisani!

Its like mtu ambaye amezoea kuingia kwenye mtihani na Karatasi ya majibu, siku akikuta kuna Usimamizi wa Kutosha basi hata mtihani uwe Mrahisi kivipi hataweza kuufanya kwa sababu mind yake inamwambia kwamba hawezi

Sasa as far as tunategemea Viongozi wanaokuwa groomed through Chipukizi, sijui Umoja wa Vijana tusitemee mabadiliko yeyote

Ili kuwe na Mabadiliko anatakiwa Kiongozi mwenye Mtazamo tofauti kabisa Kimfumo na Mtazamo wa Viongozi wetu, We Need some one ambaye hajaonja Raha/Ladha ya Mfumo Tegemezi, tunahitaji mtu ambaye atasema kwamba Kuna mambo inabidi tufanye wenyewe
 
Mimi ningekuwa mshauri wa serikali, ningesema kabisa in the next say 5 yrs tuchague mikoa 5 yenye potential ya kuwa na success haraka kwenye kilimo, investment, viwanda nk na ndio serikali ipeleke asilimia kubwa ya funds na upendeleo huko ili maendeleo ya haraka yafanyike na iwe magnet ya watu kupunguza bomu la mauaji litakalofukuta Dar in the very near future.
Unaweza kupick Kilimanjaro/Arusha/Mbeya/Iringa/Ruvuma na kuanzia hapo.

What up Mo...

Hili wazo lako sio zuri. Sio zuri kwa sababu ingawa lengo lako linaweza kuwa zuri, lakini itakuwia vigumu sana kuwaelewesha wananchi ya mikoa ambayo itajisikia na kujiona imekuwa neglected. Wazo hili linaweza kupandikiza chuki ambazo gharama yake itakuwa kubwa sana.

Hapo juu umetaja mikoa hiyo mitano lakini hujautaja mkoa wangu wa Shinyanga. Unadhani akina ngosha hawatajisikia kutelekezwa? Wakiamua kujitenga na kuanzisha taifa lao utawalaumu?
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?

Hakuna kitu kama hicho kuna mifano mingi tu ya success story kwenye makampuni yanayoongozwa na Watanzania nk. Katika Africa angalia Botswana ingawa population yao ni ndogo nk.

Hata sisi Tanzania kuna mambo mengi ambayo tunaweza kujivunia, ni katika awamu hii ya watoto watukutu ambao wanajilimbikizia mali na kufyonza rasilimali zetu kwa kushirikiana na wageni walafi wachache. Hili litapita na ni jukumu la hii generation kusimama kidete na kuwa counted. Je, tunafanya nini wakati Loliondo imeuzwa? Kwa nini hii generation hawapigi kelele kwa maandamano nk. Fweza za BOT, EPA, Dowans, Richmond et al kwa nini hii generation iko kimya?

Chenge, Mkapa na Lowasa kwa nini hawachukuliwi hatua? Je Watanzania wanaridhika kuishi na mafisadi papa kama Rostam Azizi ambaye atapata millioni 46 za ubunge pamoja na wizi wake wa mali ya umma? Kwa nini Pinda anawachekea wahujumu wa uchumi wa taifa hili? Je tumeshindwa nini sisi raia kuchukua sheria mikononi mwetu? Je, hii generation ingeweza kumtoa mkoloni na kujitawala kama tungerudisha clock nyuma?

Ukweli wa mambo yote hayo yanawezekana lakini tunatakiwa tupate viongozi madhubuti ambao wako radhi kuswekwa ndani na kupigwa virungu au kuuawa kwa kupigania maslahi ya hili taifa.
 
Back
Top Bottom