Kifupi sisi hatuna culture ya kuwa na vision na kuweka goals, tunaelea tu.....

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?

- Heshima sana Rev, nina wasi wasi sana na our nature, nina rafiki yangu majuu anamiliki Travel Agency, anasema experience yake na wabongo ni kwamba wakitaka tiketi yeye huwa anawakubalia tu lakini hafanyi lolote kwa sababu anawajua jinsi walivyo wabadilikaji na wanapokuwa serious wanataka tiketi right away anajua, anasema kabla ya kuwajua vizuri alipata hasara sana maana anawabukia tiekti wanabadilika dakika ya mwisho au hawampigii tena!

- Anasema alichofanya ni kujiunga na wakata tiketi wote za kwenda Tanzania pale town, kwa hiyo mbongo akipiga kwake, the next minute anapiga kwa mwingine tayari wanabonyezana, and then anapiga kwa mwingine wanabonyezana, sasa akiona amebanwa ndio anarudi tena alipoanzia, badala ya kupiga simu tu na kuuliza bei kabla ya ku-commit anything, yeye hupiga na ku-book bila kujali hasara kwa yule agent, wala kujali kwamba next time akiwa na shida kweli itakuwaje! Gues what next time akiwa na shida kweli basi hutuma mtu mwingine ndiye amuulizie! Bwa! ha! ha!

- Hizi ndio tabia zetu na nachelea kusema ni nature yetu!

Respect.


FMEs!
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?


It is the combination of all of the above-highlighted.
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?
It is true and I just don't know why.

Angalia Haiti iliyopata uhuru takriban miaka 210 iliyopita ulinganishe na Singapore iliopta uhuru miaka 50 iliyopta. Angalia Tanzania na Singapore ziliziopta uhuru wakati mmoja.
 
Mkuu kama utakumbuka kuna document linaitwa vision 2025, hilo ndio wanaliita dira ya maendeleo ya Tanzania. Mkiweza tafuteni mlisome. Mimi nimelipitia, ukiangalia unaweza kusema ni mwelekeo mzuri kweli, lakini utekelezaji wake ni sufiri. Nililisoma miaka kumi iliyopita lakini leo miaka 10 baadaye nikijaribu kuoanisha yale yaliyosemwa, kuhusu siasa, uchumi, mambo ya jamii na miundo mbinu naona sifuri hakuna kitu, tumerudi nyuma kuliko kupiga hatua yoyote. At least Ben Mkapa alijaribu kupiga hatua kwenye miundo mbinu.

Wakati wa utawala wa awamu ya kwanza kulikuwa na clear vision, ambayo kiongozi wa wakati ule alikuwa akiipigania na kuitekeleza (leave alone uzuri au ubaya), na tulikuwa tunaona wazi kabisa.

Hili sio tatizo la JK, wala Pinda, ni la kwetu watanzania, may be ndivyo tulivyo, kazi zetu na mipango yetu ni ya mkono uende Kinywani. Tunaangalia mwaka huu tu, au mambo yanaweza kutufanya tushinde ubunge kipindi kinachofuata.
 
Tatizo letu haliko mahali popote isipokuwe kwenye uongozi; wakati tulipopata uhuru kulikuwa na matarajio. Matarajio kwamba na sisi "tunaweza".

The whole concept of "self determination" presumes some sort of readiness on the part of the people demanding it. Mnakumbuka ule wimbo wa enzi zile "juzi na jana siyo leo"? Tulipopata uhuru tulikuwa na matarajio kuwa we could do better than the colonialists and we could pave our own path into the virgin territory of own history.

Kwa hiyo, wazazi wetu walikuwa na jukumu kubwa la kutuongoza katika kuweza. Ni kwa sababu hiyo utaona wale vijana wa miaka ya sitini na sabini mwanzoni they were the most confident, most ambitions most daring and I'll propose most ready to lead. Mafundi wetu walioshirikiana na wachina kujenga Tazara, waliojenga barabara, kubuni miradi ya mashule na vyuo mbalimbali n.k vyote vilikuwa na lengo la kutupa hisia kuwa na sisi tunaweza.

Tulifikia mahali tukaweza kufuta ujinga zaidi ya asilimia 80; tuliweza kuja na kampeni ya nyumba bora ambapo vijiji vya ujamaa (ambavyo kuna watu wanaamini vimefeli) uliweza kukuta watu wanajenga nyumba za matofali ya kuchoma na serikali inawasaidia mabati ya kuezekea (nilioni mwenyewe kwa macho yangu kule Mkongo, Songea mwanzoni mwa 1980s); tulikuja na kampeni ya "mtu ni afya" na kampeni ya "chakula bora" (mnakumbuka "kuleni kuku, mayai, mboga samaki maziwa"..? Vyote hivyo vilikuwa vinatulenga kutupa uwezo wa kufanya.

Tukaanza kujenga viwanda vyetu vya nguo vikiwa na wachoraji na wabunifu wake; tukawa na UFI pale Ubungo, tukawa na viwanda vya viatu (Bora!), tukajaribu kujipa uwezo wa ndani sisi wenyewe; pole pole tukajenga betri, radio za nation na phillips (sauti safi, sauti kubwa, ndiyo yenyewe!) vyote hivi vilifanyika Tanzania. Nimesahau kukumbushia na baskeli zetu za "swala!).

Nyerere alitaka tuwe na uwezo sisi wenyewe kufanya mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu. Hakutaka tubweteke kwa kutegemea vya nje. Sabuni (mbuni, malaika n.k), mafuta, n.k vingi tulikuwa tunafanya sisi wenyewe. Ukienda kwenye maduka yetu ya RTC utakuta bidhaa zetu. Wakenya wakija na Blue Band sisi tunaibuka na TanBond; maziwa ya mgando, chai, n.k (what else can I say!).

Lakini Nyerere alipoondoka tukaambiwa kuwa ameshindwa. Tukakubali kuwa ameshindwa. Tukakumbatia mtu mwenye uwezo. Mwinyi akaingia na kuja na kitu kinachoitwa ruhusa (maarufu kama Ruksa). Hakujali nini tunaweza kufanya sisi akasema Watanzana wamenyimwa anasa. Hivyo, akafungulia vya wageni kuja nchini na mara moja kuanza kuua vya kwetu; tukaanza kupoteza ule uwezo tuliotaka kujijengea; tukakubali kuwa hatuwezi.

Tukaanza kuagiza mitumba (wenyewe tukacheka kuvaa nguo za vitambaa vya mwatex na urafiki!), tukaanza kuingiza kwa nguvu Kimbo na wenzake, tukaanza kuona vya muhimu ni Televisheni n.k (wapo watu wanalalamika ati kwanini hatukuwa na TV wakati wa Nyerere!); elimu ya watu wazima ikatupwa pembeni, usalama wa taifa ukaharibiwa na matokeo yake Mkapa anapoingia hakurudi kwenye fikra za Mwalimu akaja na dhana yake ya wawekezaji.

Wakaanza kukaribisha wawekezaji kwenye kila kitu hata vile ambavyo sisi wenyewe tuliviweza (fikiria NBC na Bima) wakaanza kubinafsisha hata vyenye faida. Badala ya kutafuta mbinu ya kutengeneza vya kwetu na kutupa uwezo wakatuletea hadi polisi ili kulazimisha wageni watuendeshee Tanesco; Tukageuka na kuwa taifa la watu duni na tegemezi.

Akaja ndugu yetu Kikwete; akiwa ni mwathirika wa fikra tegemezi ameendelea kueneza itikadi ya uongo kuwa bila wageni hatuwezi kuendelea, bila wawekezaji hatuwezi kitu. Amepita huko na huko akiomba wenye akili kuja kutuendeshea uchumi wetu. Wawekezaji kwenye kila kitu na Watanzania wakibakia kuwa wadau tu. Matokeo yake Tanzania ya leo hata mkoloni anatushangaa! Tumefikaje hapa?

Ninachosema ni kuwa hatukuanza hivyo. Rudi tuwaulize wazee wetu, jamani kina Salim walikuwa wanavutia nje ya nje, tulikuwa na wasomi waliobobea miaka hiyo, tulikuwa na wataalamu wengi tu na wenye uwezo. Leo hii, tumebakia kuomba omba utaalamu. Leo hii ukienda kwenye maduka yetu utakuta hadi vitunguu toka nje! mazuria toka ng'ambo na kandambili na viatu toka nje!

Mtanzania hana fahari ya kitu chake tena; hizo ofisi za serikali ni ngapi zimenunua fanicha toka ndani? Ni ofisi ngapi zinatumia maua toka ndani, marumaru wanazotandaza katika nyumba zao zinatoka wapi? Uliza kuhusu mapazia?

Mtu mmoja alisema ufisadi ukikomeshwa tutaandamana; siwezi kushangaa. Kwa sababu kwa mara ya kwanza tunaweza kulazimishwa kujiangalia sisi wenyewe! Kuna siku ambayo tutaitwa kuita nguvu kutoka ndani yetu na kutafuta asili ya nguvu hiyo kutoka kwa watu wetu. Lakini yote inaanzia na uongozi kwanza.

Uongozi wenye fikra tegemezi, hauwezi kuongoza taifa kuelekea kujiamini.

Bob Marley put it better..

Old pirates, yes, they rob I;
Sold I to the merchant ships,
Minutes after they took I
From the bottomless pit.
But my hand was made strong
By the 'and of the Almighty.
We forward in this generation
Triumphantly.
Won't you help to sing
This songs of freedom
'Cause all I ever have:
Redemption songs;
Redemption songs.

Emancipate yourselves from mental slavery;
None but ourselves can free our minds.
Have no fear for atomic energy,
'Cause none of them can stop the time.

How long shall they kill our prophets,
While we stand aside and look? Ooh!
Some say it's just a part of it:
We've got to fullfil the book.

Won't you help to sing
This songs of freedom-
'Cause all I ever have:
Redemption songs;
Redemption songs;
Redemption songs.
---
/Guitar break/
---
Emancipate yourselves from mental slavery;
None but ourselves can free our mind.

Wo! Have no fear for atomic energy,
'Cause none of them-a can-a stop-a the time.
How long shall they kill our prophets,
While we stand aside and look?
Yes, some say it's just a part of it:
We've got to fullfil the book.
Won't you have to sing
This songs of freedom? -
'Cause all I ever had:
Redemption songs -
All I ever had:
Redemption songs:
These songs of freedom,
Songs of freedom.
 
Mwanakijiji, hayo yote au mengi ya uliyoyasema na kuyataja yanahusu Tanzania. Je, ina maana na kwingineko Afrika hususan kusini mwa sahara (black Africa) na kwenyewe tatizo lao ni uongozi mbovu? Kama ni hivyo ina maana uongozi mbovu ni common denominator Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara. Sasa kwa nini kote huko kuwe na uongozi mbovu? Ndivyo Tulivyo kuwa hatuwezi uongozi? What is it? Maana mimi siamini kabisa kuwa hizo nchi zingine za Kiafrika zimetuzidi kihivyo. Nimeshabahatika kutembela baadhi ya nchi za Kiafrika na sikuona lolote la ziada tulilozidiwa. Kama ufisadi hata Cameroun upo. Kama vya kupenda vya Ulaya basi hata Niger wanapenda vya Ulaya. Sasa nisichoelewa ni kwa nini Afrika nzima kusini mwa sahara ni sehemu iliyo ktk kundi la nchi za ulimwengu wa tatu. Sielewi kabisa hili. Inakuwa kuwaje eneo kubwa kama hili kiwango cha maendeleo kinakuwa kimefanana sana?

Bara la Ulaya sio nchi zote zilizoendelea saana kihivyo. Hakuna uniformity ya maendeleo. Huwezi kulinganisha kwa mfano maendeleo ya Ujerumani na Uholanzi na yale ya Romania. Lakini hata hao Romania wameendelea kuliko nchi karibu zote kama sio zote kabisa za Afrika, Sasa huu uongozi mbovu ina maana upo Afrika nzima? WTF.....
 
Mwanakijiji, hayo yote au mengi ya uliyoyasema na kuyataja yanahusu Tanzania. Je, ina maana na kwingineko Afrika hususan kusini mwa sahara (black Africa) na kwenyewe tatizo lao ni uongozi mbovu? Kama ni hivyo ina maana uongozi mbovu ni common denominator Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara. Sasa kwa nini kote huko kuwe na uongozi mbovu? Ndivyo Tulivyo kuwa hatuwezi uongozi? What is it? Maana mimi siamini kabisa kuwa hizo nchi zingine za Kiafrika zimetuzidi kihivyo. Nimeshabahatika kutembela baadhi ya nchi za Kiafrika na sikuona lolote la ziada tulilozidiwa. Kama ufisadi hata Cameroun upo. Kama vya kupenda vya Ulaya basi hata Niger wanapenda vya Ulaya. Sasa nisichoelewa ni kwa nini Afrika nzima kusini mwa sahara ni sehemu iliyo ktk kundi la nchi za ulimwengu wa tatu. Sielewi kabisa hili. Inakuwa kuwaje eneo kubwa kama hili kiwango cha maendeleo kinakuwa kimefanana sana?

Bara la Ulaya sio nchi zote zilizoendelea saana kihivyo. Hakuna uniformity ya maendeleo. Huwezi kulinganisha kwa mfano maendeleo ya Ujerumani na Uholanzi na yale ya Romania. Lakini hata hao Romania wameendelea kuliko nchi karibu zote kama sio zote kabisa za Afrika, Sasa huu uongozi mbovu ina maana upo Afrika nzima? WTF.....

Mkuu Julius, unayosema ni kweli. Lakini ukiangalia kwa undani unaona wazi kabisa kuwa we can be better than we are, kama hatuna akili basi tushindwe tu kurusha roketi, au tushindwe kupeleka mtu kwenye sayari ya Mars, mengi ambayo ninhakika tunaweza kufanya hatifanyi. Tunaweza kuwa better kwenye mambo mengi tu hata kuliko nchi za Ulaya. Before ujinga kuanza cote d'ivorie nchi ilikuwa better hata wafaransa wenyewe walikuwa wanatamani kwenda kila siku, Zimabbwe yenyewe ilikuwa nzuri mpaka wazungu wanang'ang'ania kubaki huko. Botswana mpaka leo iko much better hata kuliko nchi za Ulaya Mashariki. Leo bongo kuna watu wengi sana wanachukua mshara mzuri kuliko watu wa karibu nchi nyingi a Ulaya mashariki, lakini still wenzetu licha ya kuwa na mishahara midogo they live better than us.

Tatizo kubwa la sisi ni ubinafsi kupita kiasi. Ni viongozi wachache sana wenye uzalendo kwa Tanzania, hata sisi watanzania wenyewe tunakatishwa tamaa na viongozi wetu. I have always been thinking why should work my damn ass off, while someone else (not me, not my country) will benefit from my sweat. Viongozi wetu wetu creativity yao iko kwenye destruction and embezzlement, hili ni tatizo.
 
Mwanakijiji, hayo yote au mengi ya uliyoyasema na kuyataja yanahusu Tanzania. Je, ina maana na kwingineko Afrika hususan kusini mwa sahara (black Africa) na kwenyewe tatizo lao ni uongozi mbovu?

Jibu langu ni ndiyo; yote yanaanzia kwenye uongozi na wale wanaowapa watu uongozi. Siyo sawa hasa kusema uongozi mbovu lakini zaidi ni uongozi usiona uwezo (si kwamba umeharibika).

Kama ni hivyo ina maana uongozi mbovu ni common denominator Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara. Sasa kwa nini kote huko kuwe na uongozi mbovu? Ndivyo Tulivyo kuwa hatuwezi uongozi? What is it? Maana mimi siamini kabisa kuwa hizo nchi zingine za Kiafrika zimetuzidi kihivyo. Nimeshabahatika kutembela baadhi ya nchi za Kiafrika na sikuona lolote la ziada tulilozidiwa.

Hapana siyo Tanzania tu.. suala la uongozi linahusu sehemu nyingi duniani; siyo za watu weusi tu bali hata za watu weupe. Kinyume na unavyofikiria utaona kuwa hata hizo nchi za weupe si zote zimepiga hatua kubwa za maendeleo. Bado kuna watu wanaishi katika umaskini katika baadhi ya nchi hizo. Ukienda Bulgaria, maeneo ya Georgia, Ukraine, Urusi n.k bado kuna sehemu watu wanatumia jembe la mkono na huwezi kuamini! Hiyo china yenyewe pamoja na "maendeleo" tunayoyaona Beijing, Shanghai na Hong Kong bado inamaeneo watu wanaishi kama wako Kyela! Lakini katika Afrika hii hii utaona kuna nchi ambazo zinapiga hatua zaidi pole pole na ndio maana wengine tunaangalia ka nchi kama Rwanda kana potential ya kufanya kile ambacho nchi kama Uganda, Kenya na Tanzania zimeshindwa. Na Kagame amejifunza sana kwa Mwalimu; as a matter of fact anacopy program zile zile za Mwalimu wakati wa Uhuru lakini sitoshangaa akija Rais mwingine huko Rwanda ikajikuta inaelekea huku huku tulikofikia sisi.


Kama ufisadi hata Cameroun upo.
Hata Marekani, Japani, Ujerumani na UK ufisadi upo! Kipimo hakiwezi kamwe kuwa ufisadi. Kama uhalifu upo Detroit kama ulivyo Dar, kama wizi wa magari upo Miami kama ulivyo Nairobi; so hatuwezi kuweka kipimo kiwe uhalifu. Kama ni uchangudoa basi upo mitaa ya Ohio Dar kama ilivyo barabara ya nane hapa Detroit; hatuwezi kutumia uchangudoa kama kipimo.


Kama vya kupenda vya Ulaya basi hata Niger wanapenda vya Ulaya.

Hata wamarekani wanapenda vya Ulaya, na Wajapani wanapenda vya Marekani, na Wa Korea wanapenda vya US; hatuwezi kutumia kupenda vya ulaya kama kipimo.

Sasa nisichoelewa ni kwa nini Afrika nzima kusini mwa sahara ni sehemu iliyo ktk kundi la nchi za ulimwengu wa tatu. Sielewi kabisa hili. Inakuwa kuwaje eneo kubwa kama hili kiwango cha maendeleo kinakuwa kimefanana sana?

Ni uongozi; uongozi; uongozi;. Damu ya mzungu ni nyekundu kama ilivyo damu ya mfipa; mtandao wa mfumo wa fahamu wa Mjerumaini umetandazwa mwili kama ulivyotandazwa mfumo wa fahamu wa Mmakua! Ukienda kwa wazungu utaona kuwa makundi yao ya damu ni sawa kabisa na yale ya wanyaturu! Ndio maana utaona kuwa katika sayansi watu weusi, wachina, wahindi, wazungu, wajapani, waarabu n.k siyo species tofauti za binadamu! Sisi sote tuko specie moja tu. So hakuna sababu ya kibaiolojia wala ya kigenetic inayoweza kumfanya mtu wa Afrika kushindwa kufanya kile ambacho kinafanywa na mtu mwingine.

Ni kutokana na hilo usishangae wapo Waafrika ambao wameweza kusomea na kufanya yale ambayo tulidhania ni ya "wazungu". Tunaendesha magari yao, tunachezea kompyuta zao, tunajifunza fizikia yao na kufanya vizuri kama wao kama siyo zaidi n.k I do not believe in the INFERIORITY THEORY OF BLACK PEOPLE.

Bara la Ulaya sio nchi zote zilizoendelea saana kihivyo. Hakuna uniformity ya maendeleo. Huwezi kulinganisha kwa mfano maendeleo ya Ujerumani na Uholanzi na yale ya Romania. Lakini hata hao Romania wameendelea kuliko nchi karibu zote kama sio zote kabisa za Afrika,

Sasa hapa ni lazima tuangalie kitu kingine cha tofauti sana; ni kwamba huwezi kuelewa kutoendelea kwa haraka kwa Afrika bila ya kuangalia historia ya Afrika. Kwa kiasi kikubwa unaposema kuendelea kwa Europe unataka kujaribu kukutenganisha na kutoendelea kwa Afrika. There is an inversely relationship between the development of Europe and the underdevelopment of Africa. The two can not be taken singularly.

Sasa huu uongozi mbovu ina maana upo Afrika nzima? WTF.....

the answer again is Yes! unless we change the nature of our leadership and how we are governed we are doomed to perpetual underdevelopment. Africa suffer from an acute shortage of inspiring, daring and robust leadership. It is a sort of leadership anemia.
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?

Je hawa watanzania wakiwa nje ya nchi ndio tabia zao ni hizo hizo ulizozitaja?

Kwenye story nyingi za wazee wetu wa karne ya 18 machifu, ma mangi, watemi n.k, mbona inaonekana walikuwa na vision na kutekeleza waliyoyapanga?

matatizo uliyootodhesha ya kizazi cha sasa yameanza lini? maana hata JKN alikuwa mzuri kusimamia anayoyapanga na kuamua.

I believe kuna 'connection' imekatika somewhere, but I fail to believe that matatizo uliyoyataja ni nature. Unless watanzania wanatabia ya Kinyonga, wakifika Tz wanadumaa akili wakienda Egypt akili zinaongezeka kidogo wakienda first world countries akili zinaongezeka kabisa!!

why Tanzanian with such behaviours anaweza aka-adapt kwa aharaka maisha na mikikimikiki ya maisha ya dunia ya kwanza?
 
Ni uongozi; uongozi; uongozi;. Damu ya mzungu ni nyekundu kama ilivyo damu ya mfipa; mtandao wa mfumo wa fahamu wa Mjerumaini umetandazwa mwili kama ulivyotandazwa mfumo wa fahamu wa Mmakua! Ukienda kwa wazungu utaona kuwa makundi yao ya damu ni sawa kabisa na yale ya wanyaturu! Ndio maana utaona kuwa katika sayansi watu weusi, wachina, wahindi, wazungu, wajapani, waarabu n.k siyo species tofauti za binadamu! Sisi sote tuko specie moja tu. So hakuna sababu ya kibaiolojia wala ya kigenetic inayoweza kumfanya mtu wa Afrika kushindwa kufanya kile ambacho kinafanywa na mtu mwingine.

.

Supported!
 
Jibu langu ni ndiyo; yote yanaanzia kwenye uongozi na wale wanaowapa watu uongozi. Siyo sawa hasa kusema uongozi mbovu lakini zaidi ni uongozi usiona uwezo (si kwamba umeharibika).

Nayakumbuka maneno ya FMES...'viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe wananchi'

Hapana siyo Tanzania tu.. suala la uongozi linahusu sehemu nyingi duniani; siyo za watu weusi tu bali hata za watu weupe.

Ni kweli. Lakini sisi tumezidi.

Kinyume na unavyofikiria utaona kuwa hata hizo nchi za weupe si zote zimepiga hatua kubwa za maendeleo.

Sijui unadhani mimi nafikiri nini lakini kama unadhani mimi nafikiri kuwa nchi zote za weupe zimepiga hatua "kubwa" kimaendeleo unakosea. Natambua kuwa viwango vya maendeleo ktk nchi hizo vimetofautiana. Lakini kwa ujumla, nchi hizo nyingi ukizilinganisha na maendeleo ya nchi nyingi za Kiafrika bado kuna gap kubwa. Nakuhakikishia leo hii Tanzania ingekuwa na maendeleo kama yale ya Ukraine au Urusi...somebody would have never heard the end of it. Guarantee that.

Bado kuna watu wanaishi katika umaskini katika baadhi ya nchi hizo. Ukienda Bulgaria, maeneo ya Georgia, Ukraine, Urusi n.k bado kuna sehemu watu wanatumia jembe la mkono na huwezi kuamini! Hiyo china yenyewe pamoja na "maendeleo" tunayoyaona Beijing, Shanghai na Hong Kong bado inamaeneo watu wanaishi kama wako Kyela!

Hata Marekani, Ujerumani, Uingereza na kwingineko bado kuna watu wanaishi ktk umaskini. Umaskini hauwezi kufutwa kabisa kabisa hata iweje. Kusema unaweza kabisa kufutwa....hiyo ni utopia!

Lakini katika Afrika hii hii utaona kuna nchi ambazo zinapiga hatua zaidi pole pole na ndio maana wengine tunaangalia ka nchi kama Rwanda kana potential ya kufanya kile ambacho nchi kama Uganda, Kenya na Tanzania zimeshindwa.

Miaka 12 au 13 iliyopita Uganda ndio ilikuwa poster child ya success stories za Afrika mpaka wakapata "heshima" ya kutembelewa na Bill Clinton 1998. So I'm not too impressed by Rwanda. Soon they are going to hit a plateau and we will be back here again wondering what happened. Mark my words.

Na Kagame amejifunza sana kwa Mwalimu; as a matter of fact anacopy program zile zile za Mwalimu wakati wa Uhuru lakini sitoshangaa akija Rais mwingine huko Rwanda ikajikuta inaelekea huku huku tulikofikia sisi.

Lakini Rwanda si wana TV? Sisi hatukuwa nazo....so kuna tofauti kidogo!

Hata Marekani, Japani, Ujerumani na UK ufisadi upo! Kipimo hakiwezi kamwe kuwa ufisadi. Kama uhalifu upo Detroit kama ulivyo Dar, kama wizi wa magari upo Miami kama ulivyo Nairobi; so hatuwezi kuweka kipimo kiwe uhalifu. Kama ni uchangudoa basi upo mitaa ya Ohio Dar kama ilivyo barabara ya nane hapa Detroit; hatuwezi kutumia uchangudoa kama kipimo.

Nakubaliana nawe. Je, kipimo ni kipi?

Hata wamarekani wanapenda vya Ulaya, na Wajapani wanapenda vya Marekani, na Wa Korea wanapenda vya US; hatuwezi kutumia kupenda vya ulaya kama kipimo.

Ndio unaweza kwa sababu sisi tumezidi mno kwa kupenda vya nje. Mwenyewe hapo mwanzo umetolea mfano wa mitumba ya ulaya dhidi ya nguo tulizokuwa tunatengeneza wenyewe. Leo hii watu humu wanawaona Kiranga na Bluray kuwa ma genius kwa sababu wanaandika Kiingereza "kigumu". Unachoona humu ni akisi tu ya kile jamii nzima ilivyo. Rejea kusoma kitabu chat The Beautyful ones are not yet born.....

Ni uongozi; uongozi; uongozi;. Damu ya mzungu ni nyekundu kama ilivyo damu ya mfipa; mtandao wa mfumo wa fahamu wa Mjerumaini umetandazwa mwili kama ulivyotandazwa mfumo wa fahamu wa Mmakua! Ukienda kwa wazungu utaona kuwa makundi yao ya damu ni sawa kabisa na yale ya wanyaturu! Ndio maana utaona kuwa katika sayansi watu weusi, wachina, wahindi, wazungu, wajapani, waarabu n.k siyo species tofauti za binadamu! Sisi sote tuko specie moja tu. So hakuna sababu ya kibaiolojia wala ya kigenetic inayoweza kumfanya mtu wa Afrika kushindwa kufanya kile ambacho kinafanywa na mtu mwingine.

Really? Ok...elezea basi sababu za ugonjwa wa sickle cell anaemia maana naambiwa unawadhuru zaidi watu wenye wa sub saharan Africa

Ni kutokana na hilo usishangae wapo Waafrika ambao wameweza kusomea na kufanya yale ambayo tulidhania ni ya "wazungu".

Yeah...wapo wamesomea kwa wazungu chini ya uangalizi au usimamizi wa wazungu na mengi waliyosomea yameandikwa na wazungu na wameyasoma kwa kujifunza na kutumia lugha za wazungu. What's new there?

Tunaendesha magari yao, tunachezea kompyuta zao, tunajifunza fizikia yao na kufanya vizuri kama wao kama siyo zaidi n.k I do not believe in the INFERIORITY THEORY OF BLACK PEOPLE.

Tatizo hatuwezi kutengeneza vya kwetu. Kazi yetu ni kutumia vya kwao. Amini au usiamini ktk complex yoyote ile lakini ukweli haubadilshwi na imani yako.

Sasa hapa ni lazima tuangalie kitu kingine cha tofauti sana; ni kwamba huwezi kuelewa kutoendelea kwa haraka kwa Afrika bila ya kuangalia historia ya Afrika. Kwa kiasi kikubwa unaposema kuendelea kwa Europe unataka kujaribu kukutenganisha na kutoendelea kwa Afrika. There is an inversely relationship between the development of Europe and the underdevelopment of Africa. The two can not be taken singularly.

Hii ni BS. Kwa kifupi nitatumia mfano wa Raj Patel. Kati ya Punda na binadamu nani mwenye akili? Ukipata jibu lake sasa jiulize kati ya hao wawili nani anamwongoza nani.

the answer again is Yes! unless we change the nature of our leadership and how we are governed we are doomed to perpetual underdevelopment. Africa suffer from an acute shortage of inspiring, daring and robust leadership. It is a sort of leadership anemia.

I can't argue much about that although I think it is just more than leadership that is needed to develop.
 
Hata Marekani, Ujerumani, Uingereza na kwingineko bado kuna watu wanaishi ktk umaskini. Umaskini hauwezi kufutwa kabisa kabisa hata iweje. Kusema unaweza kabisa kufutwa....hiyo ni utopia!

Umeshawahi kusikia nchi ya Malta?


Miaka 12 au 13 iliyopita Uganda ndio ilikuwa poster child ya success stories za Afrika mpaka wakapata "heshima" ya kutembelewa na Bill Clinton 1998. So I'm not too impressed by Rwanda. Soon they are going to hit a plateau and we will be back here again wondering what happened. Mark my words.

ndicho nilichokisema; ni uongozi.



Lakini Rwanda si wana TV? Sisi hatukuwa nazo....so kuna tofauti kidogo!

sasa na leo sisi tunazo?



Nakubaliana nawe. Je, kipimo ni kipi?

swali zuri.



Ndio unaweza kwa sababu sisi tumezidi mno kwa kupenda vya nje. Mwenyewe hapo mwanzo umetolea mfano wa mitumba ya ulaya dhidi ya nguo tulizokuwa tunatengeneza wenyewe. Leo hii watu humu wanawaona Kiranga na Bluray kuwa ma genius kwa sababu wanaandika Kiingereza "kigumu". Unachoona humu ni akisi tu ya kile jamii nzima ilivyo. Rejea kusoma kitabu chat The Beautyful ones are not yet born.....

ni kwa sababu ya uongozi; mwanzoni tulikuwa tunapenda vya kwetu na kuvitumia kwa fahari.



Really? Ok...elezea basi sababu za ugonjwa wa sickle cell anaemia maana naambiwa unawadhuru zaidi watu wenye wa sub saharan Africa

Yapo magonjwa mengine yanayowapata watu weupe zaidi vile vile lakini haina maana huwezi kupata mweupe mwenye sickle cell!



Yeah...wapo wamesomea kwa wazungu chini ya uangalizi au usimamizi wa wazungu na mengi waliyosomea yameandikwa na wazungu na wameyasoma kwa kujifunza na kutumia lugha za wazungu. What's new there?

sidhani kama hiyo ni hoja; wakati wa Warumi lugha iliyotawala ilikuwa ni Kilatini! Leo hii lugha kubwa ni kiingereza usije kushangaa huko tunakokwenda tukajifunza Kichina zaidi. Mambo mengine ni histojiografia inaoongoza.



Tatizo hatuwezi kutengeneza vya kwetu. Kazi yetu ni kutumia vya kwao. Amini au usiamini ktk complex yoyote ile lakini ukweli haubadilshwi na imani yako.

Hatuwezi kutengeneza vya kwetu kwa sababu ya uongozi. Hivi unajua hata huko kwa wazungu na wenyewe walikuwa wanafanya madudu tunayoyafana sisi wakati huu?





[/quote]I can't argue much about that although I think it is just more than leadership that is needed to develop.[/QUOTE]

nope. It starts and ends with leadership; bear in mind I'm not speaking of political leadership only!
 
...aah, Mungu hajapenda bana! (ndiye wa kulaumiwa na excuse 'yetu' kubwa)
 
Quoting the one and Only Kiranga, let me open a window of debate and slugs! If not the statement sort of quantify Nyani/Julius Ndivyo tulivyo.

Be it in Social aspect, economy, political, cultural, production, education entrepreneurship, management, leadership ot whatever, we always fail if not falling short and one has to wonder, TUNA MATATIZO GANI?

Is it psychological issues, colonial wounds, inferiority complex or just our nature?
NATURE BABA!ndivyo tulivyo.ndo maana wapo wataalamu ambao HAWATAKI KABISA KURUDI KWAO TANZANIA...!ukiwauliza kwanini wanakwambia ''bongo pamechoka''
 
NATURE BABA!ndivyo tulivyo.ndo maana wapo wataalamu ambao HAWATAKI KABISA KURUDI KWAO TANZANIA...!ukiwauliza kwanini wanakwambia ''bongo pamechoka''

sasa huko Bongo si wataalamu nao wapo au hao wa huko siyo wataalamu hadi waje walioko nje?
 
sasa huko Bongo si wataalamu nao wapo au hao wa huko siyo wataalamu hadi waje walioko nje?
NAAMINI kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu......ndo maana tuna-hire experts kila leo...ndo maana tunaenda india kutibiwa kila leo,we need our professionals back here.....!hizi kelele za chura tumezichoka.wanapiga kelele huku 'THEY ARE WORKING FOR U.S ECONOMY' hell tanzanians
 
NAAMINI kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu......ndo maana tuna-hire experts kila leo...ndo maana tunaenda india kutibiwa kila leo,we need our professionals back here.....!hizi kelele za chura tumezichoka.wanapiga kelele huku 'THEY ARE WORKING FOR U.S ECONOMY' hell tanzanians

mbona maneno makali! haijalishi kama wote watarudi huko nyumbani; ulimwengu hauendi hivyo. Kama mnawahitaji kama maexpatriate hakikisheni mnatangaza ofa kama ma expatriates. Kama watalaalamu waliopo sasa nyumbani hawasikilizwi na kufuatwa unafikiri wakija wataalamu watanzania kutoka majuu ndio watasikilizwa? As a matter of fact mbona wapo wengi wamesharudi, wanasikilizwa?

Maendeleo ya Tanzania yasilaumiwe kukosekana kwa watalaamu ambao hawapo.
 
NAAMINI kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu......ndo maana tuna-hire experts kila leo...ndo maana tunaenda india kutibiwa kila leo,we need our professionals back here.....!hizi kelele za chura tumezichoka.wanapiga kelele huku 'THEY ARE WORKING FOR U.S ECONOMY' hell tanzanians

Umegusa penyewe haswaaa!!!!
 
Umegusa penyewe haswaaa!!!!

mimi nafikiri ni nature yaani uweusi. angalia nchi zenye watu weusi kuanzia africa, southern asia, latin america ndo umaskini unatishia life. May be wanasayansi wazidi kufanya tena utafiti kama kweli genetically hatutofautiani na hawa weupe. kadiri rangi inavyokolea uweupe na akili na development pia. check white above yellow, yellow too above black.hata weusi waliozaliwa America miaka na miaka ni bado utofauti unaonekana tu na ni asilimia kubwa tu ya population. wavumbuzi wengi, mabigwa wanasayansi wengi na hata research nyingi zenye impact factor kubwa duniani wengi ni weupe tu. S. africa kwa sababu ya makaburu angalia utofauti wake hii ngozi inatugharimu kweli
 
Back
Top Bottom