Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Krup hadi ndani police! Police wa zamu wamepigwa butwaa kumuona kijana mmoja kaingia police post kwa ghafla na kwa kasi ya ajabu huku akihema. Kabla hawajaanza kumuhoji kulikoni wanaliona kundi la vijana kama saba hivi nje wakipaza sauti kwa maaskari hao wamtoe yule kijana aliyeingia ndani ghafla kwa vile ni mgonjwa wa akili na kwamba amewatoroka wakati wakimpeleka hospitali. Wakati wale askari wakijiandaa kumtoa yule kijana akawaambia wale askari, "hawa jamaa ni waongo na ukweli ni kwamba nimempora mmoja wao simu tena hii hapa hivyo mkiniachia tu wanakwenda kuniua". Unajua ni nn kilifuata, ntarudi nakwenda break