zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Mkuu, mimi kama binadamu, ninaelewa mipaka ya wajibu na haki zangu kama raia. Kama raia na kama binadamu, siwezi kutii amri za serikali kama hizo ni kandamizi, kama amri hizo zinaniwekea amri ambapo wengine zinawaruhusu. zomba, tuombe Mungu mimi na wewe kuwa mfumo huu uliopo sasa ubadilike, vyenginevyo hii nchi itafika pabaya, siombi iwe hivyo lakini ikitokea uelewe sababu ni hii ya amri za upendeleao, kibaguzi na kandamizi.
Naona bado unakwepa suala la kwa nini siku hiyo hiyo CDM walipovamiwa na polisi kwa kufungua matawi, Bububu walikuwa na mkutano wa hadhara wa nje, tafauti ipo wapi? Kwa nini kila ambapo polisi hawaingilii mikutano ya CDM kunakuwa na amni lakini amani huvunjika pale wanapopigwa mabomu?
Unaweza kujibu kijazba na upofu wa moyo, lakini usidhani kama tukifikia huko mimi na wewe, watoto wetu, jamaa zetu na marafiki zetu tutasalimika na hilo. Vita havina macho, mara nyingi huathirika zaidi waliomo kuliko waliomo.
MUNGU AINUSURU TANZANIA!
Hu mfumo unaendeshwa na katiba na sasa hivi kuna mchakato wa kubadili katiba. Usijidanganye kuwa kubadili chama ndio mwisho wa matatizo. Vyama vipya na hususan chama chenye mfumo kama wa chadema havifai kabisa, unaona wazi kabisa kuwa viongozi wa chadema hata maadili hawana, halafu unategemea lipi jema kutoka kwao?
Unaona kabisa jinsi wanavyoongea, wanavyosambaza chuki mpaka wanafikia kusema wazi kabisa kuwa hii nchi "haitatawalika" halafu bado unafikiri kuwa wao watakuwa bora? huo ni ufinyu wa mawazo. Nyota njema huonekana alfajiri. Chadema hawana madaraka ya nchi tunaona damu zikimwagika kila wanapopita wakishika madaraka jee?
Kwanza wasahau kupewa madaraka kwa kura, za nani? msidanganyike.