Kifo kupitia mikono ya POLISI – Kosa la Marehemu?

AshaDii

Platinum Member
Apr 16, 2011
16,190
18,077
Habari wana JF,

Hali ya nchini kwetu Tanzania hadi hapa tulipofika kwa sasa haijalishi kuwa tunaenda wapi mana tayari tumefika pabaya… Kwa kundi ama hali yoyote ile ifikapo pabaya dawa pekee ni suluhu ya hio hali mbaya iliyopo iondolewe mara moja kwa njia mbadala. Ikumbukwe kuwa unapokuwa na hali mbaya mara nyingi kama sio zote HAIJALISHI hio njia mbadala ni ipi maadamu tu ipatikane nafuu ya hio hali mbaya kutoweka.

Ifikapo hali imedorola hadi kuwa mbaya kwa wahusika, maneno matamu na kutia moyo hayana maana tena! Ahadi za kuwekewa uahueni kwa maneno yaliyowahi tayari kutamkwa na kujirudia kama nyimbo za chorus hazina maana tena! Kupozana na kupeana pole kwa maneno ya faraja na kusihi hakuna mana tena! Hii yote kwa sababu hali inapokuwa mbaya kamwe haipati unafuu bila suluhu ya kupunguza ama kuitoa kabisa hio hali ambayo kwa wakati huo tayari ni sugu.

Mara nyingi hata magonjwa kama vile kansa inapokuwa imepatwa katika kiungo na ikaonekana ni sugu ipo njia mbili tu za kutibu; unaua kabisa kiungo kwa kukata kabisa kitoke ili kisisambaze maeneo mengine, ama unaacha na hatima yake ni kifo cha kutaraji ukibaki unahesabu siku za kufa. Swali linabaki kama unaweza kupona kwanini ukubali kuhesabu siku za kifo chako?

Kwa muda mfupi sana kumetokea vifo (ambavyo tuna habari navyo) kwa mkono wa Jeshi la Polisi viwili. Ndani ya mda mfupi vijana wawili wenye nguvu ya kutosha kabisa kujenga taifa letu hili lililo sugu ya kutojengeka wamefariki.

Tarehe 27/08/2012 Ally Zona kafariki Morogoro baada ya polisi kuingilia kati maandamano yaliyokuwa sio rasmi ya CHADEMA kusababishia vurugu zilizopelekea kurushwa kwa risasi na hatimae kumpata yeye kichwani moja wapo ya risasi hizo, iliyopelekea kifo cha papo hapo.

Siku 5 baadae Jana tarehe 02/09/2012 kimetokea kifo kingine tena, safari hii mmoja wa wanahabari mashuhuri anaejulikana kwa jina la David Mwangosi. Vifo hivi vinasikitisha sana… Natoa pole toka moyoni kwangu kwa wafiwa wa hao marehemu. Sie tunalia kama taifa, wao wanalia kuwa mtoto/baba/kaka/mjomba na pengine tegemezi la familia limeyeyuka ghafla kwa njia ambayo ingeweza kabisa kuepushwa! Inasikitisha… Na inauma pia.

Maswala/swali ya msingi ya kujiuliza tokana na matukio hayo (Na mtazamo wangu juu ya hayo):-

Ni kweli kuwa kila vifo vya polisi ambavo vimekuwa vikitokea vinahusiana moja kwa moja na CHADEMA?
Kumekuwa na misemo kwa baadhi ya wananchi na hata pia wanajamvi kuwa chanzo cha vifo hivi ni vurugu za wana CDM; labda kwa sababu tu hizo vurugu chanzo chake huwa uwepo wa CDM hapo. Nabaki najiuliza na kushangaa, jamani watu wanapoteza maisha lakini bado tu hamfunguki na kutakasika hayo macho kuona picha halisia jinsi ilivo? Mie nakataliana na hii Imani kuwa CDM ndio wanasababisha kupelekea vifo hivo.

Wananchi wenzangu wanaomini katika hili, naombeni sababu za msingi za kuamini hivo na hapo hapo mnipe jibu kuwa wale vijana wanao uwawa kule migodi ya Barrick tena kwa kulinda maslahi ya wageni sio wazawa ni CDM husababisha? Mnasemaje kuhusu vifo vya vijana watatu walio uwawa hata wiki haijaisha kama tu wanyama Fulani, ha hapo hapo ni dhahiri kuwa case closed?

Ni kweli kila itokeapo kifo hicho kwa njia moja ama nyingine hao marehemu linakuwa ni kwa ajili ya makosa yao na uzembe wao hao marehemu?
Ingekuwa kuwa kila wanaofariki wapo katika kundi husika ambalo kwa kesi hizi za vurugu ni CDM, walau kunaweza kukajengwa chembe ya mbegu kichwani kuwa marehemu alikuwa akirusha mawe na kuletea fujo hao polisi wa kutuliza vurugu. Inakuwaje pale mtu ambae yupo kando kabisa anauwawa? Hapa ni dhahiri kabisa kuwa makosa na uzembe (tena wa makusudi) husukumwa na polisi wenyewe. Ni dhahiri pia kuwa Polisi wanakuwa hawana umakini na kazi yao, inakuwa kama vile wanabahatisha tu. Kwa kusahau wajibu wao kuwa wao ndio tegemeo na ulinzi wa mwananchi wa kawaida dhidi ya lolote lile ambalo laweza mtishia usalama!

Katika kutuliza hizo vurugu utumiaji wa silaha wa polisi hulenga nini hasa?
Ni ajabu sana, pamoja na kusema sio polisi na sina ujuzi huo - mimi nadhani na ninaamini kuwa katika taratibu za kazi kila kazi ina namna yake ya kufanya tokana na level ya hio dhana inayofanyiwa kazi. Inakuwa vipi kuwa kutuliza vurugu kunasababishia kutumika kwa vyombo vyo moto moja kwa moja kwa wananchi badala ya mbadala kama vile angani? Inakuwaje pale ambapo mwananchi wa kawaida hana silaha yoyote anauwawa bila kifikiria hata mara mbili? Hapa inanifanya nitoke na hitimisho kuwa polisi wanakuwa wamelenga kabisa kuwa lazima wajeruhi ama kuua mmoja kama kukomesha/fundisho ama kwa sababu zozote zile walizo nazo!

Madhara ya Vifo kwa mkono wa Polisi yanasukumwa zaidi na muitikio kuliko tukio lenyewe!

Maelezo na muitikio wa Wakubwa wa Polisi
Kutokea kifo tokana na uzembe wa kutumia silaha kwa polisi ni swala moja, Ila inapokuja swala la polisi kushindwa kuvaa kosa lao na kuwajibika ipasavo ni KERO ambayo kimsingi inaumiza na kushindwa kutoa picha kamili. Kuwa wao polisi ni wajinga ama wanatambua kuwa wananchi ndio wajinga? Mfano mdogo Kifo cha Marehemu Ally Zona Morogoro kimeelezwa na kamanda wa Polisi Morogoro kuwa kilisababishwa na kitu kizito kilichomgonga marehemu kichwani na sio risasi kama ilivodhaniwa…

Hii inaibua wazo na imani kwangu kuwa; yawezekana kabisa imesemekana hivo ili yeyote Yule asikamatwe kwa ajili ya kifo cha marehemu, kuwe na kielezo kuwa haieleweki hicho kipande kilitoka katika silaha ipi tofauti na kuripoti kuwa ni risasi.

Muitikio wa Viongozi wa juu wa Serikali
Katika hali ya kawaida ilitakiwa viongozi kuonesha ushirikiano hata kwa matamko ya swala zima lililotokea Morogoro kwa kusababisha kifo cha huyo kijana. Sio tu kwa msingi wa kifo cha marehemu, ila kwa msingi wa kusema chama kilicho kikubwa kwa upinzani kwa njia moja ama nyingine kinahusika na kufariki kwa Marehemu. Hasa baada ya kuingilia shughuli ambayo tayari ilishatolewa taarifa kuwa ipo na kutajajiwa. Kama lipo lililosemwa basi nimepitwa anatambua tafadhali anijuze.

Wanachi kuchukuliwa kuwa ni wajinga na wapumbavu!
Kwa mtitiriko na mwenendo mzima wa jeshi la polisi ni wazi wamechukulia kuwa mwananchi hana haki (kwa upande mwingine naweza kubaliana na hii mana jamii kwa upana haijuwi haki zake). Kwamba wanaweza kuvamia na kuamua lolote hata kuua. Na haijalishi kabisa wakiua wanaweza eleza lolote lile maadamu tu ionekane wameitikia hata kama ni kwa kusafisha jina lao ili kuonekana wana haki ya kufanya hivo maadamu wanafanya kazi yao.

Marehemu kuchukuliwa kana kwamba ni 'disposable'
Mwananchi wa kawaida na chini amechukuliwa kama vile mtu ambae hata haki, hana maana,hana tija wala umuhimu wa kulindwa. Anaendeshwa vyovyote vile na kupelekeshwa watakavo. Hata hivo Polisi inatakiwa watambue hizi ni nyakati nyingine… Na kubwa kuliko wananchi tumechoka! Hio inafanya hata kumshusha thamani huyo mwananchi anapofariki. Jinsi alivokufa na kuharibiwa Marehemu David Mwamgosi, maneno hayatoshelezi… Inasikitisha.

Kwa mtiririko unavoenda, kwa namna inavochukuliwa na sharia pamoja na jeshi la polisi ikiambatana na serkali ni kana kwamba vifo hivi vya kusikitisha ni kosa lao marehemu. Kana kwamba kufa kwao hakuna mana wala tija, kana kwamba ni sawa tu na kwa namna nyingine ikicheza kama ahadi kuwa inaweza kutokea na HAKUNA ambalo tunaweza kufanya.

Kwa kiasi Fulani inaweza kuwa wapo sawa na ni ukweli. Na hio yote itaonesha na kudhihirishwa na nguvu ya sisi wenyewe wananchi kwa kuwapa nguvu hio kwa ukimya, woga na tabia yetu ya kutotaka shari. Nadhani imefika wakati wa kila mmoja wetu kujihusisha kwa njia moja ama nyingine kuwa kila mmoja wetu, haijalishi upo ndani ya chama, haijalishi upo CDM ama CCM, haijalishi lolote lile zaidi ya Utambuzi, Ujuvi, Uzalendo wa kutaka kusongesha nchi yetu kuwa mahala salama kwa KILA mwananchi!

Kitu ambacho CHADEMA wanatakiwa kujifunza:

Wamepokelewa kwa mikono miwili na wananchi, inatakiwa wajipange hasa. Hizi vurugu ambazo zimekuwa mara nyingi zikihusishwa na wao kwa namna moja ama nyingine wanawajibika. Inawezekana Serkali inafanya makusudi kabisa ili kuwachafua kuwa wao wanaleta fujo hadi kusababisha vifo – Nasihi kama mkereketwa wasafishe hilo ili Watanzania wajue ukweli.

Wanafanya kazi nzuri ya kuhamasisha na kuwaamsha wananchi kwa silaha yao ya ‘Movement for Change'. Ila hio pekee haitoshi… Kazi, Malengo, Mipango na nguvu zaidi inahitajika. Wanaweza wakawa wamekubalika na kuzidi kuongeza wafuasi kila kuchapo; ila ukweli unabaki kuwa CCM wana mizizi mirefu hivo silaha kubwa ya kung'oa huo mzizi ni lazima iandaliwe kwa Uadilifu, Umakini, Uzalendo, Nguvu na Umoja!

Kitu ambacho CCM inatakiwa kujifunza:

Uhakika wa kudumu kwao katika uongozi daima wa Serkali unazidi kupungua kadri siku zinavoenda. Ni wazi kuwa matatizo ya ndani ya chama hasa yalioendeshwa tokana na mgawanyiko imekuwa kazi kurekebisha. Wanachi wamechoka na wanatambua kila ambalo linafanywa na serkali, kuwa hata kama wakitaka kutokujihusisha katika kashfa kama hizi wanahusika moja kwa moja. Kwa maana wakiwa kama wao ndio tuliowapa dhamana ya kuwa viongozi wetu, wametuangusha na wanatuumiza. CDM inaweza isiwe na nguvu kama CCM, ila kwa sasa ni dhahiri nguvu ya Umma ipo mgongoni kwao…

Kitu ambo Wanaharakati/Wananchi tunatakiwa kujifunza:

Kuongea ama kukemea mitaani/majumbani/kwenye vyombo vya habari pekee HAITOSHI! We have to take action, na action sio lazima uende ukapigane na mtu. Jamii yetu imezungukwa na wananchi ambao hawaelewi nini kinaendelea kwa mapana hapa nchini. Kuna ambae ukimuuliza habari zozote za siasa alizosikia hapa karibuni atakujibu kwa kujidai kabisa kuwa "Diamond kaalikwa Ikulu"; kwake hio ni siasa na anakuwa kamaliza.

Nadhani imefika wakati kama vile ambavo ilisisitizwa kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kugusia katika mkusanyiko wowote wa watu zaidi ya watano bila kujali ni mkutano wa kijiwe/kazi/shughuli BASI hata elimu ya yajirio (na umuhimu wa kujua hayo) kwa wanachi wenzetu iwe hivo. Hasa wale ambao kabisaa haelewi pa kuanzia ama kuishia hasa kwa yale yanayojiri nchini kwetu kwenye hii Tanzania yetu.

Hii kelele ya mara moja haitatibu tatizo letu sugu… Tukitaka kutambua kuwa na sie tuna tatizo; tujiulize kelele zote kuhusu Dr. Ulimboka yakwapi? Nini kimefanyika cha maana? Kwa mtindo huu kweli tunadhani kunaweza kukakwa na mabadiliko chanya yoyote? Kwa njia moja ama nyingine turudishe uzalendo tulioupoteza na kuujenga upya…. Habari na namna alivofariki Marehemu David imenigusaa… Nawasilisha hayo yote juu yakisukumwa na hicho kifo kama moja ya sababu.

Pamoja Sana.

AshaDii.


"Usually when people are sad, they don't do anything. They just cry over their condition. But when they get angry, they bring about change" - Malcom X
 
AshaDii,

Polisi ni wafanyakazi wenye taaluma ya kukabiliana na hali mbali mbali za usalama.

Jukumu la Polisi ni kulinda wananchi na mali zao. Katika hali ya kawaida Polisi analazimika tu kutumia nguvu pale ambapo njia zote zimeshindikana au usalama wao upo mashakani.

Nchi nyingi polisi hutumia virungu, maderaya ya maji pamoja na mabomu ya machozi kwa kujua kuwa wanakabiliana na wananchi hasa katika maandamano ambapo uwezekano wa kutumia risasi za moto na kuleta madhara ni mkubwa.

Kwa hapa nyumbani inaonekana kama jeshi la Poilisi ni genge la mauaji lililoajiri wendawazimu na siyo wataalamu.
Ukiangalia picha za Iringa utaona kuwa Marehemu Mwangosi alikuwa kazini na wala si kwenye mkutano.

Uwepo wake katika mkutano ni sawa na uwepo wa daktari wodini, au mhasibu benki. Tena kwa vigezo vyote fani ya uandishi inatakiwa wawepo katika maeneo salama na hata yale ya hatari. Kwa muhtasari huo tu ni wazi kuwa Mwangosi alikuwa kazini na wala hakukuwa na uhusiano wa uwepo wake na shughuli za kisiasa.

Picha zinaonyesha askari zaidi ya sita wenye nguvu wakikabiliana na mrehemu. Mwangosi alikuwa amebeba kamera yake hadi mauti ya kulipuliwa yanamfika. Haingii akilini kuwa askari zaidi ya sitta wenye mafunzo walishindwa kumkamata Mwangosi bila madhara. Haieleweki ni kitu gani walihisi Mwangosi amekinukuu au kukupiga picha kabla hawajamrudia.

Hapo tu inaweza kujibu hoja kuwa mauaji haya huwa ni ya kukusudia kama yale yaliyotakiwa kufanywa Mabwepande.

Unyama huu umekuwa unafanyika kwa kuwa wananchi hawajasimama na kusema hapana! tumechoka kugeuzwa wanyama wa porini na wananchi tuliowaajiri.

Ni kutokana na hayo wananchi huridhika na sababu za kipuuzi kama zile alizotoa waziri nchimbi. Poilisi hawawezi kutuhumiwa kuua halafu ukawapa kazi ya kujichunguza. Matokeo yake tunaambiwa mtu alipigwa na kitu kizito.

Kesho asubuhi utamsikia Mwema na Nchimbi wakiunda tume ya kuchunguza kama Mwangosi ameuawa kweli na kama hakukanyagwa na tembo. Ndiyo, ni kwasababu wanajua sisi ni mazezeta na hatuna la kuwafanya

Licha ya picha ambazo hazihitaji degree au certificate kubaini kuwa huu ni unyama na ukatili uliopita uvumilivu wa wanadamu, wakuu hao watatumia mbinu za Rais JK za kutuliza hasira kwa kuunda tume za kipuuzi zisizo na majibu kwa maisha ya wanadamu.

Sisi wananchi wa Tanzania tumeaminishwa kuwa nchini kuna amani na utulivu.
Sijui mke au mtotoo, mzazi, ndugu na jamaa wa Mwangosi usiku huu wana amani.

Sijui ndugu na jamaa wa Ali Nzola kule Muheza wana amani na utulivu. Tumekumbatia amani na utulivu kiasi cha kuwekewa mabomu tumboni na kufumua miili yetu mithili ya vita baina ya dola na wananchi.

Tumekumbatia amani na utulivu kiasi sasa wanatoa roho zetu bila haya tena mchana wa jua kali.

Ni amani na utulivu huo ndio umefanya Chadema waendelee kutoa rambi rambi huku wananchi wakiuawa.

Bila kuwahusisha marehemu na matukio ya kisiasa, Chadema kama cha kikuu cha upinzani na kinachojiandaa kuchukua dola kina dhima ya kusimama na kuanza kuwaongoza wananchi kuanzia sasa. Mamia ya wananchi wameuawa na Chadema haionekani kuchukua hatua. Pengine ni rahisi wananchi kuhusisha vurugu hizi na Chadema vinginevyo wangeshachukua nafasi ya uongozi kutokana na ombwe la uongozi lililopo sasa.

Na sisi wananchi tunasehemu kubwa ya lawama. Tumekuwa wepesi wa kudanganywa na tume za kipuuzi tukijua tunadanganywa. Tunatunguliwa na kulipuliwa kama vicheche mwituni huku tunatumiana salam za rambi rambi.

Hatujaweza kufika mahali pa kusema si Kikwete au Polisi wenye nchi hii. Nchii hii ni yetu na kama wameshindwa kulinda watu na mali zao basi wamekiuka viapo vyao vya kazi.

Ni kwa maana hiyo mimi nasisitiza kuwa hakuna sababu ya kumpa waziri wa mambo ya ndni Nchimbi nafasi nyingine ya kuughilibu umma. Mauaji na damu ilioyotapakaa mikononi mwake kama ile iliyojaa katika viganja vya IGP mwema, havina uhalali wa kusimamia haki tena. Hawa ni sehemu ya uhalifu na kama si hivyo wachukue hatu za kujiuzulu kama ishara ya kuwajibika na kutohusika na unyama na uhalifu huu.usiovumilika.

Vinginevyo hatuna sababu ya kuwalaumu askari waliopokea maagizo kutoka ngazi za
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3 na AshaDii,

Wakuu jambo hili si la kuanza kusema nani ajiuzulu au nani abaki, kwa kuwa hapa Tanzania mbali na mzee Mwinyi sijui kama kuna yeyote aliyewahi kujiuzulu. So that is not gonna happen, as a result unaweza kusikia kuwa wahusika watakuwa promoted, kuna mifano mingi tu. Hapa hata picha za waloshiriki mauaji hayo zipo lakini hakuna atakayechukuliwa hatua yeyote, sana sana tutazugwa kuwa amekamatwa na kufikishwa mahakamani, na kesi kuendelea miaka 10 halafu kosa litakuwa na marehemu.

Issue hapa ni kuwa, matukio haya sasa yanaongezeka. La Ulimboka halijaisha na hainoekani kama kuna mtu yeyote atachukuliwa hatua, kuna mengine mengi ambayo hatujui. Kama picha zisingewekwa hapa hakuna ambaye angejua yaliyofanyika.

Hapa kuna suala la kubadilisha sheria, Polisi wawatumikie wananchi, wasiitumike serikali, au kuwatumikia baadhi ya watu wa chama na serikali. Let us try to be fools and agree that the guy was supposed to die, but was he supposed to die like that? was one bullet on head not enough to kill him? kulikuwa na haja gani ya kumuua kwa unyama kiasi hicho? Kulikuwa na haja ya kumuua? hakukuwa na njia nyingine ya "kumuua" mbali na kumtoa uhai kinyama namna hii?

Hali inaendelea kuwa ya namna hii. Kina Lunkombe mpaka leo hakuna justice, Ulimboka naye asahau kuwa justice itatendeka, na huyu pia asahau [uzoefu unaonesha wazi kabisa], and this is pilling up. Kama tukiendelea na sheria za namna hii, na kama wabunge wakiendelea kupuuza tunapouawa tutaendelea kuuawa, na kama tukianza kujidefend itakuwa hatari sana kwa nchi yetu. Ni vizuri wabunge wakasaidia kubadilisha sheria na kutoawapa polisi nguvu ya kupiga watu kuua na kutochukuliwa hatua, ni vizuri wauaji wawe wanakamatwa.
 
Last edited by a moderator:
Bongolander,

Ni kweli unachokisema lakini lazima tuwe na mahali pa kuanzia.

Wabunge hawawezi kusimamia sheria zibadiilke kwasababu ni wale wale wanaowajibika kwa Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama chao na asiyejali maisha ya raia wake labda kama awe mwanamtandao mwenzake.

Nimekuewa vizuri sana, ninachosema mimi ni kuwa kubadilisha sheria ni process na inaweza kuchukua miaka 10.

Kukamata watu ili kupeleka kesi mahakamani inaweza kuzaa miaka 20 kama ulivyosema.

Lakini basi ni lazima wacheza sinema wengine walipe gharama 'pay the price' ili kila mmoja ajue sinema itaendelea wakati hayupo ofisini.

Mkuu hivi kwanini sisi Watanzania ni watu wepesi sana kusema hiki au kile hakiwezekani?

Ni lazima tuanze sasa ili hizi habari za 'upepo utapita' zifike kikomo

Rais JK huko aliko wala halimsumbui kuwa kuna mtu katolewa roho kwa namna ambayo ni ya kikatili, kinyama na kihalifu.

Nchimbi anafikiria kutunga hadithi za tume ya kuchunguza kama kweli Mwangos amefariki hata kama picha zipo.

IGP mwema siajabu yupo Oysterbay akipanga namna ya kuwatetea waliokamilisha kazi za wazee.

Hakuna njia ya mkato ya kuwaamsha ila ni kufanya jambo litakalowashtua.

Umma uwatake Nchimbi na IGP Mwema waondoke haraka sana kwasababu wamejaa damu za kutosha na hawana uhalali wa kusimamia haki.

Ikishindikana basi umma umwambie JK alipoifikisha nchi ni pabaya, siyo udhaifu bali hatari ya machafuko na akae pembeni ili kuinusuru Tanzania. Umma umwambie JK kuwa kazi imemshinda na nchi inatumbukia katika machafuko akiwa IIkulu

Tukiendelea kuogopa, damu za watu zitazidi kumwagika, na hao wenzetu viganja vimejaa damu ndio maana hawajali, tunahitaji kuwaambia.

Watanzania there should be a time to say enough is enough.
 
Last edited by a moderator:
AshaDii, inaaminika kwamba zamani makamanda waliowasulubu sana wapinzani waling'ara miongoni mwa watoa maamuzi.

Nisichokubaliana nacho ni hii tabia mbaya ya kuanza kuua na kuona kwamba ni kitu kidogo ambacho mkuu wa polisi atasimama mbele ya vyombo vya habari na kuhalalisha tukio hilo.

Kuwanyima watu haki zao za kikatiba si halali na hakuna mamlaka wala chombo kinakachodumu muda mrefu kikitumia mbinu hizo. Ulingo wa siasa unazidi kuwa mgumu kadri watu wanavyoanza kujifunza wanataka kupata nini kutoka kwa watawala. Hoja za kuzima fikra za watu kwa mabavu hazina dalili njema kwa nchi yoyote inayoamua kuzitumia.

Swali kubwa ninalojiuliza ni competence ya askari polisi wetu? Are they that competent to know they are guided by rule of law? Training zao zinawaandaa kuhandle changamoto za sasa ndani ya Taifa letu? Au wao wanajua kupiga tu ndio suluhisho?
 
Taratibu tunaanza kujenga kizazi kilichojaa Hasira, Chuki na Visasi na katika hili tusipochukua hatua sasa kamwe hatuwezi kubaki salama.

Polisi waachane na hizi nyimbo za "Kudhibiti CHADEMA" sababu they are making things much worse! Wasifikiri kuwa kwa kuendeleza mauaji ya namna hii wanafanikiwa kuwafitinisha wananchi na CDM sana sana wanazidi kuwapa umaarufu!
 
Hao polisi wanafanya kazi kwa maslahi ya watu wachache waliowatuma.

Na tena inawezekana sio polisi wote wana matatizo bali ni wale wachache wanaonunuliwa na CCM ili kuvuruga amani kwa sababu zao binafsi. Mbaya zaidi inaelekea viongozi waote wa polisi nao wamenunuliwa...

Kwa hali ilivo sasa solution ya matatizo haya ni ngumu...mie naona damu ikiendelea kumwagika (God forbid)
 
Hao polisi wanafanya kazi kwa maslahi ya watu wachache waliowatuma.

Na tena inawezekana sio polisi wote wana matatizo bali ni wale wachache wanaonunuliwa na CCM ili kuvuruga amani kwa sababu zao binafsi. Mbaya zaidi inaelekea viongozi waote wa polisi nao wamenunuliwa...

Kwa hali ilivo sasa solution ya matatizo haya ni ngumu...mie naona damu ikiendelea kumwagika (God forbid)

Nikiangalia picha za mahala alipouawa huyu ndugu yetu inaonyesha ni kwenye Kota za Polisi, hivyo alikuwa kwenye mikono salama kwa nizijuavyo kazi za Polisi ni kurinda usalama wa watu na mali zao, na kinachonitisha zaidi pamoja nakuwa mikononi mwa Polisi kulikuwa na umuhimu gani wa kumuua? alikuwa amehatarisha Uhai wa polisi? Any way ngoja tusubiri matokeo ya uchunguzi mtasikia tuu wakisema Polisi walikuwa wanajihami.
 
Mini nianze mchango wangu na dondoo hizi: Kwa upande mmoja kuna hizi kauli za Kamuhanda:
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Michael Kamuhanda, alisema awali kwamba anaipenda kazi yake, hivyo hawezi kuruhusu mikutano katika mkoa wake mpaka atakapopata maelezo ya ziada.
Alisema: "Ni kweli jana saa mbili tuliwapa barua ya kuruhusu shughuli zao ila hili ni agizo na mimi ninakaribia kustaafu na kazi yangu ninaipenda, hivyo siwezi kuruhusu maandamano kinyume na maagizo yaliyopo."
Alisema CHADEMA hawawezi kufanya mikutano kwa kuwa hawana jeshi wala vifaa vya kupambana na Jeshi la Polisi, hivyo wakijaribu kutotii sheria ni lazima washurutishwe: Tanzania Daima

Kwa upande wa pili, kuna kauli za Dk. Slaa:
Dk. Slaa alisema alipopata taarifa za kusitisha mikutano juzi, alimpigia IGP Mwema kutaka ufafanuzi kwani makubaliano yao ya awali yalikuwa kwamba wasitishe mikutano kwa siku nne au tano kisha waendelee na ratiba yao."Katika nia njema nilimpigia IGP kujadiliana juu ya hili. Hakupokea simu mpaka nilipomtumia ujumbe mkali, akaniambia angepiga saa mbili usiku; pia hakufanya hivyo. Na nilipomtafuta alisema zuio linaendelea.
"Nikamuuliza kwa nini watu ambao ni asilimia tano ya Watanzania wote, tena wakiwa wameelekezwa wawatafute waandikishaji wa sensa kwa namba za simu, wawe sababu ya kuzuia shughuli zetu halali? Mwema hakuwa na jibu," alisema Dk. Slaa.


Alisisitiza hata baada ya kushindwa kutolea maelezo hoja hiyo, IGP alisema hilo ni agizo na ni lazima litekelezwe kwa sababu ni amri iliyotolewa kisheria.


Dk. Slaa alisema hata alipomuuliza ni sheria gani inayozuia hali hiyo, hakumjibu huku akisisitiza amri yake ifuatwe.
"Sisi hatuna bunduki, hatuna mabomu wala majeshi, lakini Serikali ya CCM na polisi wanapaswa kutambua haya tunayoyafanya ni sawa na gharika. Kuyazuia ni vigumu, hata kama watatuua viongozi wote, watambue mioyo ya Watanzania itaendelea kulilia mabadiliko haya," alisema Dk. Slaa.
Ninachokiona kwenye kauli za kamanda wa polisi ni kuwa alizuwia mkutano baada ya kuwa alikwisha uruhusu lakini baada ye akapogea agizo, bila ya kutaja kapokea toka kwa nani.

Na katika kauli ya kauli Mwema, na yeye pia kasema kuwa hilo lilikuwa agizo na lazima lifuatwe? Ninachojiuliza, ni nani nayetoa maagizo haya? Mwema alitoa agizo yeye binafsi kwa Kamanda, au na yeye alipokea agizo? Hili la pili ndio linaloelekea kwa sababu hata alipotakiwa aeleze ni agizo na sheria gani, alijiumauma na kukata simu. Na kwa sababu hiyo, nalazimika kuamini kuwa mauaji na manyanyaso yote haya yanayowakumba raia, ni maagizo kutoka serikalini/chamani.

Ama kuhusu kauli nyengine ya Dk. Slaa hapo blue, nasikitika sana kuwa mpaka sasa wanaokufa zaidi ni wananchi, pengine wafuasi wa Chadema, pengine watu wasiohusika kabisa kama Ally Zona, muuza magazeti na David Mwangosi, mwandishi wa habari, ambao kwa bahati mbaya walikuwepo mahali sipo, wakati sio.

Rai yangu kwa CDM na vyama vyote vya upinzani, makosa mawili hayafanyi jema moja. Tumeshaona kuchanganyikiwa kwa CCM kiasi wamefikia pahali tayari wanaua na kuwatesa wale wasiokubaliana nao kwa ajili ya kubaka madarakani; vyama vya upinzani visiwe tayari kufa kwa ajili ya kuingia madarakani. Kama tunavyoona, wanaokufa ni raia wa kawaida na sio viongozi, na hata kama wanaokufa au watakao uliwa ni viongozi, bado taifa linawahitaji. Busara itumike. CCM wameshaonja damu, hawatasita. Tusiwaridhishe kwa yale wanayoyataka. Tutafute njia mbadala ya kupambana nao bila ya kupoteza maisha ya watu wasio na hatia kwani tukifanya hivyo itakuwa hakuna tafauti baina ya mjinga na mwenye akili.
 
Polisi nao bado magamba. Ile kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa(na wilaya) mwenyekiti huwa ni RC/DC(makada wa CCM) na hawa makamanda wa Polisi hupeleka mipango yao huko na kupokea amri pia. Hizi kamati haziko kisheria ila zina mamlaka na nguvu nyingi sana.Nina hakika ndio wanaotoa directives kuhusu mikutano ya CHADEMA
 
Ni hali ya asili ya mwanadamu na inayotegemewa kabisa, kumkimbilia na kumsadia mtoto mdogo aliyeanguka kwa kujikwaa mbele yako na kujaribu kumsaidiana kumpa moyo wa kusimama na kuenedelea kuikabili maisha. Ni jambo lakibinadamu na kudhihirisha utu na maadili yake kwa kumsaidia Mama mjamzitokubeba sanduku linalomuelema anapoelekea hospitalini kujifugua.

Kuutekeleza uasili wetu unaotutofautisha na viumbe wengine wote ulimwenguni nakumpa wanadamu utambulisho wetu si jambo la kusomweshwa shule au chuo chochote.Viumbe hai wote kujitambulisha na uasili wao ni kitu cha asili kuliko vyote nakilicho na msukumo wa kujitegemea usio hitaji msaada wa msukumo mwingine ilikujikamilisha.

Ndio maana kindege kinajenga kiota ambacho huwa kinaweza kuonekana "complicated" kuliko hata ndege mwenyewe. Lakini hili linatokea nisema "naturally"bila ya kutegema msukumo wowote toka kwa kamanda, kada au mwenyekiti.

Pale serengeti ndama wa nyumbu au punda milia kati ya dakikamoja anapozaliwa anapata msukumo wa asili unaompa utambulisho na mazingira yakekuwa hakika akishindwa kukimbia kasi ya ajabu dhidi ya adui yake anapoteza maisha na kizazi cheke kinafutika hapo serenegeti.

Na hao ndama wa serengeti hawafundishwi na mfumo wowote toka nje yao wenyewe.Wanatii na kufuata misuko ya UASILI wao BILA KUBABAISHA!

Tusemeje kuhusu Mwanadamu amabye AMEASI UASILI WAKE ambao unamjengea UTAMBULISHO WAKE?

Tumuweke wapi Mwanadamu ambaye anashindwa na ndama wa serengeti katikakutekeleza UASILI wake? Ndama wa seregeti katu hawezi kuasaliti na kuasi Uasiliwa undama wake.

Lakini Kamanda Mkuuwa Polisi anaweza kuasi na kusaliti uasili wa UTU NA UBINADAMU WAKE. Si ajabuKamanada huyo badala ya kumsadia Mama mjamzito ili kufika hospitalini kujifungua .. anaweza kwa kuwa kapoteza uasili wake... Akambaka na mwishowe kumuibia Mali zake zote. Si ajabu badala ya Kumkibiliana kumukota Mtoto aliyeanguka na anaye onekeana kukosa matumaini .. Yeye akampigamateka na kumtukana au kumdhalilisha. Kwani kama Mtu amepoteza Uasili ulio utuna maadili yake yote afanye nini zaidi ya HILO?

HILO Ndilo jeshi letu la Polisi. Hiyo ndio serekali yetu.Hapo ndipo ulipofikia Utanzania wetu.

Wanyama na Mimea yote haiwezi kamwe kusaliti Uasili wao! Mwanadamu wa ainafulani peke yake anaweza Kuusaliti uasili wake hadi kufikia kiwango cha kujaribukuungamiza na kuutokomeza ubinaadamu wake mwenyewe na HICHO NI KIWANGO CHA JUUKABISA NA CHA MWISHO KATIKA KUPOTOKA KWA MWANDAMU NDANI YA USO WA DUNIA ... !Na hatuamini hili kutokea na kuongozwa na vinogozi mbalimbali wa jamhuri ya muugano wa Tanzania.

Kumkandamiza mtu kinyume na heshima ya utu na maadili yake kunaweza kutoaMOTOKEO fulani ya kujenga utii wa woga kwa mwanadamu. Na serekali iliyokwishapotoka, KUFILISIKA na iliyosimamai nje ya maadili ya ubinadamu inaweza sana kutumia njiahiyo kupata LOYALTY YA JAMIIYAKE!!

Yaani TOUCHER AND INTIMIDATE TO SUBMISSION!! (KUTESA NA KUTISHAHADI KUJENGA UTII)Kwa kawaida jambo hilo likifanyika mara moja na likaleta matunda namafnikio kwa kundi husika lazima kundi hilo litabidi kubadilisha mifumo yakeyote ya kiuatwala na kufanya hiyo ndio kuwa njia kuu ya Utatuzi na upatikanajiwa majibu ya matatizo yote yaliyoshindikana kwenye jamii. Lakini hiyo ni isharazaidi kuwa TAIFA LINATEKETEA! TAIFA LINAPOTEZA UTU NA UBINADAMU WAKE, TAIFALINAKUWA NA THAMANI NDOGO KULIKO HATA NDAMA WA SERENGETI, TAIFA LINATIA AIBU MBELEYA UASILI ULIO UTU NA MAADILI YAKE YOTE HAPA DUNIANI!!!

Kwa yeyote amabaye bado hajasaliti au kuathiri uasili wake ambao ni mali ya buretoka kwa Muumba wake anaweza akatambua fika kuwa kutesa na kutisha hadi kujengautii kikuweki ina maana UA, TEKETEZA NA ANGAMIZA KWA AJILI YA "KUTATUA" MATATIZOYA JAMII ILI KUPATA "MAENDELEO".

Serekali iliyofikia kina hicho ni serekali iliyopteza na kufiliska UASILI NAUTU WAKE!! Imepoteza uwezo wa asili wa kutatua matatizo KIUTU NA KIBINADAMU!Hiyvo itabidi IKOPE UASILI WA TABAKA LA VIUMBE WENGINE KUJAZIA KILE ILICHO ASINA KUKITUPILIA AMBALI!

Itabidi iige Simba na chui wanavyo tatua matatizo ya njaa AU kutafuta ubingwawa aina nyingine huko Porini! Simba anatisha kwa sauti ya juu kabisa NA mara moja ananasakati punda wote waliko mbeel yake yupi anazailisha WOGA, SHAKA AU WASIWASI kwakiwango Kikubwa. MARAMOJA Anamweka alama na kumkibiza hadi kumuua kutatuatatizo la njaa yake mzazi na wanae kwani huyo ndiye mnyoge kwa udhibitisho wa uzalishaji wa Shaka, woga na hasia hasi nyingine.

Mtanzania timamu katika UTU NA UBINADAMU Wake atagundua kuwatangu nchi hii ipate Uhuru Mbinu hii haijawahi kutumika HADHARANI na MCHANA KWEUPE kama ILIVYO HIVIsasa. Na hii ni ONYO LA NCHI INAKOKWENDA kuwa sio kwenye UHURU hata kidogo.

Serekali inapotumia njia hiyo anayotumia Simba, Chui na Mnyama yeyote mlanyama inaoyesha kufilisika kwake, inakiuka MISINGI YA UTU NA UBINADAMU kwani kwa SIMBA NA CHUI KUFANYAHIVYO Wao hawaja ASI usali wao na hivyo ni sawa kabisa ku Intimidate toucherfor submission of the pray! Serekali na vyombo vyake vinapotumia Uasili wawanyama pori vinakiuka UASILI WA UTU NA MAADILI YAKE ...NA HII NI KULIIGIZA TAIFA GIZANI!!!

Lakini PIA huu ni ujinga na kupotoka kwani hakuna kati ya viumbe wote dunianikinachoweza KUASI UASILI WAKE NA KIUMBE AU SEREKALI HIYO IKABAKI SALAMA...!! HAKUNA SEREKALI YEYE MAMLAKA NA NGUVU KUZIDI NGUVU NA MALAKA YA UTU NAMAADILI YAKE KAMA UASILI WAKE.

HEBU TIZAMA HILIKWA MAKINI.
MATISHO, MATESO NA KIFO VINAVYOGEUKA NA KUTUMIKA KAMA NYENZO YA KUTATULIA MATATIZO

1. Hata kama serekali na vyombo vyake havikuhusika na Unyama aliofanyiwa Drulimboka ... Inaweza kukana kuwa HAIKUFAIDIKA NA TUKIO LILE LA KUTESWA NAKUTISHWA kwa DR Uli .. KATIKA KUTATUA TATIZO LA MGOMO WA MA DR? HIVI SI KWELIUTATUZI ULIPATIKANA TU BAADA YA TUKIO LILE? HIVI SI KWELI KUWA KILA MTU AMEFUNGA MDOMO KWA WOGA, SHAKA, WASIWASI NA KUNYONGONYEA? Binadamu wote ambao wana uasili waokatika ukamilifu wote watajihoji whata coincidence? Mgomo kufikia utatuzi tu baada ya tukio La Dr Uli?

2. Namna ambavyo Kesi yake imepelekwa na kuyeyuka! HIVI SIKWELI KUWA INATAMANISHA MBINU HIYO KUENDELEA KUTUMIKA TENA NA TENA NA KUTUMIWA NA MAKUNDI MENGINE kwenye jamii? ...Hvi si kweli kuwainaedeela kutumika? Tangu Dr Uli, Matukio mangapi yametokea kwa namna hiyohiyo labda hata kutumia msitu ule ule? Na vibaya zaidi yatakomweshwa lini na nina atajitwika Mzigo huo?

TAFAKARI

Kama ninachosemwa hapa ni kweli kuwa BADALA YA UTU na MAADILI yake kuwamsingi wa utatuzi wa matatizo ya serekeali sasa utatuzi umehamia kwenye MATISHO NAMATESO MAKALI HADI KIFO, KAMA JIBU!! Ona yafuatayo!

1. Leo jamii yetu inakiona kifo chenye mahusiano na serekali au vyombo ya vyakekama kitu cha kawaida.

2. Kumpiga mtu risasi kama njiwa au pundamilia wa serengeti ili kufikia malengofulani inakuwa jambo la kawaida tu!

3. Viongozi wa kiserekali kutambiana kuhusu silaha zao za KUUA na KUANGAMIZAhata kutembea nazo kwenye majukuwaa kwa lengo la kutisha ili kufikia MALENGO ... Linakuwa jambo la kawaida wala lisilo hitaji kukemewa.

4 Kundi la walinda usalama Kuhusika na KUUA ili kufikia Malengo limekuwa lakawaida tizama picha za Iringa jana tizama swala la Morogoro … leo hakunaanayekumbuka ni njiwa tu amaelengwa kufikia matokeo ya kuganga njaa ya Bosi!!

5. Maisha ya Mtanzania sasa yako karibu na kifo kuliko wakati mwingine Tangunchi hii kujitangazi Uhuru.

UTATUZI


Nina amini kabisa kabisa na kuafikiana na AshaDii kuwa ni ELIMU katika ngazi ya chini kabisa. Walasi kukimbizana na Polisi mtaani. Ni elimu kwa kila familia ni elimu kwa kilarafiki na ndugu. Ni elimu kuwa wale swala wa seregeti wangeweza kufanya mkutano na kuamua KATU WASIOGOPE,WASITISHIKE, WASIWE NA WASIWASI AU KUZALISHA HISIA HASI NYINGINE DHIDI YA SIMBA NA CHUI ..WANGEJENGA UJASIRI NAUHODARI KAMILI NA WASINGEKUWA KITOWEO KWA MAADUI WAO.

Lakini hilo sio sahihi na wala halitafikiwa kamwe na TABAKALA WANYAMA KWANI HILO HALIKO KWENYE UASILI WAO. HILO NI TUZO na KARAMA KWAUASILI WA MWANDAMU PEKE YAKE. YEYE PEKE YAKE ANA MAAMUZI NA MAMLAKA HAYO!!!

Ujasiri na uhodari ni Utu ambao hatimaye unazaa Maadili yoteya kijamii na Kitaifa. Ujasiri na uhodari dhidi ya kutetea na kurejesha Utu namaadili yote ya kibinadamu ni Utanzania usio ijua tofauti ya kidini, kikabila,kiitikadi, kikanda... TUSAMABZE ELIMU HII KAMA ILIVYOKUWA KWA ELIMU YA UKIMWI!!

ELIMU KUWA NGUVU YA KUJIKOMBOA HAIKO MBALI, SI YA KUNUNUA, KILA MTU ANAYO NI YA KUAMSHA TU!!!!!
 
Kitu ambacho CHADEMA wanatakiwa kujifunza:
Wamepokelewa kwa mikono miwili na wananchi, inatakiwa wajipange hasa. Hizi vurugu ambazo zimekuwa mara nyingi zikihusishwa na wao kwa namna moja ama nyingine wanawajibika. Inawezekana Serkali inafanya makusudi kabisa ili kuwachafua kuwa wao wanaleta fujo hadi kusababisha vifo – Nasihi kama mkereketwa wasafishe hilo ili Watanzania wajue ukweli.

Wanafanya kazi nzuri ya kuhamasisha na kuwaamsha wananchi kwa silaha yao ya ‘Movement for Change'. Ila hio pekee haitoshi… Kazi, Malengo, Mipango na nguvu zaidi inahitajika. Wanaweza wakawa wamekubalika na kuzidi kuongeza wafuasi kila kuchapo; ila ukweli unabaki kuwa CCM wana mizizi mirefu hivo silaha kubwa ya kung'oa huo mzizi ni lazima iandaliwe kwa Uadilifu, Umakini, Uzalendo, Nguvu na Umoja!

Well said AshaDii, cdm wafahamu kuwa mission yao ni kuwaondoa ccm madarakani na wasitegemee kama ccm na serikali yake wataacha kampeni hiyo iendelee bila vikwazo. Tutegemee matatizo zaidi ya haya kadiri siku zinavyoenda kuelekea 2015.

Itachukua sacrifice, ujasiri, hekima na ya hali ya juu kuongoza mageuzi katika bahari inazidi kuchafuka kila uchao. Wananchi wakikosa uongozi ni wepesi wa kukata tamaa, na hili ndilo hasa watawala wanalodhamiria kila wanapotumia nguvu kuvuruga harakati za kisiasa.

Wanamkakati wa cdm itabidi wakae chini watafakari strategy nzuri ya ku-contain hujuma hizi vinginevyo wataingizwa katika mtego utakaopelekea kukatisha tamaa wafuasi wao katikati ya safari.

Sisi tulioshuhudia Mageuzi wakati yanaanza miaka ya '90 tunakumbuka NCR walivyotuahidi pepo kisha wakatuacha porini na na njaa pamoja na kiu. Sipendi kuamini kama cdm nao watawaacha watu kabla safari haijafika mwisho.
 
Binafsi yangu nalitazama swala hili kama ni la kimfumo zaidi ya kuwalalamikia Polisi nchini maana tumesha poteza DIRA yetu. Kwa mtazamo wa haraka unaweza kabisa kuwalaumu zaidi Polisi na kutoa tafisri zote za kazi na majukumu yao lakini pia tunatakiwa kutazama amri waliyopewa ktk shughuli na kazi zao za siku hiyo.

Nimefuatiulia sana mijadala mbali mbali ktk ukumbi huu wa JF kusema kweli nimeshindwa hata kuchangia kwa sababu watu wote mnakwepa ukweli kuwa mfumo wa Utawala nchini bado ni wa chama kimoja chenye mamlaka juu ya ya kuwepo vyama vingi. Tunajidanganya sana kuwepo kwa UHURU wa vitabuni, HAKI za vitabuni na USAWA unaotazama ujenzi wa siasa za Ujamaaa na Kujitegemea..Kifupi Wadanganyika wamezidi kuchanganyikiwa zaidi..

Wadanganyika kwa fikra za Kijamaa tumeunda makundi ya chuki badala ya kukubali tofauti zetu kuwa msingi wa maendeleo yetu. Tofauti ya CCM na Chadema kuwa ni za kiitikadi na sio Kijamii, tofauti baina ya waislaam na Wakristu ni za kiimani na sii za kijamii lakini imefikia tunalazimishana hata ya kiimani na Kiitikadi kama yale ya Kikomunist tuwe jamii moja isiyotambua tofauti (diversity) hizi. Huwezi kupambana na tofauti hizi za jamii pasipo kuweka sheria inayopingana na kuwepo tofauti hizi kama alivyofanya Nyerere, ama Warusi ama Wachina. Hutaki tofauti ziwepo unazikwaza tofauti hizo kwa sheria (left) au kama unazikubali tofauti kuwa sehemu ya jamii basi unaziwezesha tofauti hizi kushiriki sawa ktk ujenzi wa jamii hiyo (right) - Hakuna kitu nusu nusu ingekuwa hivyo wanafalsafa wangeisha andika aina hii ya mfumo wa kiutawala ktk jamii.

Kina Nyerere hawakuwa wajinga kuzima kabisa Ukabila, Udini na makundi baina yetu kwa serikali kuchukua jukumu lote la uongozi na kufuta kuwepo kwa tofauti za kiimani na makundi ya kisiasa (vyama vingi) ili kujenga Taifa moja lenye fikra moja na mwelekeo mmoja tofauti na nchi za Ulaya ambao walitambua tofauti zao (diversty) wakaziwezesha tofauti hizo kwa haki na usawa ili wapate kuishi pamoja kwa kutambua na kuthamini UTU wao. Diversity ni pamoja na ku accept one another for who we are, hivyo kuwepo kwa vyama vingi hakuna maana ya Uadui isipokuwa kukubali kutokubaliana ktk misingi ya kiitikadi..

Maadam leo tumekubali kuwepo kwa vyama vingi inatulazimu tukubaliane na kuwepo kwa falsafa zinazokinzana na ndizo hua nguzo ya usajili wa vyama. Lakini bahati mbaya tanzania usajili wa vyama umetokana na chuki baina ya watu na watu ndani ya vyama. Kama simpendi dr.Slaa siwezi kuwa Chadema na kama zimpendi JK basi lazima nijiunge na Chadema sio CCM. Siwapendi waislaam siwezi kuwa CUF na sasa imefikia Uchadema nao kupewa tafirisi ya zile zile za chuki baina ya makundi ya watu. Yote haya yanatokana na mfumo mbovu wa kiutawala unalenga kujenga Taifa moja lenye watu waitwao WATANZANIA lakini tofauti zao za kijamii (diversity) haikubaliki. Leo hii Chadema ni adui wa CCM hata kama mtajaribu vipi kupamba hoja zenu za Utaifa.

Ndugu zangu, tunaelekea kubaya sana, tumechukua mfumo ambao sii wa Kikokumunist wala Kibepari isipokuwa kati kati na kwa kuiga ambapo tunataka Utaifa kwa kujenga Taifa la watu wasiokuwepo. Tunazo tofauti zetu wenyewe sio sawa na zile za Urusi, ama Ulaya na lazima tuzikubali na kuziwezesha kisheria ili tupate kuishi pamoja laa sivyo CCM na Chadema watakuwa maadui wa kudumu na mwenye kushika Mpini (nguvu ya dola) ndiye mwenye haki zote (winner takes all). Tunaendeleza mfumo wa kikoloni kwa sababu mfumo mzima haukutokana na watu wake bali tumeiga na kuchambua chambua manyambuyambu ya ukoloni.

Hivyo basi, kutofautiana kimawazo ni jambo moja tofauti na kutokubali kuwepo kwa fikra ama kundi pinzani. Kinachotokea Tanzania ni kwamba tofauti zetu hazikubaliki na wala hazitakiwi kuzungumziwa ktk UTANZANIA maana sisi wote tunaamini kuwa ni Watanzania hatuna makundi kumbe makundi hayo yapo na yanakubalika kijamii. Na ndio maana hata maandamano haya yanasemekana ni ya Chadema, wanaofanya fujo ni Chadema sio wanaCCM, wanaCUF na wala hawataitwa watanzania ktk dhana ile ya Utanzania japokuwa msingi wa maandamano haya ni kwa Watanzania.

Nitaendelea kuomba tusiwalaumu sana Polisi kwa sababu wao wamepewa order ya kuchukua hatua yoyote necessary kuzuia maandamano ya Chadema (sio Watanzania) na wanaifanya kazi hiyo kwa kufuata maagizo toka juu kwa wenye kushika mpini. Tutaendelea kuwa katika hali hii hadi siku tutakapo kubali kwamba sisi ni watanzania na tuna tofauti zetu za kifira ambazo zimepewa haki ya kikatiba kushiriki kikamilifu ktk ujenzi wa taifa hili. Kama hatutakubali kuwepo kwa fikra tofauti kama za wanaChadema dhidi ya Utawala wa CCM ama hata fikra za mwalimu, basi itakuwa kazi bure hata kuwa hukumu wote watakao endeleza chuki maana mfumo wenyewe umejengwa kututenganisha..
 
Wakuu,
Jana tumeandika sana kuwa kitakachofuata ni kuunda tume za kipuuzi.
Kamishna Chagonja anasema wnanchi watulie hadi uchunguzi ukamilike na tujue matokeo.
Ni upuuzi ule ule wa siku zote wanaendelea nao kwasababu wanajua Watanzania ni mazezeta.

Tume ina wajumbe kutoka jeshi linalotuhumiwa siku nyingi la mauji la Polisi na katika kudanganya kuwa ni uchunguzi huru wameshirikisha wataalam wa JWTZ.

Watanzania inafika mahali lazima tufanye kitu. Hawa watu wanacheza na akili zetu sana.
Tumesema siku nyingi kuwa IGP amejaa damu inayotokana na mauaji ya Polisi, viganja vyake havina usafi wa kufanya uchunguzi.

Mwema anatakiwa ajiuzulu kwanza, pengine baada ya presha ndio ameamua kuwa kuongoza tume, ukweli ni kuwa IGP Said Mwema ameongoza na kushuhudia mauaji ya kutosha na hana usafi wala uhalali wa kuongoza chombo kinachotafuta haki.

Pili, waziri Nchimbi lazima aondoke. Kwa muda mfupi amekuwa sehemu ya tatizo la mauaji na hana uhalali wa kulinda usalama wa wa Watanzania kwasababu ni incompetent.

Picha zipo askari wakimburuza chini Mwango, wakielekeza kifaa tumboni mwa marehemu, wakimbeba mwenzao ambaye haionekani ana majeraha zaidi ya mshtuko, picha za mwili wa marehemu zinaonekana kama zinavyoonekana, gari la mkubwa wa polisi lipo, Sura za polisi walioshiriki mauaji zipo, leo tunaambiwa unafanyika uchunguzi!!!!

IGP Mwema, huu ni upuuzi wa hali ya juu sana. Mwema anaongoza tume kubaini kama Mwangos amefariki au bado yupo wodini, anaongoza tume kujua kama amepigwa na kitu butu au alikanyagwa na waandamanaji.
Huu nasema ni upuuzi wa hali ya juu sana na taifa lazima lione na lisikie uchungu si kwa vifo tu bali kwa utamadanui wa watu kama IGP mwema wa kuufanya umma wa wajinga.

IGP Mwema ni shemeji ya Rais JK, pengine ndio maana wanashirikiana kutufanya wendawazimu kila siku. Hakuna mauaji ambayo IGP amewahi kuyatolea maelezo,hata jariobio la mabwepande anajua Polisi walikuwa wanafanya nini.
Amekubali upuuzi wa kova kwa kujua kuwa Watanzania ni mazezeta. Kama IGP Mwema alikuwabili taarifa ya kijinga na kipuuzi ya kova aliyoshindwa kuitetea, hivi IGP ana uhalali gani wa kuchunguza mauaji Iringa?

WANAHABARI
Kwanza kabisa lazima muungane dhidi ya uhalifu huu. Huu ni uhalifu si tu kwa wananchi bali kwenu pia.
Mumeona jinsi Marehemu alivyovunjiwa utu wa kibinadamu. Simameni katika viatu vya marehemu halafu mjitathmini kulingana na kile mnachokihisi. Unganeni na Wananchi kupinga uchunguzi wa tume ya kipuuzi ya IGP Mwema.
IGP anakwenda Iringa kudhalilisha taaluma yenu! hana uhalali wa kuchunguza kifo cha mwenzenu hata kidogo

NDUGU, MARAFIKI NA JAMAA WA MWANGOS
Tume inakuja kufanya dhihaka! inachunguza kitu gani dunia isiyojua?
Katika wakati huu mgumu, mzito wenye uchungu sana ningeshauri mjiweke mbali na tume.
Sote tufkikirie namna ya kumpunzisha Mwangos na tuidharau tume ya kipuuzi ya IGP inayolenga kudhihaki, dhalilisha, unyama, ukatili na ubazazi uliofanywa na wenye silaha.

Wananchi kwa pamoja tusiposimama kuona Nchimbi na Mwema wanaondoka basi tutaendelea kutunguliwa kama ndege, kuvurugwa kama vicheche na kudhalilika kama tunavyoona askari wanavyoangalia mwili wa mwangos bila chembe ya huruma, utu au ubinadamu.

Tumechoka kuuawawa, lazima tusimame pamoja kusema IGP Mwema, Nchimbi Waondoke, la sivyo JK aondoke.
Tumechoka kuona wanadamu wanfumuliwa kwa kutumia zana za vita, wanadamu wasio na hatia!
 
Well said Mkandara

Tuna matatizo makubwa kwenye mfumo wa utawala na kubwa zaidi ni nchi kukosa falsafa inayotuongoza. Haya matukio ni dalili tu za ugonjwa tunaoumwa kama jamii na kinachosikitisha zaidi ni jitihada nyingi zimeelekezwa kwenye kujaribu kuzitibu hizi "dalili" za ugonjwa bila kuutibu ugonjwa wenyewe na bahati mbaya dalili zipo nyingi, ukiacha "UCCM na UCDM" tuna "UKRISTO na UISLAM" tuna "UKANDA",wenye vipande chungumbovu ndani yake, na nyingine zitaendelea kujitokeza kila uchao.
 
Last edited by a moderator:
Mabadiliko yanakuja....ila yatakuja kwa njia mbili na tuna uamuzi wa kuchagua ni njia ipi tunataka mabadiliko haya yaje:
1. Njia ya amani na maelewano
2. TUNISIA STYLE
 
Katikati ya Michongoma, umekitupa kichanga cha wiki moja. Iweje leo ushangae madonda yake?

Umefuga manyigu, iweje utarajie kulina asali? ACHA YAKUNG'ATE, LABDA AKILI ITAKUKAA SAWA!

Taka tusitake..."MANTIKI YA UTU INAPOKIUKWA, BINADAMU HUGEUKA KUWA KAMA SAMAKI BAHARINI, MKUBWA KUMMEZA MDOGO" Ni unyama, unyama kila kona! Mauaji, vita, njaa, mateso, rushwa, unyonyaji, uduni, maradhi, unyonge, chuki na visasi, matabaka...n.k. BINAFSI, SIONI GENI HATA MOJA, sioni jipya!

Chanzo kikuu cha matatizo yoyote katika taifa lolote, ni Mfumo mbovu wa siasa! Na mfumo mbovu ni ule usiosadifu maisha halisi ya eneo husika.

Wanaafrika wenzangu, leo mkiambiwa tafakarini mlichonacho leo, mnatoa visingizio...et TIME FACTOR-the reality of the world... tumeshamezeshwa sumu kali, hatuoni haja ya kunywa maziwa! Tulivyo wanafiki tunashangaa kuishiwa nguvu, hali tumekataa maziwa! Inauma sana kufikiri. Lakini....TUMAINI LIPO.

Mungu wetu anaita sasa!
 
I haven't fully read the article but I have seen one of the pictures. Clearly it indicates that the use of deadly force in this incident wasn't necessary. First, the journalist was unarmed. Second, the number of police who were trying to apprehend was good enough to accomplish their job.
 
I haven't fully read the article but I have seen one of the pictures. Clearly it indicates that the use of deadly force in this incident wasn't necessary. First, the journalist was unarmed. Second, the number of police who were trying to apprehend was good enough to accomplish their job.

Zakumi from what we see in pics we can say that there was no intent of apprehending the suspect, the aim was to brutally kill him, that is what they did. You can say that they did not need to use a deadly weapon, but the way it looks like that is exactly what they intended.

I do believe that there was something that the journalist had, which they did not like to be seen by Tanzanians.

Believe me with these pictures nothing will happen, all those police officers will not be take into account, they will all be rewarded by brutally killing unarmed man.
 
Back
Top Bottom