Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naona hili neno limekuwa likitumika sana katika kutoa faraja kwa watu, utasikia mtu anamwambia mwenzake, "Pole sanaa ni mipango ya Mungu" ikiwa ni njia ya kumfanya mtu aone hilo jambo ni la kawaida na ni mipango ya Mungu mtu huyo kufa.
Siamini kwamba kila kifo ni mpango wa Mungu.
Imani yangu ni kwamba Mungu katuumba tuishi na tuzeeke tufe.
Mifano ya watu wote walioishi katika njia za Mwenyezi mungu kwenye vitabu vitakatifu inaniambia walizaliwa wakaishi wakazeeka wakafariki wakiwa wenye umri wa kutoendelea kuishi tena. Vifo vya namna hiyo hata mimi naamini ndio mpango wa Mungu.
Mtoto wa miaka minne, ameugua maralia, wazazi wamechelewa kumpeleka hospital au amepelekwa madakatar wakakosea katika vipimo akafa, watu wanasema ni mpango wa Mungu.
Juzi ajali ile ya mabasi ya city boys, dereva badala ya kuendesha kwenye njia yake, kapita njia ya mwenzake watu 42 wakafa tunasema ni mpango wa Mungu kwamba alipanga watu wale 42 wafe siku hiyo.
Unajenga nyumba kizembe zembe mtu anakaa anaangukiwa na ule ukuta unasema ni Mpango wa Mungu.
Nilikuwa naangalia records za vifo vya watoto chini ya miaka 5 kwa upande wa marekani na Tanzania, nikazifanyia comparison, Marekani wana idadi ndogo sanaaaa ya watoto wanaokufa chini ya miaka 5 wakati Tanzania idadi hiyo ni kubwa sana, kwanini? Marekani uangalizi wa watoto wadogo ni mkubwa sana na hata matibabu yake ni ya uhakika wakati Tanzania uangalizi kwa watoto wadogo na matibabu yake ni ya kubahatisha. Je vifo vya hawa watoto ni mpango wa Mungu?
Hivyo hivyo ukiangalia hata hapa kwetu, vifo vya watoto wadogo Masaki na vifo vya watoto wadogo Mbagala utaona kuna ratio ya 1:10 au zaidi ya hapo, Je ni mpango wa Mungu kwamba watoto wengi wafe Mbagala na sio Masaki?
Unaendesha bodaboda kwa speed unaanguka unakufa unasema ni mpango wa Mungu, Mtu katoka huko anaendesha gari lake bila kuwa makini anamgonga raia mwema aliyesimama pembezoni mwa barabara tunasema ni mpango wa Mungu,
Hapana, huo sio mpango wa Mungu, Ni mpango wa binadamu.
Hata katika biblia na Qur'aan ukisoma kama kuna kifo ambacho kilitokea kabla mtu hajazeeka basi fuatilia kuna UZEMBE aliufanya mahali fulani au yeye au wazazi wake wakapelekea akafa.
Kwa kusema hayo, ni imani yangu na ninaomba niwashawishi kwambaa, vifo kabla ya uzee vinaepukika, kutokana na mazingira, kulinda afya yako, namna unavyoishi na watu unaweza kuepuka vifo ambavyo sio mpango wa Mungu.
Kama wewe ni Mkristo na unaiamini Biblia acha nijaribu kukuonyesha imani yangu kwa ishu ya kifo, ni hivi:Una maana gani mkuu
Kifo ni mpango wa mungu amini hvyo
Asante kwa sababu umekubali kwamba wale jamaa walikufa kwa sababu walitenda dhambi.Kama wewe ni Mkristo na unaiamini Biblia acha nijaribu kukuonyesha imani yangu kwa ishu ya kifo, ni hivi:
Kitabu cha kwanza katika Biblia kinaeleza kwamba Mungu alimuumba mtu wa kwanza, Adamu, na kumpa makao katika paradiso. (Mwanzo 2:7, 15) Baada ya kuumbwa, Adamu alipewa kazi, na vilevile sheria iliyomkataza katakata asile matunda ya mti fulani katika bustani ya Edeni. Mungu alimwambia hivi kuhusu matunda ya mti huo: “Usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.”* (Mwanzo 2:17) Kwa hiyo, Adamu alielewa kwamba angeweza kuepuka kifo. Angekufa tu kama angevunja sheria ya Mungu.
Inahuzunisha kwamba Adamu na mkewe Hawa hawakutii. Waliamua kupuuza mapenzi ya Muumba wao, nao wakapatwa na matokeo mabaya ya uamuzi wao. Alipotaja matokeo ya dhambi hiyo Mungu alisema hivi: “Wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.” (Mwanzo 3:19) Walitiwa dosari kubwa, yaani, kutokamilika. Wangekufa kwa sababu ya kutokamilika au dhambi.
Wazao wa Adamu na Hawa, yaani wanadamu wote, walirithi dosari hiyo ya dhambi. Kwa hiyo, dhambi inaweza kulinganishwa na ugonjwa unaorithiwa. Adamu alipoteza taraja la kuishi milele bila kufa, na wazao wake walirithi kutokamilika kutoka kwake. Wanadamu wakaja kuwa watumwa wa dhambi. Biblia inasema hivi: “Hiyo ndiyo sababu, kama vile kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.”—Waroma 5:12.
ExactlyNarrow Thinking!! Amini hivyo pasipo sababu/Maelezo ndio ujinga gani??
If you dont have any competitive advantage dont compete.
Sasa ni mpango wa Mungu huo? Au mpango wakoNataka kufa nina niko na miaka 20+,
Hapo wewe hujafanya uzembe wowote, ila mazingira yako ndo yamekufanya ufe. Yaan soma vizur thread, ni kama mfano niliotoa wa vifo vya watoto wadogo kwa uzembe wa wazazi wao.Sikuumba Majini na Watu ila Wapate kuniabudu.
Naishi vizuri tu na Majirani halafu nalogwa Natupiwa Jini na mtu mwenye Husda kisha Nafariki.
Je hapo pia nimefanya Uzembe upi Kwa mujibu wa Biblia??
Ama kweli watu wangu Wanaangamia kwa kukosa Maarifa..
Vitabu vyetu vipi?basi hata huyo mnaemuomba kwa jina lake alifanya UZEMBE maana alikuwa bado kijana kwa mujibu wa vitabu vyenu!
Wewe ni mshenzibasi hata huyo mnaemuomba kwa jina lake alifanya UZEMBE maana alikuwa bado kijana kwa mujibu wa vitabu vyenu!
JamiiForums hili si tusi..? hebu mpeni haki yakeWewe ni mshenzi
Nakuita mshenzi kwa kudhihaki Nuru na Kweli tuliyoipokeaJamiiForums hili si tusi..? hebu mpeni haki yake