Kifo cha Swetu Fundikira

Injinia

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
849
26
i1534_wauaji.jpg


Michuzi ameandikia kwenye blog yake juu ya kifo cha Swetu Fundikira. Habari zinasema kuwa alipigwa na wanajeshi.

Kuna mtu mwenye habari zaidi?

Hivi wanajeshi wa Tanzania wako above the law? Na ni mafunzo gani ya kijeshi yanayowaelekeza kupiga raia asiyekuwa na silaha (nadhani) hata kama yeye amewatukana nk? Hamna mbinu nyingine ya kumtia mtu nguvuni?

Je nini hatima ya gari alilokuwa akiendesha? Maanake inasemekana rafiki yake alipofika eneo la tukio pamoja na polisi hawakulikuta

RIP bro!!
 
Nasikia wamekamatwa tangu jana....na hii itakuwa murder wamekwisha hao!!
 
Ndio maana kila siku nasema tuacheni tujikalie huku ughaibuni bongo hakuna sheria....Ni vipi mwanajeshi apige mtu hadi kuuwa????Huyu jamaa(Swetu) alikuwa pouwa sana hana ugomvi gomvi wa kipumbavu au matusi/dharau ni mpole sana.Kweli wema hawadumu.
RIP broda Swetu.Ameen
 
Michuzi ameandikia kwenye blog yake juu ya kifo cha Swetu Fundikira. Habari zinasema kuwa alipigwa na wanajeshi.
RIP bro!!
Is it so?

Unadhani hawa jamaa wangemnyanganya hadi gari?
Si huu ni ushahidi wa live?
Anyway...lets keep the ears high!
 
Hii ni alert nyingine kwa viongozi wa Jeshi la Wananchi la Tanzanian na Serikali kwa ujumla. Kwa kipindi kirefu wanajeshi wamekuwa wako mbele sana katika uhalifu na kupiga wananchi na kujichukulia sheria mkononi (Si mnakumbuka askari wa barabarani alivyoadhibiwa pale ubungo mataa). Na pia tumeshuhudia mara nyingi sana hawa wanaoitwa ni walinzi wa amani wakivunja amani sehemu nyingi sana za nchi yetu na serikali na jeshi ni mara nyingi zimeahidi kulishughulikia hili swala lakini hakuna hata chembe ya positive feedback.

Hawa watu nadhani hawana kazi ya kutumia maguvu yao.

My take:

Wawekwe bize kwa kunzishiwa miradi endelevu ya kusaidia jamii kama ujenzi na kilimo. Pia wawe wanapelekwa ktk sehemu za maafa kama kilosa wakasaidie kujenga nyumba huko. Wanakosa shughuliza kufanya ktk kipindi wanachoita wenyewe ni wakati wa amani na badala yake wake wanavunja hiyo amani. Wenzao wa Marekani wako Haiti sasa wanasaidia binadamu na wao wanaua-what a country, what a system?
 
Issue ni kwamba Swetu na wenzake walikuwa kwenye club ya Ben Kinyaiya kinondoni na hao jamaa wajeshi nao walikuwepo na kukatokea kutoelewana kati yao. Wakati wa kuondoka ndio wajeshi wakataka kuwafanyizia maeneo ya Mango na jamaa zake Swetu wakasepa so he was alone.

Jamaa wakamchukua hadi maeneo ya Palm Beach na kumpa kichapo! That was on Friday and he died today morning
 
Hakuna hatari kubwa kama kuwa na Jeshi lisilo na nidhamu. Taratibu mmomonyoko wa maadili unaingia Geshini.Wanapiga raia at will kama vile wao hawana sheria
 
In fact I am very opposed to the system of society in which we live today, not because I lack the natural equipment to do for myself but because I am not satisfied to make myself comfortable knowing that there are thousands of my fellow men who suffer for the barest necessities of life

Remember that man's business on this earth was to look out for himself that was the ethic of the jungle the ethic of the wild beast. Take care of yourself, no matter what may become of your fellow man. Thousands of years ago the question was asked; ''Am I my brother's keeper?'' That question has never yet been answered in a way that is satisfactory to civilized society….the problem of our community lacks freedom of mind, we are mastered by few closed minds which Whatever we hold in our minds mind will tend to occur in our life. Because we are continuing to believe as we have always believed at the end of time we will continue to act as we have always acted as a result we will always continue to get what we have always gotten. The issue comes if we want different results in community all we have to do is change our mind completely

Our problem is we have few Great spirits which always encounter violent opposition from mediocre minds... If particular care and attention is not paid to the citizens and community as whole, we are determined to foment a rebellion, and will not hold ourselves bound by any laws in which we have no voice or representation… under any circumstances when protest against the injustice of long-established laws and customs, does not disprove the fact of the oppressions the satisfaction of the many can proves their apathy and deeper degradation, I don't see if the really freedom we are talking have a purpose, when it does not wish to know anything about the rule of law engraved in the hearts of men and women, when it does not listen to the voice of conscience, it turns against humanity and society. The clearest way to show what the rule of law means to us in everyday life is to recall what has happened to this young man then you can tell me is that the really RULE OF LAW we are claiming? who should be blamed??????

GOOD BLESS TANZANIA

ANTHONY KASSAMALI
 
Haka kanchi banaah nomaa,Polisi nao ni majambazi,wajeshi nao wauaji,mafisadi mmm....halafu mitu inakuja na kelele rudini mjenge nchi...HOW?????acha nijibebee mabox mie.
 
Ndio maana kila siku nasema tuacheni tujikalie huku ughaibuni bongo hakuna sheria....Ni vipi mwanajeshi apige mtu hadi kuuwa????Huyu jamaa(Swetu) alikuwa pouwa sana hana ugomvi gomvi wa kipumbavu au matusi/dharau ni mpole sana.Kweli wema hawadumu.
RIP broda Swetu.Ameen

Inatia uchungu sana kumpoteza ndugu au rafiki kwa jambo ambalo lingeweza kuzuilika;
hivi wakati wanampiga hapakuwa na watu?
Ni mkosa gani kubwa alilofanya kustahili mauti ya kikatili?
ni pombe tu au?

Kwako ndugu yangu mauza uza... acha kuchanganya madesa wewe, damilola taylor, yule dogo mzanzibari, walter mazula na mwenzake, dogo wetu wa docebit (aliyeuwawa texas three years ago, huko south africa kila mwezi mbongo anarudi kwenye sanduku)... lets be fair on this, Swetu amekumbwa na mabaya na ni aibu kwa watanzania, lakini tusianze kupaint picha ya kufunika matatizo yetu
 
Ndio maana kila siku nasema tuacheni tujikalie huku ughaibuni bongo hakuna sheria....Ni vipi mwanajeshi apige mtu hadi kuuwa????Huyu jamaa(Swetu) alikuwa pouwa sana hana ugomvi gomvi wa kipumbavu au matusi/dharau ni mpole sana.Kweli wema hawadumu.
RIP broda Swetu.Ameen


usihalalishe kushindwa kwako kurudi nyumbani kusaidia familia au hata kujenga kibanda ...kwa sababu za kitoto....we are going to America and europe at our wish ...and we work clean home [not with gorvernment]....kama ni kuuwana kwa bunduki night clubs sio ajabu ....America its even worse and the legal system has done nothing to stop rather its increasing plus a lot of frustrations in the army ..... wanaorudi au ambao ni cripled au relatives pia wana violent behaviour.....
wanajeshi wetu pia ni vijana kama vijana wengine ambao ugomvi mkubwa unaweza kuwa wanawake.....na that has to do with personal behaviour ....na sio jeshi!!

rudi nyumbani mzee ..bongo siku hizi tambarare....achana na enzi za kishtobe !!
 
Rip hawa watoto wa wakubwa nao ahh!

........Hili swala linaweza kumpata mtu yoyote, si watoto wa wakubwa tu. Kwenye club kuna mchanganyiko wa watu wa aina mbali mbali, hivyo hili swla litaweza kutokea kwa mtu mwingine.
Muhimu hawa wanajeshi inabidi wahukumiwe tu, ili iwe fundisho kwa wanajeshi wengine wanaopenda kuchukua sheria mkononi ya kupiga mtu.
 
usihalalishe kushindwa kwako kurudi nyumbani kusaidia familia au hata kujenga kibanda ...kwa sababu za kitoto....we are going to America and europe at our wish ...and we work clean home [not with gorvernment]....kama ni kuuwana kwa bunduki night clubs sio ajabu ....America its even worse and the legal system has done nothing to stop rather its increasing plus a lot of frustrations in the army ..... wanaorudi au ambao ni cripled au relatives pia wana violent behaviour.....
wanajeshi wetu pia ni vijana kama vijana wengine ambao ugomvi mkubwa unaweza kuwa wanawake.....na that has to do with personal behaviour ....na sio jeshi!!

rudi nyumbani mzee ..bongo siku hizi tambarare....achana na enzi za kishtobe !!

Thanks Mkuu, haya ndio matatizo ya kuchanganya mambo... sijui kwanini mauza uza ameleta mauza uza tena!!
 
Lets face it. Bongo is near anarchy or anarchy is already in town.

Hebu imagine majambazi wanafunga mtaa?? Halafu wewe unakuja na ngonjera za bongo tambarare?? Acheni dhana za ajabu nyie.
 
Lets face it. Bongo is near anarchy or anarchy is already in town.

Hebu imagine majambazi wanafunga mtaa?? Halafu wewe unakuja na ngonjera za bongo tambarare?? Acheni dhana za ajabu nyie.

hakuna sehemu ambarare duniani... period!!!
 
Hivi ni kweli kuwa hawa askari, wanajeshi wanayohaki au wanaruhusiwa kuchukua sheria mkononi? Ni mara ngapi tunasikia habari za hawa kujichukulia sheria mikononi na hakuna tamko lolote linalotolewa la ujumla.

Mimi nafikiri kama wanaruhusiwa basi ruhusa hiyo iishie kwao wenyewe yaani wanajeshi kwa wanajeshi na police kwa police na kamwe si kwa raia. Iamriwe kuwa askari yeyote akimpiga raia kwa sababu yoyote ile basi ahukumiwe kwa kosa la kujichukulia sheria mkononi ah wanabore sana hawa kwani wao ni kina nani hadi waruhusiwe kuishi kibabe babe humu nchini?
 
waliomuua Swetu ni askari ambao ni Mke na Mme tayari wameshakamatwa na wapo kikaangoni. tusubiri labda yatakuwa kama ya akina ZOMBE kuachiwa kwa kwenda mbele
 
May his soul RIP ,
hawa wanajeshi inabidi washtakiwe ktk mahakama ya kiraia.akae ukonga,or segerea mpaka hukumu itakapotolewa,
mafunzo ya kijeshi ni ya kujeruhi na kutoa uhai,sasa yametumiwa vibaya uraiani,viongozi wa jeshi TZ ,wapelekwe cozi za uongozi ili waweze kumanage vijana wao
 
Michuzi ameandikia kwenye blog yake juu ya kifo cha Swetu Fundikira. Habari zinasema kuwa alipigwa na wanajeshi.

Kuna mtu mwenye habari zaidi?

Hivi wanajeshi wa Tanzania wako above the law? Na ni mafunzo gani ya kijeshi yanayowaelekeza kupiga raia asiyekuwa na silaha (nadhani) hata kama yeye amewatukana nk? Hamna mbinu nyingine ya kumtia mtu nguvuni?

Je nini hatima ya gari alilokuwa akiendesha? Maanake inasemekana rafiki yake alipofika eneo la tukio pamoja na polisi hawakulikuta

RIP bro!!

Kaka binafsi nimepitia jeshi kwa mujibu wa sheria - JKT. kule tunafunzwa nidhamu na utii pamoja na heshima. sasa unajua hawa wanajeshi wa vyeo vya chini wasiwe ndiyo wanaharibu dhana nzima ya jeshi letu.

Ukiangalia sana wenye matatizo makubwa ni hawa wenye vyeo vya chini, kwa mafano huyu jamaa ni sajenti na mkewe ni koplo kulingana na habari tuliyopewa.

Sasa ngoja nikupangie vyeo vya kijeshi kuanzia cheo cha chini kabisa kwa wale wasiopewa comisheni na Raisi wa nchi.

1. Kuruta - Mwanajeshi anayeanza mafunzo ya mwanzo kabisa
2. Private - Mwanajeahi anayehitimu mafunzo ya mwanzo kabisa na
anapewa force number - sisi pia tupo kundi hili tulipitia JKT
3. Lansi Koplo - Anavaa V moja chini ya bega
4. Koplo - Anavaa V mbili chini ya bega
5. Sajenti - Anavaa V tatu chini ya Bega
6. Staff Sanjenti - Anavaa V tatu ngao ya adamu na hawa chini ya bega
7. Sir Meja - anavaa Saa mkononi - mara nyingi ni wazee wanaokaribia
kustaafu mara nyingi wanakuwa watu wa nidhamu
8. Senior Sir Meja - Wanakuwa wakuu wa nidhamu wa kikosi

----------------------------------------------------------

Hawa huwa hawapigiwi saluti na ukiangalia sana vyeo 1 - 5 hapa ndo kwenye matatizo makubwa, kwa hiyo katika kujadili hii mada angalieni msiwaingize maofisa wa jeshi kuanzia Luteni Usu na kuendelea, wenye matatizo ni hawa wenzangu mie, ni wakali kweli na wanafujo sana wanajifanya wao ndio serikali ya nchi hii.

Kwanza kama kweli wamempiga jamaa kwa kosa la kuchubua gari lao tu hadi jamaa kufa basi wachukuliwa hatua kali ili na wenzao wajue kwamba hakuna aliye juu ya sheria.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom