Kifo cha mwenyekiti wa CHADEMA Usa river-Arumeru - Arusha

tpmazembe

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
2,469
581
NIMEJARIBU KUTAFAKARI KIFO HICHI NIMEPITA PICHA HALISI YA SIASA ZA TZ BAADHI NI:-
  • Watanzania tuna siasa za chuki na za kulipana kisasi ,hii ni kutokana na tulivoiweka siasa maana unakuta uchaguzi mdogo mgombea mmoja bajeti anayotumia inakaribia mil 600,ukijiuliza kazitoa wapi?,atazilipaje? hupati jibu,Kutokea yaliyotokea inakuwa kitu cha kawaida maana anayeshindwa anayeruhiwa vibaya sana kiuchumi.
  • VYAMA VYETU TUNAVYOVISHABIKIA VIKO KIMASLAHI ZAIDI HAVIJALI WATU WAKE:-Angalia Mwenyekiti amekufa chadema kama chadema wametuma tu wabunge wawili wamezika hakuna kinachoendelea,hatujasikia kama wameunda timu kuchunguza mauaji au kutoa onyo kwa serikali ,wako kimya,SASA VYAMA VYA SIASA KAMA CDM kuna umuhimu gani kushabikia.wakati viongozi hawa value watu.
 
Mimi ni cdm damu,lakini sasa naweza kukaa pembeni kama mambo yatachukuliwa kinyemela namna hii
 
Hapana, CHADEMA wako makini kabisa na fuatilia vyombo mbalix2 vya habari; Mbowe alisema CHADEMA wako mbioni kutoa tamko. Mtoa mada subiri, hakuna papara wala udhaifu mzee, kifo kinauma hasa katika mazingira yale.
 
Mimi ni cdm damu,lakini sasa naweza kukaa pembeni kama mambo yatachukuliwa kinyemela namna hii

Kwani polisi wangetaka siwangewajumuisha CDM kwenye huo uchunguzi? Nakuhakikishia CDM hawana dola kwa hiyo wanachokijua kuhusu hicho kisa usishangae kukandamizwa na dola. Ila kaa pembeni kama huelewi vitani kuna majeruhi na wahanga.
 
Mimi ni cdm damu,lakini sasa naweza kukaa pembeni kama mambo yatachukuliwa kinyemela namna hii
WEWE HUKUSOMA MAJUZI TU CHADEMA WAMESEMA WANAIPELEKA SERIKALI MAHAKAMANI KWA MAUAJI YA WANACHAMA WAKE? SIKUMBUKI NI MAGAZETI YA LINI LKN KAMA SIYO WIKI HII NI MWISHONI MWA WIKI JANA. Nafikiri siyo vema kulaumu CDM wakati bado Polisi wanaendelea na Uchunuzi.
 
Mimi ni cdm damu,lakini sasa naweza kukaa pembeni kama mambo yatachukuliwa kinyemela namna hii

Hakuna maana kujiita CDM damu wakati huwezi kujibu hoja ya mleta mada. Sote tulisikia yaliyosemwa siku ya mazishi ya mwenyekiti sasa unataka nini. Wewe ondoka tu maana CDM inaundwa na wanaojitolea kwa hali na mali hata maisha pia. Kumbuka watu wengi sana wamekufa hapa dunia wakidai haki ambao mimi na wewe tunajivunia. Soma alama na historia ya dunia. Shame on you.
 
Wewe si mfuatiliaji wa hoja hii. Ni mara ngapi Mwenyekiti kalitolea maneno makali jambo hili? Au kuna cha ziada unataka kukileta.
 
Mtoa mada hujui mtiririko wa Idara ya John mnyika,juzi alilitolea ufafanuzi..pengine wewe ni gamba.
 
Mi cdm damu,ukisema 2chunguze utakuwa unaingilia kazi ya polisi..2silaumu chama.[/QUOTE
juzi tu polisi wametangaza ktk gazeti la mwananchi watatoa 10m Tshs kwa mtu yeyote atakaetoa taarifa za kuwakamata waliohusika tafadhali mwana JF soma vyanzo vingine vya habari za ndani Serikali haijafuraishwa na mauaji ya binadamu yeyote yule hapa TZ juu ya kujitoa ktk chama nijukumu lako binafsi huitaji kujitangaza humu
 
Mi cdm damu,ukisema 2chunguze utakuwa unaingilia kazi ya polisi..2silaumu chama.


hakusema mchunguze, kasema yeye kama raia hajaona ni kwa kiasi gani CHADEMA imelichukulia swala hilo katika uzito unaolipasa...yule jamaa alikufa kwasababu ya CHADEMA, alichangia kwa kiasi kikubwa Nasari kushind katika kata yake, ni mtu muhimu lakini je, kweli msiba ule ulikuwa wa kutuma wabunge wawwili kama mtoa mada anavyosema??????? labda katika kuelimisha na kuutarifu umma ni kwa kiasi gani CHADEMA inawajali wanachama/ makamanda wake wanaopatwa na mambo mabaya katika harakatin za wao kukitumikia chama hebu tuwekeeni mifano CHADEMA imesimama vipi katika kushughuilikia ile kesi nya mauaji ya kamanda aliyetoka Ubungo kwenda Igunga kama wakala...wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga baada ya Rostam kung'atuka.
 
Mtoa mada hujui mtiririko wa Idara ya John mnyika,juzi alilitolea ufafanuzi..pengine wewe ni gamba.

1. Sio kila mtu alimsikia Mnyika, so ulichopaswa kusema ni kumwambia mtoa mada Mnyika aliongea nini wakati analitolea jambo ufafanuzi
2. Ni UJINGA uliokomaa kudhani kila anyetofautiana na wewe kimtazamo au kuhoji baadhi ya mambo ya CHADEMA ni Gamba..ni fikra mgando, njia nzuri moja wapo ya kukijenga chama ni KUKIKOSOA kwa kutoa constructive cricisms...usidhani kukisifia chama siku zote ndio upenzi wa chama, huo sio upenzi ni ushabiki na unafiki..
 
1. Sio kila mtu alimsikia Mnyika, so ulichopaswa kusema ni kumwambia mtoa mada Mnyika aliongea nini wakati analitolea jambo ufafanuzi
2. Ni UJINGA uliokomaa kudhani kila anyetofautiana na wewe kimtazamo au kuhoji baadhi ya mambo ya CHADEMA ni Gamba..ni fikra mgando, njia nzuri moja wapo ya kukijenga chama ni KUKIKOSOA kwa kutoa constructive cricisms...usidhani kukisifia chama siku zote ndio upenzi wa chama, huo sio upenzi ni ushabiki na unafiki..

Polepole, utakuwa upo kijijini na hujui nini kinaendelea duniani. Ulofa wako usiuexpose kwa jamii erevu. Pole mdau mzembe!
 
NIMEJARIBU KUTAFAKARI KIFO HICHI NIMEPITA PICHA HALISI YA SIASA ZA TZ BAADHI NI:-
  • Watanzania tuna siasa za chuki na za kulipana kisasi ,hii ni kutokana na tulivoiweka siasa maana unakuta uchaguzi mdogo mgombea mmoja bajeti anayotumia inakaribia mil 600,ukijiuliza kazitoa wapi?,atazilipaje? hupati jibu,Kutokea yaliyotokea inakuwa kitu cha kawaida maana anayeshindwa anayeruhiwa vibaya sana kiuchumi.
  • VYAMA VYETU TUNAVYOVISHABIKIA VIKO KIMASLAHI ZAIDI HAVIJALI WATU WAKE:-Angalia Mwenyekiti amekufa chadema kama chadema wametuma tu wabunge wawili wamezika hakuna kinachoendelea,hatujasikia kama wameunda timu kuchunguza mauaji au kutoa onyo kwa serikali ,wako kimya,SASA VYAMA VYA SIASA KAMA CDM kuna umuhimu gani kushabikia.wakati viongozi hawa value watu.

Nikisema mtoa mada ni Mpumbavu wengine watasema nimemwonea! Basi wacha nisisema hivyo.
Kwanza kabisa wewe si mwanachadema ndiyo maana hujui nini kiliendelea.
Pili hujui utaratibu wa uwakilishi wa chama au taasisi kwenye mazishi.
Tatu hujui taratibu za kutoa tamko. Chama makini lazima itafakari, ifanye uchunguzi wa tukio siyo kukurupuka kama wewe unavyotaka.
Vile vile nchi hii kuna taratibu za kisheria, ambayo uchunguzi wa tukio unafanywa na idara ya upelelezi. CDM kuingilia uchunguzi wa jeshi la polisi ni kukiuka taratibu za upelelezi, lakini inaweza kufanya uchunguzi wake kimya kimya then inakuja na conclusion.

Wewe siyo CHADEMA
 
Mimi ni cdm damu,lakini sasa naweza kukaa pembeni kama mambo yatachukuliwa kinyemela namna hii[/

Huwezi kuwa CHADEMA damu halafu ujisalimishe kirahisi namna hiyo, kumbuka kuwa CHAMA kilifanya kitu cha muhimu sana kutuma ujumbe wake kwenye msiba ule huku ukizingatia kuwa bado chanzo cha mauaji yale bado hakijajulikana kama ni siasa au la.
 
NIMEJARIBU KUTAFAKARI KIFO HICHI NIMEPITA PICHA HALISI YA SIASA ZA TZ BAADHI NI:-
  • Watanzania tuna siasa za chuki na za kulipana kisasi ,hii ni kutokana na tulivoiweka siasa maana unakuta uchaguzi mdogo mgombea mmoja bajeti anayotumia inakaribia mil 600,ukijiuliza kazitoa wapi?,atazilipaje? hupati jibu,Kutokea yaliyotokea inakuwa kitu cha kawaida maana anayeshindwa anayeruhiwa vibaya sana kiuchumi.
  • VYAMA VYETU TUNAVYOVISHABIKIA VIKO KIMASLAHI ZAIDI HAVIJALI WATU WAKE:-Angalia Mwenyekiti amekufa chadema kama chadema wametuma tu wabunge wawili wamezika hakuna kinachoendelea,hatujasikia kama wameunda timu kuchunguza mauaji au kutoa onyo kwa serikali ,wako kimya,SASA VYAMA VYA SIASA KAMA CDM kuna umuhimu gani kushabikia.wakati viongozi hawa value watu.

Kazi ya Kukulinda wewe, na mimi na mwingineyo yeyote katika jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kazi ya Serekali iliyopo madarakani, na kama serekali imeshindwa kuwalinda wananchi wake inasubiri Matamko ya wana siasa Ujue Kuna Tatizo Kubwa sana!! Unless ututhibitishie Kuwa Jeshi la polisi Linafanya kazi yake kwa shinikizo la wanasiasa.
Ila pia Ujue wauwaji wameshafanya Uhalifu wao (Na Mungu awalaani) Kitendo cha CDM kutuma mwakilishi naona ni sawa Kabisa ila Ningeomba lile Wazo la wanachama Kuchangia Hela Kwa Ajili ya Kuwasemesha Watoto Waliobaki Hai Lizingatiwe!! Hata kwa Michango ya wanachama
 
Hapana, CHADEMA wako makini kabisa na fuatilia vyombo mbalix2 vya habari; Mbowe alisema CHADEMA wako mbioni kutoa tamko. Mtoa mada subiri, hakuna papara wala udhaifu mzee, kifo kinauma hasa katika mazingira yale.

Ni kweli ni suala la subira, bado wako makini lakini masuala ya jamii/ watu wengi yanahitaji takwimu/ bird watching/ busara/ hekima kuja kwenye mrejesho na hatimaye maamuzi magumu. Lets give ourselves time!:clap2:
 
Nani anae value watu,CCm walioua au CDM iliyopeleka wabunge?
CCM NI CHAMA KICHAFU NA KISICHOKUWA NA TIJA KWA SASA KWA TAIFA LA TANZANIA,MIMI NI MWANA CDM KWA KUWA NAPENDA MABADILIKO,ccm wanajulikana ni malaika waliofukuzwa mbinguni kwa jeuri na sasa waiihamishia hiyo jeuri dunia na adhabu yao iko wazi ni moto wa milele, lakini cdm ningetegemea wafanye mambo katika hali ya tofauti kidogo LAKINI katika hili CDM wamechukulia juu juu sana,Polisi wahawezi chunguza chochote,ilitakiwa iundwe timu ya cdm viongozi wakuu kama slaa wangeweka kambi arumeru walau kwa wiki moja lakini hilo halijatokea na sasa kila mtu kasahau
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom