Mkurugenzi wa habari na uenezi (CHADEMA) John Mnyika leo akiongea na waandishi wahabari katika ofisi ya chama, amemtaka Kikwete kuchukua hatua za haraka kwa wahusika kwa kumpiga na bomu la machozi mwandishi wa habari Mwangosi hadi kumpelekea kupoteza maisha.
Pili amemtaka kumsimamisha kazi Paul Chagonja na RPC (Iringa) Kamuhanda kusimamishwa kazi wakati uchunguzi unaendelea.
Tatu alitaka uchunguzi ufanyike wa kujua kifo cha Mwangosi ni shinikizo kutoka kwa nani?
Kuhusu wahusika wa mauaji anasema kuwa tayari wanajulikana huku akionesha picha gazeti la jana la mwananchi wakati polisi nane wakimsulubu Mwangosi. hao ambao wameonekana kwenye picha ndio wa kwanza wanapaswa kukamatwa, sababu hata wao polisi wakati raia ameuawa huwa wanaanza na wale watu walikua karibu na tukio.
Kwa maana hiyo polisi nane wanapaswa kuwa wa kwanza kukamatwa.
source ITV- habari za saa.
Pili amemtaka kumsimamisha kazi Paul Chagonja na RPC (Iringa) Kamuhanda kusimamishwa kazi wakati uchunguzi unaendelea.
Tatu alitaka uchunguzi ufanyike wa kujua kifo cha Mwangosi ni shinikizo kutoka kwa nani?
Kuhusu wahusika wa mauaji anasema kuwa tayari wanajulikana huku akionesha picha gazeti la jana la mwananchi wakati polisi nane wakimsulubu Mwangosi. hao ambao wameonekana kwenye picha ndio wa kwanza wanapaswa kukamatwa, sababu hata wao polisi wakati raia ameuawa huwa wanaanza na wale watu walikua karibu na tukio.
Kwa maana hiyo polisi nane wanapaswa kuwa wa kwanza kukamatwa.
source ITV- habari za saa.