Kifo cha Mholanzi huko Serengeti na mwitikio wa mawaziri wawili...

katika taarifa ya habari ya leo nimeshuhudia mawaziri wawili(yule wa mambo ya ndani na yule wa maliasili na utalii) wa JMT wakifika katika eneo la tukio.
sio muda mrefu tuliwahi kusikia mauaji ya kutisha mfano kiongozi wa chadema kuchinjwa na chainsaw,vijana wanne kunyongwa,zeru zeru kuuliwa kikatili na viungo vyake kunyofolewa.

swali;je mawaziri wanathamini wazungu kuliko watanzania?



KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Waziri wa maliasili na utalii lazima afuatilie kwa sababu aliyeuawa ni mtalii. Kwa sheria za kimataifa mtu anapouliwa kwenye nchi isiyo yake lazima nchi husika itoe taarifa za kueleweka kwa nchi ya aliyeuliwa. Waziri wa mambo ya ndani lazima atoe ushirikiano kwa waziri wa utalii kwa sababu yeye ndio anahusika na usalama wa mtu yeyote(m-tz/mgeni) aliyeko nchini. Ukizingatia kila KLM inapotua KIA, inashusha watallii zaidi ya mia na kupakiza wengine zaidi ya mia(wengi wao waholanzi) serikali inaingiza pesa nyingi sana kutoka kwao(ingawa wanazila, na hawakarabati uwanja) wakiogopa kuja revenue itapungua. Majirani zetu wametupaka matope sana, huku napoishi wazungu wengi wanaamini wakija Tz watauawa, unaweza ukaamini Tz kuko hivyo?
Kuhusu kutofuatilia mauaji ya watanzania Wizara ya mambo ya ndani ndio wahusika isipokuwa hawawajali wananchi, wanapaswa kulaumiwa kwa hilo.
 
Kwani hao chadema ni watalii (wageni) humu nchini?

Kwani hao watalii walikuwa wakiandama? au ni wananchama wa chadema? ulipaswa kujibu hoja kwa uzito wake si kulopoka, na kuleta ushabiki. Uzito uko pande zote sababu vyote ni vifo ila huu wa wazungu unaimpact kimataifa, inaeleweka tz askari wamekuwa wakiosama raia, hivyo hata kama mawaziri wameenda sidhani mataifa ya majuu yana imani na system ya usalama wa hapa tz,
 
katika taarifa ya habari ya leo nimeshuhudia mawaziri wawili(yule wa mambo ya ndani na yule wa maliasili na utalii) wa JMT wakifika katika eneo la tukio.
sio muda mrefu tuliwahi kusikia mauaji ya kutisha mfano kiongozi wa chadema kuchinjwa na chainsaw,vijana wanne kunyongwa,zeru zeru kuuliwa kikatili na viungo vyake kunyofolewa.

swali;je mawaziri wanathamini wazungu kuliko watanzania?



KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

mambo mengine anaweza akashughulikia mkuu wa wilaya! lakini inapokuja mgeni mambo ya diplomatic issues hata rais anaweza akaenda
 


mambo mengine anaweza akashughulikia mkuu wa wilaya! lakini inapokuja mgeni mambo ya diplomatic issues hata rais anaweza akaenda
na wewe unaona sawa tu kwa hilo?
Kuna mwanafunzi wa kitanzania aliuawa huko india unaweza kueleza ni kilitokea?
Kwa nini tusikubali kuwa damu yetu ni dhaifu kwa mdhungu?
Kuna mkenya aliuawa kwenye maandamano arusha mbona sikuona waziri kwenda arusha?au hii diplomasia imetufunza kuogopa wageni wa mbali na Tanzania?


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
katika taarifa ya habari ya leo nimeshuhudia mawaziri wawili(yule wa mambo ya ndani na yule wa maliasili na utalii) wa JMT wakifika katika eneo la tukio.
sio muda mrefu tuliwahi kusikia mauaji ya kutisha mfano kiongozi wa chadema kuchinjwa na chainsaw,vijana wanne kunyongwa,zeru zeru kuuliwa kikatili na viungo vyake kunyofolewa.

swali;je mawaziri wanathamini wazungu kuliko watanzania?



KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

serikali na viongozi wetu ni watu wa hovyo sana..kwao wazungu ndo watu ....sijaelewa mantiki ya mawaziri wawilikwenda eneo la tukio wakati diwani alitosha ku handle hiyo kitu
 
Mi nadhani kuna njama ili watalii wasije Tanzania.Hizi ni njama za makusudi kabisa ili Tanzania ionekane si salama kwa watalii,tumeshuhudia hivi karibuni jirani yetu akisema Tanzania sio salama kwani Zanzibar kuna vurugu na wakati huohuo ikumbukwe kwa muda mrefu waliwahadaa walimwengu kuwa Kilimanjaro iko Kenya. Serikali ifanye uchunguzi wa kina juu ya suala hili.

Nakubaliana nawe mkuu.
Alafu na kwa wale wasio fahamu, hii lodge ipo nje ya hifadhi ya Serengeti. Near Fort Ikoma.
Pili, hili ni shambulizi la pili kwenye hotel hiyo hiyo kwenye kipindi cha miezi miwili.
Ila, ni aibu kwa govt kujali watu wa nje zaidi ya watu wao.
Na ushauri hapa ni JWTZ wapewe jukumu la kulinda hifadhi wakishirikiana na game rangers kabla hawa maharamia hawajaingia ndani ya hifadhi kufanya maafa.
JWTZ wapelekwe na Zanzibar kulinda vituo vya polisi na makanisa. Mtu akienda jaribu tia moto vituo au kanisa, JWTZ itahakiki tunaona maiti ya mtuhumiwa. Hii itasaidia kubaini kama kweli UAMSHO wanasingiziwa.
 
Kwani hao watalii walikuwa wakiandama? au ni wananchama wa chadema? ulipaswa kujibu hoja kwa uzito wake si kulopoka, na kuleta ushabiki. Uzito uko pande zote sababu vyote ni vifo ila huu wa wazungu unaimpact kimataifa, inaeleweka tz askari wamekuwa wakiosama raia, hivyo hata kama mawaziri wameenda sidhani mataifa ya majuu yana imani na system ya usalama wa hapa tz,

Tatizo lako hujui kanuni na sheria za mikataba ya Mahusiano ya Kimataifa ya kisiasa na ya kibiashara, unakurupuka tu.

Mgeni wa Kimataifa wa Kibiashara ambayo unatumia fedha nyingi kuitangaza huko nje, anapatwa na maafa wenzake wengine bado wako huko, wamejaa hofu na simanzi na waziri husika anaweza kwenda kujuwa tatizo nini, asiende? au akienda iwe mwao? hivi huwa mnafikiri kutumia vichwa vyenu? Halafu hayo mauaji yametokea Kaskazini! unawajuwa watu wa Kaskazini au unawasikia tu?

Juzi juzi tu, hukohuko Kaskazini kakutwa "albino" kakatwakatwa na kunyofolewa viungo vya mwili, jee inawezekana hawa waliofanya haya mauaji kwa hawa wazungu wamewafikiria kuwa ni "maalbino"? wacheni viongozi wa Serikali wafanye kazi zao inavyopaswa, wakikosea mseme, lakini hili la mawaziri kwenda huko sio kosa na ni uwajibikaji uliotukuka. Ningefurahi zaidi hata Rais angekwenda huko.
 
Serikali imehofu kwani image ya nchi imekuwa 'turnshed'. Habari hiyo imetangazwa na vyombo vya habari vya kimataifa, hivyo Tanzania itaonekana siyo salama.Tutakosa misaada na watalii hawatakuja kwetu na kuleta fedha za kigeni tusipofanya kama mawaziri walivyofanya.

Kwani hao chadema ni watalii (wageni) humu nchini?

Akili nyingine za kushikiwa kweli kweli. Nchi za wenzetu huku mambo kama hayo huwezi kuta waziri anaenda kwenye eneo la tukio. Ni polisi tu ndo wanaoshughulikia.
Kwani nani hajui kuwa duniani ni Tanzania pekee where mgeni anapewa kipaumbele kuliko mwenye nchi?
 
Kama mpaka leo hii majangili ya kisomali yanasumbua wamasai ngorongoro unategemea nchi ni salama?


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
dhaifu & reactive government! sijapenda kifo cha mholanzi nimekerwa na double standard ya serikali, hii serikali imeingia kwenye dini ya WHITE SUPREMACY. hope this silly season itaishia 2015
 
dhaifu & reactive government! sijapenda kifo cha mholanzi nimekerwa na double standard ya serikali, hii serikali imeingia kwenye dini ya WHITE SUPREMACY. hope this silly season itaishia 2015

hata mimi ndicho ninachokiona hapa.ni ukweli usiopingika kuwa serikali haimthamini mtanzania kama inavyomthamini mdhungu,hii inapelekea hata wazungu kwatemea mate askari polisi wetu.
 
Kuna sehemu nilikuwepo yaani wameondoka watalii 30 jana kurudi makwao yaani balaa tupu.
 
yale yale,RPC kauawa lakini sijasikia responce ya waziri wa mambo ya ndani


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Back
Top Bottom