MABARAZA YA CHADEMA ITUNZENI HESHMA YA MHE REGIA KWA KUKAMATA MAJIMBO YOTE MIKOA YA DAR ES SALAAM NA MOROGORO BILA AJIZI!!!
Mi-Baraza yetu ya BAVICHA na AWACHA mkoani Morogoro, hakikisheni kwamba kiuhakika hatumuaibishi Mhe Regia na azma yake yo kuwakomboa wanyonge vijijini wasiokua na pa kusemea.
Shambulieni Mkoa huu wa Morogoro kwa mtindo wa kijiji kwa kijiji, kata kwa kata, na kigango kwa kigango mpaka elimu ya uraia usambae kila mahala na majimbo yote kuwekwa chini ya vijana machachari na wenye moyo kama Mhe Regia ndani ya CHADEMA kunakowadia 2015.
Kumbukeni yale maneno mazito na yenye busara kubwa kutoka kwa Mzee Mtema (Baba ya Regia) kwamba CHADEMA japo mmepoteza kamanda kwa maana ya huyu mwanangu lakini naamini kwamba Mungu atawaibua Regia wengine wengi zaidi ndani ya chama siku si nyingi.
BAVICHA na BAWACHA kazi kwenu kwa kuhakikisha mkoa mzima wa Morogoro na Tabata Dar es Salam aliko Mhe Regia mambo shwaaaari mapema iwezekanavyo bila kuendelea kuwakilishwa kwa siku zaidi na Magamba maeneo hayo. Kazi iendeleeee sasa huku uongozi wetu wa Taifa wakiendelea kuwa karibu sana na juhudi zenu katika hili.
Mwisho wa siku NEC ndo msema kweli baada ya kura kupigwa..
Tangu lini marehemu akawa na uwezo wa kupigana?Baada ya kuulizwa kuhusu mgogoro huo mkubwa,Dr Slaa alikiri kupewa taarifa hizo na kusema kuwa alikuwa anategemea kuanza kuushughulikia lakini kwa sasa kwa kuwa tupo kwenye msiba hatuwezi kuzungumzia hilo.kifo cha rejia kina siri nyingi na susan kiwanga ana mengi ya kutueleza kuhusu mgogoro wake na marehemu na jinsi ulivyokiathiri chama hadi inafikia walitaka kupigana na marehemu.
RAIS Kikwete hivi karibuni alishuhudia Live kifo cha CCM yake kule Ifakara katika mazishi ya mbunge wa viti maalum chadema Rejia Mtema.
ni ukweli ulio wazi kuwa kutokan na picha ile jamani CCM bye bye.
kazi ilianza pale msafara uliobeba mwili wa Rejia Mtema, kufika Kilombero mkoa wa Morogoro, msafara huo uliokuwa ukiongozwa na spika wa Bunge ana makinda na baadhi ya mawaziri wengine wa serikali ya Jk akiwemo Stephan Wasira, njia nzima ilikuwa ji salamu za chadema , ilikuwa bomba la mtihani kwa wanaccm kuitikia salamu ile ama Laah, nadhani ndio maana hata wakati wa kuaga mwili wa mbunge wa CCM Solomon Sumari makinda alidai kuwa tusichanganye siasa wakati wa misiba, its True aliliona hilo lakini wale ni wananchi wapenda chadema,ki ujumla kilombero , ifakara ni ngome ya chadema,
Kipigo kingine kwa CCM ni pale makaburini ambapo baada ya mazishi Rais na msafara wake waliondoka , na alipoanza kuondoka DK Slaa wananchi walianza kuimba Rais Rais, na kuwaancha vinywa wazi CCM,
watanzania wa sasa hawana woga tena kama zamani, hivi sasa ukikosea unapewa Kubwa tu
pia Tukio Lingine ni pale mbunge wa wa CCM Abdul Mteketa alipozomewa Live mbele ya viongozi wa kitaifa wa CCM, jamani picha Hii yote imemdhihirishia wazi Jk kuwa kifo cha CCM kimefika.
mkuu twanga kote kote sasa hivi vijijini wanajua kuwa mjini wamehamia Chadema nao watahamia huko maana mijini kuna maendeleo kuliko vijijini nani hapendi maendeleoSahihi kabisa mkuu!elimu ya uraia inahitajika sana,mimi wewe na yule popote pale tulipo itolewe!cdm nao waache kujikita sana mijini,pembezoni nako kuna kura,matawi zaidi na yawe rahisi kufikika,kadi,scuff nk zikosekane matawini!hv vitu upatikanaji wake mgumu sana hata mijini,sijuhi kwa nini!vimahamsha hamasa hv!Moro yetu ina kila kitu ila imestuck kutokana na viongozi hovyo hovyo wenye mipango hovyo hovyo,tunahitaji waje kina Regia(R.I.P) zaidi ya 20 kuiamsha na kuikomboa Moro yetu na Tz kwa jumla,naamini ikiwa hivyo Regia nae atafarijika huko alipo
CCM haitishiwi Nyau wana mbinu zaidi ya mia mbili wana ifakara kuweni makini msijeletewa Mvua ya Njaa... Siasa ni Mchezo Mchafu! wanaofaidika ni Wachache..
Kweli mkuu wako wengi mno ka zamadamu aka tyson.Mfagia choo wa Nepi utamjua tu.Wala hajifichi.