KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF mambo vp?Kuna kifaa fulani kinachotumika kusafishia rangi ya tv sikijui jina lake kinaitwaje niliwahi kukiona nchini Kenya kwa fundi mmoja kama miaka mitano iliyopita.Kifaa chenyewe ukubwa wake unalingana na lile boksi la dawa ya whitedent ile ya sh 1000.Hicho kifaa kinatumia umeme unapokiwasha kinawaka na kuunguruma kama ilivyo mashine ya kunyolea unapokielekeza kwenye uso wa tv iliyoharibika rangi kinaanza kuchanganya rangi na unapokizima tu tayari tv inakuwa imerudisha rangi yake ya asilia.Natumai kwa maelezo haya machache kama yupo anayekifahamu kifaa hiki kinapopatikana kwa huku bongo tafadhali tujulishane.Natanguliza shukrani