Kisoda2
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 2,475
- 745
Wadau habari hii nimeisikia jana toka radio sauti ya Amerika.Imenifanya nijiulize maswali mengi kuhusu kauli ya mtu alie pewa dhamana na taifa kusimamia taasisi hii(EWURA)
Katika sakata na mafuta ya petrol na aina nyinginezo za nishati hiyo kukumbwa na mtindo kuchanganywa na aidha maji ama aina nyingine ya nishati ili kujipatia faida kubwa kunakofanywa na wafanyabiashara hapa nchini kulisababisha mtafaruku katika msafara wa rais(muungwana)huko Moshi.
Mtendaji mmoja toka taasisi hiyo(EWURA) alisema wahusika katika sakata hilo wamepewa wiki moja wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua kwa kitendo hicho.
Hivi kweli kwa kauli kama hii tutafika?
Katika sakata na mafuta ya petrol na aina nyinginezo za nishati hiyo kukumbwa na mtindo kuchanganywa na aidha maji ama aina nyingine ya nishati ili kujipatia faida kubwa kunakofanywa na wafanyabiashara hapa nchini kulisababisha mtafaruku katika msafara wa rais(muungwana)huko Moshi.
Mtendaji mmoja toka taasisi hiyo(EWURA) alisema wahusika katika sakata hilo wamepewa wiki moja wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua kwa kitendo hicho.
Hivi kweli kwa kauli kama hii tutafika?