Kibanda ajitoa kamati ya Nchimbi...

Kamati yenyewe ni ya usanii mtupu. Vazi la Taifa lilikwisha patikana miaka ya nyuma pale Dodoma na washindi walipewa zawadi zao!
 
Kibanda ana ndoto zake za mchana Dr Slaa, akiwa rais atakuwa msemaji wa Ikulu!

You guy!! Wakati mwingine sio ujanja..ni upumbavu,kama una la kusema sio lazima kuchangia,is better to read and to remain quite you will be considered as a person who having wisdom...otherwise this habit which you build in yourself nowdays of just drop whatever comes from your mind it deteriorates your status to your family especialy your wife Jane and your five chidren Michael,Miriam,Mathias,Matrida and Mathayo and I don't think if it is good at all....Jiheshimu mkuu!!
 
Kama alivyosema my dude, mi nikafikiri ningeweza kupata fundamental na philosophical differences kama zile za kusema kwamba haamini vazi la taifa linaweza kupatikana kwa top down approach.

Kufungua nakuta squabling za a thinnly disguised "umimi". Kibanda anachotuambia ni kwamba asingekuwa na beef na the powers that be angekuwa tayari kushiriki katika hii charade.

All in all, afadhali ya huyu aliyejitoa (hata kama kwa personal quabbles, as opposed to fundamental principles) kuliko wale waliobaki.
 
vazi halibuniwi, vazi linatokana na watu wenyewe wanavyovaa tofauti na mataifa mengine.

Inachekesha kuona serikali iko mstari wa mbele sana kuhimiza tume za vazi la taifa wakati haina mpango wowote wa kuokoa viwanda vya nguo.

Hata ukisema uondoe philosophical differences, useme unakubali vazi la taifa linaweza kubuniwa na viongozi, utoe hili ndio vazi la taifa, vazi litashoneshwa wapi wakati nchi haina viwanda vya nguo?

Au ndo tunataka tuwape tender wa Pakistan watushoneshee vazi la taifa?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Hongera kaka Kibanda. Vazi la taifa uchuro gani huo? Nchi haina mwelekeo wo wote katika masuala ya msingi; mambo ya mavazi mwachieni Lundenga na biashara yake feki ya kuwatembeza dada zetu uchi!! Simple minds kama za viongozi wa Magamba haziwezi kwenda mbali zaidi ya mavazi.
 
Inachekesha kuona serikali iko mstari wa mbele sana kuhimiza tume za vazi la taifa wakati haina mpango wowote wa kuokoa viwanda vya nguo.

Hata ukisema uondoe philosophical differences, useme unakubali vazi la taifa linaweza kubuniwa na viongozi, utoe hili ndio vazi la taifa, vazi litashoneshwa wapi wakati nchi haina viwanda vya nguo?

Au ndo tunataka tuwape tender wa Pakistan watushoneshee vazi la taifa?
Mkuu tatizo letu hatuna vipao mbele katika maamuzi na mipango yetu ya kila siku kama nchi. Tumejaa ubinafsi mno. Hapa watu wametengeza ulaji na kama ulivyosema tutaingia mkataba na Pakistan watushonee vazi la Kitaifa. Siku unapata Kitambulisho chako cha uraia unatakiwa ununue na vazi la Kitaifa. Ni ujanja ujanja tu.
 
Vazi la taifa kamati husika ilikuwa ni kujitolea kwa mujibu wa barua walizoandikiwa sasa unaposema kuna ulaji sijajua watu wanamaanisha nini hapa.....kazi kubwa.kuhusu vipaumbele mbalimbali ni kuwa kila wizara ina kipaumbele chake....utamaduni wana vazi,habari wanaandaa sheria mpya bora zaidi.....michezo wanaandaa mpango mkakati wa michezo utakaoainisha wajibu wa kila mwanamichezo na mwananchi chini ya baraza la michezo na vijana sijajua bado.sasa wewe ukisema waongelee umeme au maji hayo yana wizara zake....
 
Hivi kibanda amejua serikali inanyanyasa waandishi baada ya yeye kunyanyaswa?

Mwanakijiji sitaki kuamini kwamba umesahau haraka hivi. Nimetambua unyanyasaji wa waandishi wa habari miaka mingi na ushahidi upo. Kwanza niliongoza maandamano ya kulaani kumwagiwa tindikali kwa Saed Kubenea nikiwa Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania tena baada ya baadhi ya wahariri 'kuingia mitini'. Mimi ndiye niliyetoa tamko la kulaani kitendo hicho. Nilishiriki kikamilifu kuanzisha Jukwaa la Wahariri mwaka 2008 kama moja ya njia ya kutetea uhuru wa uhariri na wa kutoa maoni. Nimeshiriki katika mikutano na shughuli mbalimbali za kudai Sheria Mpya ya Habari nchini sambamba na kufutwa kwa sheria kandamizi kupitia makala zangu na kupitia mikutano ya wadau wa habari. Mwaka jana wakati waandishi waliponyanyaswa katika safari za kampeni za wagombea wa vyama vya siasa, niliitisha mkutano wa dharura wa wahariri na kulaani vitendo hivyo na tamko langu likaripotiwa katika vyombo mbalimbali nchini...

Mwisho sababu za kujitoa katika kamati ziko bayana. Zinanigusa mimi mwenyewe na ni zaidi ya kupinga unyanyasaji wa waandishi wa habari.
 
Mwanakijiji sitaki kuamini kwamba umesahau haraka hivi. Nimetambua unyanyasaji wa waandishi wa habari miaka mingi na ushahidi upo. Kwanza niliongoza maandamano ya kulaani kumwagiwa tindikali kwa Saed Kubenea nikiwa Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania tena baada ya baadhi ya wahariri 'kuingia mitini'. Mimi ndiye niliyetoa tamko la kulaani kitendo hicho. Nilishiriki kikamilifu kuanzisha Jukwaa la Wahariri mwaka 2008 kama moja ya njia ya kutetea uhuru wa uhariri na wa kutoa maoni. Nimeshiriki katika mikutano na shughuli mbalimbali za kudai Sheria Mpya ya Habari nchini sambamba na kufutwa kwa sheria kandamizi kupitia makala zangu na kupitia mikutano ya wadau wa habari. Mwaka jana wakati waandishi waliponyanyaswa katika safari za kampeni za wagombea wa vyama vya siasa, niliitisha mkutano wa dharura wa wahariri na kulaani vitendo hivyo na tamko langu likaripotiwa katika vyombo mbalimbali nchini...

Mwisho sababu za kujitoa katika kamati ziko bayana. Zinanigusa mimi mwenyewe na ni zaidi ya kupinga unyanyasaji wa waandishi wa habari.
Asante Kibanda kwa kauli yako, watu wamehoji kwa nini leo wamesahau hii vita si yakushinda siku moja zinatakiwa mbinu mbalimbali kama hizi, tukawaambia kila mtu na mipango yake na kila jambo na wakati wake, safi Kibanda, wakasema umejitoa kwa sababu ya kukamatwa na polisi ofcourse nayo ni sababu tosha kwa sababu mvaa kiatu ndiye anajua kinapomchoma zaidi. Ingawa umesema sababu kubwa zinakugusa wewe lakini hata kujitoa kwako kumesaidia kuwaonyesha watawala kuwa hilo vazi halina umuhimu mkubwa sana kama wanavyofikiria.

Nchimbi angeanzisha kamati ya kufuatilia mambo yanayogusa watu wengi kama sheria mbovu za habari, Timu yetu ya Taifa na ukosefu wa ajira kwa vijana angeonekana na busara kuliko kuhangaika na vitu ambavyo hata Hashimu Lundenga angefanya na kamati yake ya warembo.
 
Nampongeza kwa dhati ndugu Kibanda kwa uamuzi wake wa kuachana na hili zoezi la kipuuzi. Tanzania tuna matatizo lukuki lakini Nchimbi anaona jambo la muhimu ni mavazi?

We ungemshauri lipi kati ya mambo yake ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo...?
 
Vazi la taifa kamati husika ilikuwa ni kujitolea kwa mujibu wa barua walizoandikiwa sasa unaposema kuna ulaji sijajua watu wanamaanisha nini hapa.....kazi kubwa.kuhusu vipaumbele mbalimbali ni kuwa kila wizara ina kipaumbele chake....utamaduni wana vazi,habari wanaandaa sheria mpya bora zaidi.....michezo wanaandaa mpango mkakati wa michezo utakaoainisha wajibu wa kila mwanamichezo na mwananchi chini ya baraza la michezo na vijana sijajua bado.sasa wewe ukisema waongelee umeme au maji hayo yana wizara zake....

bado Vijana..... Umesahau..
 
Alipochaguliwa alikubali na kufurahi sana na kesho yake kulikuwa na column kubwa kwenye gazeti analoliongoza lenye heading ya " Kibanda aula kamati ya Vazi la Taifa" na mbaya zaidi aliye mteua ni waziri wa habari...hizi habari za leo kujitoa kwa ajili ya unyanyasaji ni ubinafsi wa hali ya juu, na ikumbukwe kuwa huyu jamaa ni mwenyekiti wa wahariri bongo.

Ni kweli kabisa mkuu! Huyu jamaa amekerwa na kitendo cha yeye kukamatwa na wala si uchungu unaotokana na unyanyasaji wa waandishi wa habari!
 
Nilisikitika sana niliposikia kibanda umeteuliwa kwenye kamati yamavazi, walikushusha hadhi sana na ndo ulikuwa mpango kabambe wa kufunga ndoa na serikali hii. Waache kina kusaga na sasa wakamchague hashimu lundenga ajaze nafasi yako. Mtanzania gani anataka kuwa na vazi lataifa by tha way!. Dahh! Tanzania kwa kubuni njia za matumizi tupo juu, shida ipo kwenye kubuni kubana matumizi,hapo kama unajipenda usiguse kabisa utapotezwa kama.......
 
Mara nyingi wanaompiga mawe kibaka ni vibaka wenzake, ila wanafanya hivyo kwa kuwa option ya kumuokoa kwa wakati huo hakuna, na wakijaribu kufanya hivyo na wao wanaweza kushushiwa kipigo. Karibuni tutakuja kujua wanaompiga kibaka mwenzao ccm ilhali na wao ni vibaka...
 
Back
Top Bottom