Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

Maswala yanayohusu serikali ya Mapinduzi Zanzibar Serikali ya muungano inayaingilia kati yapo mengi tu mojawapo ni hii hapa : Membe akalia 200bn za Zanzibar Bonyerza hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/303380-membe-akalia-200bn-za-zanzibar.html Mkuu Mkandara
Dah ama kweli wewe mgumu sana kuelewa mapana ya Muungano..Yaani wewe na mkeo akipewa fedha toka nje azilete tu ndani ya nyumba na halali yake?. Ebu kwa kiola unapofikiria jambo iweke ndoa yako na mkeo halafu ndio ujue yapi na mke na yapi na ya ndoa ruksa.. Na labda nikuulize MEMBE Ni nani? anaiwakilisha serikali ya bara au ya Muungano? iweje swala hili liwe na Zanzibar ikiwa wawekezaji wote nchini wanapitia njia hiyo hiyo. Nini azma yao na deni hili litawahusu kina nani ikiwa Zanzibar inajulikana sio Nchi nje ya Muungano wetu. Mwinyi alipowauzia Saidia Loliondo ilikuwa kaingilia maswala ya bara?..Hivi rais akitokea Zanzibar hawezi kuweka ama kukataa misaada na mikataba inayohusu Bara!..

labda nikwambie hivi hata Marekani kwenyewe walioanza kabla yetu Sii Senator, Governor wala Member wa Congress anaweza kwenda nje na kuweka mikataba ya aina yoyote wala kupokea misaada toka nje pasipo kupitishwa na serikali kuu. Mkuu mahusiano yoyote ya kimataifa ni lazima yapitie Ofisi wa Membe maana ndiye mwakilishi wetu sote. Mama Clinton majuzi alikuwa Malawi anawakilisha Marekani na hadi zozote anazozitoa zitawahusu Wamarekani wote..

Hivi kuna tatizo gani kwa Zanzibar kupitia serikali ya Jamhuri ya muungano kuwawakilisha ktk mikataba yake nje ua mpaka awepo Mzanzibar ndio mnaiona haki..Rais kachaguliwa na sisi wote iweje nyie mjiweke kimbelembele kwenda kuweka mikataba ambayo inahusu zaidi mahusiano yetu KITAIFA. nani huko anaijua Bendera ya Zanzibar au Tanganyika!

Hawa walioleta hiyo misaada walielewa vizuri sheria na walijua ktk kutaka kugombanisha serikali hizi mbili ni kuonyesha lengo la kutoa fedha kwa serikali ya Zanzibar wakati wanajua fika haiwezekani huu sio Utawala wa Kisultan ambao Sultan wa UAE anaweza kuweka mikataba pasipo Sultan wa Dubai au Sharja kuhusika. Hii ni serikali ya JAMHURI babuu mbona hamuelewi.

Wewe hapo ulipo unaweza kabisa kupinga mkopo wowote unaotolewa ama kupokelewa kutoka nchi ambazo zinalenga kuharibu mahusiano ya muungano wetu...Hao Oman watoe misaada kwetu wakati maisha yao wenyewe yanawashinda, Oman wana struggle kiuchumi hizi sadaka zimetokea wapi. Wazanzibar waliohamia huko tu wanabaguliwa na hata kupewa Soweto yao leo wawe na huruma sana kwa Zanzibar....
 
Dah ama kweli wewe mgumu sana kuelewa mapana ya Muungano..Yaani wewe na mkeo akipewa fedha toka nje azilete tu ndani ya nyumba na halali yake?..Na labda nikuulize MEMBE Ni nani? anaiwakilisha seriikali ya bara au ya Muungano? iweje swala hili liwe na Zanzibar ikiwa wawekezaji wote wanapitia njia hiyo hiyo. Mwinyi alipowauzia Saidia Loliondo ilikuwa kaingilia maswala ya bara?..Hivi rais akitokea Zanzibar hawezi kuweka kuweka mikataba inayohusu Bara!..

labda nikwambie hivi hata Marekani kwenyewe walioanza kabla yetu hawezi Senator, Governor wala Member wa Congress anaweza kwenda nje na kuweka mikataba ya aina yoyote wala kupokea misaada toka nje pasipo kupitishwa na serikali kuu. Mahusiano yoyote ya kimataifa ni lazima yapitie Ofisi wa Membe maana ndiye mwakilishi wetu sote.

Hivi kuna tatizo gani kwa Zanzibar kupitia serikali ya Jamhuri ya muungano kuwakilisha ktk mikataba yake nje..rais kachaguliwa na sisi wote iweje nyie mjiweke kimbelembele kwenda kuweka mikataba ambayo inahusu zaidi mahusiano yetu KITAIFA.

Hawa walioleta hiyo misaada walielewa vizuri sheria na walijua ktk kutaka kugombanisha serikali hizi mbili ni kuonyesha lengo la kutoa fedha kwa serikali ya Zanzibar wakati wanajua fika haiwezekani huu sio Utawala wa Kisultan mabo Sultan wa UAE anaweza kuweka mikataba pasipo Sultan wa Dubai au Sharja kuipitisha. Hii ni serikali ya JAMHURI babuu mbona hamuelewi.

Wewe hapo ulipo unaweza kabisa kupinga mkopo wowote unaotolewa ama kupokelewa kutoka nchi ambazo zinalenga kuharibu mahusiano ya muungano wetu...Hao Oman watoe mkopo kwetu wanakati maisha yao wenyewe yanawashinda, Wazanzibar waliohamia huko tu wanabaguliwa na hata kupewa Soweto yao leo wawe na huruma sana kwa Zanzibar....
Nakuacha kwa leo najiandaa kula Futari Nalog Off inaonyesha ukishindwa malumbano ya Siasa unaleta maneno ya matusi wewe Mkandara Masuala ya mke na mume yamehusiana na nini na mambo ya kisiasa?Tangu mwanzo nilikwambia usilete maneno ya Pumba lakini hujasikia nakuacha kwa leo usiniharibie saumu yangu baadae kwa sasa nalog off mkuu Mkandara
 
Last edited by a moderator:
Mie naona Wazanzibar wanatubore sana kila kukicha ni malalamiko kibao.Nionavyo mimi kitu cha msingi ni kkukubali au kukataa kuwepo na Muungano. Kama wanaona muungano hawautaki ni bora tukaachana nao. Wengi hawajui athari za kuuvunja bado wanadhani itakuwa bizness as usual ? Kutengena kwa kulazimishana ni kubaya zaidi kwa mtizamo wangu.
Litatoka wimbi la timua timua hiyo mkae nyinyi wazanzibar mkijua hilo. Wenye mnakumbuka baada ya kuvunjika kwa afrika mashariki sijui wengine hamkuona kilichotokea ? wanadamu ni wanyama ndugu zangu kama ni mpemba utachukuliwa juu juu bila kurudi nymbani , mimi tafrani hiyo naiona inanyelea nchi hii. Watu wamekata tamaa kwa sasa , matatizo ni mengi sasa mkitaka kuanza varangati la watu kurudi kwao itakuwaje ? Maana tunaishi kwa kujuana waunguja na wapemba wametapakaa nchi nzima na wanajulikana ikitokea mshike mshike kuna madhara mengi . TUTAFAKARI
 
Hata tuyazime, maswali yale yale kuhusu Muungano yanaturejea



HUKO nyuma nimeeleza kwamba haiwezekani kuijadili Tanzania pasipo kuujadili Muungano, na kwamba dalili za makundi ya watu kuhoji Muungano wetu kama ulivyo leo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara bila kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Fursa tuliyo nayo hivi sasa ya kujadili na kuandika katiba mpya ni fursa adhimu tunayoipata kuujadili Muungano kwa kina na kuupatia ufumbuzi utakaotupeleka masafa marefu kidogo.

Ye yote anayetaka kujua jinsi masuala ya Muungano yalivyotusumbua katika historia yetu ya takriban nusu karne atakumbuka mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na tume na kamati mbalimbali zilizoundwa katika jitihada za kujaribu kurekebisha baadhi ya masuala yaliyoonekana kukera makundi ndani ya nchi, na jinsi ambavyo jitihada hizo zote na kamati na tume hizo hazikufanikiwa kuondoa malalamiko kuhusu Muungano.

Sasa itakuwa ni jambo la ajabu iwapo, wakati tunasema tunataka kuandika katiba mpya, tutajinyima wasaa wa kuujadili Muungano kwa kuwauliza wananchi wa pande mbili (Tanganyika na Zanzibar) ni nini wanachotaka, iwapo wanataka Muungano au hawautaki.
Swali hilo la msingi likiiisha kupatikana, na jibu likawa kwamba wanautaka Muungano, ndipo sasa itawezekana kuangalia kwa undani ni mambo gani ndani ya mfumo na taratibu za Muungano yafanyiwe marekebisho ili kuyaweka sawa na kukidhi matarajio ya pande mbili zilizoungana.

Binafsi nakataa dhana ya kuwaambia watu kwamba kuujadili Muungano ni sharti tujadili namna ya kuuboresha. Mtu huboresha jambo analotaka kuendelea nalo, na kama hataki kundelea nalo ni upuuzi kuanza kuliboresha. Haina maana hata kidogo. Na si kweli kwamba hatujasikia sauti za watu wanosema kwamba hawautaki Muungano, na wala pia si kweli kwamba hawana haki ya kuwa na mawazo kama hayo.

Njia pekee kwa wale wanaopenda Muungano uendelee kuwapo (pamoja na marekebisho yatakayokubaliwa) ni kuwaacha wana-Muungano wenyewe waseme kwamba wanataka kuuendeleza kwa kuuboresha. Iwapo watasema kwamba hawautaki, na tujue kwamba hiyo ndiyo kauli yao, huo ndio utashi wao. Kujidai kwamba tutauendeleza Muungano bila ridhaa ya Watanganyika na Wazanzibari ni ndoto za Alinacha.

Katika historia yetu tumekuwa na matukio kadhaa yaliyoutikisha Muungano lakini ikawezekana kuyazima kwa njia moja au nyingine. Tutakumbuka sakata la “kuchafuka kwa hali ya hewa” Visiwani mwaka 1983-84, iliyosababisha kuondolewa madarakani aliyekuwa rais wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi.
Kimsingi alichokuwa akisema Jumbe ni kwamba Muungano ulihitaji marekebisho katika muundo wake ili uweze kukidhi mahitaji ya Wazanzibari.

Tukumbuke pia kwamba wakati Jumbe akichukua hatua za kufanya mapendekezo ya kuuboresha Muungano kadri alivyoona inafaa, alikuwa ni kipenzi cha Mwalimu Nyerere, ambaye alijiona raha kufanya kazi na ‘msomi’ mwenzake baada ya kusumbuana sana na Abeid Karume, muasisi mwenzake wa Muungano, Karume akiwa ni mtu asiyetabirika, na mwenye maamuzi yaliyotatanisha.

Inawezekana kwamba usiri wa hatua alizokuwa akitaka kuzichukua Jumbe ndio uliomuudhi Nyerere hata akaamua kumwadhibu Jumbe. Hata hivyo, haijulikani msimmao wa Mwalimu ungekuwa upi iwapo Jumbe angepeleka mapendekezo yake mbele ya kikao rasmi cha CCM au serikali na kuomba ridhaa juu ya mawazo yake ya kuboresha Muungano.

Tofauti na hii leo, ambapo majadiliano ndani ya NEC ya chama-tawala yanajulikana Kariakoo na Manzese kabla kikao hakijafungwa, wakati ule wa sakata la Jumbe kikao cha siri maana yake ilikuwa ni kikao cha siri. Kikao hicho hakina hata ‘hansard’. Ndiyo maana itakuwa vigumu kujadili kwa undani maudhui ya mjadala uliofanyika ndani ya kikao kilichohitimishwa kwa kumvua Jumbe nyadhifa zake zote na kumpeleka ‘uhamishoni’ Mji Mwema.

Muongo mmoja baadaye kundi la wabunge wa CCM lililojulikana kama G-55 (jina lilinuniwa na Issa Shivji) likaibuka na kudai marekebisho katika muundo wa Muungano kwa kuasisi serikali ya Tangayika na kuwa na muundo wa Shirikisho.
Hoja iliyopelekwa bungeni na kundi hili iliungwa mkono kwa nguvu kubwa na watu wengi na hatimaye serikai ikaridhia hoja hiyo na kukubali marekebisho hayo yafanyike.

Kwa mara nyingine tena ilikuwa ni Mwalimu Nyerere aliyesimama na kuipinga hoja hiyo, ikiwa tayari imekwisha kupitishwa na Bunge, na hatimaye juhudi zake zikafanikiwa kuitengua hoja hiyo.
Ikumbukwe kwamba Mwalimu wakati huo hakuwa rais wala mwenyekiti wa chama chake, lakini kwa ushawishi aliokuwa nao aliweza kufanya alivyofanya.

Nakumbuka, nikiwa mmoja wa kundi la G-55, tulikuwa na mabishano mengi na Mwalimu nyumbani kwake Msasani katika kipindi hicho, na nakumbuka kwamba Mwalimu alishikilia msimamo wake bila kutetereka, ingawaje baadhi yetu hatukuona mantiki ya kile alichokuwa akikitetea.

Kimsingi, msimamo wake ulikuwa kwamba muundo wa serikali tatu ungevunja Muungano. Sisi tulikuwa na mawazo tofauti, kimsingi, kwa sababu tulikuwa hatuoni matiki ya kuwa na serikali mbili, moja ikiwa ni ya Zanzibar na ya pili ikiwa ni ya Zanzibar na Tanganyika.
Hiyo ni historia. Lakini sasa zimejitokeza sauti zinazotoa mwangwi wa haya ninayoyasimulia, kwa mara nyingine zikidai muundo wa serikali tatu. Hizi ziko pande mbili za Muungano, nazo zinadhihirisha ukweli kwamba jambo hili halijaondoka; lipo na linahitaji mjadala wa kina ndipo lipatiwe ufumbuzi. Kulizimazima hakutasaidia sana.

Nimekuwa nikikagua kumbukumbu ili kujua kama Mwalimu Nyerere aliwahi kupiga marufuku mjadala kuhusu Muungano. Sikumbuki. Alimtoa Jumbe madarakani. Aliizima hoja ya G-55. Lakini sikumbuki hata mara moja akisema kwamba ni marufuku kuujadili Muunagno. Aliwaachia waliomzunguka waelewe kwamba kwake Muungano ulikuwa kitu azizi kwake na hapendi kichezewe, lakini hakusema kinagaubaga kwamba ni marufuku kuujadili.

Ninaweza kwenda mbali zaidi na kusema kwamba, hata kama Mwalimu angekuwa amesema waziwazi kwamba ni marufuku kuujadili Muungano, bado tungeweza, katika mazingira ya leo, tukasema kwamba pamoja na heshima yetu kubwa kwake, lakini Muungano unajadilika. Mambo yamebadilika, na dunia inasonga mbele, na alichokiamini baba yako sicho unachotakiwa lazima ukiamini leo.

Kama hivyo ndivyo, hakuna sababu yo yote ya kuweka makatazo katika majadala kuhusu Muungano. Acheni ujadiliwe kwa uwazi mkubwa kiasi kinachowezekana, mawazo yanayokinzana yashindanishwe na mumo tupate elimu ya kuuboresha Muungano.
Mimi binafsi ni muumini mkubwa wa mamlaka ya watu ndani ya sehemu wanamoishi, kwa sababu mamlaka hayo ndicho kielelezo thabiti cha dhana ya kujitawala.

Hatua yo yote inayopunguza uwezo wa wananchi wa sehemu fulani kujiendeshea shughuli zao kwa uhuru mpana kiasi kinachowezekana ndani ya umoja wa jumla, ni kitendo kinachokinzana na maendeleo.
Wako Wazanzibari wanaosema uhuru wao wa kuendesha mambo yao umebinywa mno; wako Watanganyika wanaodhani kwamba katika

Muunago huu Wazanzibari wanapewa nafasi ambazo si zao, na kwa hiyo wanawanyima nafasi Watanganyika. Hususan, dhana ya u-Zanzibari imekuzwa mno hadi inaamsha jawabu la u-Tanganyika.
Shetani naye amejiingiza. Waziri wa zamani wa mafuta nchini Venezuela aliwahi kusema kwamba mafuta ya peteroli ni kinyesi cha Shetani nasi sote tunaogelea ndani yake.

Inaelekea Shetani ametutembelea hivi karibuni, na tunasikia kelele za “Yangu! Yangu!” Baadhi ya Wazanzibari wameanza kuogelea mumo kabla hata Shetani hajaenda msalani.

Bila shaka viyu kama hivyo (mafuta, gesi asilia, ardhi, misitu, rasilimali-bahari na kadhalika) vitakuja kutusumbua huko tuendako. Na tutakumbana na ile dhana ya mzandiki anayesema, “Chako chetu, changu changu.” Njia pekee ya kuondokana na uzandiki huo ni kuwa na mjadala mpana, wa wazi, na wa kituo.
Chanzo: Raia Mwema
 
Nakuacha kwa leo najiandaa kula Futari Nalog Off inaonyesha ukishindwa malumbano ya Siasa unaleta maneno ya matusi wewe Mkandara Masuala ya mke na mume yamehusiana na nini na mambo ya kisiasa?Tangu mwanzo nilikwambia usilete maneno ya Pumba lakini hujasikia nakuacha kwa leo usiniharibie saumu yangu baadae kwa sasa nalog off mkuu Mkandara
Alaaa hata mfano basi au naposema mke wewe unachukulia nawatukana kwa sababu uwezo wa mwanamke ni hafifu kwenu hivyo ni matusi?.. Wahi futur isifanye kufur, mimi bado hadi saa tatu usiku. Ukirudi utayakuta yamejaa tele kama pichi..

Haya niseme mke wangu miye sio wako, hawezi kuleta fedha alizoahidiwa na mwanamme ndani ya nyumba pasipo kushauriana nami. Na usichukulie naposema Mke ukaona nawadhalilisha nyie maana kwangu mke mume sote ni wamoja, uwezo sawa na nafasi sawa ndani ya ndoa tena mwanamke ana mamlaka zaidi. Ningekuwa mwanamke ningesema Mume wangu hawezi kuleta hela alizoahidiwa nje na mwanamke kuziingiza nyumbani. Halafu Hivi ni nani naibu waziri wa Membe vile?..
 
Mie naona Wazanzibar wanatubore sana kila kukicha ni malalamiko kibao.Nionavyo mimi kitu cha msingi ni kkukubali au kukataa kuwepo na Muungano. Kama wanaona muungano hawautaki ni bora tukaachana nao. Wengi hawajui athari za kuuvunja bado wanadhani itakuwa bizness as usual ? Kutengena kwa kulazimishana ni kubaya zaidi kwa mtizamo wangu.
Litatoka wimbi la timua timua hiyo mkae nyinyi wazanzibar mkijua hilo. Wenye mnakumbuka baada ya kuvunjika kwa afrika mashariki sijui wengine hamkuona kilichotokea ? wanadamu ni wanyama ndugu zangu kama ni mpemba utachukuliwa juu juu bila kurudi nymbani , mimi tafrani hiyo naiona inanyelea nchi hii. Watu wamekata tamaa kwa sasa , matatizo ni mengi sasa mkitaka kuanza varangati la watu kurudi kwao itakuwaje ? Maana tunaishi kwa kujuana waunguja na wapemba wametapakaa nchi nzima na wanajulikana ikitokea mshike mshike kuna madhara mengi . TUTAFAKARI



Wacha kuwatisha Wazanzibari, wao wameshapaangalia hapo ndio maana wadai nchi yao haijalishi, kwani huko Syria, Libya, Misri, Yemen, Tunisia ndio hivohivo baada ya mda si wametulia, basi na Zenji wala hawatafikia kama hivo tunavofikiria.

Mimi nawajua Wazanzibari wakiona tu kuna harufu ya kufukuzwa Tanganyika wataondoka kabla ya kufukuzwa na wala hamtawaona hata watakapopita na mtawatafuta kwa udi na uvumba.

Na wala kwa hilo tusitishane tugawane mbao tuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Alaaa hata mfano basi au naposema mke wewe unachukulia nawatukana kwa sababu uwezo wa mwanamke ni hafifu kwenu hivyo ni matusi?.. Wahi futur isifanye kufur, mimi bado hadi saa tatu usiku. Ukirudi utayakuta yamejaa tele kama pichi..

Haya niseme mke wangu miye sio wako, hawezi kuleta fedha alizoahidiwa na mwanamme ndani ya nyumba pasipo kushauriana nami. Na usichukulie naposema Mke ukaona nawadhalilisha nyie maana kwangu mke mume sote ni wamoja, uwezo sawa na nafasi sawa ndani ya ndoa tena mwanamke ana mamlaka zaidi. Ningekuwa mwanamke ningesema Mume wangu hawezi kuleta hela alizoahidiwa nje na mwanamke kuziingiza nyumbani. Halafu Hivi ni nani naibu waziri wa Membe vile?..
Mkuu Mkandara tuchukulie huo mfano wako mbovu uliotoa wa kuhusu Mke na Mume ninavyojuwa mimi kati ya Mke na Mume wakiishi sana kwenye Ndoa yao inafika wakati Mmoja kati ya hao wawili anamchoka mwenzie kitabia ? au wote wawili wanachokana kitabia ?Na ikifika

hatua ya Mmoja kumchoka mwenzie inakuwa Ndoa yao kati ya hao wawili Mume na Mke haidumu wanatengana na hivyo hivyo Muungano wa Miaka 48 wa Tanganyika na Zanzibar umefika kikomo ndugu zetu wa Zanzibar Wamesha choka na Kero ya

huo Muungano wanachohitaji watengane kwa salama an Amani Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena imekuwa ni basi tena inatosha miaka 48. Na kama ilivyo kwenye ndoa ya Miaka 48 kwa mfano wewe na mke wako mupo pamoja katika Ndoa yenu ya muda wa miaka 48 itakuwa wewe ndie wa kwanza Kumchoka Mke wako au Mke wako atakuchoka wewe kitabia na itakuwa ndio mwisho wa hiyo ndoa yenu ni kuachana sasa wewe unasemaje huo mfano wangu mkuu Mkandara?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara tuchukulie huo mfano wako mbovu uliotoa wa kuhusu Mke na Mume ninavyojuwa mimi kati ya Mke na Mume wakiishi sana kwenye Ndoa yao inafika wakati Mmoja kati ya hao wawili anamchoka mwenzie kitabia ? au wote wawili wanachokana kitabia ?Na ikifika

hatua ya Mmoja kumchoka mwenzie inakuwa Ndoa yao kati ya hao wawili Mume na Mke haidumu wanatengana na hivyo hivyo Muungano wa Miaka 48 wa Tanganyika na Zanzibar umefika kikomo ndugu zetu wa Zanzibar Wamesha choka na Kero ya

huo Muungano wanachohitaji watengane kwa salama an Amani Wa Zanzibar hawautaki Muungano tena imekuwa ni basi tena inatosha miaka 48. Na kama ilivyo kwenye ndoa ya Miaka 48 kwa mfano wewe na mke wako mupo pamoja katika Ndoa yenu ya muda wa miaka 48 itakuwa wewe ndie wa kwanza Kumchoka Mke wako au Mke wako atakuchoka wewe kitabia na itakuwa ndio mwisho wa hiyo ndoa yenu ni kuachana sasa wewe unasemaje huo mfano wangu mkuu Mkandara?
Sasa haya maneno..nashiukuru umerudi kuwa mdogo kidogo tulingane. basi kama ungesema toka zamani tumechokana au Wazanzibar wameichoka ndoa wala tusingefika huku. Sii kuweka visingizio wakati tumeishi pamoja ktk ndoa kwa miaka 48 sasa ati abuse zote ndio zinasemwa leo na iwe sababu ya kutalakiana.. I mean kwa mwenye kuelewa mtu anayekuwa Abused hahitaji miaka 40 ndani ya ndoa, unless wewe mwenyewe una matatizo binafsi.

Sasa hata ktk hili la kuchoshwa, maajabu wa Wazanzibar hawataki talaka bali talaka rejea... wanachotaka tutalakiane lakini relationship yetu iendelee kwa sababu gani sijui.. nasi Bara tunasema kama waitaka talaka tusijuane maana ndio maana ya talaka. Wazanzibar wanasema hapana tume na makubaliano mpya lakini tusiwe wanandoa kila mtu awe na uhuru wa kufanya takavyo mbona kuna watu wanaishi kama wapenzi na wanatambuliwa kishieria(common in law). Mapenzi haya ndio bara hatuyataki...tunachowaambiamake up your mind, kila mlichokitaka ktk miaka 48 tumeenda kwa kadhi na kuyarekebisha, mkadai mengi na mengine..

Hii picha ndio haijengi mantiki kwetu sisi, maadam tulishafunga ndoa tukiachana tuachane hakua mtu kumtegemea mwingine wala habari za kujuana tena. lakini kinachowapa shida Zanzibar ni kwamba watoto wake wengi wanaishi na mama custudy tunayo sisi bara. na kama itafanyika referendum wazanzibar wanahofia watoto hawa Wazanzibara kupinga kuvunjika kwa ndoa..Well, sasa amueni basi mnataka kubakia ktk ndoa au.. Oooh Bara tuwapeni talaka, alaah! kwani kadhi nani, mlete kadhji tumalize maneno. Hivi kweli mnanataka kuondoka au miyeyusho tuongeze dau la kuwapa matumizi kila siku?.

Majuzi tu mliposikia YAWEZEKANA kuna mafuta Pemba mtumee! mnataka tuwekeane mipaka ijulikane wapi mwisho wa Zanzibar utadhani mmeshinda lotto tayari.. hamna tofauti na huyu Mama Banda alosikia kuna uwezekano wa mafuta North ya lake Malawi basi anaweka madai ziwa lote ni la Malawi na kuonyesha hati za Mkoloni zinazoonyesha nchi inayoitwa NYASALAND..Haya Mafuta tu yamewatoa roho watu na Inslaallah naomba sana Mwenyezi Mungu hayo mafuta yasipatikane Pemba wala lake Malawi tuyapate Tanga na na dryland Mbeya halafu tutawaona mtabadilisha vipi tamaa hizi..
 
Sasa haya maneno..nashiukuru umerudi kuwa mdogo kidogo tulingane. basi kama ungesema toka zamani tumechokana au Wazanzibar wameichoka ndoa wala tusingefika huku. Sii kuweka visingizio wakati tumeishi pamoja ktk ndoa kwa miaka 48 sasa ati abuse zote ndio zinasemwa leo na iwe sababu ya kutalakiana.. I mean kwa mwenye kuelewa mtu anayekuwa Abused hahitaji miaka 40 ndani ya ndoa, unless wewe mwenyewe una matatizo binafsi.

Sasa hata ktk hili la kuchoshwa, maajabu wa Wazanzibar hawataki talaka bali talaka rejea... wanachotaka tutalakiane lakini relationship yetu iendelee kwa sababu gani sijui.. nasi Bara tunasema kama waitaka talaka tusijuane maana ndio maana ya talaka. Wazanzibar wanasema hapana tume na makubaliano mpya lakini tusiwe wanandoa kila mtu awe na uhuru wa kufanya takavyo mbona kuna watu wanaishi kama wapenzi na wanatambuliwa kishieria(common in law). Mapenzi haya ndio bara hatuyataki...tunachowaambiamake up your mind, kila mlichokitaka ktk miaka 48 tumeenda kwa kadhi na kuyarekebisha, mkadai mengi na mengine..

Hii picha ndio haijengi mantiki kwetu sisi, maadam tulishafunga ndoa tukiachana tuachane hakua mtu kumtegemea mwingine wala habari za kujuana tena. lakini kinachowapa shida Zanzibar ni kwamba watoto wake wengi wanaishi na mama custudy tunayo sisi bara. na kama itafanyika referendum wazanzibar wanahofia watoto hawa Wazanzibara kupinga kuvunjika kwa ndoa..Well, sasa amueni basi mnataka kubakia ktk ndoa au.. Oooh Bara tuwapeni talaka, alaah! kwani kadhi nani, mlete kadhji tumalize maneno. Hivi kweli mnanataka kuondoka au miyeyusho tuongeze dau la kuwapa matumizi kila siku?.

Majuzi tu mliposikia YAWEZEKANA kuna mafuta Pemba mtumee! mnataka tuwekeane mipaka ijulikane wapi mwisho wa Zanzibar utadhani mmeshinda lotto tayari.. hamna tofauti na huyu Mama Banda alosikia kuna uwezekano wa mafuta North ya lake Malawi basi anaweka madai ziwa lote ni la Malawi na kuonyesha hati za Mkoloni zinazoonyesha nchi inayoitwa NYASALAND..Haya Mafuta tu yamewatoa roho watu na Inslaallah naomba sana Mwenyezi Mungu hayo mafuta yasipatikane Pemba wala lake Malawi tuyapate Tanga na na dryland Mbeya halafu tutawaona mtabadilisha vipi tamaa hizi..
Kwani wewe ukiachana na Mke wako ambaye Mumezaa watoto basi kutakuwa na uaduwi wowote? Marehemu baba yangu aliishi

na Marehemu Mama yangu zaidi ya miaka 32 na waliachana mwaka 1980 mbona walikuwa wanaonana uso kwa uso na baba aliowa Mwanamke Mwengine wa kingoni. kuchana au kutengana sio ndio sababu ya kuweka uaduwi kati yetu sisi Wa

Tanganyika na ndugu zetu wa Ki Zanzibar ? Tumeowana tumezaana tuko kitu kimoja ila Wenzetu WaZanzibar wamechoka na huo Umoja wetu Muungano wenu sasa kama mwenzako amechoka wewe bado unangojea nini tena kitokee Vita? Mauaji?

uaduwi? Wananchi wa Visiwa vya Unguja na Pemba Havizidi zaidi ya Watu Millioni 2 sasa kwanini tuumize vichwa kwa Watu ambao hawazidi zaidi ya Millioni 2? Mkuu Mkandara Wa Zanzibar hawataki Muungano wetu Tuwaache kama walivyo unaonaje mkuu?
 
Last edited by a moderator:
Kwani wewe ukiachana na Mke wako ambaye Mumezaa watoto basi kutakuwa na uaduwi wowote? Marehemu baba yangu aliishi

na Marehemu Mama yangu zaidi ya miaka 32 na waliachana mwaka 1980 mbona walikuwa wanaonana uso kwa uso na baba aliowa Mwanamke Mwengine wa kingoni. kuchana au kutengana sio ndio sababu ya kuweka uaduwi kati yetu sisi Wa

Tanganyika na ndugu zetu wa Ki Zanzibar ? Tumeowana tumezaana tuko kitu kimoja ila Wenzetu WaZanzibar wamechoka na huo Umoja wetu Muungano wenu sasa kama mwenzako amechoka wewe bado unangojea nini tena kitokee Vita? Mauaji?

uaduwi? Wananchi wa Visiwa vya Unguja na Pemba Havizidi zaidi ya Watu Millioni 2 sasa kwanini tuumize vichwa kwa Watu ambao hawazidi zaidi ya Millioni 2? Mkuu Mkandara Wa Zanzibar hawataki Muungano wetu Tuwaache kama walivyo unaonaje mkuu?
Kuonana uso kwa uso, sii hata Kenya tunaonana, Uganda tunaonana tena rais wetu mzuri sana anapenda viwanja atakuja sana Zanzibar lakini msimpe mke tu ili kusiwepo na mahusiano ya kimwili maana ndicho mkitakacho kuendeleza zinaa..

Kama tunavunja muungano tukubaliane maana tunajua mnaye mke mwingine akilini naye ni mwarabu mweupe wa rangi, mwenye pua ya Upanga, mtoto nywele za singa hadi mgongoni halafu ukoo wa mfalme, na ndio anawatoa roho kiasi kwamba umenipa mfano wa hizo bil 200.

Alaa wauze vichwa vipi wakati ndio wanaopata kuchagua wake/waume wengi kutoka kwetu bara?.. Sisi wabara tutaweza vipi kuingiliana na watu millio 2 au advantage ni yao kuweza kuuza mali zao kwa watu millini 40. Sisi hatuoni soko Zanzibar zaidi ya kutalii beach...Fikirieni kiuchumi na sio idadi ya kumezwa kwani sisi tumekuwa chewa!
 
Mh. Tundu Lissu akitoa hotuba Mbadala ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Wizara inayohusu maswala ya Muungano.

Kambi rasmi ya upinzani inasema baada ya katiba ya Muungano kuchakachuliwa na kuwekewa viraka vingi kinyume na makubaliano ya kuundwa kwa Muungano ya mwaka 1964, hivi sasa kuna nchi mbili ndani ya muungano yaani Tanganyika na Zanzibar.


Video kwa hisani ya chadematv ya youtube.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo serikali ya Muungano ni serikali ya kina nani?.. Si Wanzanzibar na Wabara ndio wameunda muungano huo ama? Mkuu wangu unajua hasa maana ya muungano au unazungumza tu vitu visivyojulikana mkidhani muungano ni sawa na JUMUIYA. Uliona wapi Federal Government haihusiki na maswala yanayohusu Muungano?. Hivi unataka kunambia Obama ni rais wa Illinois hawezi kuingilia maswala ya state nyingine ktk muungano wao. Ni yapi hayo ya serikali ya mapinduzi ambayo mliyakubali kikatiba leo yawe ya Zanzibar? na yapi ni ya bara. Haya nambie wakati Mwinyi alipokuwa rais alikuwa akiingilia maswala ya bara au... Mbona nyie mnaingilia kila siku ya bara kwa kutumia kiti cha muungano na hatusemi..

" naam kwa mujibu wa makubaliano, serikali ya muungano ni yetu sote kwa yale yanayohusu muungano, matatizo ni kwamba hata kayo mambo yasiyo ya muungano SMT inatuingilia kwa kutuamulia, lakini vile vile kuna uhalali gani kwa yale yasiyo ya muungano upande wa tanganyika kuhudumiwa na SMT kwa jina la tanzania? "
 
" naam kwa mujibu wa makubaliano, serikali ya muungano ni yetu sote kwa yale yanayohusu muungano, matatizo ni kwamba hata kayo mambo yasiyo ya muungano SMT inatuingilia kwa kutuamulia, lakini vile vile kuna uhalali gani kwa yale yasiyo ya muungano upande wa tanganyika kuhudumiwa na SMT kwa jina la tanzania? "
Unadhani Wazanzibar wanaliona hili?..Vikao vyote vya bunge Dodoma wawakilishi wa Zanzibar wapo toka kinafunguliwa hadi kinafungwa na wanachangia ktk maswala yote. Wapo katika mabaraza yote ya bara na serikali ya muungano, toka vikao vya vyama hadi taifalakini hawaoni kama wameingia kila sehemu bara..Na Wabara hawaruhusiwi kuingia ktk Bunge lao, wizara zao, hata kupiga kura za ucguzi mkuu wa Taifa hawatakiwi japokuwa ni wakazi wa Zanzibar ama wanafanya kazi za jamhuri ya muungano.

Imefikia hadi wakati wa uchaguzi mkuu, wabara wanatakiwa warudi Bara japokuwa hawapigi kura za kumchagua mwakilishi wa serikali ya Mapinduzi ila ya Muungano. Kwa ujinga wao husimama ktk vituo vya kura na kuwaondoa Wabara ambao wanaishi Zanzibar wasipige kura kumchagua rais wa Jamhuri ya Tanzania.. Can U imagine that!..
Haya hakuna Mbara ktk mabaraza yote la Wawakilishi ama la Mapinduzi japokuwa Wabara walishiriki ktk Mapinduzi hayo, huku bara wanataka wawe sehemu zote kwa sababu ni serikali ya muungano....Yaani hawaeleweki watu hawa kabisa halafu wanajiita wao sii wabaguzi walilelewa vizuri kupenda watu wote pasipo kuwabagua kwa trangi zao, dini, zao ama jinsia zao...
 
Kuonana uso kwa uso, sii hata Kenya tunaonana, Uganda tunaonana tena rais wetu mzuri sana anapenda viwanja atakuja sana Zanzibar lakini msimpe mke tu ili kusiwepo na mahusiano ya kimwili maana ndicho mkitakacho kuendeleza zinaa..

Kama tunavunja muungano tukubaliane maana tunajua mnaye mke mwingine akilini naye ni mwarabu mweupe wa rangi, mwenye pua ya Upanga, mtoto nywele za singa hadi mgongoni halafu ukoo wa mfalme, na ndio anawatoa roho kiasi kwamba umenipa mfano wa hizo bil 200.

Alaa wauze vichwa vipi wakati ndio wanaopata kuchagua wake/waume wengi kutoka kwetu bara?.. Sisi wabara tutaweza vipi kuingiliana na watu millio 2 au advantage ni yao kuweza kuuza mali zao kwa watu millini 40. Sisi hatuoni soko Zanzibar zaidi ya kutalii beach...Fikirieni kiuchumi na sio idadi ya kumezwa kwani sisi tumekuwa chewa!
Unazungumza wewe Maneno ya Porojo hakuna Maneno yoyote yale ya msingi wowote ule unao zungumza wewe. Muhimu kuwa WaZanzibar hawautaki huo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wanachotaka WaZanzibari Muungano uvunjike wanataka wawe huru kujiamulia mambo yao yenyewe acha porojo zako. mkuu Mkandara
 
Last edited by a moderator:
Mh. Tundu Lissu akitoa hotuba Mbadala ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Wizara inayohusu maswala ya Muungano.

Kambi rasmi ya upinzani inasema baada ya katiba ya Muungano kuchakachuliwa na kuwekewa viraka vingi kinyume na makubaliano ya kuundwa kwa Muungano ya mwaka 1964, hivi sasa kuna nchi mbili ndani ya muungano yaani Tanganyika na Zanzibar.


Video kwa hisani ya chadematv ya youtube.
Mkuu bagamoyo Kurudi kwa Tanganyika itarudi kwa njia nyepesi tu nayo ni moja Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uvunjike ndio itarudi hiyo Tanganyika pasipo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuvunjika Tanganyika haiwezi kurudi hilo ndilo jibu kwa chama cha Chadema.
 
Last edited by a moderator:
Unazungumza wewe Maneno ya Porojo hakuna Maneno yoyote yale ya msingi wowote ule unao zungumza wewe. Muhimu kuwa WaZanzibar hawautaki huo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wanachotaka WaZanzibari Muungano uvunjike wanataka wawe huru kujiamulia mambo yao yenyewe acha porojo zako. mkuu Mkandara
Sawa wewe chukulia porojo lakini ndio facts.. watu mil 2 wanaweza sana ku benefit kwa soko la watu mil 40 kuuza mali zao bila ushuru wa kuingiza mali, lakini Bara hawahitaji soko la Zanzibar, think about that jinsi gani tunavyowapa taabu wakenya na Waganda. Tuvunje muungano mjifungie wenyewe halafu tutaona huo mzunguko ndani kama utaweza kuwasaidia kiuchumi.

Haya nambie ni kiongozi gani anayetaka muungano uvunjike lakini pasiwepo na mkataba mwingine...Maana bara hatutaki mkataba wowote na Zanzibar zaidi ya muungano au tuvunje muungano.. wape mtihani huu viongozi wa Zanzibar halafu waje na jibu.. Nakuapia hutalipata.

Wewe mwambie kiongozi yeyote wa Zanzibar:-
1. Tuvunje muungano na hakuna ushirika wowote isipokuwa ule wa EA
2. Tuendelee na Muungano uliopo turekebishe tu kuwa na serikali tatu kila upande ujitegemee. This is what Mainland offer hakuna zaidi wala pungufu.
 
Wewe ni aibu hata kukujibu lakini wacha nikujibu tu. Wewe kenge unatoka mkowa gani wa hiyo Bongo chafu na jee mkowa wako una haya yafuatayo. Serikali kamili, Mawaziri, Wimbo wa Taifa, Jumba la Bunge, Raisi, Mahakama kuu na mipaka, Na jee hicho kakimkowa wako kishawahi kuwa na kiti Umoja wa Mataifa. Ndomaana nikasema aibu hata kukujibu wewe Sofulo.
 
Hiyo serikali ya Muungano ni serikali ya kina nani?.. Si Wanzanzibar na Wabara ndio wameunda muungano huo ama? Mkuu wangu unajua hasa maana ya muungano au unazungumza tu vitu visivyojulikana mkidhani muungano ni sawa na JUMUIYA. Uliona wapi Federal Government haihusiki na maswala yanayohusu Muungano?. Hivi unataka kunambia Obama ni rais wa Illinois hawezi kuingilia maswala ya state nyingine ktk muungano wao. Ni yapi hayo ya serikali ya mapinduzi ambayo mliyakubali kikatiba leo yawe ya Zanzibar? na yapi ni ya bara. Haya nambie wakati Mwinyi alipokuwa rais alikuwa akiingilia maswala ya bara au... Mbona nyie mnaingilia kila siku ya bara kwa kutumia kiti cha muungano na hatusemi..

Mkuu Mkandara
Tanzania ina states ngapi? nitajie kwa majina.

Muungano wa Tanzania una wanachama wangapi? Nitajie kwa majina.
Je unaona usanii wa muungano wetu?

US ni muungano wa states ngapi? Zinaeleweka kwa majina?
UK ni muungano wa nchi/ states ngapi? Zinajulikana kwa majina?

Je Kiini macho cha Tanzania kimeundwa na nchi/ states ngapi?

Dhana ya serikali kuu kwa Tanzania. Ifafanue.

Serikali ya Muungano ina mamlaka yake?
Serikali ya Tanganyika ina mamlaka yake?
Serikali ya Zanzibar ina mamlaka yake?

Je umewahi kusikia kuwa Tanzania ina mamlaka tatu za kisheria?
Hint, mambo ya Muungano, Mambo ya bara(Tanganyika) mambo ya Zanzibar.

Je hutaki kukubali kuwa Muungano huu wa Tz ni mazingaombwe?

Mkuu Mkandara huu mfano wa mke na mume / baba na mama unaupenda sana unapozungumzia Muungano.
Je EAC nayo ni ndoa nyengine? Unaelewa kuwa hatimae lengo ni kuunda shirikisho la Afrika ya Mashariki. Huku pia utatumia lugha ya mke na mume?

Halafu mkuu, ni lazima mtu anayeelezea mizengwe ya Muungano awe Mzanzibari? Muomani au mwarabu,sultani?
Ona tayari unamwita MziziMkavu, ninyi wazanzibari, mta....

Prof Shivji au Lissu wanapoonesha dosari za muungano huwa wanabadilika na kuwa wazanzibari?
 
Sawa wewe chukulia porojo lakini ndio facts.. watu mil 2 wanaweza sana ku benefit kwa soko la watu mil 40 kuuza mali zao bila ushuru wa kuingiza mali, lakini Bara hawahitaji soko la Zanzibar, think about that jinsi gani tunavyowapa taabu wakenya na Waganda. Tuvunje muungano mjifungie wenyewe halafu tutaona huo mzunguko ndani kama utaweza kuwasaidia kiuchumi.

Haya nambie ni kiongozi gani anayetaka muungano uvunjike lakini pasiwepo na mkataba mwingine...Maana bara hatutaki mkataba wowote na Zanzibar zaidi ya muungano au tuvunje muungano.. wape mtihani huu viongozi wa Zanzibar halafu waje na jibu.. Nakuapia hutalipata.

Wewe mwambie kiongozi yeyote wa Zanzibar:-
1. Tuvunje muungano na hakuna ushirika wowote isipokuwa ule wa EA
2. Tuendelee na Muungano uliopo turekebishe tu kuwa na serikali tatu kila upande ujitegemee. This is what Mainland offer hakuna zaidi wala pungufu.
Hakuna Kiongozi wa Serikali iliyopo Madarakani anaye zungumzia Kuvunjika kwa Muungano mpaka sasa mkuu Mkandara. Wanaye Zungumzia Suala la Kuvunja Muungano ni wananchi walala hoi Masikini

Wazawa wa KiZanzibar ndio wanaotaka huo Muungano uvunjike wananchi wamechoshwa na Kero za Muungano mimi niliwahi kuwauliza Wa Zanzibar munachotaka kitu gani wakasema hatutaki Muungano tunachotaka tuwe huru wa kujiamuliwa mambo

yetu wenyewe nikasema lakini nyinyi mupo wachache mpaka suala hilo walikubali Wenzenu wa Tanganyika walinirukia kiasi cha kutaka kunipiga na kusema kwenda zako wewe na hao Wa Tanganyika sisi tumesha choka na huo Muungano wenu

tunachotaka tuwe huru Hatuutaki huo Muungano sasa Mkuu ikiwa kama ni wewe uliye wahoji hao Wa Zanzibar na hawautaki huo muungano utasema kitu gani Mkuu Mkandara
 
Wewe ni aibu hata kukujibu lakini wacha nikujibu tu. Wewe kenge unatoka mkowa gani wa hiyo Bongo chafu na jee mkowa wako una haya yafuatayo. Serikali kamili, Mawaziri, Wimbo wa Taifa, Jumba la Bunge, Raisi, Mahakama kuu na mipaka, Na jee hicho kakimkowa wako kishawahi kuwa na kiti Umoja wa Mataifa. Ndomaana nikasema aibu hata kukujibu wewe Sofulo.
Mkuu acha Matusi hapa hatuzungumzi mambo ya matusi tunashauriana kuhusu suala la Muungano na hatima yake kama wewe huwezi malumbano ya siasa nenda kalumbane mambo ya Simba na Yanga nani ni Kiboko yake. Jibu kwa heshima na tadhima usijibu kwa kuleta chuki zako utakula BAN Mkuu jiheshimu utaheshimiwa usilete maneno ya Pumba hapa mkuu Dezo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom