Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Shahidi abanwa kesi ya kina Mramba
Na Gladness Mboma
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemtaka shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Bw. Godwin Nyelo, kuwasilisha barua iliyokuwa ikitoka benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwenda Kampuni ya
M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi.
Agizo hilo lilitolewa jana katika kesi inayomkabili Waziri wa zamani wa Fedha, Bw. Basil Mramba aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Daniel Yona na aliyekuwa Katibu Mkuu Hazina, Bw. Grey Mgonja.
Hakimu Saul Kinemela alitoa agizo hilo baada ya Wakili Bw. Eliasa Msuya anayemtetea Bw. Yona, kuitaka mahakama imlazimishe shahidi huyo kutoa barua hiyo kama sehemu ya ushahidi wao.
Awali, Bw. Nyelo alidai kuwa anaikumbuka barua hiyo, lakini hawezi kuiongelea wala kuitoa kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi mahakamani hapo, kwa sababu siyo yake wala hakuwa hakuwa anafanyia kazi taasisi iliyohusika.
Akitoa uamuzi juu ya hoja hiyo, Hakimu Kinemela alisema ili kutenda haki, mahakama inamlazimisha shahidi kutoa barua hiyo kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi.
Barua hiyo inadaiwa kuandikwa na aliyekuwa Msaidizi wa Gavana wa BoT, Bibi. Kesisia Mbatia Novemba 28, 2002 akiitaka kampuni ya M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation kuwasilisha mchanganuo uliosaidia kuingiwa kwa mkataba kati ya kampuni hiyo na BOT.
Mawaziri hao na katibu mkuu kwa pamoja wanatuhumiwa kuingia mkataba na kuisamehe kodi kinyume cha sheria kampuni ya M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation, jambo linalodaiwa kuwa lilisababisha serikali kupata hasara ya sh.bilioni 11.7.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo kwa nyakati tofauti kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 .
Na Gladness Mboma
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemtaka shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Bw. Godwin Nyelo, kuwasilisha barua iliyokuwa ikitoka benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwenda Kampuni ya
M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi.
Agizo hilo lilitolewa jana katika kesi inayomkabili Waziri wa zamani wa Fedha, Bw. Basil Mramba aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Daniel Yona na aliyekuwa Katibu Mkuu Hazina, Bw. Grey Mgonja.
Hakimu Saul Kinemela alitoa agizo hilo baada ya Wakili Bw. Eliasa Msuya anayemtetea Bw. Yona, kuitaka mahakama imlazimishe shahidi huyo kutoa barua hiyo kama sehemu ya ushahidi wao.
Awali, Bw. Nyelo alidai kuwa anaikumbuka barua hiyo, lakini hawezi kuiongelea wala kuitoa kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi mahakamani hapo, kwa sababu siyo yake wala hakuwa hakuwa anafanyia kazi taasisi iliyohusika.
Akitoa uamuzi juu ya hoja hiyo, Hakimu Kinemela alisema ili kutenda haki, mahakama inamlazimisha shahidi kutoa barua hiyo kama kielelezo cha ushahidi kwa upande wa utetezi.
Barua hiyo inadaiwa kuandikwa na aliyekuwa Msaidizi wa Gavana wa BoT, Bibi. Kesisia Mbatia Novemba 28, 2002 akiitaka kampuni ya M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation kuwasilisha mchanganuo uliosaidia kuingiwa kwa mkataba kati ya kampuni hiyo na BOT.
Mawaziri hao na katibu mkuu kwa pamoja wanatuhumiwa kuingia mkataba na kuisamehe kodi kinyume cha sheria kampuni ya M/S Alex Stewart Government Bussines Cooparation, jambo linalodaiwa kuwa lilisababisha serikali kupata hasara ya sh.bilioni 11.7.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo kwa nyakati tofauti kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 .