Mkuu naona unanipa tafsiri ya Wamarekani wakati jina Al-Qaida sio lao.
Nipe tafsiri ya walioanzisha kundi ilo 1988 kina Bin Laden.
"The base"
Mkuu naona unanipa tafsiri ya Wamarekani wakati jina Al-Qaida sio lao.
Nipe tafsiri ya walioanzisha kundi ilo 1988 kina Bin Laden.
Utakuwa sahihi. Hata mimi nilianza kushangaa kama Musa Nkangaa ninayemfahamu (Aliyewahi kuwa waziri na mkuu wa mkoa) ndiye katoa tafsiri hiyo kituko ya Al Qaeda.anaitwa kiusahihi Musa Hamis Mkanga, sio Nkangaa; aliwahi kuwa diwani wa kata ya Sombetini akafukuzwa kwa kashfa ya ubadhirifu!
Hivi huyu bwana Mkangaa katika uko kina mama ndio wanaongoza familia? Vitabu vya Mungu vimeandika "mwanaume ni kichwa cha nyumba". Nyumba ambazo wanaume wameproof failure ndiyo wanawake wanalazimika kuwa wasemaji wa familia hata ukoo. Sina hakika kama Arusha imekosa mtu kuiongoza. Lema amesema, hajasema nina hakika watu wa Arusha kwa kipindi hiki hawawezi kumchagua huyu mama. Kwani adha wanazopata watu wa Hanang ndiyo ingewapata, mtu mnampa ubunge baada ya uchaguzi anakwenda kuishi na familia yake nje ya wilaya kufurahia posho na mshahara ambao hajaufanyia kazi wananchi tukaridhika kwa kutokuwepo kwake wilayani.
Wakuu
Kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge Arusha mjini imeanza kusikilizwa,baada ya kujitoa kwa Jaji Aloyce Mujuluzi.Jana upande wa mashtaka ulianza kutoa ushahidi,ambapo shahidi wa kwanza Musa Nkangaa,aliieleza Mahakama kuwa Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema,aliwataka wapiga kura kutomchagua Batilda Burian,kwa kuwa eti ni Al qaeda.
Mahojiano yalikuwa hivi..
1.shahidi.Mh Mbunge wakati wa kampeni kwenye mkutano Terat,aliwaambia wapiga kura wasimchague Batilda Burian,maana ni Al qaeda
2.Wakili wa utetezi..Unawafahamu Al qaeda?
3.Shahidi.Ndio nawafahamu,ni Mtu yeyote anayefunga kitambaa kichwani
4.Wakili wa utetezi..Je masista nao ni Al qaeda?
5.Shahidi.Ndio ni Al qaeda,kwa kuwa nao masista wanafunga vitambaa kichwani
Shahidi Musa Nkangaa ataendelea na ushahidi wake leo,nitaendelea kuwajuza kitakachojiri
Huyu Juma MKangaa ni mnafiki tu,
aliwahi kupigwa chini udiwani wa CCM kwa kashfa ya kuuza kiwanja pale soko la KIlombero,
hivyo nina wasiwasi na uadilifu wake
Huyu jamaa ni kesi kila siku! Hivi ana muda wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi? Uwakilishi wake una mashaka sana.
Huyu Juma MKangaa ni mnafiki tu,
aliwahi kupigwa chini udiwani wa CCM kwa kashfa ya kuuza kiwanja pale soko la KIlombero,
hivyo nina wasiwasi na uadilifu wake
Ritz,nimeripoti mtiririko wa maswali ya wakili wa utetezi,na shahidi wa mashitaka,kama na wewe una ya nyongeza ongezea sio kuanza kushtumu,
Nadhani ata wewe umeshindwa kujua Al-Qaida ni nani, sio magaidi wote ni wanaitwa Al-Qaida, ina wezekana huyo shahidi yupo right kwenye ya tafsiri ya Al-Qaida..
Lema, yeye alivyosema Al-Qaida alikuwa anajua ni kina nani?
Heshima kwanu wanajamvi,
Nilisema mara baada ya matokeo ya uchaguzi yalipotangazwa kwamba ushindi wa Mheshimiwa Lema ukitinga mahakamani lazima atapigwa chini kwasababu yapo matamko mengi ambayo hakupaswa kutamka hadharani.Huo ndiyo ukweli wa mambo lipo suala la Redio Safina likifikishwa mbele ya Jaji hakika lazima maandalizi ya uchaguzi mwingine yafanyike.
Mheshimiwa Lema bado ana nafasi ya kushinda tena uchaguzi mwingines si kwasababu kafanya mambo mazuri lahasha atashinda kwakuwa bado siasa za kishabiki zitachukua nafasi yake.