Kesi ya Cameron Todd Willingham: Baada ya kunyongwa yabainika hakuwa na hatia…….!

Na huyu naye mawakili walikuja kutengua kesi yake kuwa hakusababisha,
so kuwaacha watoto alighafirika tu kama yule wa TV.
 
Uzembe mwingine wa kujitakia, Yaani unaamshwa na mwanao kwamba nyumba inaungua badala ya kuwahi kuokoa uhai wa binadamu tena watoto wako wa kuwazaa unakimbilia kuokoa gari!! Stupid boy, acha anyongwe tena angenyongwa kwa kukatwa shingo kabisa.

Kwa roho hiyo ya ukatili na ushahidi wa kimazingira hata mimi ningekuwa hakimu lazma ningemtia hatiani kwa kosa hilo.
 
It is so sad,
Kwa kweli hii kesi inautata mwingi sana but hili la kukimbiza gari badala ya watoto mhh???
Ufunguo wa gari ulikuwa wapi?

Lakini pia yawezekana mambo ya ukata aliokuwa nao, akili ilimpeleka moja kwa moja kwa kile alichokuwa anaona ndio mali aliyo nayo tu, na akitegemea kuwa angeweza kuwahi kubeba watoto kumbe huku nyuma moto ukawa umezidi.

Kuna mafuriko yametokea hapa bongo mama mmoja kakimbiza TV kaacha mtoto kitandani, kurudi mtoto kisha CHUKULIWA NA MAJI.

Sijui huwa akili zinakutoka ukipata janga hata sielewi maana huyu mama ingekuwa ulaya sijui angeshtakiwa kwa kuua makusdi? Nashindwa kuelewa.
Haaaaa kaokoa TV kisha kawacha mtoto??Mi nakubaliana na ww kwamba huyo jamaa alikosea kuprioritize aokoe nn kwanza na inawezekana alikuwa into something yaani hakuwa sawa kichwani background yake ni utata tayari ganja ilikuwa kumkichwa ...Na kitu kingine ni kwamba kuna watu wengine ikitokea hali kama hio hawajui wafanye nn wanapanick balaaa yaani anakuwa na kimuhemuhe mpaka faham zikimrudia inakuwa too late.... ushaona wale wanaume wanaokuwa chumba cha uzazi wakiona dam tu anazirai yeye ha ha ha.....au yule ambaye akiona panya anapanda yeye juu ya kiti anakimbia....
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom