Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,221
- 1,788
Ile kesi ya Maandamano ya January 5,inayowakabili viongozi waandamizi wa CHADEMA,akiwepo Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe,katibu Mkuu Taifa,Dr Slaa, Wabunge Ndesamburo, Selasini, Lema, na viongozi wengine wa mkoa, wilaya na wanachama, itaendelea kusikilizwa tena kesho Jumatatu tarehe 28, katika mahakama ya hakimu mkazi Arusha.
Juzi Ijumaa wakili wa utetezi aliweka mapingamizi kwenye mashtaka yote yanayowakabili kwa kuwa yamefunguliwa kinyume cha sheria na taratibu, hivyo akaomba hakimu aitupilie mbali.
Ndipo wakili wa serikali akaomba hadi Jumatatu ili aweze kuyapitia.
Juzi Ijumaa wakili wa utetezi aliweka mapingamizi kwenye mashtaka yote yanayowakabili kwa kuwa yamefunguliwa kinyume cha sheria na taratibu, hivyo akaomba hakimu aitupilie mbali.
Ndipo wakili wa serikali akaomba hadi Jumatatu ili aweze kuyapitia.