KESI haiishi,WAHITIMU hawaishi...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Ile kesi ya wanafunzi 172 na wengine inayohusu wanafunzi hao kukataa vyeti vya Chuo Kikuu cha Ardhi na kutaka vya UDSM imechukua sura mpya.Kesi hii iliyoanza mwaka 2007 ipo mbele ya Jaji Dr.Feuz Twaib wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Kanda ya Dar es Salaam.

Ilivyokuwa: Wanafunzi walipata udahili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya UCLAS(sasa Ardhi University).Wakati wameshasajiliwa na kuanza masomo,UCLAS ikawa chuo kamili:Ardhi University.Walipomaliza masomo yao,Ardhi wakataka kuwatunuku vyeti wanafunzi hao.Wanafunzi wakagoma.Wakafungua kesi.Wakaiomba Mahakama Kuu itoe amri kukishinikiza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kiwape vyeti vyao.Jaji Twaib akawapa amri waliyoiomba.Utekelezaji ukaanza.Katikati pakatokeo jambo.UDSM na Ardhi wakataka kugawana wanafunzi wa kuwapa cheti huku na kule.

Wanafunzi wakagomea hilo tena.Wakamrudishia Jaji Dr.Feuz Twaib hukumu yake aitafsiri kwa njia ya maombi maalumu kisheria.Jana ilikuwa siku ya hukumu.Kesi imeahiriswa hadi tarehe 19 mwezi huu.

Kimsingi,wanafunzi hawa hadi sasa hawana vyeti.Hawaajiriki.Wataishije? Nani alaumiwe hapa?

Kesi yajulikana kama:Lelo Didas and 171 Others versus 1.ARDHI UNIVERSITY 2.UDSM 3.ATTORNEY GENERAL
 
Ile kesi ya wanafunzi 172 na wengine inayohusu wanafunzi hao kukataa vyeti vya Chuo Kikuu cha Ardhi na kutaka vya UDSM imechukua sura mpya.Kesi hii iliyoanza mwaka 2007 ipo mbele ya Jaji Dr.Feuz Twaib wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Kanda ya Dar es Salaam.

Ilivyokuwa: Wanafunzi walipata udahili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya UCLAS(sasa Ardhi University).Wakati wameshasajiliwa na kuanza masomo,UCLAS ikawa chuo kamili:Ardhi University.Walipomaliza masomo yao,Ardhi wakataka kuwatunuku vyeti wanafunzi hao.Wanafunzi wakagoma.Wakafungua kesi.Wakaiomba Mahakama Kuu itoe amri kukishinikiza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kiwape vyeti vyao.Jaji Twaib akawapa amri waliyoiomba.Utekelezaji ukaanza.Katikati pakatokeo jambo.UDSM na Ardhi wakataka kugawana wanafunzi wa kuwapa cheti huku na kule.

Wanafunzi wakagomea hilo tena.Wakamrudishia Jaji Dr.Feuz Twaib hukumu yake aitafsiri kwa njia ya maombi maalumu kisheria.Jana ilikuwa siku ya hukumu.Kesi imeahiriswa hadi tarehe 19 mwezi huu.

Kimsingi,wanafunzi hawa hadi sasa hawana vyeti.Hawaajiriki.Wataishije? Nani alaumiwe hapa?

Kesi yajulikana kama:Lelo Didas and 171 Others versus 1.ARDHI UNIVERSITY 2.UDSM 3.ATTORNEY GENERAL

Hoja yako nzuri sana lakini hasa unataka tuchangie nini/kwa vipi. labda kwa swali la nani alaumiwe, ni vyuo hivyo tu hasa UDSM, mkataba wa masomo upo na UDSM and not otherwise. Kama kungelikuwa na transfer of contract, both parties should agree to the terms of transfer and not one side. Remember in law of contract,m, both parties agree to the terms of the contract. It seems in this case one party dictated the terms of the contract by transfering student registration to UCLAS without the consent of the other party(students). The UDSM is the ones to blame
 
Nadhani uongozi wa UDSM na hata UCLAS/AU ulikurupuka katika kufanya maamuzi kuhusiana na transitional arrangements.

Hata hivyo ni kwa nini hao wanafunzi wasingekubali vyeti vya AU na kisha kudai hivyo vya UDSM mabavyo ndio kimsingi/kisheria wanastahili? Wakati wanaendelea na kesi wangetumia hivyo vya AU kuajiriwa au kuendelea na masomo ya juu badala ya kupoteza muda wote huu wa miaka 5!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom