Kesho ya Kikwete ni chungu kuliko leo ya Mkapa

Kibanda

Member
Aug 27, 2009
87
45
Makala hii ilichapwa katika Tanzania Daima Jumatano wiki hii.


Kikaango cha JK kitampiku Mkapa (1)

Na Absalom Kibanda


WIKI iliyopita nilihitimisha mjadala uliokuwa ukidurusu historia ya ushabiki wa kisiasa katika nchi hii ambao kwa mtazamo wangu nilieleza kwamba ndiyo uliolifikisha taifa katika ukomo wa kushindwa kufikiri na kuchukua maamuzi yanayofaa.

Mwisho wa mjadala huo nilieleza namna hulka za kishabiki katika taifa hili zilivyotufikisha Watanzania katika hatua ambayo sote tulijikuta hatimaye tukimfikisha Ikulu, mwanasiasa ambaye aghalab sifa na uwezo alionao kama kiongozi mkuu wa nchi vinaendelea kuibua maswali mengi kuliko majibu.


Aidha, katika mjadala huo ambao ulinichukua kuukamilisha kwa muhtasari tu katika kipindi cha wiki mbili, niliweza kuyaeleza pia matokeo ya ushabiki huo ambao kwa bahati mbaya ulifikia hatua hata ya kumtisha na kumyumbisha rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ambaye ndiye aliyekuwa na turufu ya mwisho kabla ya kuwaaachia wananchi waamue nini cha kufanya.


Ninapogeuka nyuma leo hii na kuangalia mtitiriko wa matukio ya kihistoria ambayo hatimaye yalimfikisha Rais Jakaya Kikwete Ikulu, mwaka 2005, nabaini jambo moja kwamba, taifa lilikuwa likihitaji kuwa na kiongozi mwenye mamlaka ya ushawishi kama aliyokuwa nayo Baba wa Taifa mwaka 1995 ili kuzuia yale yaliyotokea wakati huo yasitokee.


Katika kusema hili simaanishi jambo jingine lolote, zaidi ya kueleza tu kwamba kama ilivyotokea mwaka 1995 wakati Mwalimu Julius Nyerere alivyofanikiwa kumzuia Augustine Mrema kuingia Ikulu ndivyo alivyopaswa kufanya Mkapa, miaka 10 baadaye.


Kwa maneno rahisi kabisa, alichopaswa kufanya Mkapa kilikuwa ni kuthubutu kuchukua maamuzi magumu ambayo hatimaye yangekiwezesha CCM kudhibiti kishindo cha Kikwete na jeshi lake la mtandao kuingia Ikulu kwa njia ya mlango wa nyuma.


Miaka mitano tangu Mkapa afanye kosa hilo, wadadisi wa mambo wameendelea kukuna vichwa vyao wakijiuliza ni kitu gani hasa kilimfika kiongozi huyo ambaye wengi walikuwa wakimuona kuwa mtu madhubuti hata afikie hatua ya kuyumba na kuongoza vikao katika mwelekeo ambao ulionyesha bayana kumbeba Kikwete na kuwaumiza wengine.


Pamoja na kukosekana kwa jibu halisi katika swali hilo hasa kutokana na ukweli kwamba, Mkapa mwenyewe hajapata kueleza kwa undani juu ya kile kilichomsibu hata akajikuta akiyumba na kupoteza mwelekeo, ni ukweli kwamba matokeo ya kosa hili ndiyo ambayo leo hii mbali ya kulitafuna taifa yanamtafuna hata yeye mwenyewe.


Ninayo imani ya dhati kwamba, katika hali ya uwazi na ukweli, iwapo Mkapa atapata fursa ya kusema kile kilicho moyoni mwake leo, si ajabu (nasisitiza si ajabu) kiongozi huyo mstaafu anaweza akaeleza majuto dhidi ya maamuzi aliyosimamia ambayo mbali ya kumgharimu yeye binafsi sasa yanaligharimu taifa.


Ni dhahiri kwamba, leo hii Mkapa huwa anaugulia maumivu makali kila anapogeuka nyuma na kuangalia namna Watanzania kwa makumi na mamia wanavyomsimanga, wakimhusisha na tuhuma za ufisadi, zake binafsi au zile zinazowagusa mawaziri na watendaji wakuu wa zama zake.


Hata hivyo, anachopaswa kutambua Mkapa ni kwamba, kuugulia maumivu kwake chinichini hakupaswi kuishia hapo, bali kama tulivyopata kuwaasa wengine kabla yake, anawajibika kujipanga kwa ajili ya kuomba toba ya wazi kwa wananchi kwa namna alivyoliingiza taifa matatizo.


Ili kufanikisha hili, Mkapa anapaswa kufanya kile kilichopaswa kufranywa na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere wakati alipokuwa amestaafu ambaye mara kadhaa alipata kuitisha mikutano na waandishi wa habari na kukiri kufanya makosa mbalimbali wakati akiwa madarakani.


Naamini Mkapa ambaye umakini wake si wa kutiliwa shaka katika masuala ya habari, anakumbuka namna Mwalimu alivyopata kueleza kusikitishwa na tabia ya Watanzania kuyaangalia mabaya tu yaliyopata kufanywa na serikali yake na kuyaacha mazuri mengi.


Katika kauli zake za namna hiyo, mara kadhaa, Mwalimu alipata kunukuliwa akiomba radhi, akifanya hivyo hadharani na wakati mwingine kwa kutoa machozi kabisa kama alivyofanywa wakati alipomuomba radhi Mzee Rashidi Kawawa kwa kubeba lawama nyingi kwa makosa ambayo wakati mwingine aliyafanya yeye.


Si Mwalimu tu, Mkapa anapaswa kujifunza kutoka kwa Papa Benedict na mtangulizi wake ambao wamepata kuomba radhi hadharani kwa makosa ambayo ama yalifanywa na kanisa au makasisi wake katika maeneo mbalimbali duniani.


Katika hili, Mkapa anapaswa kukiri hadharani kwa njia ya kuzungumza na wanahabari kama alivyokuwa akifanya Mwalimu na kueleza namna alivyoteleza katika kuvisimamia vyema vikao vya uteuzi ndani ya CCM ambavyo hatimaye chini ya uenyekiti wake, vilimpa fursa Kikwete kuteuliwa mwaka 2005.


Katika kuomba radhi kwa kosa hilo, Mkapa anapaswa kuwaeleza wananchi hadharani, kwamba kosa lake hilo ambalo alililifanya kwa kujua au kutokujua akiamini lingemsaidia kujihami akiwa mstaafu, leo hii linamgharimu kwa kiwango ambacho taswira yake katika jamii imechafuka.


Pamoja na kukiri kosa hilo, Mkapa ambaye kimsingi anapaswa kufanya hivyo kabla ya kuanza kwa kazi ya uteuzi ndani ya CCM, atatakiwa kueleza na kuyakiri hadharani baadhi ya makosa ya kimaamuzi na yale ya kimaadili ambayo aliyafanya yeye binafsi, mawaziri wake au serikali aliyokuwa akiiongoza kwa namna ile ile alivyopata kufanya Mwalimu Nyerere miaka ya mwanzo ya 1990.


Baada ya kuomba radhi kwa makosa hayo, Mkapa atapaswa kuweka sawasawa rekodi yake kwa kueleza namna jina lake linavyotajwa na kuhusishwa kwa makosa na umiliki wa mgodi wa makaa ya mawe Kiwira na namna ambavyo hakupata kuyatumia madaraka yake kufanya biashara au kujihusisha na rushwa au matendo ya ufisadi kwa namna yoyote ile katika kipindi chote cha miaka 10 cha utawala wake.


Ninao uhakika kwamba, iwapo Mkapa atauzingatia ushauri huu, kwanza atakuwa ametoa mchango muhimu kabisa wa tiba ya bongo za Watanzania ambao tumelishwa ujinga na uzushi mwingi kuhusu kiongozi huyo na serikali yake hata katika mambo ambayo wakati mwingine lawama zinapaswa kwenda kwingine na si kwake.


Lakini pia kwa kufanya hivyo, Mkapa atawapa fursa wana CCM wenzake na Watanzania kwa ujumla kupata fursa ya kutulia na kupima sawasawa mwenendo wa kikazi na kimaadili wa serikali ya Kikwete ambayo naamini, nyuma ya pazia imebeba uchafu mwingi ambao Watanzania wengi hatuujui.


Mwisho kwa kufanya hivyo, Mkapa atakuwa ameanza kujenga msingi imara kwa wananchi walio wengi katika kuwajua viongozi wao na hivyo kuwapa fursa ya kushiriki ipasavyo katika uteuzi na hatimaye uchaguzi wa viongozi wakati wa uchaguzi mkuu ujao.


Lakini kubwa katika yote ni kwamba, baada ya kufanya hivyo, kama ilivyo kuwa kwa Mwalimu Nyerere, basi na Mkapa naye ataweza kuanza upya kuwaeleza wananchi kwa kufanya ulinganifu na sasa, namna serikali yake ya awamu ya tatu ilivyofanya kazi kubwa katika kuwajengea wananchi wake misingi imara ya maendeleo kiuchumi na kijamii.


Ni wazi kwamba, leo hii kabla ya toba hiyo, Mkapa anapata wakati mgumu kuitetea rekodi ya kipekee iliyosheheni nidhamu ya hali ya juu ya utendaji katika serikali yake ambayo ilikuwa na matokeo mema kiuchumi.


Leo hii kabla hajafanya toba hiyo, ni wazi kwamba, Mkapa anapata shida hata kutetea rekodi yake kipekee ya miaka 10 ya kujenga upya uchumi ulioparanganyika kwa kuudhibiti mfumuko wa bei kutoka kiwango cha asilimia 27.1 mwaka 1995 hadi asilimia 4.2 mwaka 2004.


Ni katika misingi hiyo hiyo ya kuandamwa na kivuli cha dhambi ya maamuzi ya hovyo ndicho kinachomfanya Mkapa leo hii akwame kujivunia kupandisha pato la taifa imeongezeka kutoka asilimia 3.6 mwaka 1995 hadi 6.7 mwaka 2004.


Kama hiyo haitoshi, jeuri ya Mkapa kukataa kujiona mnyonge kwa kutuomba radhi inamnyima fursa pia ya kutembea kifua mbele kwamba, zama zake aliweza kuongeza pato la serikali kutoka wastani wa sh.37.4 bilioni kwa mwezi katika mwaka wa fedha wa 1995/96 hadi kufikia wastani wa zaidi ya sh.140 bilioni kwa mwezi katika mwaka wa fedha wa 2004/05.


Matokeo ya jeuri hii ya Mkapa kudharau vyombo vya habari na kukataa kuomba radhi ndiyo ambayo inamfanya Mkapa kujitokeza hadharani na kutetea sera na sheria ya madini ambayo pamoja na mapungufu yake ilichangia ukuaji wa rekodi kiuchumi.


Ni wazi kwamba kiburi hiki cha Mkapa cha kutotaka kuonekana mnyonge, au mtu mwenye makosa ndicho ambacho kinasababisha ashindwe hata kujitokeza na kutamba kwamba katika kipindi cha miaka 10 cha utawala wake, zaidi ya dola za Marekani 1.4 bilioni kiliwekezwa katika sekta ya madini na kubabisha migodi mikubwa sita ya dhahabu kuanzishwa.


Angeachana na jeuri yake hii ya kibabe, Mkapa angeweza leo kuitisha mkutano wa waandishi wa habari na akamjibu kwa kishindo Waziri wa Kilimo na Chakula Stephen Wasira ambaye majuzi aliweza kusimama kwa mbwembwe na kuinyoshea kidole serikali kuhusu sekta ya madini.


Katika hili Mkapa angeweza kumkumbusha kirahisi Wasira na wanasiasa wengine kwamba pamoja na kuinyoshea serikali kidole kwa kuruhusu madini yaibwe na wawekezaji wa nje, sera zake ziliiwezesha Tanzania kuwa ni nchi ya tatu barani Afrika kwa wingi wa dhahabu inayozalishwa, baada ya Afrika Kusini na Ghana.


Katika hili, Mkapa angeweza kumkumbusha Wasira kwamba kabla ya kuruhusu uchimbaji mkubwa, mwaka 1995 Tanzania ilizalisha tani tatu tu za dhahabu na miaka 10 baadaye wakati akiondoka madarakani kiwango rasmi kilipanda hadi kufikia tani 50, ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mara 16.


Kwa hakika katika hilo, majibu hayo ya Mkapa kwa Wasira ambaye hakuna shaka kwamba mawazo aliyonayo ndiyo pia anayo Kikwete (rejea sera ya uwajibikaji wa pamoja serikalini) yasingeishia hapo bali yangekwenda mbele zaidi kwa kueleza kuwa mauzo ya dhahabu nje ya nchi katika kipindi cha kati ya mwaka 1997 na 2004 yaliongezeka kutoka dola za Marekani milioni 2 hadi kufikia dola 593.2 milioni kiwango ambacho ni ongezeko la karibu mara 300.


Ni wazi kwamba majibu hayo ya Mkapa kwa mara ya kwanza yangekuwa turufu ya kwanza ya kupima utendaji wa zama ya serikali yake dhidi ya huu wa serikali ya Kikwete uliojaa blah blah, majungu, fitina, uzushi, ushabiki, visasi na mambo yanayofanana na hayo. Tutaendelea na mada hii wiki ijayo.
 
Shukrani mzee kwa uchambuzi wako wa kina kuhusu mema aliyoyafanya Rais mkampa, lakini nadhani ingekuwa bora kama ungegusia hizo economic policies zake kwa mwananchi wa kawaida, je alinufaika au la?

Pili, umetaja mikataba ya madini ambayo iliiweze Tanzania kuwa namba tatu Afrika kwa uzalishaji wa madini, sasa suala ni je, hali ya Watanzania, haswa wale wakazi wa maeneo hayo na wengineo, walinufaiki vipi?, kwa sababu data nyingi zinaonyesha kwamba ni UMASKINI NDIO UNAOTAWALA, na hakuna zaidi.

Mwisho kabisa, labda ungewatendea haki Walala hoi kwa kuelezea scandals zote ambazo zilfanyika mbele ya macho yake kama Commander-In-Chief wa nchi. Yaani kuanzia RADAR, DOWANS, MEREMETA, KIWIRA N.K. Naamini suala sio kuongelea mema tu, kuna mengi mabaya yaliyofanyika under his Supervision, na ambayo yanahitaji majibu. Vinginevyo, natumani historia ya Tanzania ndio itamukumu, ipo siku tu.
 
Nimeipenda sana sana hii makala kwani hata mimi huwa najiuliza kila siku ni nini kilichomsibu Mkapa mpaka akawaachia wanamtandao kuchukua nchi ilhali walikuwa wanajulikana kabisa ni genge la watu wasio na sifa za kiuongozi, achilia mbali fedha nyingi walizotumia kuhonga?

Mkapa alikuwa rais na jemedari mkuu wa majeshi. Alikuwa na nyenzo zote za kumwezesha kujua nani ni nani na nani anafanya nini! Kwa nini alifyata mkia kwa watu wa kuja kama Rostam Aziz na genge lake? Kwa nini hakutumia vyombo vya usalama , ikibidi hata mbinu chafu (.... na hata kupoteza baadhi yao) ili Tanzania na Watanzania waokoke na hili genge?

....Anyway hata mimi nakubaliana na wewe hata iwe 2020 lakini panapo majaaliwa washiriki wa huu usanii unaoendelea sasa (kina Kikwete) watafikishwa kwenye vyombo vya haki. Jambo la muhimu ni kila mtu kukusanya ushahidi wa matukio machafu yanyoendelea sasa ili wakati ukifika tuweze kuwakaanga vizuri........
 
Shukrani mzee kwa uchambuzi wako wa kina kuhusu mema aliyoyafanya Rais mkampa, lakini nadhani ingekuwa bora kama ungegusia hizo economic policies zake kwa mwananchi wa kawaida, je alinufaika au la? Pili, umetaja mikataba ya madini ambayo iliiweze Tanzania kuwa namba tatu Afrika kwa uzalishaji wa madini, sasa suala ni je, hali ya Watanzania, haswa wale wakazi wa maeneo hayo na wengineo, walinufaiki vipi?, kwa sababu data nyingi zinaonyesha kwamba ni UMASKINI NDIO UNAOTAWALA, na hakuna zaidi.
Mwisho kabisa, labda ungewatendea haki Walala hoi kwa kuelezea scandals zote ambazo zilfanyika mbele ya macho yake kama Commander-In-Chief wa nchi. Yaani kuanzia RADAR, DOWANS, MEREMETA, KIWIRA N.K. Naamini suala sio kuongelea mema tu, kuna mengi mabaya yaliyofanyika under his Supervision, na ambayo yanahitaji majibu. vinginevyo, natumani historia ya Tanzania ndio itamukumu, ipo siku tu.

Kweli historia itamuhukumu , lakini kama historia hiyo ni fair haitasahau uzuri wake na alichokifanyia nchi hii! that also will never be forgotten
 
Hata kama kiasi cha dhahabu inayouzwa nje kiliongezeka kwa asilimia 300% bado swali liko pale pale. Watanzania wamefaidikaje na mwongezeko huo?
Ndiyo yale yale ya afadhali kupata asilimia 3% kuliko kutopata chochote.
 
Hata kama kiasi cha dhahabu inayouzwa nje kiliongezeka kwa asilimia 300% bado swali liko pale pale. Watanzania wamefaidikaje na mwongezeko huo?
Ndiyo yale yale ya afadhali kupata asilimia 3% kuliko kutopata chochote.

Hawakufaidika na wala hawafaidiki, Kibdana alitakiwa kuwliweka hilo bayana kwenye article yake, ni aibu kuzungumzia uzalishaji wa dhahabu bila kuhusisha inawasaidiaje wananchi.
 
Kweli historia itamuhukumu , lakini kama historia hiyo ni fair haitasahau uzuri wake na alichokifanyia nchi hii! that also will never be forgotten

Hawakufaidika na wala hawafaidiki, Kibdana alitakiwa kuwliweka hilo bayana kwenye article yake, ni aibu kuzungumzia uzalishaji wa dhahabu bila kuhusisha inawasaidiaje wananchi.

Pia ni jambo jema kueleza bayana ni uzuri upi ambao historia haitasahau maana wanaweza kuwepo wengine ambao hawauoni wala kuuelewa huo 'uzuri' bila kuuzungumzia kinaga ubaga.
 
Katika kauli zake za namna hiyo, mara kadhaa, Mwalimu alipata kunukuliwa akiomba radhi, akifanya hivyo hadharani na wakati mwingine kwa kutoa machozi kabisa kama alivyofanywa wakati alipomuomba radhi Mzee Rashidi Kawawa kwa kubeba lawama nyingi kwa makosa ambayo wakati mwingine aliyafanya yeye.

Si Mwalimu tu, Mkapa anapaswa kujifunza kutoka kwa Papa Benedict na mtangulizi wake ambao wamepata kuomba radhi hadharani kwa makosa ambayo ama yalifanywa na kanisa au makasisi wake katika maeneo mbalimbali duniani.

Katika hili, Mkapa anapaswa kukiri hadharani kwa njia ya kuzungumza na wanahabari kama alivyokuwa akifanya Mwalimu na kueleza namna alivyoteleza katika kuvisimamia vyema vikao vya uteuzi ndani ya CCM ambavyo hatimaye chini ya uenyekiti wake, vilimpa fursa Kikwete kuteuliwa mwaka 2005.

Katika kuomba radhi kwa kosa hilo, Mkapa anapaswa kuwaeleza wananchi hadharani, kwamba kosa lake hilo ambalo alililifanya kwa kujua au kutokujua akiamini lingemsaidia kujihami akiwa mstaafu, leo hii linamgharimu kwa kiwango ambacho taswira yake katika jamii imechafuka.

Pamoja na kukiri kosa hilo, Mkapa ambaye kimsingi anapaswa kufanya hivyo kabla ya kuanza kwa kazi ya uteuzi ndani ya CCM, atatakiwa kueleza na kuyakiri hadharani baadhi ya makosa ya kimaamuzi na yale ya kimaadili ambayo aliyafanya yeye binafsi, mawaziri wake au serikali aliyokuwa akiiongoza kwa namna ile ile alivyopata kufanya Mwalimu Nyerere miaka ya mwanzo ya 1990.

Baada ya kuomba radhi kwa makosa hayo, Mkapa atapaswa kuweka sawasawa rekodi yake kwa kueleza namna jina lake linavyotajwa na kuhusishwa kwa makosa na umiliki wa mgodi wa makaa ya mawe Kiwira na namna ambavyo hakupata kuyatumia madaraka yake kufanya biashara au kujihusisha na rushwa au matendo ya ufisadi kwa namna yoyote ile katika kipindi chote cha miaka 10 cha utawala wake.

Ninao uhakika kwamba, iwapo Mkapa atauzingatia ushauri huu, kwanza atakuwa ametoa mchango muhimu kabisa wa tiba ya bongo za Watanzania ambao tumelishwa ujinga na uzushi mwingi kuhusu kiongozi huyo na serikali yake hata katika mambo ambayo wakati mwingine lawama zinapaswa kwenda kwingine na si kwake.

Kaka Kibanda asante sana kwa nakala hii nzuri ila kuna vitu nakubaliana na wewe na kuna vitu ninavinpinga tena sana

1. Mkapa hapaswi kuomba msamaha wowote ule kwa yeyote yule! hana kosa lolote lile alilolitenda mpaka sasa hivi unless mahakama iseme kuwa ni guilty, tukishindwa kufikia hatua hii then, tukubali kuwa systems zetu ni mbovu na hatuwezi kumuwajibisha kiongozi kwa namna au jinsi yeyote ile.Msamaha siyo suluhisho, sisi ni waajiri wa viongozi kama hatuna system zinazodhihirisha hivyo then we are done!

2. Kuna uozo mkubwa sana sana kwenye idara ya habari na nyie wengi wenu mnaingia kwenye hili kapu. Nyerere siku moja alisimama kwa hasira wakati mwandishi wa habari mmoja alikuwa anasema "nasikia" nasikia" nasikia" uozo huu hata Mkapa unayemsifia kuwa ni mwandishi mzuri ameusema mara nyingi, leo hii hamna chombo chochote cha kusimamia ethic zenu za uandishi, kuna taarifa hata mimi nisiye mtaaluma wa habari naona kinyaa kusoma! hamna utafiti, hamna professionalism, taaluma ya habari haikui! hakuna washawishi, huyo Mkapa pamoja na ugumu wake still kuna watu wanaweza kumwona na kumuhoji wakitaka! this ushawishi ni kiwango cha juu kabisa kudhihirisha wana habari wanaweza kupenya pasipo penyeka,Mkapa anajua udhaifu wenu! na anakaa kimya kabisa kwani bila kuongea hampati lolote.

Nimejaribu kumfuatilia Mkapa hata kutoka kwa mate wenzake aliosoma nao, kujua alikuwa na tabia gani shuleni,huko Marekani n.k kuna mzee nilikutana naye kwenye msiba mmoja na akanipa contact za watu fulani wa karibu na Mkapa. Visiona za Mkapa na tabia zake nyingi ni very interesting! kuna vitu vingi very shocking vya Mkapa ambavyo hakuna anayeandika, let me tell you, Mkapa anahojika anaingilika, You just need to be clever na kujua vitu vingi! Ni aghalabu kujua leo hii ni waandishi wangapi wanajisomea, wanajiendeleza, uandishi wa habari ni sawa kabisa na electronics engineering you need to learn everyday, na ndio maana mashirika makubwa kuna waandihi waliobbea kwenye uchumi, uhandisi, vita, saikolojia, n.k sisi hatuna! yet mkiambiwa nakasirika. Sasa nikiangalia Mkapa niliyetafuta habari zake kujua tabia yake ya karibu na kuona unavyosema aombea msamaha nabaki nacheka hapa huku nikipata coca yangu! mmeishiw hamumjui Mkapa! Nyerere alifichwa hakumjua Mkapa , sifa nyingi mbaya na nzuri anazo huyu mtu, kwa kifupi anajiamini sana , anasoma sana, anaelewa mambo mengi sana, ni mlevi sana ( nadhani walikutana na sumaye na kujenga urafiki kwenye Pombe), ana kiburi sana pia, majivuno, ana dharau, HANA KITU KINACHOITWA ujamaa!!! kwenye theory zake hili hana! ana kitu kinachoiwa fanya kazi ule! anaamini katika uwajibikaji na ukweli tu! ANA TABIA YA KUZIRA! na kibaya zaidi akishawaona nyie wajinga atajitahidi uendelee kuwa mjinga tu!!! amekuwa hivi tangu shuleni, ni mtu anayetoa msaada wa mwazo na mali kama ukimwomba, ukijifanya mjuaji hana time na wewe, MKAPA ni mtoto wa mjini!! Kutokana na chuki zake za ujamaa wengi wa marafiki zake wa karibu walimwona hafai au hana uzalendo kuliongoza taifa, mzee niliyekutana naye ambaye nilimuhoji swala la uzalendo, alisema tulijua tangu awali kuwa Mkapa yuko against na Nyerere! ila tulishangaa Nyerere kusema anataka Mkapa awe rais!!! mzee anasema walimweleza Nyerere kuhusu hilo , Nyerera akajibu kwa kufupi "najua"!!!!!!!!!!!! dunia tunayoenda anahitajika anayeijua hiyo dunia!! tabia ya Mkapa ya kuuza kila kitu ni hulka yake ya kutaka Tanzania iwe kama UK kwa miaka mitano!! ilikuwa tabia personal zaidi kuliko hali halisi, hasira zake juu ya failure ya migodi ndiyo iliyopelekea kumwambia hao watu wake wa karibu wauchukue Mgodi ili aone tatizo letu liko wapi. Kwa uchungu huu Mkapa akaanza kusoma vitabu vya migodi!!!! Ili kuthamini professionals uhandisi Mkapa huyu alibadilisha sana hali ya wahandisi wa taifa hili kuliko kipindi kingine, simply kwa sababu alikuwa anawapenda! I bet leo hii anatamani angekuwa engineer!! kuliko waandishi wa habari

Kibanda habari ziko waandishi mmelala jamani. ANY TIME media

Let me tell you loud and clear, Mkapa mnaye-mpaint vibaya hajachafuka kihivyo! tena kukaa kwake kimya ndio kumempa heshima kubwa tu, upepo wa Kikwete ulivyotulia, Mkapa akaanza kuinuka , pamoja na tuhuma zote zile Mkapa umaarufu wake kwa jamii ya waliosoma ni mkubwa mno! ugumu wa maisha na hali ya sasa ya nchi unamfanya avuke na kupendwa na hata walidhaniwa kumchukia, so kuomba kwako kuwa aombe msamaha hakusaidii lolote, AOMBE AU ASIOMBE MSAHAMA, AJIBU AU ASIJIBU TUHUMA reality inabaki kuwa Mkapa yuko juu sana ya Kikwete kwa mabli sana. Yote tisa kumi ni kuwa wote ni CCM so hawatisaidii kwa lolote!

Najua umezungumza kama mwanahabari na hizi ndizo chuki mlizokuwa nazo juu yake, wanahabari nchi hii mmefanya mazuri lakini kuna historia zinawaanika vibaya kuliko hiyo chungu ya Kesho ya Kikwete, ni wanahabri mliomuweka Kikwete madarakani na kuwachafua watu innocent kabisa msioweza kuthibitisha uchafu wao. Ni wanahabari mlianza nchi hii kwa kutosema baya lolote lile la Kikwete, 2005-2007 Ulikuwa ni mwaka wa kusemwa Mkapa, purposely ili mjikombea kwa Kikwete, mlipoona Mkapa hakgusiki na hamtafanya lolote kwani hali halisi inasema Kikwete ndiye mbovu zaid mkageuka woote na kuanza kuusema utawala wa Kikwete! Kikwete huyu alikuwa hagusiki, hasemwi juzi tu, leo hii mmebadilika sana. Mkapa huyu anaona haya! siyo mjinga! ilifikia hatua mpaka Kikwete anasema jamani msimseme mzee Mkapa!!!! mlijikomba mno kwa Kikwete na hili halisahauliki

Leo wanahabari Tanzani ni Mungu watu, habari zako haziandikwi mpaka mpewe fedha, wanahabari leo hii mnajua na mnasema ndiyo mmhimili wa nne wa serikali! then mkishajua hilo ndiyo nyie mnaoweza kusema fulani awe rais na fulani asiwe!

Ndiyo nyie mnaingilia uchaguzi wa ndani wa vyama!!!?? nyie ni wa kusikilizwa, mtu akiwa adui yenu basi mtamuandika mpaka basi

Kama niishivyo Kibanda haijalishi mnafanya nini ila sitasahau jinsi mlivyolihandle swala la Zito, I can write from A-Z , Kubenea ndiyo anajisifia kabisa kuwa nilimweleza Zito asigombee!

Ebu jisafisheni kwanza kwani mnanuka, taaluma yenu haina heshima tena, hata kama nyie ni baba wa watoto kumi na mume wa wake wawili, hamna heshima, hata kama mnapata. Ili kuthibitisha hilo, hilo la kukazania Mkapa aombe msamaha ni ishara ya tosha kuwa hujui taifa linataka nini!!! we need systems, waambieni hao cuf na chadema wawaze mseto zaidi. if we real mean to prosper

Piganieni system zibadilike, mkibaki kwenye majungu na kuanza kuwasema akina Kikwete na Mkapa certainly hamjui wakati mliopo! waandishi wa habari is superior and lively professionalism than any existing professionalism, you can change world, you can impact lives, you can move the nations the way you want, you just need to change and think and aim higher!

Mkapa hataomba msamaha hana kosa lolote lile! wenye makosa wako segerea. period! tusipokubali hili then tutaanze kujua udhaifu wetu uko wapi na tufanye nini! 'wezi' wa aina ya Mkapa siyo wa kuomba msamaha! siyo!

Kama swala ni kuomba msamaha basi Kibanda unatakiwa uombe msamaha! sana tu ulivyoivuruga chadema, zito, eventually kurudisha nyuma swal zima la demokrasia nchi hii, kwa tu kupandikizwa kuwa upinzani ni sehemu ya magomvi, yes, you did those kuuza magazeti! then what?? unajua tuko vitani n adui yetu ni CCM wana habari msipojua haya nani atawaeleza, hata vitaniaskari mwenzako akipigwa risasi unambeba unamweka begani safari inaendelea! hamuangalii movies?
 
Wantanzania ni vichwa vya Panzi kabisa! Its so surprising some people are trying to decorate BWM. Kwa lipi unaweza simama na kujigamba kwamba tulikuwa na uongozi awamu iliyopita! Au ni hizo biashara za maandazi mpaka ikulu! Actually nchi ilikuwa inavunwa! Mtu discent hawezi akawa na sura 2 tofauti! Ameuza nchi kwa bei ya kutupa 3% for christ's sake! Kajiuzia kiwira! Mfanyakazi amesota sana manake alikuwa anaongezewa 10000 tu! Tunasahau nini jinsi media na vyama vya upinzani vilivyokuwa vinanyanyasika! He was protective of his allies! He was intimidating!

Maufisadi mengi tumeyarithi toka kwake! Halafu mtu anamwita kiongozi mwenye heshima, makini blablalaaaaa!! It's so pathetic!

Kwa ujumla hatujapa Musa na Joshua katika nchi yetu atayewaongoza wana wa Israeli katika nchi ya Kanan! Ili tutoke hapa tulipo tunahitajika kiongozi mwenye wito wa kipekee, Uzalendo na uadilifu mkubwa! We need Charismatic leaders with bold intention kama akina Mahathir bin Mohamad wa Malaysia daima huhitaji kupekuwa record zao za utumishi uliotukuka!
 
Kaka kibanda sante sana kwa nakala hii nzuri ila kuna vitu nakubaliana na wewe na kuna vitu ninavinpinga tena sana

1. Mkapa hapaswi kuomba msamaha wowote ule kwa yeyote yule! hana kosa lolote lile alilolitenda mpaka sasa hivi unless mahakama iseme kuwa ni guilty, tukishindwa kufikia hatua hii then, tukubali kuwa systems zetu ni mbovu na hatuwezi kumuwajibisha kiongozi kwa namna au jinsi yeyote ile.Msamaha siyo suluhisho, sisi ni waajiri wa viongozi kama hatuna system zinazodhihirisha hivyo then we are done!

2. Kuna uozo mkubwa sana sana kwenye idara ya habari na nyie wengi wenu mnaingia kwenye hili kapu. Nyerere siku moja alisimama kwa hasira wakati mwandishi wa habari mmoja alikuwa anasema "nasikia" nasikia" nasikia" uozo huu hata Mkapa unayemsifia kuwa ni mwandishi mzuri ameusema mara nyingi, leo hii hamna chombo chochote cha kusimamia ethic zenu za uandishi, kuna taarifa hata mimi nisiye mtaaluma wa habari naona kinyaa kusoma! hamna utafiti, hamna professionalism, taaluma ya habari haikui! hakuna washawishi, huyo Mkapa pamoja na ugumu wake still kuna watu wanaweza kumwona na kumuhoji wakitaka! this ushawishi ni kiwango cha juu kabisa kudhihirisha wana habari wanaweza kupenya pasipo penyeka,Mkapa anajua udhaifu wenu! na anakaa kimya kabisa kwani bila kuongea hampati lolote.

Nimejaribu kumfuatilia Mkapa hata kutoka kwa mate wenzake aliosoma nao, kujua alikuwa na tabia gani shuleni,huko Marekani n.k kuna mzee nilikutana naye kwenye msiba mmoja na akanipa contact za watu fulani wa karibu na Mkapa. Visiona za Mkapa na tabia zake nyingi ni very interesting! kuna vitu vingi very shocking vya Mkapa ambavyo hakuna anayeandika, let me tell you, Mkapa anahojika anaingilika, You just need to be clever na kujua vitu vingi! Ni aghalabu kujua leo hii ni waandishi wangapi wanajisomea, wanajiendeleza, uandishi wa habari ni sawa kabisa na electronics engineering you need to learn everyday, na ndio maana mashirika makubwa kuna waandihi waliobbea kwenye uchumi, uhandisi, vita, saikolojia, n.k sisi hatuna! yet mkiambiwa nakasirika. Sasa nikiangalia Mkapa niliyetafuta habari zake kujua tabia yake ya karibu na kuona unavyosema aombea msamaha nabaki nacheka hapa huku nikipata coca yangu! mmeishiw hamumjui Mkapa! Nyerere alifichwa hakumjua Mkapa , sifa nyingi mbaya na nzuri anazo huyu mtu, kwa kifupi anajiamini sana , anasoma sana, anaelewa mambo mengi sana, ni mlevi sana ( nadhani walikutana na sumaye na kujenga urafiki kwenye Pombe), ana kiburi sana pia, majivuno, ana dharau, HANA KITU KINACHOITWA ujamaa!!! kwenye theory zake hili hana! ana kitu kinachoiwa fanya kazi ule! anaamini katika uwajibikaji na ukweli tu! ANA TABIA YA KUZIRA! na kibaya zaidi akishawaona nyie wajinga atajitahidi uendelee kuwa mjinga tu!!! amekuwa hivi tangu shuleni, ni mtu anayetoa msaada wa mwazo na mali kama ukimwomba, ukijifanya mjuaji hana time na wewe, MKAPA ni mtoto wa mjini!! Kutokana na chuki zake za ujamaa wengi wa marafiki zake wa karibu walimwona hafai au hana uzalendo kuliongoza taifa, mzee niliyekutana naye ambaye nilimuhoji swala la uzalendo, alisema tulijua tangu awali kuwa Mkapa yuko against na Nyerere! ila tulishangaa Nyerere kusema anataka Mkapa awe rais!!! mzee anasema walimweleza Nyerere kuhusu hilo , Nyerera akajibu kwa kufupi "najua"!!!!!!!!!!!! dunia tunayoenda anahitajika anayeijua hiyo dunia!! tabia ya Mkapa ya kuuza kila kitu ni hulka yake ya kutaka Tanzania iwe kama UK kwa miaka mitano!! ilikuwa tabia personal zaidi kuliko hali halisi, hasira zake juu ya failure ya migodi ndiyo iliyopelekea kumwambia hao watu wake wa karibu wauchukue Mgodi ili aone tatizo letu liko wapi. Kwa uchungu huu Mkapa akaanza kusoma vitabu vya migodi!!!! Ili kuthamini professionals uhandisi Mkapa huyu alibadilisha sana hali ya wahandisi wa taifa hili kuliko kipindi kingine, simply kwa sababu alikuwa anawapenda! I bet leo hii anatamani angekuwa engineer!! kuliko waandishi wa habari

Kibanda habari ziko waandishi mmelala jamani. ANY TIME media

Let me tell you loud and clear, Mkapa mnaye-mpaint vibaya hajachafuka kihivyo! tena kukaa kwake kimya ndio kumempa heshima kubwa tu, upepo wa Kikwete ulivyotulia, Mkapa akaanza kuinuka , pamoja na tuhuma zote zile Mkapa umaarufu wake kwa jamii ya waliosoma ni mkubwa mno! ugumu wa maisha na hali ya sasa ya nchi unamfanya avuke na kupendwa na hata walidhaniwa kumchukia, so kuomba kwako kuwa aombe msamaha hakusaidii lolote, AOMBE AU ASIOMBE MSAHAMA, AJIBU AU ASIJIBU TUHUMA reality inabaki kuwa Mkapa yuko juu sana ya Kikwete kwa mabli sana. Yote tisa kumi ni kuwa wote ni CCM so hawatisaidii kwa lolote!

Najua umezungumza kama mwanahabari na hizi ndizo chuki mlizokuwa nazo juu yake, wanahabari nchi hii mmefanya mazuri lakini kuna historia zinawaanika vibaya kuliko hiyo chungu ya Kesho ya Kikwete, ni wanahabri mliomuweka Kikwete madarakani na kuwachafua watu innocent kabisa msioweza kuthibitisha uchafu wao. Ni wanahabari mlianza nchi hii kwa kutosema baya lolote lile la Kikwete, 2005-2007 Ulikuwa ni mwaka wa kusemwa Mkapa, purposely ili mjikombea kwa Kikwete, mlipoona Mkapa hakgusiki na hamtafanya lolote kwani hali halisi inasema Kikwete ndiye mbovu zaid mkageuka woote na kuanza kuusema utawala wa Kikwete! Kikwete huyu alikuwa hagusiki, hasemwi juzi tu, leo hii mmebadilika sana. Mkapa huyu anaona haya! siyo mjinga! ilifikia hatua mpaka Kikwete anasema jamani msimseme mzee Mkapa!!!! mlijikomba mno kwa Kikwete na hili halisahauliki

Leo wanahabari Tanzani ni Mungu watu, habari zako haziandikwi mpaka mpewe fedha, wanahabari leo hii mnajua na mnasema ndiyo mmhimili wa nne wa serikali! then mkishajua hilo ndiyo nyie mnaoweza kusema fulani awe rais na fulani asiwe!

Ndiyo nyie mnaingilia uchaguzi wa ndani wa vyama!!!?? nyie ni wa kusikilizwa, mtu akiwa adui yenu basi mtamuandika mpaka basi

Kama niishivyo Kibanda haijalishi mnafanya nini ila sitasahau jinsi mlivyolihandle swala la Zito, I can write from A-Z , Kubenea ndiyo anajisifia kabisa kuwa nilimweleza Zito asigombee!

Ebu jisafisheni kwanza kwani mnanuka, taaluma yenu haina heshima tena, hata kama nyie ni baba wa watoto kumi na mume wa wake wawili, hamna heshima, hata kama mnapata. Ili kuthibitisha hilo, hilo la kukazania Mkapa aombe msamaha ni ishara ya tosha kuwa hujui taifa linataka nini!!! we need systems, waambieni hao cuf na chadema wawaze mseto zaidi. if we real mean to prosper

Piganieni system zibadilike, mkibaki kwenye majungu na kuanza kuwasema akina Kikwete na Mkapa certainly hamjui wakati mliopo! waandishi wa habari is superior and lively professionalism than any existing professionalism, you can change world, you can impact lives, you can move the nations the way you want, you just need to change and think and aim higher!

Mkapa hataomba msamaha hana kosa lolote lile! wenye makosa wako segerea. period! tusipokubali hili then tutaanze kujua udhaifu wetu uko wapi na tufanye nini! 'wezi' wa aina ya Mkapa siyo wa kuomba msamaha! siyo!

Kama swala ni kuomba msamaha basi Kibanda unatakiwa uombe msamaha! sana tu ulivyoivuruga chadema, zito, eventually kurudisha nyuma swal zima la demokrasia nchi hii, kwa tu kupandikizwa kuwa upinzani ni sehemu ya magomvi, yes, you did those kuuza magazeti! then what?? unajua tuko vitani n adui yetu ni CCM wana habari msipojua haya nani atawaeleza, hata vitaniaskari mwenzako akipigwa risasi unambeba unamweka begani safari inaendelea! hamuangalii movies?
Waberoya

Mbona umeandika kama kasuku umechanganya mambo mengi sana hayaeleweki mengi ni irrelevant na topic yenyewe yako very personal, inavyoonekana hukusoma swali kama umesoma hukulielewa au hukumwelewa Kibanda alichokusudia. Kibanda ameelezea mafanikio ya Mkapa na udhaifu wa kutoomba msamaha kwa makosa aliyotenda wakati wa utawala wake.

Binafsi sijakuelewa kama una support au unapinga zaidi ya kusema Mkapa ni mlevi ana hasira anajisomea sana anatujua sisi ni wajinga nk sasa hayo yanauhusiano gani na hoja Mengine umesema waandishi wananuka rushwa hata kama wananuka siyo mahala pake, unaposema Kibanda anadumaza demokrasia this is more personal, mara Zitto mara Chadema hizi nazo zinaingiaje kwenye hoja.

Baada ya mwenyewe kumponda Mkapa mwisho ukasema Mkapa hana kosa, jaribu kuwa focused na unachotarajia kukiandika body of information isitofautiane na conclusion, ni ushauri tu.
 
Kibanda

Pamoja na yote aliyoyafanya Mkapa faida yake ilitakiwa ionekane kwenye maendeleo ya wananchi ungekuja pia na takwimu za shule ngapi zilijengwa kipindi chake 1995-2004 tungekuelewa kusema tu dhahabu iliongezeka haisaidii mikataba yenyewe inafahamika watanzania tuliachiwa 3% ya faida baada ya kutoa mtaji ambao ulikuwa haulipiwi kodi kwa miaka mitano.

Kama unavyosema pato la taifa liliongezeka kutoka asilimia 3.6 - 6.7 hiyo ziada ilikuwa ikienda wapi angalau ingejenga university hata moja basi huo uwanja wa taifa ni mkopo kutoka China tutaulipa hadi watoto wetu wataulipa. Pamoja na mazuri mchanganyiko na mabaya yote lakini doa ambalo hatalisahau ni la kufanya biashara wakati akiwa ikulu nafikiri hata yeye analijutuia hilo.
 
Waberoya

Mbona umeandika kama kasuku umechanganya mambo mengi sana hayaeleweki mengi ni irrelevant na topic yenyewe yako very personal, inavyoonekana hukusoma swali kama umesoma hukulielewa au hukumwelewa Kibanda alichokusudia. Kibanda ameelezea mafanikio ya Mkapa na udhaifu wa kutoomba msamaha kwa makosa aliyotenda wakati wa utawala wake.

Binafsi sijakuelewa kama una support au unapinga zaidi ya kusema Mkapa ni mlevi ana hasira anajisomea sana anatujua sisi ni wajinga nk sasa hayo yanauhusiano gani na hoja Mengine umesema waandishi wananuka rushwa hata kama wananuka siyo mahala pake, unaposema Kibanda anadumaza demokrasia this is more personal, mara Zitto mara Chadema hizi nazo zinaingiaje kwenye hoja.

Baada ya mwenyewe kumponda Mkapa mwisho ukasema Mkapa hana kosa, jaribu kuwa focused na unachotarajia kukiandika body of information isitofautiane na conclusion, ni ushauri tu.

Nadhani tumetofautiana kimawazo na mtazamo, mimi naandika general sina upande wowote mkuu wangu, wewe kama ushachukua side kama kawa hutanielewa na sijaandika lazima unielewe wewe!, unaweza ukiona jina la waberoya ukaruka post haina tatizo kabisa. Nimeeleza MAkapa ninavyo mfahamu, nimeeleza uhsuinao wake na waandishi wa habari , jnimeeleza anaamini nini, nimeeleza kumpa challenge Kibanda kuwa wanatakiwa kumjua zaidi ,adui ' yao kuliko kubaki kuandika na kusema aombe msamaha! Nashukuru pia kwa ngau kuweza kumuelewa kasuku!

Kuhusu personal hilo liko wazi Kibanda hana usafi wa kuzungumzia mstakabali wa hili taifa!, hana usafi wa kuzungumia upinzani wala ufisadi! ndio maana nimemweleza anachopaswa aelezwe, uwezo wao wa kitaaluma na huwa wanafanya nini! Sasa mtu alimweka Kikwete madarakani leo hii anakuwekea hiyo title na wewe Luteni unaona ipite tu bila kuelezwa ukweli!

Sentensi ipi inayoonyesha kuwa nimesema Mkapa hana kosa? na je mtu akiwa na kosa hastahili kusifiwa kama ana mazuri?
 
Kibanda

Pamoja na yote aliyoyafanya Mkapa faida yake ilitakiwa ionekane kwenye maendeleo ya wananchi ungekuja pia na takwimu za shule ngapi zilijengwa kipindi chake 1995-2004 tungekuelewa kusema tu dhahabu iliongezeka haisaidii mikataba yenyewe inafahamika watanzania tuliachiwa 3% ya faida baada ya kutoa mtaji ambao ulikuwa haulipiwi kodi kwa miaka mitano.

Kama unavyosema pato la taifa liliongezeka kutoka asilimia 3.6 - 6.7 hiyo ziada ilikuwa ikienda wapi angalau ingejenga university hata moja basi huo uwanja wa taifa ni mkopo kutoka China tutaulipa hadi watoto wetu wataulipa. Pamoja na mazuri mchanganyiko na mabaya yote lakini doa ambalo hatalisahau ni la kufanya biashara wakati akiwa ikulu nafikiri hata yeye analijutuia hilo.

So ulichonifundisha ni nini na wewe umeandika nini kasuku mdogo?
 
Asanteni wachangiaji wote wa thread hii.Yote haya yanaonyesha kwa nini viongozi wengi hawapendi kuachia madaraka, na kama inabidi, basi huwaachi wananwe. Tanzania bado hatujafikia hapo, lakini badala yake utawala wa CCM unafidia kasoro hiyo kwa kuwa na kile kinachoitwa 'kulindana kwa hali ya juu kabisa' baina ya viongozi. Wanaiba ile mbaya na utawala ujao hukaa kimya. Hivyo hata hiyo 'kesho ya JK' ingawa nakubali itakuwa chungu zaidi ya ile ya Mkapa, lakini naye atapeta tu kama anavyoonekana kupeta Mkapa hivi sasa.

Lakini naogopa iko siko haya yote yataisha tu, tena kwa kishindo kikubwa na pengine madhara m akubwa. Kumbukeni yaliyotokea Ghana m wishoni mwa miaka ya 70 Rawlings aliposhika nchi -- aliwafyeka viongozi wote waliokuwa wanaiba, wanaachiliana madaraka (au kupinduana) na kujilinda madhambi yao!

Pamoja na kusema haya, naomba Mungu hapa kwetu mabadiliko yasije kwa njia hiyo.
 
Wantanzania ni vichwa vya Panzi kabisa! Its so surprising some people are trying to decorate BWM. Kwa lipi unaweza simama na kujigamba kwamba tulikuwa na uongozi awamu iliyopita! Au ni hizo biashara za maandazi mpaka ikulu! Actually nchi ilikuwa inavunwa! Mtu discent hawezi akawa na sura 2 tofauti! Ameuza nchi kwa bei ya kutupa 3% for christ's sake! Kajiuzia kiwira! Mfanyakazi amesota sana manake alikuwa anaongezewa 10000 tu! Tunasahau nini jinsi media na vyama vya upinzani vilivyokuwa vinanyanyasika! He was protective of his allies! He was intimidating!
Maufisadi mengi tumeyarithi toka kwake! Halafu mtu anamwita kiongozi mwenye heshima, makini blablalaaaaa!! It's so pathetic!
Kwa ujumla hatujapa Musa na Joshua katika nchi yetu atayewaongoza wana wa Israeli katika nchi ya Kanan! Ili tutoke hapa tulipo tunahitajika kiongozi mwenye wito wa kipekee, Uzalendo na uadilifu mkubwa! We need Charismatic leaders with bold intention kama akina Mahathir bin Mohamad wa Malaysia daima huhitaji kupekuwa record zao za utumishi uliotukuka!


it is boldly true kwamba kila mtu ana mapaungufu yake , ila with any basis huwezi kumlinganisha BWM na JK lazima tuwe wakweli kuwea mkapa amefanya mengi kwa Taifa hili angalia miradi yote mikubwa iliyozinduliwa na mkapa kama barabara, madaraja na viwanja mbalimabali.
BWM alijipatia heshima kubwa kitaifa na kimataifa, MSEMINARI huyu alionesha njia bora ya uongozi kwa kuweka nizamu ya matumizi ya serikali daima mkapa ataendelea kuwa the second ever best president aliyewahi kuexist hapa Tanzania baada ya mwalimu, long live mkapa achana na vijembe na huyo mkwere na wapambe wake.
 
Yale yale kusifiana bila sababu...mkapa amefanya alichofanya kwasababu aliomba kura kufanya hicho alichofanya ...kizuri...ni wajibu wake period! wananchi tumemfanyia mengi zaidi, tumemlipa timely and reasonably kila kitu halipii chochote yaani anakula na kulala bure period!

Besides, amefanya mabaya kupita rais yeyote katika historia ya nchi yetu ....mikataba mibovu, ujeuri, mauaji ya wananchi (mwembechai) (pemba), kuwatia nguvuni wapinzani, list goes on...mshe.....nzi tu hana lolote ananitia kichefuchefu....

Article yako unaongelea upupu na utumbo uleule wa kila siku kusifiana kwa ...
 
Kaka kibanda sante sana kwa nakala hii nzuri ila kuna vitu nakubaliana na wewe na kuna vitu ninavinpinga tena sana

1. Mkapa hapaswi kuomba msamaha wowote ule kwa yeyote yule! hana kosa lolote lile alilolitenda mpaka sasa hivi unless mahakama iseme kuwa ni guilty, tukishindwa kufikia hatua hii then, tukubali kuwa systems zetu ni mbovu na hatuwezi kumuwajibisha kiongozi kwa namna au jinsi yeyote ile.Msamaha siyo suluhisho, sisi ni waajiri wa viongozi kama hatuna system zinazodhihirisha hivyo then we are done!
2. Kuna uozo mkubwa sana sana kwenye idara ya habari na nyie wengi wenu mnaingia kwenye hili kapu. Nyerere siku moja alisimama kwa hasira wakati mwandishi wa habari mmoja alikuwa anasema "nasikia" nasikia" nasikia" uozo huu hata Mkapa unayemsifia kuwa ni mwandishi mzuri ameusema mara nyingi, leo hii hamna chombo chochote cha kusimamia ethic zenu za uandishi, kuna taarifa hata mimi nisiye mtaaluma wa habari naona kinyaa kusoma! hamna utafiti, hamna professionalism, taaluma ya habari haikui! hakuna washawishi, huyo Mkapa pamoja na ugumu wake still kuna watu wanaweza kumwona na kumuhoji wakitaka! this ushawishi ni kiwango cha juu kabisa kudhihirisha wana habari wanaweza kupenya pasipo penyeka,Mkapa anajua udhaifu wenu! na anakaa kimya kabisa kwani bila kuongea hampati lolote.

Nimejaribu kumfuatilia Mkapa hata kutoka kwa mate wenzake aliosoma nao, kujua alikuwa na tabia gani shuleni,huko Marekani n.k kuna mzee nilikutana naye kwenye msiba mmoja na akanipa contact za watu fulani wa karibu na Mkapa. Visiona za Mkapa na tabia zake nyingi ni very interesting! kuna vitu vingi very shocking vya Mkapa ambavyo hakuna anayeandika, let me tell you, Mkapa anahojika anaingilika, You just need to be clever na kujua vitu vingi! Ni aghalabu kujua leo hii ni waandishi wangapi wanajisomea, wanajiendeleza, uandishi wa habari ni sawa kabisa na electronics engineering you need to learn everyday, na ndio maana mashirika makubwa kuna waandihi waliobbea kwenye uchumi, uhandisi, vita, saikolojia, n.k sisi hatuna! yet mkiambiwa nakasirika. Sasa nikiangalia Mkapa niliyetafuta habari zake kujua tabia yake ya karibu na kuona unavyosema aombea msamaha nabaki nacheka hapa huku nikipata coca yangu! mmeishiw hamumjui Mkapa! Nyerere alifichwa hakumjua Mkapa , sifa nyingi mbaya na nzuri anazo huyu mtu, kwa kifupi anajiamini sana , anasoma sana, anaelewa mambo mengi sana, ni mlevi sana ( nadhani walikutana na sumaye na kujenga urafiki kwenye Pombe), ana kiburi sana pia, majivuno, ana dharau, HANA KITU KINACHOITWA ujamaa!!! kwenye theory zake hili hana! ana kitu kinachoiwa fanya kazi ule! anaamini katika uwajibikaji na ukweli tu! ANA TABIA YA KUZIRA! na kibaya zaidi akishawaona nyie wajinga atajitahidi uendelee kuwa mjinga tu!!! amekuwa hivi tangu shuleni, ni mtu anayetoa msaada wa mwazo na mali kama ukimwomba, ukijifanya mjuaji hana time na wewe, MKAPA ni mtoto wa mjini!! Kutokana na chuki zake za ujamaa wengi wa marafiki zake wa karibu walimwona hafai au hana uzalendo kuliongoza taifa, mzee niliyekutana naye ambaye nilimuhoji swala la uzalendo, alisema tulijua tangu awali kuwa Mkapa yuko against na Nyerere! ila tulishangaa Nyerere kusema anataka Mkapa awe rais!!! mzee anasema walimweleza Nyerere kuhusu hilo , Nyerera akajibu kwa kufupi "najua"!!!!!!!!!!!! dunia tunayoenda anahitajika anayeijua hiyo dunia!! tabia ya Mkapa ya kuuza kila kitu ni hulka yake ya kutaka Tanzania iwe kama UK kwa miaka mitano!! ilikuwa tabia personal zaidi kuliko hali halisi, hasira zake juu ya failure ya migodi ndiyo iliyopelekea kumwambia hao watu wake wa karibu wauchukue Mgodi ili aone tatizo letu liko wapi. Kwa uchungu huu Mkapa akaanza kusoma vitabu vya migodi!!!! Ili kuthamini professionals uhandisi Mkapa huyu alibadilisha sana hali ya wahandisi wa taifa hili kuliko kipindi kingine, simply kwa sababu alikuwa anawapenda! I bet leo hii anatamani angekuwa engineer!! kuliko waandishi wa habari

Kibanda habari ziko waandishi mmelala jamani. ANY TIME media

Let me tell you loud and clear, Mkapa mnaye-mpaint vibaya hajachafuka kihivyo! tena kukaa kwake kimya ndio kumempa heshima kubwa tu, upepo wa Kikwete ulivyotulia, Mkapa akaanza kuinuka , pamoja na tuhuma zote zile Mkapa umaarufu wake kwa jamii ya waliosoma ni mkubwa mno! ugumu wa maisha na hali ya sasa ya nchi unamfanya avuke na kupendwa na hata walidhaniwa kumchukia, so kuomba kwako kuwa aombe msamaha hakusaidii lolote, AOMBE AU ASIOMBE MSAHAMA, AJIBU AU ASIJIBU TUHUMA reality inabaki kuwa Mkapa yuko juu sana ya Kikwete kwa mabli sana. Yote tisa kumi ni kuwa wote ni CCM so hawatisaidii kwa lolote!

Najua umezungumza kama mwanahabari na hizi ndizo chuki mlizokuwa nazo juu yake, wanahabari nchi hii mmefanya mazuri lakini kuna historia zinawaanika vibaya kuliko hiyo chungu ya Kesho ya Kikwete, ni wanahabri mliomuweka Kikwete madarakani na kuwachafua watu innocent kabisa msioweza kuthibitisha uchafu wao. Ni wanahabari mlianza nchi hii kwa kutosema baya lolote lile la Kikwete, 2005-2007 Ulikuwa ni mwaka wa kusemwa Mkapa, purposely ili mjikombea kwa Kikwete, mlipoona Mkapa hakgusiki na hamtafanya lolote kwani hali halisi inasema Kikwete ndiye mbovu zaid mkageuka woote na kuanza kuusema utawala wa Kikwete! Kikwete huyu alikuwa hagusiki, hasemwi juzi tu, leo hii mmebadilika sana. Mkapa huyu anaona haya! siyo mjinga! ilifikia hatua mpaka Kikwete anasema jamani msimseme mzee Mkapa!!!! mlijikomba mno kwa Kikwete na hili halisahauliki

Leo wanahabari Tanzani ni Mungu watu, habari zako haziandikwi mpaka mpewe fedha, wanahabari leo hii mnajua na mnasema ndiyo mmhimili wa nne wa serikali! then mkishajua hilo ndiyo nyie mnaoweza kusema fulani awe rais na fulani asiwe!

Ndiyo nyie mnaingilia uchaguzi wa ndani wa vyama!!!?? nyie ni wa kusikilizwa, mtu akiwa adui yenu basi mtamuandika mpaka basi

Kama niishivyo Kibanda haijalishi mnafanya nini ila sitasahau jinsi mlivyolihandle swala la Zito, I can write from A-Z , Kubenea ndiyo anajisifia kabisa kuwa nilimweleza Zito asigombee!

Ebu jisafisheni kwanza kwani mnanuka, taaluma yenu haina heshima tena, hata kama nyie ni baba wa watoto kumi na mume wa wake wawili, hamna heshima, hata kama mnapata. Ili kuthibitisha hilo, hilo la kukazania Mkapa aombe msamaha ni ishara ya tosha kuwa hujui taifa linataka nini!!! we need systems, waambieni hao cuf na chadema wawaze mseto zaidi. if we real mean to prosper

Piganieni system zibadilike, mkibaki kwenye majungu na kuanza kuwasema akina Kikwete na Mkapa certainly hamjui wakati mliopo! waandishi wa habari is superior and lively professionalism than any existing professionalism, you can change world, you can impact lives, you can move the nations the way you want, you just need to change and think and aim higher!

Mkapa hataomba msamaha hana kosa lolote lile! wenye makosa wako segerea. period! tusipokubali hili then tutaanze kujua udhaifu wetu uko wapi na tufanye nini! 'wezi' wa aina ya Mkapa siyo wa kuomba msamaha! siyo!

Kama swala ni kuomba msamaha basi Kibanda unatakiwa uombe msamaha! sana tu ulivyoivuruga chadema, zito, eventually kurudisha nyuma swal zima la demokrasia nchi hii, kwa tu kupandikizwa kuwa upinzani ni sehemu ya magomvi, yes, you did those kuuza magazeti! then what?? unajua tuko vitani n adui yetu ni CCM wana habari msipojua haya nani atawaeleza, hata vitaniaskari mwenzako akipigwa risasi unambeba unamweka begani safari inaendelea! hamuangalii movies?

Mkuu Waberoya, umeandika mengi yapo ya kukubaliana na wewe na yapo ya kupinga.

Mkapa anapaswa kuomba msamaha maana yapo makosa aliyoyafanya akiwa Rais. Kuomba msamaha ni uungwana. Kwa hoja za Kibanda Mkapa kwa namna moja ama nyingine amewakosea wananchi walimuamini na kumpa dhamana ya kuwaongoza lakini akawageuka akaweka maadili pembeni, akapindisha mambo, akataka kujitajirisha kwa kutumia nafasi aliyopewa na wananchi. Jeuri ya kudhani kwamba hana sababu ya kuomba msamaha ndiyo inayofanya akae kimya na kuwacheka wananchi kwa mbali!

Kudai kwamba lazima awe proven guilty na Mahakama, yapo makosa mengine ya kimaadili ambayo si lazima yafikishwe Mahakamani hukumu iko kwa wananchi wenyewe. Kibanda ameeleza kwamba Mwalimu aliwahi kuomba radhi kwa makosa yaliyotendwa ama aliyoyatenda katika uongozi wake, na alifanya hivyo kwa nia njema na bila shaka alikuwa anaweka mfano wa kuigwa na viongozi watakaofuata. Kwa nini Mkapa ashindwe kufanya hivyo? Pia ni kiongozi gani ambaye amewahi kuwa proven guilty na kupelekwa Segerea? Tunaona wanaokwenda Segerea ni wananchi wanyonge ambao hatia zao wala hazileti hasara iwa taifa kama hasara inayoletwa na viongozi kwa maanuzi yao mabaya na vitendo vyao vya kifisadi.

Nakubaliana na wewe kabisa kwamba Chama cha Mapinduzi hususan Serikali yake vinahitaji kuhukumiwa ipasavyo na kuchukuliwa hatua na wananchi. Nakubaliana pia kwamba waandishi wa habari wanachangia kwa kiasi kikubwa sana kuliangamiza Taifa hili kwa waandishi hao kutumikia mabwana wengine badala ya kuwatumikia wananchi na Taifa kwa ujumla kwa ukamilifu na kwa uadilifu unaostahili. Waandishi wako tayari kuvunja maadili na kuwasaliti wananchi na Taifa kwa ajili ya vijisenti wanavyopewa na viongozi corrupt.
 
Mkuu Waberoya, umeandika mengi yapo ya kukubaliana na wewe na yapo ya kupinga.

Mkapa anapaswa kuomba msamaha maana yapo makosa aliyoyafanya akiwa Rais. Kuomba msamaha ni uungwana. Kwa hoja za Kibanda Mkapa kwa namna moja ama nyingine amewakosea wananchi walimuamini na kumpa dhamana ya kuwaongoza lakini akawageuka akaweka maadili pembeni, akapindisha mambo, akataka kujitajirisha kwa kutumia nafasi aliyopewa na wananchi. Jeuri ya kudhani kwamba hana sababu ya kuomba msamaha ndiyo inayofanya akae kimya na kuwacheka wananchi kwa mbali!

Kudai kwamba lazima awe proven guilty na Mahakama, yapo makosa mengine ya kimaadili ambayo si lazima yafikishwe Mahakamani hukumu iko kwa wananchi wenyewe. Kibanda ameeleza kwamba Mwalimu aliwahi kuomba radhi kwa makosa yaliyotendwa ama aliyoyatenda katika uongozi wake, na alifanya hivyo kwa nia njema na bila shaka alikuwa anaweka mfano wa kuigwa na viongozi watakaofuata. Kwa nini Mkapa ashindwe kufanya hivyo? Pia ni kiongozi gani ambaye amewahi kuwa proven guilty na kupelekwa Segerea? Tunaona wanaokwenda Segerea ni wananchi wanyonge ambao hatia zao wala hazileti hasara iwa taifa kama hasara inayoletwa na viongozi kwa maanuzi yao mabaya na vitendo vyao vya kifisadi.

Nakubaliana na wewe kabisa kwamba Chama cha Mapinduzi hususan Serikali yake vinahitaji kuhukumiwa ipasavyo na kuchukuliwa hatua na wananchi. Nakubaliana pia kwamba waandishi wa habari wanachangia kwa kiasi kikubwa sana kuliangamiza Taifa hili kwa waandishi hao kutumikia mabwana wengine badala ya kuwatumikia wananchi na Taifa kwa ujumla kwa ukamilifu na kwa uadilifu unaostahili. Waandishi wako tayari kuvunja maadili na kuwasaliti wananchi na Taifa kwa ajili ya vijisenti wanavyopewa na viongozi corrupt.

Asante BoraMaisha, kwa hiyo tukubali kuwa hatuna mifumo mizuri ya kuweza kuwawajibisha viongozi. Kwa hiyo ngivu zetu tuelekeze kubailisha hiyo mifumo, tutatawaliwa na akina Idd Amin hum na akina Mobutu, Mugabe Gadafi , Hitler at the end wanaomba msamaha? Kwa kweli Bora maisha wananchi tukikubali kwa nguvu moja kuwa katiba ibadilike.

Issue za mabadiliko ya katiba huwa hazizungumzwi kabisa na vyama vya upinzani, maana wameshasema kuwa hawawezi na hivyo kufuta upinzani wote. Kibanda analijua hivyo, so is nakala ni wishful thinking na zimekaa kuuza magazeti lakini hazina msaada wowote ule, i repeat wowote ule kwa Tanzania, ni nakala bora siku ziende magazeti yauzwe.

Rais anatakiwa awe rais, siyo ateue jaji mkuu, CAG, director wa Pccb, kamishana wa polisi, mkuu wa majeshi, mawaziri, n.k yaani ukiondoa bunge tu ambalo spika anachaguliwa na wabunge wengine wote waliobaki hakuna anayeweza kumuuliza rais kwa lolote lile. Rais ni mfalme nchi hii, na likely Kikwete akiondoka atafanya ya kufanya, kwa sababu hatutaki kugusa mzizi wa tatizo, tutasema aombe msamaha, that statement is good to be said by Padre! siyo mwandishi.

Tukianza na rais, then watakujaakina RA, EL, Chenge, mpaka katibu kata, kuwa kama ameifisadi nchi waombe msamaha!

asante
 
Back
Top Bottom