Kesho April 26 ni Sikukuu ya Maadhimisho ya Muungano

Wabogojo

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
354
87
Wanajamvi, kesho ni siku ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na ninadhani maadhimisho yaha yatafanyika hapa hapa BANDARI SALAMA na Mkuu wetu wa nchi kama ilivyo ada anatazamiwa kuwa ndiye atakaye kuwa MGENI RASMI. Ninatabiri kuwa hapo kesho Mkulu wetu atatoka na kile ambacho watz hatutaamini na kuachwa vinywa wazi huku wengi wakifurahi na baadhi kusononeka.

Je wewe unategemea ataongea nini katika sherehe hizi wakati wananchi tumeachwa solemba kwenye ombwe la ufisadi uliokithiri wa vilanja wetu, CCM ikilegalega wakati CDM ikipaa kwa kasi ya Chopa, wengine wakiupinga Muungano huu kwa nguvu zao zote na lingine kubwa zaidi ni hili la mchakato wa kupata KATIBA MPYA ya JMT huku BABA akikataza watoto wake kuujadili muungano kwenye huo mchakato.

Nawasilisha ................
 
Wanajamvi, kesho ni siku ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na ninadhani maadhimisho yaha yatafanyika hapa hapa BANDARI SALAMA na Mkuu wetu wa nchi kama ilivyo ada anatazamiwa kuwa ndiye atakaye kuwa MGENI RASMI. Ninatabiri kuwa hapo kesho Mkulu wetu atatoka na kile ambacho watz hatutaamini na kuachwa vinywa wazi huku wengi wakifurahi na baadhi kusononeka.

Je wewe unategemea ataongea nini katika sherehe hizi wakati wananchi tumeachwa solemba kwenye ombwe la ufisadi uliokithiri wa vilanja wetu, CCM ikilegalega wakati CDM ikipaa kwa kasi ya Chopa, wengine wakiupinga Muungano huu kwa nguvu zao zote na lingine kubwa zaidi ni hili la mchakato wa kupata KATIBA MPYA ya JMT huku BABA akikataza watoto wake kuujadili muungano kwenye huo mchakato.

Nawasilisha ................

Hizi sherehe zinatafuna tu pesa za walipa kodi na tusishangae wakija kusema imetumika bilion 2 na mapointi kibao.Kwa nini tarehe hizi za kuungana kwa Tanganyika na Zanzibar zisibaki ktk kumbukumbu(historia)tukaachana na sherehe zisizokuwa na umuhimu wowote?.Wananchi hawana maji,umeme,zahanati,hospitali zenye kukidhi haja,elimu yetu ni mbovu matatizo kibao halafu nchi inakuja kutuambia sherehe za muungano!!?.Mawaziri wamechukua chao na wataendelea kuchukua chao hakuna Wa kuwasemesha Serikali nayo inazidi kutafuna tu,waendelee kutafuna tu ipo siku tutawang'oa meno.
 
HIVI DAWA YA WALE WANANCHI WA ZANZIBAR wanaoandamana kupinga muungano ni kuwatimua kwa mabomu ya gesi?
 
Mara nyingi huazimishwa bila hotuba ya yoyote ile,but Dr Jk anapaswa kusema kitu hasa uongozi na matakwa ya wazenji kuhusu muungano,kiukweli nashangazwa kwenye kura ya maoni ya kuanzisha vyama vingi maoni ya wachache yalishinda ya wengi lakini kwenye hili la muungano maoni ya wachache hayapewi nafasi.
 
Mbona sioni matunda ya 48yrs ya huu muungano sababu haswa ya Muungano ni ili nini? Au kuwa watu wa Zanzibar Umeme kisha kuwagandamiza?
 
Kwa jinsi alivyo na utamaduni wa kutoa majibu sehemu isiyo rasmi sintashangaa kesho akatoa hatma ya hao tunao wasubiria kwa hamu wajiuzulu(mawaziri wezi)
 
Mnamo mwaka 2011 nilikuwa nikisikia kauli za baadhi ya viongozi wakidanganya umma kwamba watanzania tunasherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania huu ulikuwa uongo kwan kipindi hicho ndio tulikuwa tunatimiza miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika. Hivyo siku ya kesho tunatimiza miaka 48 ya Tanzania. Tanzania ilipatikana mnamo 6 April 1964 baada ya muungano wa Tanganyika (1961) na Zanzibar (1964 Nichukue nafasi hii kuwapongeza wanaounga mkono muungano kufikisha miaka 48 na kuwapa pole wanaonungunika kuhusu Muunga
 
Back
Top Bottom