Deodat
JF-Expert Member
- Sep 18, 2008
- 1,274
- 272
katika kumbukumbu zangu mimi Harusi mtu ulikuwa unafanya kwa uwezo wako... unaita marafiki zako na ndugu mnasherekea hicho kilichopo.
Sasa mtu anakuletea Kadi tena ina kiwango.... na Watu hawakuchangii sababu wanakupenda ni kama wanakukopesha kwamba na wao siku yao ikifika na wewe utachanga...
Michango Inafika mpaka mamilioni ya pesa.... watu wanakuja wanakunywa na kula.. wewe na mwenza wako mnaenda kuanza maisha (wengine hata nyumba hamna) na deni la watu kama mia moja waliokuchangia ambao na wewe inabidi uwachangie....
HIVI NI MIMI TU NINAYEONA KUWA HUU NI UPUUZI NA UJINGA... AU KUNA YEYOTE ANAYENIUNGA MKONO.....
Naunga mkono hoja 100%. Wengi ukiwauliza watakwambia hawapendi hako ka-utamaduni lakini hawana uwezo wa ku-resist kwakuwa jamii ndipo ilipofikia. Kama unavyosema, mtu unajikuta una madeni yasiyo rasmi lukuki, njia nzuri ya kuyakwepa hayo "madeni" ya kuchangia harusi inabidi na wewe ujiepusha kwa namna yoyote kuchangisha watu. Mie nina mpango nikifunga ndoa nitatenga kana mil. 2 hivi, na sitachangisha mtu, watakunywa chai na snacks na sherehe itaishia hapo.