Kero ya trafiki polisi

Kintiku

JF-Expert Member
Feb 3, 2011
617
319
nipo hap ubungo mataa zaidi ya dk 30, kisa ni askari kaamua kuongoza magari. kuna haja gani ya kuongoza magari asby yote hii



askari
 
nipo hap ubungo mataa zaidi ya dk 30, kisa ni askari kaamua kuongoza magari. kuna haja gani ya kuongoza magari asby yote hii askari

asubuhi DSM kuna foleni kali, kwa taarifa yako hata askari hapendi kuvuta moshi wa mkweche wako, lakini kwa kuwa ni mpango kazi ili wanaowahi kwenda kazini wawahi, analazimika kutimimiza maelekezo ya bosi wake.

kwa vile umechelewa ndo unalalama? kuna wengine wengi wanafurahi kwani atleast magari yanasogea
 
HII sijui ilitokea lini,but ni tz
41852_345124072171346_345097752173978_1260_1316_t.jpg
 
Siku kuu inakuja, lazima wazuge ili ukiwa na haraka, akuchomoe10,000. Lakini nawasihi acheni kutoa rushwa kwa ma-trafic, tuwe wepesi wa kulipa faini ili tuache kuwanenepesha polisi, ili watambue serikali yao haiwajali
 
Siku kuu inakuja, lazima wazuge ili ukiwa na haraka, akuchomoe10,000. Lakini nawasihi acheni kutoa rushwa kwa ma-trafic, tuwe wepesi wa kulipa faini ili tuache kuwanenepesha polisi, ili watambue serikali yao haiwajali

Mimi ni mmoja kati ya wachukia rushwa na niko tayari kuchelewa safari zangu ili tu nifate taratibu na nisilipe rushwa...(On a very serious note, SINA UHAKIKA KAMA VILE VITABU VYAO VYA BARABARANI NI HALALI, na RISITI TUNAZOPEWA NI ZA KWELI NA HELA INAINGIZIA PATO TAIFA, Ndio maana nimeopt kutake a long route) Mara Nyingi Traffic akikuona una msimamo wa kukubali kosa na kuwa tayari kutoa ushirikiano wa kwenda kituoni, Huwa wanakuachia....Ni wiki iliyopita tu nilikamatwa Kingolwira kosa ni kwenda 57 sehemu ya 50, nikakubali kosa na kuwaomba waniachie niendelee na safari, wakataka fine nikatoa jibu rahisi kabisa, SINA PESA HAPA... wakataka twende kituoni nikalale hadi Jumatatu nikajibu shitaka mahakamani nikakubali (nikijua kabisa nikifikishwa kituoni sitalala kwasababu ntawaomba waniachie na Police wa kituoni huwa wanaachia tu watu kwa mambo kama hayo)... Nikakaa pale kama dakika 40 baadae wakanipa leseni yangu nikaondoka, Sasa Ningekuwa na moyo wa rushwa pale ningejifanya nataka kuwahi nikawaachia nusu ya fine (15,000) Nikaondoka... Patience saved my doe...

Tusiwe wepesi wa kujifanya tuna haraka utadhani tunawahi wagonjwa tuwafanyie operation wasife, Utasikia mtu ooh watanichelewesha. kumbe anawahi bar au nyumbani kwake... Kwani unakoenda kunahama??

Traffic ni Binadamu kama sisi, wana aibu, huzuni na huruma kama watu wengine... Ukiwa na Kauli nzuri hata siku moja hawatakusumbua.
 
Mimi ni mmoja kati ya wachukia rushwa na niko tayari kuchelewa safari zangu ili tu nifate taratibu na nisilipe rushwa...(On a very serious note, SINA UHAKIKA KAMA VILE VITABU VYAO VYA BARABARANI NI HALALI, na RISITI TUNAZOPEWA NI ZA KWELI NA HELA INAINGIZIA PATO TAIFA, Ndio maana nimeopt kutake a long route) Mara Nyingi Traffic akikuona una msimamo wa kukubali kosa na kuwa tayari kutoa ushirikiano wa kwenda kituoni, Huwa wanakuachia....Ni wiki iliyopita tu nilikamatwa Kingolwira kosa ni kwenda 57 sehemu ya 50, nikakubali kosa na kuwaomba waniachie niendelee na safari, wakataka fine nikatoa jibu rahisi kabisa, SINA PESA HAPA... wakataka twende kituoni nikalale hadi Jumatatu nikajibu shitaka mahakamani nikakubali (nikijua kabisa nikifikishwa kituoni sitalala kwasababu ntawaomba waniachie na Police wa kituoni huwa wanaachia tu watu kwa mambo kama hayo)... Nikakaa pale kama dakika 40 baadae wakanipa leseni yangu nikaondoka, Sasa Ningekuwa na moyo wa rushwa pale ningejifanya nataka kuwahi nikawaachia nusu ya fine (15,000) Nikaondoka... Patience saved my doe...

Tusiwe wepesi wa kujifanya tuna haraka utadhani tunawahi wagonjwa tuwafanyie operation wasife, Utasikia mtu ooh watanichelewesha. kumbe anawahi bar au nyumbani kwake... Kwani unakoenda kunahama??

Traffic ni Binadamu kama sisi, wana aibu, huzuni na huruma kama watu wengine... Ukiwa na Kauli nzuri hata siku moja hawatakusumbua.


Mara kadhaa nimekamatwa na traffic kwa kosa halali lakini nimesalimika bila kulipa faini au rushwa kwa kuomba msamaha na kuongea lugha ya kistaarabu. Tatizo watu wanawachukulia traffic police kama mijitu fulani. Ki ukweli kazi yao ni ngumu sana sana sana. Hebu fikiria jua la mchana kuongoza magari, mvua inanyesha wapo, saa tatu usiku wako barabarani. Pamoja na mapungufu yao kama wanadamu, lakini wanafanya kazi iliyo njema sana.
 
Back
Top Bottom