Niko kituo cha mabasi yaendayo mikoani UBUNGO kuanzia saa 12:00 mpaka saa hii hatujaondoka inadaiwa kuna ukaguzi wa leseni ni mateso wana JF nijo kwenye najimunisa naenda singida
Nadhani tuwaache wahakukishe usalama wenu ili muwe na uhakika wa kufika salama; KAWIA UFIKE MKUU
Pole sana ndugu yangu ukifika SINGIDA waambie yaliyokutokea halafu ni sababu ya CCM wasimchague tena MZINZI MWIGULU MCHEMBA na yule MHINNDI mwizi.
Wangekuwa na heshima kwa binadam, wangekagua kabla abiria hawajaingia kwenye magari, (siku moja kabla ya safari) magari ambayo yangekidhi viwango wanavyovitaka yangeruhusiwa kuanza safari siku husika. Kwa kuwa binadamu wa tanzania hathaminiwi utu wake, ndio maana wanapigishwa miayo pale terminal. Poleni wasafiri, mnaokwenda iramba magharibi pelekeni m4c jimbo lipate mbunge sahihi muda ukifika.
Hapo kwenye red!Binadamu akishaingia kwenye basi anageuka kuwa mzigo.Ndiyo maana madereva wakifika mizani wanaulizwa mbona mzigo umezidi?
Mimi pia ni mmoja wa waathirika.
Niko kwenye basi la METRO tangu saa 12.30 muda huu ndio tumetoka tuko kibaha stendi.
Hakika hali imekuwa tete sana, na sijui ntafika saa ngapi Ngaleloo!
Mkuu mleta mada naomba tutafutane japo pale sehemu ya Menyu Comfort Motel. upo na basi gani?