Kero: TANESCO Arusha, Wanasumbua ukitaka kuwekewa umeme

Mukwano jebaleko

JF-Expert Member
Mar 30, 2015
402
213
Habari wanabodi,

Wadau nimekutana na kero ambayo nimeshindwa kuvumilia, Ni hivi tulituma maombi ya kuwekewa umeme Kwenye nyumba yetu iliyo katika eneo la moshono-Arusha.

Baada ya kumaliza taratibu zote tuliahidiwa kufungiwa mita mwezi wa pili, cha kushangaza jirani mwezi wa pili ulipita tukaanza kuwafuatilia na majibu yao yakawa hatuna waya.. subirini hadi tutakapopata waya..

Mwezi uliopita jirani yangu alipewa umeme.. mie nilikua mbali niliporudi kila siku nikaanza kufuatilia.leo nimeenda tena wameniambia hawana waya wiki nzima sasa najiuliza ni kweli hawana waya au kuna tatizo Jingine?

Leo wameniambia nitoe copy risiti nilizolipia, pia wameniambia nisubiri hadi watakapo pata waya watanipigia..

Je hii imekaaje wakuu? Kwa wenye uelewa wanisaidie kuepukana na kero hii.
Thanks
 
We unasema Arusha,kuja Tabora uone mziku wake,Wanataka kunyenyekewa na kubembelezwa na Mlungula juu!!!CCM ni JANGA!!!!
 
Back
Top Bottom