Kero - Magari ya serikali, mawaziri, wanajeshi wanaotanua barabarani

PatPending

JF-Expert Member
Aug 17, 2007
491
101
Kumekuwa na tabia chafu ya magari ya wizara, idara na mawakala mbalimbali wa serikali, mawaziri, spika, naibu spika, majaji na hata wanajeshi kujiona ya kwamba wao wapo juu ya sheria za usalama barabarani na hivyo kwa dharau na kejeli kubwa kuamua kutokukaa foleni na kuamua kulazimisha kupita pembeni aidha katika hifadhi ya barabara au upande mkabala wa barabara ama "kutanua" kama inavyojulikana siku hizi.
Mifano hai ipo mingi tu na ni karibia kila siku inatokea, mfano gari la Waziri wa Ulinzi halikai foleni, leo hii gari la Naibu Spika halikukaa foleni, yote licha ya kutokuwa na mwongozo wa askari polisi au ving'ora.

Hakuna sheria au kifungu chake kinachowapa haki hii na hii ni dharau na kejeli kubwa dhidi ya walipa kodi na watumiaji wengine wa barabara. Sheria ya Usalama Barabarani No.30 ya mwaka 1973 na marekebisho yake mbalimbali kuanzia yale ya mwaka 1980, 1996, n.k hayawapi ruhusa hii. Wengine wanadiriki kusema au kufikiri kwamba wao ni msafara wa kiofisi jambo ambalo si sahihi kwa mujibu wa ufafanuzi wa sehemu ya 4 kifungu namba 43(2) cha sheria hii kinachosema

"For the purposes of this section ''an official motorcade'' means
a motorcade of two or more motor vehicles escorted by or carrying a
police officer to ensure that such motorcade has a safe and unimpeded
journey to its destination"


Vile vile pia tambueni ya kwamba nyinyi si magari ya huduma za dharura kama vile sehemu ya 4 vifungu vya 54 (1), 54(2) na 54(5) vinavyoainisha.


Nawaombeni askari wa usalama barabarani mfanye kazi yenu na kuwabana hawa watu maana sisi sote tuna haraka na sio wao pekee tu. Sheria iko wazi maana watu wote wenye kutanua wanafanya makosa chini ya kifungu namba 50 kinachohusiana na "Careless or inconsiderate use of motorvehicles"

Tabia hii chafu inakera na kuhatarisha usalama wa watu, mali na vyombo vingine vinavyotumia na kuzunguka barabara.

Tabia hii chafu hutendekea zaidi majira ya asubuhi na jioni pale wakati kunapokuwa na msongamano mkubwa wa magari barabarani.

Tafadhalini jamani, kama mna haraka sana basi wahini kuamka asubuhi au kutoka kabla ya barabara kufurika.

Mnatukwaza sana sisi walipa kodi wenye kufuata sheria. Sheria za nchi ni lazima ziheshimiwe na kufuatwa na wote.
 
Ukiona waziri anafanya hivyo ujue akili zake ni kama dereva wa daladala, na ana malezi mabaya.
Cheo ni dhamana tu ya kuwaongoza wananchi, na hivyo hakitakiwi kutumika kama kichaka cha kuvunjia sheria!
Lakini lawama zingine zinatakiwa kwenda kwa traffic...kwanini wanachekelea hilo?
 
Ukiona waziri anafanya hivyo ujue akili zake ni kama dereva wa daladala, na ana malezi mabaya.
Cheo ni dhamana tu ya kuwaongoza wananchi, na hivyo hakitakiwi kutumika kama kichaka cha kuvunjia sheria!
Lakini lawama zingine zinatakiwa kwenda kwa traffic...kwanini wanachekelea hilo?

Ni double standards. Hawa ni kama vile wako kwa ajili ya kuharass magari yenye namba za kiraia. Kwanza hawa niliowataja magari yao yenyewe hayana cha bima wala hayalipii leseni ya matumizi ya barabara lakini bado tu yanapewa "kipaumbele" kushinda raia
 
hii tabia ya kunyenyekea magari ya serikali na kuogopa vyombo vya dola kama jeshi nk sijui inatoka wapi,watu wanafanya kama ni nchi ya kidikteta ambapo watawala na wanajeshi hawaguswi!
walipa kodi walio wengi hawaoni hili,bado wamelala
 
Nisi eleweke vibaya, siungi mkono uvunjaji sheria kwa kofia yoyote ile. Lakini jamani watanzania tumezoea kufanya mabo kwa kujuana. Hata muuza chips tu mtaani umewahi lakini akija jamaa anafahamiana nae akamwita kwajina tu atahudumiwa kwanza. Halikadhaliki mahospitalini, na kila mahali pemye huduma. Nikweli ikiwa zamu ya mwenzako akafanya blanda unakasirika unasahau kwamba na ww hufanya hivyo hivyo. Hata karani ukimkuta kwenye kiti chake cha enzi kama na unashida inayohitaji umwone boss wake utajuta!
Kwa ufupi watanzania tunaishi kwa mazoea na si kwa kufuata utaratibu. Tukishikana mashati kilamtu afuate utaratibu hii inchi watanzania wa sasa wationa chungu sana na fujo kili maala. Unabisha? Kamata wanaotupa uchafu hovyo wote, kamata wanaovuta sigaara hadharani, kamata wavuta bangi wote, kamata makahaba wote, kamata wenye mabaa zinazo piga mziki katika makazi ya watu, kamata magari mabovu yote, yaaaaani kamata wote wote wote.
Amini nakwambia mitaa itabaki mitupu. Na hii incha haito endelea bila ya kutokea jasiri wa kunyoosha yote. Na itabidi awe mbabe vya kutosha kwa maana uchaguzi utakao fuata hatopata kura kwa kuwa atakuwa adui wa watanzinia kwa nia yake nzuri. Nawasilisha cjamaliiza bali nimeckoka.
 
Nisi eleweke vibaya, siungi mkono uvunjaji sheria kwa kofia yoyote ile. Lakini jamani watanzania tumezoea kufanya mabo kwa kujuana. Hata muuza chips tu mtaani umewahi lakini akija jamaa anafahamiana nae akamwita kwajina tu atahudumiwa kwanza. Halikadhaliki mahospitalini, na kila mahali pemye huduma. Nikweli ikiwa zamu ya mwenzako akafanya blanda unakasirika unasahau kwamba na ww hufanya hivyo hivyo. Hata karani ukimkuta kwenye kiti chake cha enzi kama na unashida inayohitaji umwone boss wake utajuta!
Kwa ufupi watanzania tunaishi kwa mazoea na si kwa kufuata utaratibu. Tukishikana mashati kilamtu afuate utaratibu hii inchi watanzania wa sasa wationa chungu sana na fujo kili maala. Unabisha? Kamata wanaotupa uchafu hovyo wote, kamata wanaovuta sigaara hadharani, kamata wavuta bangi wote, kamata makahaba wote, kamata wenye mabaa zinazo piga mziki katika makazi ya watu, kamata magari mabovu yote, yaaaaani kamata wote wote wote.
Amini nakwambia mitaa itabaki mitupu. Na hii incha haito endelea bila ya kutokea jasiri wa kunyoosha yote. Na itabidi awe mbabe vya kutosha kwa maana uchaguzi utakao fuata hatopata kura kwa kuwa atakuwa adui wa watanzinia kwa nia yake nzuri. Nawasilisha cjamaliiza bali nimeckoka.


kaka uliyosema ni sahihi kabisa hii nchi bila kupata kiongozi atakayeongoza kwa ubabe na chembechembe za kaudikteta hatutafika, sheria zipo lakini watu wanajifanyia mambo holelaholela kama nchi iko likizo, hili la magari kutanua inanikera kupita kiasi na hata trafiki polisi nao sidhani sio wakubebeshwa lawama kwa kiasi kikubwa kwani kwa watu wenye akili timamu sio mpaka usimamiwe ndo ufuate sheria, mi nashauri kama sheria za usalama barabarani zitizamwe upya mtu anapoapatikana na kosa ni kifungo mwezi mmoja bila faini na sheria isimtizame mtu usoni
 
Kumekuwa na tabia chafu ya magari ya wizara, idara na mawakala mbalimbali wa serikali, mawaziri, spika, naibu spika, majaji na hata wanajeshi kujiona ya kwamba wao wapo juu ya sheria za usalama barabarani na hivyo kwa dharau na kejeli kubwa kuamua kutokukaa foleni na kuamua kulazimisha kupita pembeni aidha katika hifadhi ya barabara au upande mkabala wa barabara ama "kutanua" kama inavyojulikana siku hizi.
Mifano hai ipo mingi tu na ni karibia kila siku inatokea, mfano gari la Waziri wa Ulinzi halikai foleni, leo hii gari la Naibu Spika halikukaa foleni, yote licha ya kutokuwa na mwongozo wa askari polisi au ving'ora.

Hakuna sheria au kifungu chake kinachowapa haki hii na hii ni dharau na kejeli kubwa dhidi ya walipa kodi na watumiaji wengine wa barabara. Sheria ya Usalama Barabarani No.30 ya mwaka 1973 na marekebisho yake mbalimbali kuanzia yale ya mwaka 1980, 1996, n.k hayawapi ruhusa hii. Wengine wanadiriki kusema au kufikiri kwamba wao ni msafara wa kiofisi jambo ambalo si sahihi kwa mujibu wa ufafanuzi wa sehemu ya 4 kifungu namba 43(2) cha sheria hii kinachosema

"For the purposes of this section ''an official motorcade'' means
a motorcade of two or more motor vehicles escorted by or carrying a
police officer to ensure that such motorcade has a safe and unimpeded
journey to its destination"


Vile vile pia tambueni ya kwamba nyinyi si magari ya huduma za dharura kama vile sehemu ya 4 vifungu vya 54 (1), 54(2) na 54(5) vinavyoainisha.


Nawaombeni askari wa usalama barabarani mfanye kazi yenu na kuwabana hawa watu maana sisi sote tuna haraka na sio wao pekee tu. Sheria iko wazi maana watu wote wenye kutanua wanafanya makosa chini ya kifungu namba 50 kinachohusiana na "Careless or inconsiderate use of motorvehicles"

Tabia hii chafu inakera na kuhatarisha usalama wa watu, mali na vyombo vingine vinavyotumia na kuzunguka barabara.

Tabia hii chafu hutendekea zaidi majira ya asubuhi na jioni pale wakati kunapokuwa na msongamano mkubwa wa magari barabarani.

Tafadhalini jamani, kama mna haraka sana basi wahini kuamka asubuhi au kutoka kabla ya barabara kufurika.

Mnatukwaza sana sisi walipa kodi wenye kufuata sheria. Sheria za nchi ni lazima ziheshimiwe na kufuatwa na wote.

ukiona anatanua na wee mfuate nyuma.kutanua kuko pale pale,ila tunaangalia na umuhimu,fuata nyuki ule asali,au utoke manundu!
 
Hili linchi ni vurugu tu kwa kwenda mbele......kila kukicha utasikia hili mara lile.....dah!
 
Hunishindi mimi kwa kuichukia hii tabia. Juzi karibu wanisababishie ajali! Gari ya polisi inaendeshwa katikati ya mji wrong site kwa kasi utadhani kuna mashindano kumbe wanaelekea bar.. Wenyewe wanajiona wajaanja, kumbe ushamba tu.
 
Back
Top Bottom