Umekosea sana jombaa,wakenya wengi tu hata hapa jf wanamtambua magufuli sana kwa anayofanya kwa vitendo si kuengea tu kama viongozi wengi Afrika.Wacha niseme zangu,mimi binafsi nimependelea kwa sana magufuli alivoingia kazi na kuindeleza kwa kasi ya ajab.
Yaani ni kama vile mkulima anapofika shambani akaona magugu yamelemea mmea wake,kinachobaki ni kukunja shati na kuanza kazi.Hapo ndo aliponifurahisha mie inakaa yeye alitamani urais kwa madaraka atakayopata ile afanye kazi si mali ama tu sifa ya urais.
Navoona ni kama vike alikuwa ana mpangilio wake zamani sanaa atakavofanya akipata urais.Mungu ampe nguvu ya kuendelea hivo hivo, ataipeleka tanzania majirani na watani wetu mbali sana, inshallah!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.